< Ufunuo 9 >

1 Kisha malaika wa tano akapiga tarumbeta yake. Nami nikaona nyota iliyokuwa imeanguka juu ya nchi kutoka mbinguni. Nayo ikapewa ufunguo wa shimo la Kuzimu. (Abyssos g12)
Et le cinquième ange sonna de la trompette, et je vis une étoile qui était tombée du ciel sur la terre; et la clef du puits de l'abîme fut donnée à cet ange. (Abyssos g12)
2 Basi, nyota hiyo ikafungua shimo la Kuzimu, kukatoka moshi wa tanuru kubwa. Jua na anga vikatiwa giza kwa moshi huo wa Kuzimu. (Abyssos g12)
Et il ouvrit le puits de l'abîme, et il monta du puits une fumée, comme la fumée d'une grande fournaise; et le soleil et l'air furent obscurcis par la fumée du puits; (Abyssos g12)
3 Nzige wakatoka katika moshi huo, wakaingia duniani wakapewa nguvu kama ya ng'e.
Et de cette fumée, des sauterelles se répandirent sur la terre; et on leur donna un pouvoir semblable au pouvoir qu'ont les scorpions de la terre.
4 Wakaamrishwa wasiharibu nyasi za nchi wala majani wala miti yoyote, bali wawaharibu wale tu ambao hawakupigwa mhuri wa Mungu katika paji la uso.
Et il leur fut dit de ne faire aucun mal à l'herbe de la terre, ni à aucune verdure, ni à aucun arbre; mais seulement aux hommes qui n'ont pas le sceau de Dieu sur leurs fronts.
5 Nzige hao hawakuruhusiwa kuwaua watu, ila kuwatesa tu kwa muda wa miezi mitano. Maumivu watakayosababisha ni kama maumivu yanayompata mtu wakati anapoumwa na ng'e.
Et il leur fut donné, non de les tuer, mais de les torturer durant cinq mois, et leur torture était pareille à celle que cause le scorpion quand il pique l'homme.
6 Muda huo watu watatafuta kifo lakini hawatakipata; watatamani kufa lakini kifo kitawakimbia.
En ces jours-là, les hommes chercheront la mort, et ne la trouveront point; ils désireront de mourir, et la mort les fuira.
7 Kwa kuonekana, nzige hao walikuwa kama farasi waliowekwa tayari kwa vita. Juu ya vichwa vyao walikuwa na taji zilizo kama za dhahabu, na nyuso zao zilikuwa kama za binadamu.
Ces sauterelles ressemblaient à des chevaux préparés pour le combat; il y avait sur leurs têtes comme des couronnes semblables à de l'or; et leurs visages étaient comme des visages d'hommes.
8 Nywele zao zilikuwa kama nywele za wanawake, na meno yao yalikuwa kama meno ya simba.
Elles avaient des cheveux comme des cheveux de femmes, et leurs dents étaient comme des dents de lions.
9 Vifua vyao vilikuwa vimefunikwa kitu kama ngao ya chuma. Sauti ya mabawa yao ilikuwa kama sauti ya msafara wa magari ya farasi wengi wanaokimbilia vitani.
Elles avaient des cuirasses comme des cuirasses de fer; et le bruit de leurs ailes était semblable au bruit de chariots à plusieurs chevaux qui courent au combat.
10 Walikuwa na mikia na miiba kama ng'e, na kwa mikia hiyo, walikuwa na nguvu ya kuwadhuru watu kwa muda wa miezi mitano.
Elles avaient des queues semblables à celles des scorpions, et à leurs queues un aiguillon; et leur pouvoir était de nuire aux hommes pendant cinq mois.
11 Tena wanaye mfalme anayewatawala, naye ndiye malaika wa kuzimu; jina lake kwa Kiebrania ni Abadoni, na kwa Kigiriki ni Apolioni, yaani mwangamizi. (Abyssos g12)
Et elles avaient au-dessus d'elles un roi, l'ange de l'abîme, appelé en hébreu Abaddon, et dont le nom en grec est Apollyon (Exterminateur). (Abyssos g12)
12 Maafa ya kwanza yamepita; bado mengine mawili yanafuata.
Le premier malheur passé, voici il vient encore deux autres malheurs après celui-là.
13 Kisha malaika wa sita akapiga tarumbeta yake. Nami nikasikia sauti moja kutoka katika pembe nne za madhabahu ya dhahabu iliyokuwa mbele ya Mungu.
Et le sixième ange sonna de la trompette; et j'entendis une voix, qui venait des quatre cornes de l'autel d'or, qui est devant Dieu,
14 Sauti hiyo ikamwambia huyo malaika wa sita mwenye tarumbeta, “Wafungulie malaika wanne waliofungwa kwenye mto mkubwa Eufrate!”
Disant au sixième ange qui avait la trompette: Délie les quatre anges qui sont liés sur le grand fleuve de l'Euphrate.
15 Naye akawafungulia malaika hao wanne ambao walikuwa wametayarishwa kwa ajili ya saa hiyo ya siku ya mwezi huo, wa mwaka huohuo, kuua theluthi moja ya wanaadamu.
Aussitôt furent déliés les quatre anges qui étaient prêts pour l'heure, le jour, le mois, et l'année, afin de tuer la troisième partie des hommes.
16 Nilisikia idadi ya majeshi wapanda farasi ilikuwa milioni mia mbili.
Et le nombre des cavaliers de cette armée s'élevait à deux cent millions; car j'en entendis le nombre.
17 Hivi ndivyo nilivyowaona hao farasi na wapanda farasi katika hiyo njozi: Walikuwa na ngao vifuani zilizokuwa moto mtupu, zenye rangi ya samawati na njano kama kiberiti. Vichwa vya hao farasi vilikuwa kama vya simba; na moto, moshi, na kiberiti vilikuwa vinatoka kinywani mwao.
Or je vis ainsi les chevaux dans la vision; ceux qui étaient assis dessus, avaient des cuirasses de couleur de feu, et d'hyacinthe, et de soufre; les têtes des chevaux étaient comme des têtes de lions, et de leurs bouches il sortait du feu, de la fumée, et du soufre.
18 Theluthi moja ya wanaadamu waliuawa kwa mabaa hayo matatu yaani, moto, moshi na kiberiti, yaliyokuwa yanatoka katika vinywa vyao;
La troisième partie des hommes fut tuée par ces trois choses, par le feu, par la fumée, et par le soufre, qui sortaient de leur bouche.
19 maana nguvu ya farasi hao ilikuwa vinywani mwao na katika mikia yao. Mikia yao ilikuwa na vichwa kama nyoka, na waliitumia hiyo kuwadhuru watu.
Car leur pouvoir était dans leurs bouches et dans leurs queues, et leurs queues, semblables à des serpents, avaient des têtes; et par celles-ci elles faisaient du mal.
20 Wanaadamu wengine waliobaki ambao hawakuuawa na mabaa hayo, hawakugeuka na kuviacha vitu walivyokuwa wametengeneza kwa mikono yao wenyewe; bali wakaendelea kuabudu pepo, sanamu za dhahabu, fedha, shaba, mawe na miti, vitu ambavyo haviwezi kuona, kusikia wala kutembea.
Et le reste des hommes qui ne furent pas tués par ces plaies, ne se repentirent point des œuvres de leurs mains, pour cesser d'adorer les démons, et les idoles d'or, d'argent, d'airain, de pierre, et de bois, qui ne peuvent ni voir, ni entendre, ni marcher.
21 Wala hawakutubu na kuacha kufanya mauaji, uchawi, uzinzi, na wizi.
Ils ne se repentirent pas de leurs meurtres, ni de leurs enchantements, ni de leurs impudicités, ni de leurs rapines.

< Ufunuo 9 >