< Efesliler 2 >

1 Sizler bir zamanlar içinde yaşadığınız suçlardan ve günahlardan ötürü ölüydünüz.
Kama vile mlivyo kuwa mmekufa katika makosa na dhambi zenu.
2 Bu dünyanın gidişine ve havadaki hükümranlığın egemenine, yani söz dinlemeyen insanlarda şimdi etkin olan ruha uymaktaydınız. (aiōn g165)
Ilikuwa katika haya kwamba kwanza mlienenda kulingana na nyakati za ulimwengu huu. Mlikuwa mkienenda kwa kufuata mtawala wa mamlaka ya anga. Hii ndiyo roho yake yule afanyaye kazi katika wana wa kuasi. (aiōn g165)
3 Bir zamanlar hepimiz böyle insanların arasında, benliğin ve aklın isteklerini yerine getirerek benliğimizin tutkularına göre yaşıyorduk. Doğal olarak ötekiler gibi biz de gazap çocuklarıydık.
Sisi wote hapo mwanzo tulikuwa miongoni mwa hawa wasioamini. Tulikuwa tukitenda kwa namna ya tamaa mbaya za miili yetu. Tulikuwa tukifanya mapenzi ya mwili na ufahamu wetu. Tulikuwa kwa asili wana wa ghadhabu kama wengine.
4 Ama merhameti bol olan Tanrı bizi çok sevdiği için,
Lakini Mungu ni mwingi wa rehema kwa sababu ya pendo lake kubwa alilotupenda sisi.
5 suçlarımızdan ötürü ölü olduğumuz halde, bizi Mesih'le birlikte yaşama kavuşturdu. O'nun lütfuyla kurtuldunuz.
Wakati tulipokuwa wafu katika makosa yetu, alituleta pamoja katika maisha mapya ndani ya Kristo. Ni kwa neema kwamba mmeokolewa.
6 Tanrı bizi Mesih İsa'da, Mesih'le birlikte diriltip göksel yerlerde oturttu.
Mungu alitufufua pamoja na kutufanya kukaa pamoja katika mahali pa mbingu ndani ya Kristo Yesu.
7 Bunu, Mesih İsa'da bize gösterdiği iyilikle, lütfunun sonsuz zenginliğini gelecek çağlarda sergilemek için yaptı. (aiōn g165)
Alifanya hivi ili katika nyakati zijazo aweze kutuonesha utajiri mkuu wa neema yake. Hutuonesha sisi hili kwa njia ya wema wake ndani ya Kristo Yesu. (aiōn g165)
8 İman yoluyla, lütufla kurtuldunuz. Bu sizin başarınız değil, Tanrı'nın armağanıdır.
Kwa neema mmeokolewa kwa njia ya imani. Na hii haikutoka kwetu. Ni zawadi ya Mungu.
9 Kimsenin övünmemesi için iyi işlerin ödülü değildir.
Haitokani na matendo. Matokeo yake, asiwepo mmoja wapo wa kujisifu.
10 Çünkü biz Tanrı'nın yapıtıyız, O'nun önceden hazırladığı iyi işleri yapmak üzere Mesih İsa'da yaratıldık.
Kwa sababu sisi tu kazi ya Mungu, tumeumbwa katika Kristo Yesu kutenda matendo mema. Ni matendo haya ambayo Mungu aliyapanga tangu zamani za kale kwa ajili yetu, ili tutembee katika hayo.
11 Bunun için, öteki uluslardan doğan sizler bir zamanlar ne olduğunuzu anımsayın: Bedende elle yapılmış sünnete sahip olup “sünnetli” diye anılanların “sünnetsiz” dedikleri sizler,
Kwa hiyo kumbukeni kwamba hapo zamani mlikuwa watu wa Mataifa kwa jinsi ya mwili. Mnaitwa “msio na tohara” kwa kile kinachoitwa tohara ya mwili inayofanywa kwa mikono ya binadamu.
12 o zaman Mesihsiz, İsrail'de vatandaşlıktan yoksun, vaade dayanan antlaşmalara yabancı, dünyada umutsuz ve tanrısızdınız.
Kwa wakati huo mlikuwa mmetengwa na Kristo. Mlikuwa wageni kwa watu wa Israel. Mlikuwa wageni kwa agano la ahadi. Hamkuwa na uhakika wa wakati ujao. Mlikuwa bila Mungu katika ulimwengiu.
13 Ama bir zamanlar uzak olan sizler, şimdi Mesih İsa'da Mesih'in kanı sayesinde yakın kılındınız.
Lakini sasa katika Kristo Yesu ninyi ambao hapo mwanzo mlikuwa mbali na Mungu mmeletwa karibu na Mungu kwa damu ya Kristo.
14 Çünkü Mesih'in kendisi barışımızdır. Kutsal Yasa'yı, buyrukları ve kurallarıyla birlikte etkisiz kılarak iki topluluğu birleştirdi, aradaki engel duvarını, yani düşmanlığı kendi bedeninde yıktı. Amacı bu iki topluluktan kendisinde yeni bir insan yaratarak esenliği sağlamak, düşmanlığı çarmıhta öldürmek ve çarmıh aracılığıyla bir bedende iki topluluğu Tanrı'yla barıştırmaktı.
Kwa maana yeye ndiye amani yetu. Alifanya wawili kuwa mmoja. Kwa mwili wake aliuharibu ukuta wa utengano ambao ulikuwa umetutenganisha, huo uadui.
Kwamba alikomesha sheria ya amri na kanuni ili kwamba aumbe mtu mmoja mpya ndani yake. Akafanya amani.
Alifanya hivi ili kuwapatanisha makundi mawili ya watu kuwa mwili mmoja kwa Mungu kupitia msalaba. Kwa njia ya msalaba aliufisha uadui.
17 O gelip hem uzakta olan sizlere hem de yakındakilere esenliği müjdeledi.
Yesu alikuja na kutangaza amani kwenu ninyi mliokuwa mbali na amani kwao wale waliokuwa karibu.
18 O'nun aracılığıyla hepimiz tek Ruh'ta Baba'nın huzuruna çıkabiliriz.
Kwa maana kwa njia ya Yesu sisi wote wawili tuna nafasi kwa yule Roho mmoja kuingia kwa Baba.
19 Böylece artık yabancı ve garip değil, kutsallarla birlikte yurttaş ve Tanrı'nın ev halkısınız.
Hivyo basi, ninyi watu wa mataifa si wasafiri na wageni tena. Bali ni wenyeji pamoja na wale waliotengwa kwa ajili ya Mungu na wajumbe katika nyumba ya Mungu.
20 Elçilerle peygamberlerden oluşan temel üzerine inşa edildiniz. Köşe taşı Mesih İsa'nın kendisidir.
Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii. Kristo Yesu mwenyewe alikuwa jiwe kuu la pembeni.
21 Bütün yapı Rab'be ait kutsal bir tapınak olmak üzere O'nda kenetlenip yükseliyor.
Katika yeye jengo lote limeungamanishwa pamoja na kukua kama hekalu ndani ya Bwana.
22 Siz de Ruh aracılığıyla Tanrı'nın konutu olmak üzere hep birlikte Mesih'te inşa ediliyorsunuz.
Ni ndani yake ninyi nanyi mnajengwa pamoja kama mahali pa kuishi pa Mungu katika Roho.

< Efesliler 2 >