< Imbombo 10 >

1 Kwalyale umunhu jumonga muliaja ilya kaisaria, ilitavua lya mwene atambuluughwa Kornelio, alyale mbaha ghwa ipugha ikya va Kiitalia.
Kulikuwa na mtu fulani katika mji wa kaisaria, jina lake aliitwa Kornelio, alikuwa mkuu wa kikosi cha Kiitalia.
2 Alyale ikufunya kange alyale ikunsuma uNguluve mu nyumba ja mwene joni, alyahumisie indalama nyinga kuva Yahudi pe akale ikufunya kwa Nguluve ifighono fioni.
Alikuwa mchamungu na alimwabudu Mungu na nyumba yake yote; alitoa pesa nyingi kwa wayahudi na aliomba kwa Mungu siku zote.
3 Unsiki ghwa lisala lya gubia lubale pamwisi, akasaghile inyisaghilo isa vanyamola va Nguluve vikwisa kwa mwene unya mola akambula u “Kornelio!
Muda wa saa tisa za mchana, akaona maono Malaika wa Mungu anakuja kwake. Malaika akamwambia “Kornelio!
4 U kornelio akamulola unyamola kange alyale nu ludwesi uluvaha kyongo akati “Ulu lwa Luke mbaha?” unyamola aka m'bula “Inyifunyo sako nu luvonolo lwako kuva kotofu sitoghile kukyanya ndavule ing'humbukilo.
Kornelio akamwangalia malaika na alikuwa na hofu kubwa sana akasema “Hii ni nini mkuu?” Malaika akamwambia “Maombi yako na zawadi zako kwa masikini zimepanda juu kama kumbukumbu kwenye uwepo wa Mungu”.
5 Lino vomole avanhu valute mulikaja ilya Yafakuuntwala umunhu jumo juno itambulua Simon juno itambulua Petro.
Sasa tuma watu kwenda mji wa Yafa kumleta mtu mmoja anayeitwa Simoni ambaye pia huitwa Petro.
6 Ikukala nujuno itenda inguvu juno itambulua Simoni juno inyumba jamwene jili palubade pa misumbi.”
Anakaa na mtengenezaji wa Ngozi aitwaye Simoni ambaye nyumba yake iko kando ya bahari.”
7 Ye akyale unyamola juno alyale ijova nu mwene kuvuka, u Kornelio akavakemela avavomba mbombo munyumba ja mwene vavili, nu ns'sikali juno alyale ikunsuma u Nguluve pakate pava sikalisi vano valyale vikum'bombela imbombo.
Baada ya Malaika aliyekuwa akisema naye kuondoka, Kornelio akawaita watumishi wa nyumbani kwake wawili, na askari aliyekuwa akimwabudu Mungu kati ya maaskari waliokuwa wanamtumikia.
8 U Kornelio alyavavulile ghoni ghanoghalyahumile kange akavomola ku Yafa.
Kornelio aliwaambia yote yaliyotokea na akawatuma Yafa.
9 Ikighono kino kikafwatile unsiki ughwa lekela lubale valyale musila kange vakale pipi mu likaja, u Petro akatogha kukyanya ku dari na kukufunya.
Siku iliyofuata muda wa saa sita wakiwa njiani na wamekaribia mjini, Petro akapanda juu darini kuomba.
10 Pe akale ni njala neke alyale ilonda ikinu ikyakulia, Looli unsiki ghuno avanhu viteleka ikyakulia, akavonesevua inyisaghilo,
Na pia akawa na njaa na alihitaji kitu cha kula, lakini wakati watu wanapika chakula, akaonyeshwa maono,
11 akavuvwene uvulanga vudindwike ni kyombo kikwika ni kinu kinge ndavule amenda amakome ghikwika pasi palihanga mumbale isamwene soni iine.
akaona anga limefuguka na chombo kinashuka na kitu fulani kama nguo kubwa ikishuka chini kwenye ardhi katika kona zake zote nne.
12 Munkate mwa mwene mulyale ni fikano fyoni ifinyamaghulu ghane nafino fikwafula palihanga, ni fijuni ifyavulanga.
Ndani yake kulikuwa na aina zote za wanyama wenye miguu minne na watambaao juu ya ardhi, na ndege wa angani.
13 Pe ilisio likati wa mwene “sisimuka, PetroPetro hinja kange ulie”. Loli upero akati “Na lulianala, MUtwa ulwakuva
Tena sauti ikasema kwake “Amka, Petro chinja na ule”.
14 nanighelile kulia ikinu kyekyoni I'll ikivivi. Loli ilisio likisa kwa kwamwene kange
Lakini Petro akasema “Siyo hivyo, Bwana kwa sababu sijawahi kula kitu chochote najisi na kichafu.
15 ulwavuvili “Kino avalisie u Nguluve nungakiemelaghe vulamafu kange kivivi”.
Lakini sauti ikaja kwake tena kwa mara ya pili “Alichokitakasa Mungu usikiite najisi wala kichafu”.
16 Ulu lulyahumile katatu, ni kyombo kila ilyatolilue kuvulanga kange.
Hii ilitokea mara tatu, na kile chombo kikawa kimechukuliwa tena angani.
17 Unsiki ghuno u Petro alyahasing'ine vwimila vwa mbonekelo isio sihufia kiki, lolagha, avanhu vano vakomolilwe nu Kornelio vakima pavulongolo palilyango, vakaposiagha isila ijakuluta kunyumba.
Na wakati Petro akiwa katika hali ya kuchanganyikiwa juu ya hayo maono yanamaanisha nini, Tazama, watu waliokuwa wametumwa na Kornelio wakasimama mbele ya lango, wakiuliza njia ya kwenda kwenye nyumba.
18 Pe vakakemela nauposia ndavule u Simoni juno kange atambulwagha Petro ndavule kale ikukala Pala.
Na wakaita na kuuliza kama Simoni ambaye pia aliitwa Petro kama alikuwa anakaa pale.
19 Unsiki ughuo ghuno u Petro alyale isagha munyisaghilo isio, uMhepo akajova nu mwene “Lolagha avanhu vatatu vikukulonda.
Wakati huo Petro alipokuwa akiwaza juu ya hayo maono, Roho akasema naye, “Tazama watu watatu wanakutafuta.
20 Sisimuka kange ghukale pasi pe ulutaghe navene. Nungoghopaghe kuluta navene, ulwakuva nivomwile.”
Amka na ushuke chini na uende nao. Usiogope kwenda nao, kwa sababu nimewatuma.”
21 U Petro Akiva pasi kuvanave nakujova “Une nenenejuno mukunilonda. Nakii mwisile?”
Petro akashuka chini kwao na kusema “Mimi ni yule mnayemtafuta. Kwa nini mmekuja?”
22 Vakati, “Akida jumo ilitavua lya mwene Kornelio, umunhu ughwa vugholofu pe ilonda kukusuma u Nguluve, kange avanhu viujova vunofu mukisina kyoni iya kiyahudi, avulilue nava nyamola avaava Nguluve kukuvomola need valute kunyumba ja mwene, neke apulike imola inofu kuhuma kuvanave.”
Wakasema, “Akida mmoja jina lake Kornelio, mtu wa haki na hupenda kumwabudu Mungu, na watu humsema vyema katika taifa lote la kiyahudi, ameambiwa na malaika wa Mungu kukutuma ili kwenda kwenye nyumba yake, ili asikie ujumbe kutoka kwako.”
23 U Petro akavambilila vingile nkate napiukala palikimo nu mwene. Ilwakilavo jino jilyavingilile akasimuka akaluta palikimo nu mwene, na vanyalukolo vadebe kuhuma ku Yafa vakavingisaniagha naghwope.
Petro akawakaribisha kuingia ndani na kukaa pamoja naye. Asubuhi iliyofuata akaamka akaenda pamoja naye, na ndugu wachache kutoka Yafa wakaambatana naye.
24 Ikighono kino kikavingilile vakisile ku Kaisaria. Naju Kornelio alyale iuvaghulila; kange akavakemelile paliimo avanyalukolo vamwene nava manyani vamwene vano valipipi.
Siku iliyofuata walikuja Kaisaria. Na Kornelio alikuwa akiwasubiri; na alikuwa amewaita pamoja ndugu zake na marafiki zake wa karibu.
25 Unsiki ghuno u Petro akingila munkate, u Kornelio akamwambilila akafughama paasi pamaghulu gha mwene akamfughamila.
Wakati Petro akiingia ndani, Kornelio akamlaki na kuinama hadi chini kwenye miguu yake kwa kumheshimu.
26 Loli u Petro akamwamula akati “Isagha; une najune nelimunhu.”
Lakini Petro akamwinua na kusema “Simama; mimi mwenyewe pia ni mwanadamu.”
27 Unsiki ghuno u Petro akajovagha naghuope, akalutagha n'kate akavagha avanhu vakong'anile palikimo.
Wakati Petro akiwa anaongea naye, alienda ndani akakuta watu wamekusanyika pamoja.
28 Akavavula, “jumue mwevano mukagwile kuti ulu nalulaghilo lwa Kiyahudi kuhasing'ana nambe kughendelanilakughendelanila nu munhu ugwa kipelela iiki. Loli u Nguluve ansonile uneasy ulwakuti naninoghile kukunemela umunhu ghweni vulamafu nambe vunyali.
Akawaambia, “Ninyi wenyewe mnajua kuwa siyo sheria ya kiyahudi kushirikiana au kutembelewa na mtu ambaye si wa taifa hili. Lakini Mungu amenionesha mimi kuwa sipaswi kumwita mtu yeyote ni najisi au mchafu.
29 Fyenambe nisile isila kikanika, pano nikomolilue vwimila vwa uluo. Neke nivaposie nakiki mukomolivue vwimila unhealthy.”
Na ndiyo maana nimekuja bila kubisha, nilipotumwa kwa ajili ya hiyo. Kwa hiyo niwaulize kwa nini mlitumwa kwa ajili yangu.”
30 U Kornelio akati, “Ifighono fine fino fikakilile, amasiki ndavule agha nilyale nikufunya unsii ghwa kivalilo kya budika lubale pamwisi munkate munyumba jango; Nikalola pavulongolo palyune umunhu imile alyale namenda amavalafu,
Kornelio akasema, “Siku nne zilizopita, wakati kama huu nilikuwa naomba muda wa saa tisa mchana ndani ya nyumba yangu; Nikaona mbele yangu mtu amesimama akiwa na mavazi meupe,
31 Akambulile “Kornelio inyifunyo sako sipulikike Kwan Nguluve, ni mbonolo sako kuva n'kontofu silikikumbukilo pavulongolo pa Nguluve.
Akaniambia “Kornelio maombi yako yamesikiwa na Mungu, na zawadi zako kwa masikini zimekuwa ukumbusho mbele za Mungu.
32 Pa uluo omola umunhu ku Yafa akankemele umunhu jumbo juno ikemelua Simon ise kulyuve, juno kange itambulivua Petro. Juno ikukala kwajuno inosia ingwembe jumojumo juno itambulivua Simoni juno inyumba jamwene jilimulubale munyanja.
Kwa hiyo tuma mtu Yafa na akamwite mtu mmoja anayeitwa Simoni aje kwako, ambaye pia huitwa Petro. ambaye anaishi kwa mtengenezaji wa Ngozi mmoja aitwaye Simoni ambaye nyumba yake iko pembeni mwa bahari.
33 Gadilila: Ikidebe iki, “Ghwope iliva ikwisa ilijova numue,” namwale muvulembe vwa pakale.
Zingatia: Msatri huu, “Naya atakapokuja atasema nanyi,” haumo kwenye maandiko ya kale.
34 Pe u Petro aadindula umulomo ghwa mwene nakujova; “kyang'ani, nitika kuti u Nguluve nalinalo ulwa kuvaghana vamo.
Ndipo Petro akafungua mdomo wake na kusema “Kweli, nimeamini kuwa Mungu hawezi kuwa na upendeleo.
35 Pauluo kila kisina umunhu ghweni junoikufunya nakuvomba isavwakyang'ani ikwitisivua kwamwene.
Badala yake, kila taifa mtu yeyote anayemwabudu na kufanya matendo ya haki anakubalika kwake.
36 Ujimanyile imola jino akajihumisie ku vanhu va Israeli, pano akapulisiagha imola inofu ija lutengano kukilila u Yesu kilisite juno ghwe Mutwa ghwa vooni-
Unajua ujumbe alioutoa kwa watu wa Israel, alipokuwa akitangaza habari njema ya amani kupitia Yesu Kristo ambaye ni Bwana wa wote-
37 jumue mwevano mukagwile kind kikahumila, lino likahumile ku Yudea joni likatengulile ku Galilaya, ye lukilile ulwofugho luno u Yohana alupulisiagha. Lino likahumile likan'donyile u Yesu kilisite ndavule uNguluve alyam'ponisie amafuta nuMhepo Mwimike na kungufu.
ninyi wenyewe mnajua tukio lililotokea, ambalo limetokea Yudea yote na lilianzia Galilaya, baada ya ubatizo ambao Yohana alitangaza.
38 Alyaghendile nakuvomba inofuinofu nakuvuvusia voni vano vakapumusivue nu Stefano, ulyakuva uNguluve alyale paliimo nu mwene.
tukio lililokuwa linamhusu Yesu Kristo jinsi Mungu alivyomtia mafuta kwa Roho Mtakatifu na kwa nguvu. Alienda akifanya mema na kuponya wote walioteswa na ibilsi, kwa kuwa Mungu alikuwa pamoja naye.
39 Usue tulivolesi ghwa ghoni agha ghano akaghavombile mu iisi sasa vuYahudivuYahudi namu Yerusalemu- uju ghwe Yesu juno valyam'budile na kukum'paghika mumpiki.
Sisi ni mashahidi wa mambo yote aliyoyafanya katika nchi za Uyahudi na katika Yerusalemu- huyu ni Yesu waliyemuua na kumtundika mtini.
40 Umunhu ujuo u Nguluve aliyah nsyusisie ikighono ikya vutatu na kukum'pala kumanyikika,
Huyu mtu Mungu alimfufua siku ya tatu na kumpa kujulikana,
41 nakwekuti ku vanhu voni, looli kuvolesi uvano vasalulivue nu Nguluve. -usue jusue, twevano tukalile tumwene na kunyua naghwope pano ye asyukile kuhuma uvufue.
si kwa watu wote, lakini kwa mashahidi waliochaguliwa kabla na Mungu. - sisi wenyewe, tulio kula naye na kunywa naye baada ya kufufuka kutoka kwa wafu.
42 Atulaghile kudalikila na kukwolelela kuuti uju ghwejuno u Nguluve alyansaluile kuva mulamuli ghwa vumi na vafue.
Ametuagiza kuhubiri kwa watu na kushuhudia kuwa huyu ndiye ambaye Mungu alimchagua kuwa mwamuzi wa walio hai na waliokufa.
43 Mwamwene avavili voni volelaghe lulyale Kati ghweni juno ikumwitika kyang'ani ujuo ikwupilagha ulusaghilo ulwa vahosi kuhumila litavua lyamwene.”
Katika yeye manabii wote washuhudie, ili kwamba kila anayeamini katika yeye atapokea msamaha wa dhambi kupitia jina lake.”
44 Unsiki ghuno u Petrol akaghendelelagha kujova isi, u Mhepo Mwimike akavamemia voni vino vakapulikisyagha imola ija mwene.
Wakati Petro akiendelea kusema haya, Roho Mtakatifu akawajaza wote waliokuwa wakisikiliza ujumbe wake.
45 Avanhu vala vano valyahusike ni kipugha ikya vitiki vino valyavalya dumulivue- vala voni vano valisile nu Petro vaadeghagha vwimila vwa Mhepo Mwimike juno alyakung'ilue kuoni kuva panji.
Watu wale wanaohusika na kikundi cha waamini waliotahiriwa- wale wote waliokuja na Petro- walishangazwa, kwa sababu ya karama ya Roho Mtakatifu aliyemwagwa pia kwa wamataifa.
46 Ulwakuva valyapulike avapanji ava vijova ninjovele isinge na pikufunya kwa Nguluve. U Petro akamula,
Kwa kuwa walisikia hawa wamataifa wanaongea kwa lugha zingine na kumwabudu Mungu. Petro akajibu,
47 “Kwale umunhu juno anoghile kusigha amalenga ulwakuuti avanhu value kukwofughua, Avanhu ava vamwupile uMhepo Mwimike ndavule usue?”
“Kuna mtu yeyote anaweza kuzuia maji ili watu wasibatizwe, Watu hawa wamempokea Roho Mtakatifu kama sisi?”
48 Pe akalamula vofughue mulitavua lya Yesu kilisite. Pambele vakansuma ikale naghuope mufighono ndii.
Ndipo akawaamuru wabatizwe kwa jina la Yesu Kristo. Baadaye wakamwomba akae nao kwa siku kadhaa.

< Imbombo 10 >