< Yahuda 1 >

1 İsa Mesih'in kulu, Yakup'un kardeşi ben Yahuda'dan, Baba Tanrı tarafından sevilip İsa Mesih için korunmuş olan çağrılmışlara selam!
Mimi Yuda, mtumishi wa Yesu Kristo, ndugu yake Yakobo, nawaandikia ninyi mlioitwa na Mungu na ambao mnaishi katika upendo wa Mungu Baba, na katika ulinzi wa Yesu Kristo.
2 Merhamet, esenlik ve sevgi artan ölçüde sizin olsun.
Nawatakieni huruma, amani na upendo kwa wingi.
3 Sevgili kardeşlerim, size ortak kurtuluşumuzla ilgili yazmaya çok gayret ettim. Bu arada sizi kutsallara ilk ve son kez emanet edilen iman uğrunda mücadeleye özendirmek için yazma gereğini duydum.
Ndugu wapenzi, wakati nimo katika jitihada ya kuwaandikieni juu ya ule wokovu tunaoshiriki sote, nimeona lazima ya kuwaandikieni na kuwahimizeni mwendelee kupigana kwa ajili ya imani ambayo Mungu amewajalia watu wake mara moja tu kwa wakati wote.
4 Çünkü Tanrımız'ın lütfunu sefahate araç eden, tek Efendimiz ve Rabbimiz İsa Mesih'i yadsıyan bazı tanrısızlar gizlice aranıza sızdılar. Onların yargılanacakları çoktan beri yazılmıştır.
Maana watu wasiomcha Mungu wamepata kujiingiza kwa siri miongoni mwetu, watu ambao, kwa faida ya maisha yao mabaya, wanaupotosha ujumbe wa neema ya Mungu wetu na kumkana Yesu Kristo aliye peke yake kiongozi na Bwana wetu. Maandiko Matakatifu yalikwisha bashiri tangu awali hukumu inayowangojea watu hao.
5 Bütün bunları bildiğiniz halde, size anımsatmak isterim ki, ilk ve son kez halkı Mısır'dan kurtaran Rab iman etmeyenleri daha sonra yok etti.
Nataka kuwakumbusheni mambo fulani ambayo mmekwisha yajua: kumbukeni jinsi Bwana alivyowaokoa watu wa Israeli na kuwatoa katika nchi ya Misri, lakini baadaye aliwaangamiza wale ambao hawakuamini.
6 Yetkilerinin sınırı içinde kalmayıp kendilerine ayrılan yeri terk etmiş olan melekleri, büyük yargı günü için çözülmez bağlarla bağlayarak karanlığa hapsetti. (aïdios g126)
Na, malaika ambao hawakuridhika na cheo chao, wakayaacha makao yao ya asili, Mungu amewafunga gizani kwa minyororo ya milele wahukumiwe Siku ile kuu. (aïdios g126)
7 Sodom, Gomora ve çevrelerindeki kentler de benzer biçimde kendilerini fuhuş ve sapıklığa teslim ettiler. Sonsuza dek ateşte yanma cezasını çeken bu kentler ders alınacak birer örnektir. (aiōnios g166)
Kumbukeni pia Sodoma na Gomora, na miji ya kandokando yake; wenyeji wake walifanya kama wale malaika; walifanya uzinzi na mambo yaliyo kinyume cha maumbile, wakapewa hukumu ya moto wa milele, iwe onyo kwa watu wote. (aiōnios g166)
8 Aranıza sızan bu kişiler de onlar gibi gördükleri düşlere dayanarak öz bedenlerini kirletiyor, Rab'bin yetkisini hiçe sayıyor, yüce varlıklara sövüyorlar.
Hivyo ndivyo pia walivyo watu hawa. ndoto zao huwaongoza katika kuichafua miili yao wenyewe, kuyadharau mamlaka ya Mungu na kuvitukana viumbe vitukufu vya huko juu.
9 Oysa Başmelek Mikail bile Musa'nın cesedi konusunda İblis'le çekişip tartışırken, söverek onu yargılamaya kalkışmadı. Ancak, “Seni Rab azarlasın” dedi.
Hata Mikaeli, malaika mkuu, hakufanya hivyo. Katika ule ubishi kati yake na Ibilisi waliobishana juu ya mwili wa Mose, Mikaeli hakuthubutu kumhukumu Ibilisi kwa matusi; ila alisema: “Bwana mwenyewe na akukaripie.”
10 Ama bu kişiler anlamadıkları her şeye sövüyorlar. Öte yandan, akıldan yoksun hayvanlar gibi içgüdüleriyle anladıkları ne varsa, onları yıkıma götürüyor.
Lakini watu hawa hutukana chochote wasichokielewa; mambo yaleyale wanayoyajua kwa silika kama vile wanyama wanayoyajua ndiyo yanayowaangamiza.
11 Vay onların haline! Çünkü Kayin'in yolundan gittiler. Kazanç için kendilerini Balam'ınkine benzer bir yanılgıya kaptırdılar. Korah'ınkine benzer bir isyanda mahvoldular.
Ole wao! Watu hao wamefuata mwenendo uleule wa Kaini. Kwa ajili ya fedha, wamejiingiza katika mkosi uleule wa Baalamu. Wameasi kama Kora alivyoasi na wameangamizwa kama yeye alivyoangamizwa.
12 Sevgi şölenlerinizde sizinle birlikte pervasızca yiyip içen bu kişiler birer kara lekedir. Yalnız kendilerini besleyen çobanlardır. Rüzgarın sürüklediği yağmursuz bulutlara, iki kez ölmüş, kökünden sökülmüş, sonbaharın meyvesiz ağaçlarına benzerler.
Kwa makelele yao yasiyo na adabu, watu hao ni kama madoa machafu katika mikutano yenu ya karamu ya Bwana. Hujipendelea wao wenyewe tu, na wako kama mawingu yanayopeperushwa huko na huko na upepo bila ya kuleta mvua. Wao ni kama miti isiyozaa matunda hata wakati wa majira yake, wamekufa kabisa.
13 Köpüğünü savuran denizin azgın dalgaları gibi ayıplarını çevreye savururlar. Serseri yıldızlar gibidirler. Onları sonsuza dek sürecek koyu karanlık bekliyor. (aiōn g165)
Watu hao ni kama mawimbi makali ya bahari, na matendo yao ya aibu yanaonekana dhahiri kama vile mapovu ya mawimbi. Wao ni kama nyota zinazotangatanga, ambao Mungu amewawekea mahali pao milele katika giza kuu. (aiōn g165)
14 Adem'den sonraki altıncı kuşaktan olan Hanok, bu adamlara ilişkin şu peygamberlikte bulundu: “İşte Rab herkesi yargılamak üzere on binlerce kutsalıyla geliyor. Tanrı yoluna aykırı, tanrısızca yapılan bütün işlerden ve tanrısız günahkârların kendisine karşı söylediği bütün ağır sözlerden ötürü Rab, bütün insanlara suçluluklarını gösterecektir.”
Henoki, ambaye ni babu wa saba tangu Adamu, alibashiri hivi juu ya watu hawa: “Sikilizeni! Bwana atakuja pamoja na maelfu ya malaika wake watakatifu
kutoa hukumu juu ya binadamu wote, kuwahukumu wote kwa ajili ya matendo yao yote maovu waliyotenda na kwa ajili ya maneno yote mabaya ambayo watu waovu walimkashifu nayo.”
16 Bunlar hep yakınıp söylenir, kendi tutkularının peşinden giderler. Ağızlarından kurumlu sözler çıkar, kendi çıkarları için başkalarını pohpohlarlar.
Watu hawa wananung'unika daima na kuwalaumu watu wengine. Hufuata tamaa zao mbaya, hujigamba na kuwasifu watu wengine mno kusudi wafaulu katika mipango yao.
17 Ama siz, sevgili kardeşlerim, Rabbimiz İsa Mesih'in elçileri tarafından önceden söylenen sözleri anımsayın.
Lakini ninyi wapenzi wangu, kumbukeni yale mliyoambiwa hapo awali ni mitume wa Bwana wetu Yesu Kristo.
18 Size demişlerdi ki, “Dünyanın son günlerinde alay edenler, tanrısızlığa yönelip kendi tutkularına göre yaşayanlar olacaktır.”
Waliwaambieni: “Siku za mwisho zitakapofika, watatokea watu watakaowadhihaki ninyi, watu wafuatao tamaa zao mbaya.”
19 Bunlar bölücü, insan doğasıyla sınırlı, Kutsal Ruh'tan yoksun kişilerdir.
Hao ndio watu wanaosababisha mafarakano, watu wanaotawaliwa na tamaa zao za kidunia, watu wasio na Roho wa Mungu.
20 Ama siz, sevgili kardeşlerim, kendinizi tümden kutsal olan imanınızın temeli üzerinde geliştirin. Kutsal Ruh'un yönetiminde dua edin.
Lakini ninyi, wapenzi wangu, endeleeni kujijenga kikamilifu katika imani yenu takatifu. Salini kwa nguvu ya Roho Mtakatifu,
21 Rabbimiz İsa Mesih'in sizi sonsuz yaşama kavuşturacak olan merhametini beklerken kendinizi Tanrı'nın sevgisinde koruyun. (aiōnios g166)
na kubaki katika upendo wa Mungu, mkiwa mnamngojea Bwana wetu Yesu Kristo awapeni uzima wa milele kwa huruma yake. (aiōnios g166)
22 Kimi kararsızlara merhamet edin.
Muwe na huruma kwa watu walio na mashaka;
23 Kimini ateşten çekip kurtarın. Kimine de korkuyla merhamet edin. Ama günahlı bir bedenin lekelediği giysiden bile tiksinin.
waokoeni kwa kuwanyakua kutoka motoni; na kwa wengine muwe na huruma pamoja na hofu, lakini chukieni hata mavazi yao ambayo yamechafuliwa na tamaa zao mbaya.
24 Kurtarıcımız tek Tanrı, sizi düşmekten alıkoyacak, büyük sevinç içinde lekesiz olarak yüce huzuruna çıkaracak güçtedir.
Kwake yeye awezaye kuwalinda msije mkaanguka, na kuwaleta ninyi bila hatia mpaka mbele ya utukufu wake,
25 Yücelik, ululuk, güç ve yetki Rabbimiz İsa Mesih aracılığıyla bütün çağlardan önce, şimdi ve bütün çağlar boyunca Tanrı'nın olsun! Amin. (aiōn g165)
kwake yeye aliye peke yake Mungu, Mkombozi wetu, uwe utukufu, ukuu, nguvu na mamlaka kwa njia ya Kristo Bwana wetu, tangu zama zote, sasa na hata milele! Amina. (aiōn g165)

< Yahuda 1 >