< Luka 4 >

1 Kutsal Ruh'la dolu olarak Şeria Irmağı'ndan dönen İsa, Ruh'un yönlendirmesiyle çölde dolaştırılarak kırk gün İblis tarafından denendi. O günlerde hiçbir şey yemedi. Dolayısıyla bu süre sonunda acıktı.
Kisha, Yesu akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka Mto Jordani, na aliongozwa na Roho jangwani
2
kwa siku arobaini, na huko alijaribiwa na Ibilisi. Wakati huo hakula chochote, na mwisho wa wakati huo alihisi njaa.
3 Bunun üzerine İblis O'na, “Tanrı'nın Oğlu'ysan, şu taşa söyle ekmek olsun” dedi.
Ibilisi akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, liamru jiwe hili kuwa mkate.”
4 İsa, “‘İnsan yalnız ekmekle yaşamaz’ diye yazılmıştır” karşılığını verdi.
Yesu akamjibu, “Imeandikwa; 'mtu hataishi kwa mkate pekee.”
5 Sonra İblis İsa'yı yükseklere çıkararak bir anda O'na dünyanın bütün ülkelerini gösterdi.
Kisha Ibilisi alimwongoza juu kwenye kilele cha mlima, na akamwonyesha falme zote za dunia kwa muda mfupi.
6 O'na, “Bütün bunların yönetimini ve zenginliğini sana vereceğim” dedi. “Bunlar bana teslim edildi, ben de dilediğim kişiye veririm.
Ibilisi akamwambia, “Nitakupa mamlaka ya kutawala falme hizi zote pamoja na fahari zake. Naweza kufanya hivyo kwa sababu vyote vimekabidhiwa kwangu nivitawale, na ninaweza kumpa yeyote nitakaye kumpa.
7 Bana taparsan, hepsi senin olacak.”
Kwahiyo, kama utaniinamia na kuniabudu, vitu hivi vyote vitakuwa vyako.”
8 İsa ona şu karşılığı verdi: “‘Tanrın Rab'be tapacak, yalnız O'na kulluk edeceksin’ diye yazılmıştır.”
Lakini Yesu alijibu na kumwambia, “Imeandikwa, “lazima umwabudu Bwana Mungu wako, na lazima umtumikie Yeye peke yake.”
9 İblis O'nu Yeruşalim'e götürüp tapınağın tepesine çıkardı. “Tanrı'nın Oğlu'ysan, kendini buradan aşağı at” dedi.
Baadaye Ibilisi alimwongoza Yesu hadi Yerusalemu na kumweka sehemu ya juu kabisa ya jengo la hekalu na kumwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa.
10 “Çünkü şöyle yazılmıştır: ‘Tanrı, seni korumaları için Meleklerine buyruk verecek.’
Kwa sababu imeandikwa, “Atawaagiza malaika zake wakutunze na kukulinda,
11 ‘Ayağın bir taşa çarpmasın diye Seni elleri üzerinde taşıyacaklar.’”
na watakuinua juu mikononi mwao ili kwamba usiumize miguu yako juu ya jiwe.”
12 İsa ona şöyle karşılık verdi: “‘Tanrın Rab'bi denemeyeceksin!’ diye buyrulmuştur.”
Yesu akijibu alimwambia, “Imenenwa, “usimjaribu Bwana Mungu wako.”
13 İblis, İsa'yı her bakımdan denedikten sonra bir süre için O'nun yanından ayrıldı.
Ibilisi alipomaliza kumjaribu Yesu, alienda zake na kumwacha hadi wakati mwingine.
14 İsa, Ruh'un gücüyle donanmış olarak Celile'ye döndü. Haber bütün bölgeye yayıldı.
Kisha Yesu alirudi Galilaya kwa nguvu za Roho, na habari kumhusu yeye zikaenea na kusambaa katika mikoa jirani yote.
15 Oranın havralarında öğretiyor, herkes tarafından övülüyordu.
Alifundisha katika masinagogi yao, na kila mmoja alimsifu.
16 İsa, büyüdüğü Nasıra Kenti'ne geldiğinde her zamanki gibi Şabat Günü havraya gitti. Kutsal Yazılar'ı okumak üzere ayağa kalkınca O'na Peygamber Yeşaya'nın Kitabı verildi. Kitabı açarak şu sözlerin yazılı olduğu yeri buldu:
Siku moja alikwenda Nazareti, mji ambao alilelewa na kukulia. Kama ilivyokuwa desturi yake aliingia kwenye sinagogi siku ya sabato, na alisimama kusoma maandiko.
Alikabidhiwa gombo la nabii Isaya, hivyo, alilifungua gombo na akatafuta sehemu iliyoandikwa,
18 “Rab'bin Ruhu üzerimdedir. Çünkü O beni yoksullara Müjde'yi iletmek için meshetti. Tutsaklara serbest bırakılacaklarını, Körlere gözlerinin açılacağını duyurmak için, Ezilenleri özgürlüğe kavuşturmak Ve Rab'bin lütuf yılını ilan etmek için Beni gönderdi.”
“Roho wa Bwana yuu juu yangu, kwa sababu alinitia mafuta kuhubiri habari njema kwa maskini. Amenituma kutangaza uhuru kwa wafungwa, na kuwafanya wasioona waweze kuona tena. Kuwaweka huru wale wanaogandamizwa,
kuutangaza mwaka ambao Bwana ataonesha wema wake.”
20 Sonra kitabı kapattı, görevliye geri verip oturdu. Havradakilerin hepsi dikkatle O'na bakıyordu.
Kisha akalifunga gombo, akamrudishia kiongozi wa sinagogi, na akaketi chini. Macho ya watu wote waliokuwa katika sinagogi yalimwangalia yeye.
21 İsa, “Dinlediğiniz bu Yazı bugün yerine gelmiştir” diye konuşmaya başladı.
Alianza kuzungumza nao akisema, “Leo andiko hili limetimizwa masikioni mwenu.”
22 Herkes İsa'yı övüyor, ağzından çıkan lütufkâr sözlere hayran kalıyordu. “Yusuf'un oğlu değil mi bu?” diyorlardı.
Kila mmoja pale alishuhudia kile alichokisema Yesu, na wengi miongoni mwao walishangazwa na maneno ya hekima yaliyokuwa yakitoka katika kinywa chake. Walikuwa wakisema, “huyu ni kijana tu wa Yusufu, siyo hivyo?”
23 İsa onlara şöyle dedi: “Kuşkusuz bana şu deyimi hatırlatacaksınız: ‘Ey hekim, önce kendini iyileştir! Kefarnahum'da yaptıklarını duyduk. Aynısını burada, kendi memleketinde de yap.’”
Yesu akawaambia, “hakika mtasema methali hii kwangu, “Tabibu, jiponye mwenyewe. Chochote tulichosikia ukifanya Kapernaumu, kifanye hapa pia kijijini kwako.”
24 “Size doğrusunu söyleyeyim” diye devam etti İsa, “Hiçbir peygamber kendi memleketinde kabul görmez.
Pia alisema, “hakika nawaambia ninyi, hakuna nabii anayekubalika katika nchi yake.”
25 Yine size gerçeği söyleyeyim, gökyüzünün üç yıl altı ay kapalı kaldığı, bütün ülkede korkunç bir kıtlığın baş gösterdiği İlyas zamanında İsrail'de çok sayıda dul kadın vardı.
Lakini nawaambia ninyi kweli kwamba kulikuwa na wajane wengi Israel katika kipindi cha Eliya, wakati mbingu ilipofungwa kusiwe na nvua kwa miaka mitatu na nusu, wakati kulipokuwa na njaa kubwa katika nchi yote.
26 İlyas bunlardan hiçbirine gönderilmedi; yalnız Sayda bölgesinin Sarefat Kenti'nde bulunan dul bir kadına gönderildi.
Lakini Eliya hakutumwa kwa yeyote mmoja wao, lakini kwa mjane mmoja tu aliyeishi Sarepta karibu na mji wa Sidoni.
27 Peygamber Elişa'nın zamanında İsrail'de çok sayıda cüzamlı vardı. Bunlardan hiçbiri iyileştirilmedi; yalnız Suriyeli Naaman iyileştirildi.”
Pia, kulikuwa na wakoma wengi Israel katika kipindi cha Elisha nabii, lakini hakuna hatammoja wao aliyeponywa isipokuwa Naamani mtu wa Siria.
28 Havradakiler bu sözleri duyunca öfkeden kudurdular.
Watu wote ndani ya sinagogi walijawa na gadhabu walipoyasikia haya yote.
29 Ayağa kalkıp İsa'yı kentin dışına kovdular. O'nu uçurumdan aşağı atmak için kentin kurulduğu tepenin yamacına götürdüler.
Walisimama na kumsukumizia nje ya mji, na kumwongoza mpaka kwenye ukingo wa mlima wa mji ambapo mji wao ulijengwa juu yake, ili waweze kumtupa chini.
30 Ama İsa onların arasından geçerek oradan uzaklaştı.
Lakini alipita salama katikati yao na akaenda zake.
31 Sonra İsa Celile'nin Kefarnahum Kenti'ne gitti. Şabat Günü halka öğretiyordu.
Kisha alitelemkia Kapernaumu, katika mji wa Galilaya. Sabato moja alikuwa akifundisha watu ndani ya sinagogi.
32 Yetkiyle konuştuğu için O'nun öğretişine şaşıp kaldılar.
Walishangazwa na mafundisho yake, kwasababu alifundisha kwa mamlaka.
33 Havrada cinli, içinde kötü ruh olan bir adam vardı. Adam yüksek sesle, “Ey Nasıralı İsa, bırak bizi! Bizden ne istiyorsun?” diye bağırdı. “Bizi mahvetmeye mi geldin? Senin kim olduğunu biliyorum, Tanrı'nın Kutsalı'sın sen!”
Sasa siku hiyo ndani ya sinagogi, kulikuwa na mtu aliyekuwa na roho ya pepo mchafu, na alilia kwa sauti ya juu,
“Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Umekuja kutuangamiza? Ninajua wewe ni nani! Wewe ni mtakatifu wa Mungu!”
35 İsa, “Sus, çık adamdan!” diyerek cini azarladı. Cin adamı herkesin önünde yere vurduktan sonra, ona hiç zarar vermeden içinden çıktı.
Yesu alimkemea pepo akisema, “Nyamaza kimya, na umtoke mtu huyu!” Pepo yule alipomtupa mtu yule chini katikati yao, alimtoka yule mtu bila ya kumsababishia maumivu yoyote.
36 Herkes şaşkına dönmüştü. Birbirlerine, “Bu nasıl söz? Güç ve yetkiyle kötü ruhlara çıkmalarını buyuruyor, onlar da çıkıyor!” diyorlardı.
Watu wote walishangaa, na waliendelea kuzungumzia jambo hilo kila mmoja na mwenzake. Wakasema, “Ni maneno ya aina gani haya?” Anawaamuru roho wachafu kwa mamlaka na nguvu na watondoka.”
37 İsa'yla ilgili haber o bölgenin her yanında yankılandı.
Hivyo, habari juu ya Yesu zilienea kila sehemu katika maeneo yanayozunguka mkoa huo.
38 İsa havradan ayrılarak Simun'un evine gitti. Simun'un kaynanası hastaydı, ateşler içindeydi. Onun için İsa'dan yardım istediler.
Kisha Yesu aliondoka katika mji huo na akaingia katika nyumba ya Simoni. Sasa, mama mkwe wake na Simoni alikuwa anaumwa homa kali, na wakamsihi kwa niaba yake.
39 İsa kadının başucunda durup ateşi azarladı, kadının ateşi düştü. Kadın hemen ayağa kalkıp onlara hizmet etmeye başladı.
Hivyo, Yesu alimsogelea, akaikemea ile homa na ikamwachia. Ghafla alisimama na akaanza kuwatumikia.
40 Güneş batarken herkes çeşitli hastalıklara yakalanmış akrabalarını İsa'ya getirdi. İsa her birinin üzerine ellerini koyarak onları iyileştirdi.
Jua lilipokuwa likizama, watu walimletea Yesu kila mmoja aliyekuwa mgonjwa wa maradhi ya aina mbalimbali. Aliweka mikono yake juu ya kila mgonjwa na akawaponya wote.
41 Birçoğunun içinden cinler de, “Sen Tanrı'nın Oğlu'sun!” diye bağırarak çıkıyordu. Ne var ki, İsa onları azarladı, konuşmalarına izin vermedi. Çünkü kendisinin Mesih olduğunu biliyorlardı.
Mapepo pia yaliwatoka wengi wao yakilia kwa sauti na kusema, “Wewe ni mwana wa Mungu!” Yesu aliwakemea mapepo na hakuwaruhusu waongee, kwa sababu walijua kwamba yeye alikuwa ni Kristo.
42 Sabah olunca İsa dışarı çıkıp ıssız bir yere gitti. Halk ise O'nu arıyordu. Bulunduğu yere geldiklerinde O'nu yanlarında alıkoymaya çalıştılar.
Wakati kulipopambazuka, alienda eneo lisilokuwa na watu. Makutano ya watu walikuwa wakimtafuta na wakaja katika eneo alilokuwapo. Walijaribu kumzuia asiende mbali na wao.
43 Ama İsa, “Öbür kentlerde de Tanrı'nın Egemenliği'yle ilgili Müjde'yi yaymam gerek” dedi. “Çünkü bunun için gönderildim.”
Lakini akawaambia, “Lazima pia nihubiri habari njema za ufalme wa Mungu katika miji mingine mingi, kwa kuwa hii ndiyo sababu nilitumwa hapa.”
44 Böylece Yahudiye'deki havralarda Tanrı sözünü duyurmaya devam etti.
Kisha aliendelea kuhubiri ndani ya masinagogi katika uyahudi wote.

< Luka 4 >