< 1 Petro 2 >

1 Lino muvuleke uvuhosi vwoni, uvusyangi, uvukedusi, ikivini namaligho.
Kwa hiyo wekeni pembeni uovu wote, udanganyifu, unafiki, wivu na kashifa.
2 Ndavule avana avafyele, munogheluaghe utusiva utwa mwojo, kuuti mukulaghe n'kate muvupoki,
Kama watoto wachanga, mtamani maziwa safi ya kiroho, ili kwamba mweze kukua ndani ya wokovu,
3 ndavule mukagwile kuuti uMutwa nofu.
kama mmeonja kwamba Bwana ni mwema.
4 Mwisaghe kwa mwene juno ghwe livue ilyumi linolikanilue name vaanhu, neke ilio lisalulua nu Nguluve kange kwamwene lya ndalama nyanga.
Njoni kwake aliye jiwe hai linaloishi ambalo limekataliwa na watu, lakini hilo limechaguliwa na Mungu na ni la thamani kwake.
5 Najumue mulindavule amavue amumu ghanoghijengua kuva nyumba ja Mhepo u Mwimike, kuuti muuve vatekesi vimike vano vitavula ilitekelo mungufu isa Mhepo Mwimike lino likwitikisivua nu Nguluve uvwimila Yesu kilisite.
Ninyi pia ni kama mawe yaliyo hai yanayojengwa juu kuwa nyumba ya kiroho, ili kuwa ukuhani mtakatifu ambao hutoa dhabihu za kiroho zinazokubaliwa kwa Mungu kupitia Yesu Kristo.
6 Amalembe amimike ghiti ndiki, “Lolagha, mulikaja ilya Sayuni nivikile ilivue ilivaha ilya pa nguto, kange ilisalulua lya ndalama nyinga. Umunhu ghweni juno ikumwitika uvwimila umwene nangavone sooni.”
Andiko husema hivi, “Tazama, nimeweka katika Sayuni jiwe la pembeni, kuu na lililochaguliwa na la thamani. Yeyote aaminiye katika yeye hataona aibu”.
7 Mu uluo uvwoghopua uvwinu kulyumue mwevano mukumwitika. Neke Lelo, “ilivue lino likakanilue navajengi, ili lyelivue ilikome ilya pa nguto”-
Hivyo heshima ni yenu kwenu ninyi mnaoamini. Lakini, “jiwe lililokataliwa na wajenzi, hili limekuwa jiwe kuu la pembeni”-
8 kange, “livue lya kukuvala kange linalavue lyakughisia avanhu. “Avene vikuvala, vano navikulyitika ilisio, uluo lweluno unguluve akatavike vwimila avene.
na, “jiwe la kujikwaa na mwamba wa kujikwaa.”Wao hujikwaa, wanaolikataa neno, kwa lile ambalo pia walikuwa wameteuliwa kwalo.
9 Looli umwe mulikisina kisalulua, umwe muli vatekesi va Kiowa, vanhu va vuhasi vwa Nguluve jujuo, kuuti mupulisyaghe imbombo sajuno avakemelile kuhuma mung'isi nakukuvingisia mulumuli lwake ulwa kudegha.
Lakini ninyi ni ukoo uliochaguliwa, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa miliki ya Mungu, ili kwamba mweze kutangaza matendo ya ajabu ya yule aliyewaita kutoka gizani kuja kwenye nuru yake ya ajabu.
10 Umwe ulutasi namulyale vanhu va Nguluve, loolilooli lino mulivanhu vaake. Umwe namulyupile ulusungu, looli lino mwupile ulusungu.
Ninyi kwanza hamkuwa watu, lakini sasa ninyi ni watu wa Mungu. Ninyi hamkupokea rehema, lakini sasa mmepokea rehema.
11 Vanyalukolo vango, ulwakuva mulivahesia kange mulivakila Sila, nivakemelile muvuleke uvunoghelua uvwa m'bili ulwakuva vunangania amoojo ghinu.
Wapendwa, nimewaita kama wageni na wazurujaji kujinyima kutoka kwenye tamaa mbaya za dhambi, ambazo zinapigana vita na roho zenu.
12 Muvisaghe na maghendele amanono pakate pa vapanji, kuuti, navevikuvadesela kuuti muvomba inyivi, pano vikughagha amaghendele ghinu amanono vamughiniaghe uNguluve ikighono kino ilikwisa kuhigha avanhu vooni.
Mnapaswa kuwa na tabia njema kati ya mataifa, ili kwamba, kama watawasema kama kwamba mmefanya mambo maovu, wataziangalia kazi zenu njema na kumsifu Mungu katika siku ya kuja kwake.
13 Ulwakuva mulimwa Mutwa mukundaghe uvutavulilua uvwa iisi jave Ntwa ghwa iisi umwene ghwe mbaha,
Tii kila mamlaka ya mwanadamu kwa ajili ya Bwana, ikiwa mfalme kama mkuu,
14 nambe vaave vanyagila vano vikwomolua kukuvakopa avahosi nakukuvaghinia vano vivomba inofu.
ikiwa watawala waliotumwa kuwaadhibu watenda mabaya na kuwasifu wale wanaotenda mema.
15 Ulwakuva vughane vwa Nguluve, kuuti pano muvomba inofu musimia injovele sa kijasu savano van'kaguile umwene.
Kwa kuwa ni mapenzi ya Mungu, kwamba kwa kufanya mema mwanyamazisha mazungumzo ya kipuuzi ya watu wapumbavu.
16 Ndavule avanhu avavuke, neke namungavombaghe uvuhosi mukiteghe kya vwavuke, looli muvesaghe ndavule avavombi va Nguluve. Muvoghopaghe avanhu vooni.
Kama watu huru, msiutumie uhuru wenu kama kifuniko kwa maovu, bali muwe kama watumishi wa Mungu.
17 Muvaghanaghe avajinu. Mumwoghopaghe u Nguluve. Mumwoghopaghe untwa.
Waheshimuni watu wote. Wapendeni ndugu. Mwogopeni Mungu. Mweshimuni mfalme.
18 Mwevavoombi, muvisaghe vakuundi kuvavaha vinhu nakuvoghopa fiijo, nakwekuuti avavaha avanofu navakoola vene, looli kange vevahosi.
Watumwa, watiini bwana zenu kwa heshima yote, siyo tu bwana walio wazuri na wapole, lakini pia walio waovu.
19 Ulwakuva uNguluve ihovoka pono umunhu ghweni juno ikuguda muvuvafi pano ipulika musino na anaghile mulwaku m'bingilila umwene.
Kwa kuwa ni sifa kama yeyote atavumilia maumivu wakati anapoteseka pasipo haki kwa sababu ya dhamiri yake kwa Mungu.
20 Kuuli luvumbulilo luuki ndave mufivombagha uvuhosi kange mufitovuagha? Looli ndave muvombile inofu neke mupumukaghe ulwa kuhighua, mukumuhovosia uNguluve.
Ni faida gani iliyopo kama mwadumu kutenda dhambi kisha mwendelee kuadhibiwa? Lakini kama mmefanya mema na ndipo mteseke kwa kuhukumiwa, hii ni sifa njema kwa Mungu.
21 Mulyakemelilue mu uluo, ulwakuva ukilisite jujuo alyapumuike uvwimilaumwe, akavalekela ikihwanikisio kuuti muvingililaghe amaghendele ghaake.
Kwa hili mliitwa, kwa sababu Kristo pia aliteswa kwa ajili yenu, amewaachia mfano kwa ajili yenu kufuata nyayo zake.
22 Umwene nalya vombile inyivi, nambekujova ilisio limoonga ilya vusyangi.
Yeye hakufanya dhambi, wala haukuonekana udanganyifu wowote kinywani mwake.
23 Unsiki umwene ye ilighua, naalyagomwisie amaligho, yeipumusivua, naalyoghwifie looli alyamulekile sooni u Nguluve junojuno ihigha muvwakyang'ani.
Wakati yeye alipotukanwa, hakurudisha matukano, alipoteseka, hakutisha bali alijitoa mwenyewe kwake Yeye ahukumuye kwa haki.
24 Umwene jujuo alyapindile inyivi siitu mumbili ghwake mulwakufua muki kovekano, kuutikuuti tuleke kulongosevua nuvuhosi, looli tulongosevuaghe nu vugholofu. Vwimila kulemasivua kwa mwene muponile.
Yeye mwenyewe alizibeba dhambi zetu katika mwili wake kwenye mti, ili kwamba tusiwe na sehemu tena katika dhambi, na kwamba tuishi kwa ajili ya haki. Kwa kupigwa kwake ninyi mmepona.
25 Mweni mwevano mulyale mululudika hwene ng'holo sino jino jisovile, looli lino mungomokile un'dimi nu muloleleli ghwa moojo ghinu.
Wote mliokuwa mkitangatanga kama kondoo aliyepotea, lakini sasa mmerudi kwa mchungaji na mlinzi wa roho zenu.

< 1 Petro 2 >