< Warumi 14 >

1 Mkaribisheni kwenu mtu aliye dhaifu, lakini msibishane naye juu ya mawazo yake binafsi.
Him that is weake in the fayth receave vnto you not in disputynge and troublynge his conscience.
2 Watu huhitilafiana: mmoja imani yake inamruhusu kula kila kitu; lakini mwingine ambaye imani yake ni dhaifu, hula tu mboga za majani.
One beleveth that he maye eate all thinge. Another which is weake eateth earbes.
3 Mtu ambaye hula kila kitu asimdharau yule ambaye hawezi kula kila kitu; naye ambaye hula tu mboga za majani asimhukumu anayekula kila kitu, maana Mungu amemkubali.
Let not him that eateth despise him that eateth not. And let not him whiche eateth not iudge him that eateth. For God hath receaved him.
4 Wewe ni nani hata uthubutu kumhukumu mtumishi wa mwingine? Akisimama au akianguka ni shauri la Bwana wake; naam, atasimama imara, maana Bwana anaweza kumsimamisha.
What arte thou that iudgest another manes servaut? Whether he stonde or faule that pertayneth vnto his master: ye he shall stonde. For God is able to make him stonde.
5 Mtu anaweza kufikiria siku fulani kuwa ya maana zaidi kuliko nyingine; mtu mwingine aweza kuzifikiria siku zote kuwa sawa. Kila mmoja na afuate msimamo wa akili yake.
This man putteth difference bitwene daye and daye. Another man counteth all dayes alyke. Se that no man waver in his awne meanynge.
6 Anayeadhimisha siku fulani anaadhimisha siku hiyo kwa ajili ya kumtukuza Mungu; naye anayekula chakula fulani anafanya hivyo kwa kumtukuza Bwana maana anamshukuru Mungu. Kadhalika naye anayeacha kula chakula fulani anafanya hivyo kwa ajili ya kumtukuza Bwana, naye pia anamshukuru Mungu.
He that observeth one daye more then another doth it for ye lordes pleasure. And he that observeth not one daye moare then another doeth it to please ye lorde also. He that eateth doth it to please the lorde for he geveth god thankes.
7 Maana hakuna mtu yeyote miongoni mwetu aishiye kwa ajili yake mwenyewe, wala hakuna anayekufa kwa ajili yake mwenyewe
And he yt eateth not eateth not to please ye lorde wt all and geveth god thankes.
8 maana tukiishi twaishi kwa ajili ya Bwana; tukifa, tunakufa kwa ajili ya Bwana. Basi, kama tukiishi au tukifa, sisi ni mali yake Bwana.
For none of vs lyveth his awne servaut: nether doeth anye of vs dye his awne servaunt. Yf we lyve we lyve to be at ye lordes will. And yf we dye we dye at ye lordes will. Whether we lyve therfore or dye we are the lordes.
9 Maana Kristo alikufa, akafufuka ili wapate kuwa Bwana wa wazima na wafu.
For Christ therfore dyed and rose agayne and revived that he myght be lorde both of deed and quicke.
10 Kwa nini, basi wewe wamhukumu ndugu yako? Nawe, kwa nini wamdharau ndugu yako? Sisi sote tutasimama mbele ya kiti cha hukumu cha Mungu.
But why doest thou then iudge thy brother? Other why doest thou despyse thy brother? We shall all be brought before the iudgement seate of Christ.
11 Maana Maandiko yanasema: “Kama niishivyo, asema Bwana kila mtu atanipigia magoti, na kila mmoja atakiri kwamba mimi ni Mungu.”
For it is written: as truely as I lyve sayth ye lorde all knees shall bowe to me and all tonges shall geve a knowledge to God.
12 Kwa hiyo, kila mmoja wetu atatoa hoja yake mbele ya Mungu.
So shall every one of vs geve accomptes of him selfe to God.
13 Basi, tuache kuhukumiana, bali tuazimie kutokuwa kamwe kikwazo kwa ndugu yetu au kumsababisha aanguke katika dhambi.
Let vs not therfore iudge one another eny more. But iudge this rather that no man put a stomblynge blocke or an occasion to faule in his brothers waye.
14 Katika kuungana na Bwana Yesu, nina hakika kwamba hakuna kitu chochote kilicho najisi kwa asili yake; lakini, mtu akidhani kwamba kitu fulani ni najisi, basi, kwake huwa najisi.
For I knowe and am full certified in the Lorde Iesus that ther is nothinge comen of it selfe: but vnto him that iudgeth it to be comen: to him is it comen.
15 Kama ukimhuzunisha ndugu yako kwa sababu ya chakula unachokula, basi mwenendo wako hauongozwi na mapendo. Usikubali hata kidogo chakula chako kiwe sababu ya kupotea kwa mtu mwingine ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake!
If thy brother be greved with thy meate now walkest thou not charitablye. Destroye not him with thy meate for whom Christ dyed.
16 Basi, msikubalie kitu mnachokiona kuwa kwenu ni kitu chema kidharauliwe.
Cause not youre treasure to be evyll spoken of.
17 Maana Utawala wa Mungu si shauri la kula na kunywa, bali unahusika na kuwa na uadilifu, amani na furaha iletwayo na Roho Mtakatifu.
For the kyngdome of God is not meate and drinke: but rightewesnes peace and ioye in the holy goost.
18 Anayemtumikia Kristo namna hiyo humpendeza Mungu, na kukubaliwa na watu.
For whosoever in these thinges serveth Christ pleaseth well God and is commended of men.
19 Kwa hiyo tuyazingatie daima mambo yenye kuleta amani, na yanayotusaidia kujengana.
Let vs folowe tho thinges which make for peace and thinges wherwith one maye edyfie another.
20 Basi, usiiharibu kazi ya Mungu kwa sababu ya ubishi juu ya chakula. Vyakula vyote ni halali, lakini haifai kula chakula ambacho kitamfanya mtu aanguke katika dhambi.
Destroye not ye worke of god for a lytell meates sake. All thinges are pure: but it is evyll for that man which eateth with hurte of his conscience.
21 Afadhali kuacha kula nyama, kunywa divai, au kufanya chochote ambacho chaweza kumsababisha ndugu yako aanguke.
It is good nether to eate flesshe nether to drincke wyne nether eny thinge wherby thy brother stombleth ether falleth or is made weake.
22 Basi, shikilia unachoamini kati yako na Mungu wako. Heri mtu yule ambaye, katika kujiamulia la kufanya, haipingi dhamiri yake.
Hast thou fayth? have it with thy selfe before god. Happy is he yt condempneth not him selfe in that thinge which he aloweth.
23 Lakini mtu anayeona shaka juu ya chakula anachokula, anahukumiwa kama akila, kwa sababu msimamo wa kitendo chake haumo katika imani. Na, chochote kisicho na msingi wake katika imani ni dhambi.
For he yt maketh conscience is dampned yf he eate: because he doth it not of fayth. For whatsoever is not of fayth that same is synne.

< Warumi 14 >