< Vakolosai 2 >

1 ulwakuva ninoghua kuuti mukagule ndavule nilyale ni mhumhuko nyinga vwimila jiinu, ku vooni vano vali ku Laodikia na kuvoni vano navaghaghile amaaso ghango mu lwa m'bili.
Kwa kuwa nataka mfahamu jinsi ambavyo nimekuwa na taabu nyingi kwa ajili yenu, kwa wote walioko Laodikia na kwa wote ambao hawajaona uso wangu katika mwili.
2 nivomba imbombo iji kuuti inumbula saave siwesie kuhuvisivua..... kukwisa palikimo ku lughano na mu vutajili.... vwoni vwa vwinga nu vukyang'haani vwa luhala, kwa kukagula ulufiso lwa lweli ulwa Nguluve, juno ghwe Kilisite.
Nafanya kazi ili kwamba mioyo yao iweze kufarijiwa kwa kuletwa pamoja katika upendo na katika utajiri wote wa wingi wa uhakika kamili wa maarifa, katika kuijua siri ya kweli ya Mungu, ambaye ni Kristo.
3 mwa mwene vutile vwoni vwa vukoola nu luhala sifisilue.
Katika Yeye hazina zote za hekima na maarifa zimefichwa.
4 nijova ndiki neke kuuti umuunhu ghweni nangavavombelaghe igila ku njovele inya vusyangi.
Nasema hivi ili kwamba mtu yeyote asije akawafanyia hila kwa hotuba yenye ushawishi.
5 nambe kuuti nanili palikimo numue ku m'bili, looli nili numue ku numbula. nihovoka kuvona uvutavike vwinu vunono ni ngufu sa lwinu mwa Kilisite.
Na ingawa sipo pamoja nanyi katika mwili, lakini nipo nanyi katika roho. Ninafurahi kuona utaratibu wenu mzuri na nguvu ya imani yenu katika Kristo.
6 ndavule mulyamupile uKilisite Mutwa, mughendaghe mwa mwene.
Kama mlivyompokea Kristo Bwana, tembeeni katika yeye.
7 mukangasivue mwa mwene, mujengwe mwa mwene, mukangasivue mu lwitiko ndavule mulyavulanisivue na kupinyua muluhongesio lwinga.
Mwimarishwe katika yeye, mjengwe katika yeye, mwimarishwe katika imani kama tu mlivyofundishwa, na kufungwa katika shukrani nyingi.
8 mulolaghe kuuti umuunhu ghweni nangavakolaghe mu masio ghano ghasila kimonga aghavusyangi kuling'haana na vaanhu fino vikwupila nu vutaviike vwa iisi, kisila kuling'haana nu Kilisite.
Angalieni ya kwamba mtu yeyote asiwanase kwa falsafa na maneno matupu ya udanganyifu kulingana na mapokeo ya wanadamu, kulingana na kanuni za kidunia, na sio kulingana na Kristo.
9 ulwakuva mwa mwene uvunywilifu vwoni uvwa Nguluve vukukala mumbili.
Kwa kuwa katika yeye ukamilifu wote wa Mungu unaishi katika mwili.
10 umue mumemesevue mwa mwene. umwene ghwe mutu ghwa vuwesia vwoni nu vutavulua.
Nanyi mmejazwa katika yeye. Yeye ni kichwa cha kila uweza na mamlaka.
11 mwa mwene kange mulyakekilue ku tohala jino najikavombike nu muunhu kuvusisivua um'bili ghwa danda. neke je tohala ja Kilisite.
Katika yeye pia mlitahiriwa kwa tohara isiyofanywa na wanadamu katika kuondolewa mwili wa nyama, lakini ni katika tohara ya Kristo.
12 mukasyililue palikimo nu nu mwene mu lwofugho. na kusila ja lwitiko mukasyilulivue ku ngufu sa Nguluve juno akansyuluile kuhuma kuvafue.
Mlizikwa pamoja naye katika ubatizo. Na kwa njia ya imani katika yeye mlifufuliwa kwa uweza wa Mungu, aliyemfufua kutoka kwa wafu.
13 na pano mulyafwile mu vuhosi vwinu kisila kukekua amaviili ghinu, akavavombile kuva vwumi palikimo nu mwene na kutusaghila uvuhosi vwitu vwoni.
Na mlipokuwa mmekufa katika makosa yenu na kutokutahiriwa kwa miili yenu, aliwafanya hai pamoja naye na kutusamehe makosa yetu yote.
14 akafutile ikumbukumbu isa kudajivua sino sikalembilue, nu vutavike vuno natukanoghiile kuva navyo.
Alifuta kumbukumbu ya madeni iliyoandikwa, na taratibu zilizokuwa kinyume nasi. Aliiondoa yote na kuigongomea msalabani.
15 akavusisie ghoni na kupaghika pakikovekano. akavusisie ingufu nu vutavulua. akaghavika pavuvalafu na kukughahovokela ku vusindi vwimila kikovekano kyake.
Aliziondoa nguvu na mamlaka. Aliyaweka wazi na kuyafanya kuwa sherehe ya ushidi kwa njia ya msalaba wake.
16 pe lino u muunhu ghweni nangavahighaghe umue kwa kulia nambe kunyua, nambe mu kighono kya kuhovokela nambe umwesi umpya, nambe ikighono kya Sabati.
Kwa hiyo, mtu yeyote asiwahukumu ninyi katika kula au katika kunywa, au kuhusu siku ya sikukuu au mwezi mpya, au siku za Sabato.
17 ifi fye fin'sulua fya ghano ghikwisa, neke ikikome ghwe Kilisite.
Hivi ni vivuli vya mambo yajayo, lakini kiini ni Kristo.
18 umuunhu ghweni nangapokuaghe ingigha jaake kwa kunoghelua uvukoola na kukufunya avanya Mhola. Umuunhu ughwa ndikio aikwingila mu sino asaghile ka na kusyangua na masaghe ghake agha m'bili.
Mtu awaye yote asinyang'anywe tuzo yake kwa kutamani unyenyekevu na kwa kuabudu malaika. Mtu wa jinsi hiyo huingia katika mambo aliyoyaona na kushawishiwa na mawazo yake ya kimwili.
19 umwene naikolelela umutu. kuhuma ku mutu kuuti um'bili ghwoni kukilila ifilungo fyake na mafupa kulunganisivua palikimo; na kukula muvukulilo vwa Nguluve.
Yeye hakishikilii kichwa. Ni kutoka katika kichwa kwamba mwili wote kupitia viungo vyake na mifupa huungwa na kushikamanishwa kwa pamoja; na hukua kwa ukuaji utolewao na Mungu.
20 ulwakuva mlyafwile palikimo nu Kilisite mu maghendele gha iisi, ongo mukukala hwene mukujivombela iisi:
Ikiwa mlikufa pamoja na Kristo kwa tabia za dunia, mbona mnaishi kama mnawajibika kwa dunia:
21 namungakolaghe nambe kuvonja,
“Msishike, wala kuonja, wala kugusa”?
22 agha ghooni ghalaghilue vwimila uvunangifu vuno vukwisa na kutumila, kuhangilanila ni mbulanisio sa vaanhu.
Haya yote yameamuriwa kwa ajili ya uharibifu ujao na matumizi, kutokana na maelekezo na mafundisho ya wanadamu.
23 indaghilo isi sili nu vukola vwa nyifunyilo sino sitendilue ku vunoghelua vwave na nakunyenyekela mu mhumhuko sa m'bili. neke sisila lutalama mu noghelua sa m'bili.
Sheria hizi zina hekima ya dini zilizotengenezwa kwa ubinafsi na unyenyekevu na mateso ya mwili. Lakini hazina thamani dhidi ya tamaa za mwili.

< Vakolosai 2 >