< Mathayo 27 >

1 Kulipopambazuka, makuhani wakuu wote na wazee wa watu walifanya mashauri juu ya Yesu wapate kumwua.
Ko je prišlo jutro, so se vsi visoki duhovniki in starešine izmed ljudstva posvetovali zoper Jezusa, da ga usmrtijo.
2 Wakamfunga pingu, wakamchukua, wakamkabidhi kwa Pilato, mkuu wa mkoa.
In ko so ga zvezali, so ga odvedli proč ter ga izročili voditelju Ponciju Pilatu.
3 Hapo, Yuda ambaye ndiye aliyemsaliti, alipoona kwamba wamekwisha mhukumu Yesu, akajuta, akawarudishia makuhani wakuu zile sarafu thelathini za fedha.
Potem se je Juda, ki ga je izdal, ko je videl, da je bil obsojen, pokesal in trideset koščkov srebra prinesel nazaj k visokim duhovnikom in starešinam,
4 Akawaambia, “Nimekosa kwa kumtoa mtu asiye na hatia auawe.” Lakini wao wakasema, “Yatuhusu nini sisi? Hilo ni shauri lako.”
rekoč: »Grešil sem, ker sem izdal nedolžno kri.« Oni pa so rekli: »Kaj je to nam? Ti glej na to.«
5 Naye akazitupa zile fedha Hekaluni, akatoka nje, akaenda akajinyonga.
In srebrne koščke je vrgel v tempelj in odšel ter samega sebe obesil.
6 Makuhani wakuu wakazichukua zile fedha, wakasema, “Haifai kuziweka katika hazina ya Hekalu kwa maana ni fedha za damu.”
Visoki duhovniki pa so vzeli koščke srebra in rekli: »Ni zakonito, da jih damo v zakladnico, ker so cena krvi.«
7 Basi, wakashauriana, wakazitumia kununua shamba la mfinyanzi liwe mahali pa kuzika wageni.
In posvetovali so se ter z njimi kupili lončarjevo njivo, da bi v njej pokopavali tujce.
8 Ndiyo maana mpaka leo shamba hilo linaitwa Shamba la Damu.
Zatorej je bilo to polje do današnjega dne imenovano Njiva krvi.
9 Hivyo maneno ya nabii Yeremia yakatimia: “Walizichukua sarafu thelathini za fedha, thamani ya yule ambaye watu wa Israeli walipanga bei,
Tedaj je bilo izpolnjeno to, kar je bilo rečeno po preroku Jeremiju, rekoč: ›In vzeli so trideset koščkov srebra, ceno tistega, ki je bil ocenjen, ki so ga Izraelovi otroci ocenili,
10 wakanunua nazo shamba la mfinyanzi, kama Bwana alivyoniagiza.”
in dali so jih za lončarjevo njivo, kakor mi je določil Gospod.‹
11 Yesu alisimamishwa mbele ya mkuu wa mkoa. Basi, mkuu wa mkoa akamwuliza, “Je, wewe ndiwe Mfalme wa Wayahudi?” Yesu akamwambia, “Wewe umesema.”
In Jezus je stal pred voditeljem in voditelj ga je vprašal, rekoč: »Ali si ti judovski Kralj?« Jezus mu je rekel: »Ti praviš.«
12 Lakini makuhani wakuu na wazee walipokuwa wanamshtaki, hakujibu neno.
In ko je bil obtožen od visokih duhovnikov in starešin, ni ničesar odgovoril.
13 Hivyo Pilato akamwuliza, “Je, husikii mashtaka hayo yote wanayotoa juu yako?”
Tedaj mu je Pilat rekel: »Ali ne slišiš, koliko besed pričajo zoper tebe?«
14 Lakini Yesu hakumjibu hata neno moja; hata huyo mkuu wa mkoa akashangaa sana.
Pa mu ni odgovoril niti na eno besedo, tako, da se je voditelj silno čudil.
15 Ilikuwa kawaida wakati wa Sikukuu ya Pasaka mkuu wa mkoa kuwafungulia Wayahudi mfungwa mmoja waliyemtaka.
Torej, na ta praznik je imel voditelj navado množici izpustiti jetnika, ki bi ga hotela.
16 Wakati huo kulikuwa na mfungwa mmoja, jina lake Baraba.
In takrat so imeli opaznega jetnika, imenovanega Baraba.
17 Hivyo, watu walipokusanyika pamoja, Pilato akawauliza, “Mwataka nimfungue yupi kati ya wawili hawa, Baraba ama Yesu aitwae Kristo?”
Ko so bili torej zbrani skupaj, jim je Pilat rekel: »Katerega hočete, da vam izpustim? Baraba ali Jezusa, ki se imenuje Kristus?«
18 Alisema hivyo maana alijua wazi kwamba walimleta kwake kwa sababu ya wivu.
Kajti vedel je, da so mu ga izročili zaradi zavisti.
19 Pilato alipokuwa amekaa katika kiti cha hukumu, mke wake akampelekea ujumbe: “Usijitie katika shauri la mtu huyu mwema, maana leo nimeteseka sana katika ndoto kwa sababu yake.”
Ko se je usedel na sodni stol, je njegova žena poslala k njemu, rekoč: »Nič ne imej s tem pravičnim človekom, kajti danes sem v sanjah zaradi njega trpela mnoge stvari.«
20 Lakini makuhani wakuu na wazee wakawashawishi watu waombe Baraba afunguliwe na Yesu auawe.
Toda visoki duhovniki in starešine so pregovorili množico, da bi zahtevali Baraba in uničili Jezusa.
21 Mkuu wa mkoa akawauliza, “Ni yupi kati ya hawa wawili mnayetaka nimfungue?” Wakamjibu, “Baraba!”
Voditelj je odgovoril in jim rekel: »Katerega od teh dveh hočete, da vam izpustim?« Rekli so: »Baraba.«
22 Pilato akawauliza, “Sasa, nifanye nini na Yesu aitwaye Kristo?” Wote wakasema, “Asulubiwe!”
Pilat jim reče: »Kaj naj potem storim z Jezusom, ki se imenuje Kristus?« Vsi so mu rekli: »Križan naj bo.«
23 Pilato akauliza, “Kwa nini? Amefanya kosa gani?” Wao wakazidi kupaaza sauti: “Asulubiwe!”
In voditelj jim je rekel: »Zakaj, kakšno zlo je storil?« Vendar so še bolj kričali, rekoč: »Križan naj bo.«
24 Basi, Pilato alipotambua kwamba hafanikiwi chochote na kwamba maasi yalikuwa yanaanza, alichukua maji, akanawa mikono mbele ya ule umati wa watu, akasema, “Mimi sina lawama juu ya kifo cha mtu huyu; shauri lenu wenyewe.”
Ko je Pilat videl, da niti malo ne more prevladati, temveč da je bil toliko bolj storjen nemir, je vzel vodo in svoje roke umil pred množico, rekoč: »Nedolžen sem pri krvi te pravične osebe; vi glejte na to.«
25 Watu wote wakasema, “Damu yake na iwe juu yetu na juu ya watoto wetu!”
Potem so vsi ljudje odgovorili in rekli: »Njegova kri bodi na nas in na naših otrocih.«
26 Hapo Pilato akawafungulia Baraba kutoka gerezani, lakini akamtoa Yesu asulubiwe.
Tedaj jim je izpustil Baraba in ko je Jezusa prebičal, ga je izročil, da bi bil križan.
27 Kisha askari wa mkuu wa mkoa wakamwingiza Yesu ndani ya ikulu, wakamkusanyikia kikosi kizima.
Tedaj so voditeljevi vojaki Jezusa vzeli v skupno dvorano in k njemu zbrali vso četo vojakov.
28 Wakamvua nguo zake, wakamvika joho la rangi nyekundu.
In ga slekli ter mu oblekli škrlatno svečano oblačilo.
29 Kisha wakasokota taji ya miiba, wakamvika kichwani, wakamwekea pia mwanzi katika mkono wake wa kulia. Wakapiga magoti mbele yake, wakamdhihaki wakisema, “Shikamoo mfalme wa Wayahudi!”
In ko so spletli krono iz trnja, so jo dali na njegovo glavo in trst v njegovo desnico; in poklekovali so pred njim ter ga zasmehovali, rekoč: »Pozdravljen, judovski Kralj!«
30 Wakamtemea mate, wakauchukua ule mwanzi, wakampiga nao kichwani.
In pljuvali so vanj in vzeli trst ter ga udarjali po glavi.
31 Baada ya kumdhihaki, wakamvua lile joho, wakamvika nguo zake, kisha wakampeleka kumsulubisha.
Potem pa, ko so ga zasmehovali, so z njega slekli svečano oblačilo in nanj nadeli njegova lastna oblačila ter ga odpeljali proč, da ga križajo.
32 Walipokuwa wakienda, wakamkuta mtu mmoja jina lake Simoni, mwenyeji wa Kurene, wakamlazimisha kuuchukua msalaba wake Yesu.
In ko so prišli ven, so našli človeka iz Cirene, Simona po imenu; njega so prisilili, da je nesel njegov križ.
33 Walipofika mahali paitwapo Golgotha, maana yake, “Mahali pa Fuvu la kichwa,”
In ko so prišli na kraj, imenovan Golgota, ki se mu reče ›kraj lobanje, ‹
34 wakampa mchanganyiko wa divai na nyongo. Lakini Yesu alipoonja akakataa kunywa.
so mu dali piti kisa, pomešanega z žolčem; in ko je le-tega pokusil, ni hotel piti.
35 Walimsulubisha, kisha wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura.
Oni pa so ga križali in metaje žreb razdelili njegove obleke, da bi se lahko izpolnilo, kar je bilo rečeno po preroku: ›Moje obleke so si delili med seboj in za mojo suknjo so metali žrebe.‹
36 Wakaketi, wakawa wanamchunga.
In sedeli so ter ga tam stražili;
37 Juu ya kichwa chake wakaweka shtaka dhidi yake lilioandikwa, “Huyu ni Yesu, Mfalme wa Wayahudi.”
in nad njegovo glavo so namestili njegovo napisano obtožbo: TA JE JEZUS, JUDOVSKI KRALJ.
38 Wanyang'anyi wawili walisulubishwa pia pamoja naye, mmoja upande wa kushoto na mwingine upande wa kulia.
Takrat sta bila tam z njim križana dva tatova, eden na desni roki, drugi pa na levi.
39 Watu waliokuwa wanapita mahali hapo walimtukana wakitikisa vichwa vyao na kusema,
Tisti pa, ki so hodili mimo, so ga zasramovali in zmajevali s svojimi glavami
40 “Wewe! Si ulijidai kulivunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu? Sasa jiokoe mwenyewe. Kama wewe ni Mwana wa Mungu, basi shuka msalabani!”
ter govorili: »Ti, ki podiraš tempelj in ga zgradiš v treh dneh, reši samega sebe. Če si Božji Sin, pridi s križa dol.«
41 Hali kadhalika na makuhani wakuu pamoja na walimu wa Sheria na wazee walimdhihaki wakisema,
Podobno so ga zasmehovali tudi visoki duhovniki s pisarji in starešinami ter govorili:
42 “Aliwaokoa wengine, lakini kujiokoa mwenyewe hawezi! Eti yeye ni mfalme wa Wayahudi! Basi, sasa na ashuke msalabani, nasi tutamwamini.
»Rešil je druge; samega sebe ne more rešiti. Če je on Izraelov Kralj, naj sedaj pride dol s križa in mu bomo verjeli.
43 Alimtumainia Mungu na kusema eti yeye ni Mwana wa Mungu; basi, Mungu na amwokoe kama anamtaka.”
Zaupal je v Boga; naj ga sedaj osvobodi, če ga hoče imeti, kajti rekel je: ›Jaz sem Božji Sin.‹«
44 Hali kadhalika na wale waliosulubiwa pamoja naye wakamtukana.
Prav tako sta ga sramotila tudi tatova, ki sta bila križana z njim.
45 Tangu saa sita mchana mpaka saa tisa, nchi yote ikawa katika giza.
Od šeste ure je bila torej tema po vsej deželi do devete ure.
46 Mnamo saa tisa Yesu akalia kwa sauti kubwa, “Eli, Eli, lema sabakthani?” Maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”
Okoli devete ure pa je Jezus z močnim glasom zaklical, rekoč: »Elí, Elí, láma sabahtáni?« kar se reče: »Moj Bog, moj Bog, zakaj si me zapustil?«
47 Lakini wale waliosimama pale waliposikia hivyo wakasema, “Anamwita Eliya.”
Ko so nekateri izmed teh, ki so tam stali, to slišali, so rekli: »Ta človek kliče Elija.«
48 Mmoja wao akakimbia, akachukua sifongo, akaichovya katika siki, akaiweka juu ya mwanzi, akampa anywe.
In eden izmed njih je nemudoma stekel in vzel gobo ter jo napojil s kisom in jo nataknil na trst ter mu dal piti.
49 Wengine wakasema, “Acha tuone kama Eliya anakuja kumwokoa.”
Ostali so rekli: »Pústi, naj vidimo, če bo prišel Elija, da ga reši.«
50 Basi, Yesu akalia tena kwa sauti kubwa, akakata roho.
Ko je Jezus z močnim glasom ponovno zavpil, je odposlal duha.
51 Hapo pazia la Hekalu likapasuka vipande viwili, toka juu mpaka chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka;
In glej, tempeljsko zagrinjalo se je raztrgalo na dvoje od vrha do tal; in zemlja se je stresla in skale so se razklale;
52 makaburi yakafunguka na watu wengi wa Mungu waliokufa wakafufuliwa;
in grobovi so se odprli; in mnogo teles svetih, ki so spali, je vstalo
53 nao, baada ya kufufuka kwake, wakatoka makaburini, wakaingia katika Mji Mtakatifu, wakaonekana na watu wengi.
in po njegovem vstajenju so prišli iz grobov in odšli v sveto mesto in se mnogim prikazali.
54 Basi, jemadari na wale waliokuwa wakimlinda Yesu walipoona tetemeko la ardhi na yale mambo yaliyotukia, wakaogopa sana, wakasema, “Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu.”
Torej, ko so stotnik in ti, ki so bili z njim, ki so stražili Jezusa, videli potres in te stvari, ki so se zgodile, so se silno bali, rekoč: »Resnično, ta je bil Božji Sin.«
55 Mahali hapo walikuwapo wanawake wengi wakitazama kwa mbali. Hao ndio wale waliomfuata Yesu kutoka Galilaya wakimtumikia.
Tam je bilo mnogo žensk, ki so zrle od daleč, ki so Jezusu sledile iz Galileje ter mu stregle,
56 Miongoni mwao walikuwa Maria Magdalene, Maria mama yao Yakobo na Yosefu, pamoja na mama yao wana wa Zebedayo.
med katerimi je bila Marija Magdalena in Marija, Jakobova in Jožefova mati ter mati Zebedejevih otrok.
57 Ilipokuwa jioni, akaja mtu mmoja tajiri mwenyeji wa Armathaya, jina lake Yosefu. Yeye pia alikuwa mwanafunzi wa Yesu.
Ko je prišel večer, je tja prišel bogataš iz Arimateje, imenovan Jožef, ki je bil tudi sam Jezusov učenec.
58 Akamwendea Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu. Basi, Pilato akaamuru apewe.
Odšel je k Pilatu in prosil za Jezusovo telo. Tedaj je Pilat ukazal, naj bo telo izročeno.
59 Yosefu akauchukua ule mwili akauzungushia sanda safi ya kitani,
Ko je Jožef vzel telo, ga je ovil v čisto laneno oblačilo
60 akauweka ndani ya kaburi lake jipya alilokuwa amelichonga katika mwamba. Kisha akavingirisha jiwe kubwa mbele ya mlango wa kaburi, akaenda zake.
in ga položil v svojo novo grobnico, ki jo je izklesal v skalo, in k vratom mavzoleja zavalil velik kamen ter odšel.
61 Maria Magdalene na yule Maria mwingine walikuwa wameketi kulielekea kaburi.
In tam sta bili Marija Magdalena in druga Marija, ki sta sedeli nasproti mavzoleju.
62 Kesho yake, yaani siku iliyofuata ile ya Maandalio, makuhani wakuu na Mafarisayo walimwendea Pilato,
Torej naslednji dan, ki je sledil dnevu priprave, so visoki duhovniki in farizeji skupaj prišli k Pilatu,
63 Wakasema, “Mheshimiwa, tunakumbuka kwamba yule mdanganyifu alisema kabla ya kufa ati, Baada ya siku tatu nitafufuka.
rekoč: »Gospod, spominjamo se, da je ta slepar, medtem ko je bil še živ, rekel: ›Po treh dneh bom ponovno vstal.‹
64 Kwa hiyo amuru kaburi lilindwe mpaka siku ya tatu ili wanafunzi wake wasije wakamwiba na kuwaambia watu kwamba amefufuka. Uongo huu wa mwisho utakuwa mbaya kuliko ule wa awali.”
Ukaži torej, da bo mavzolej zavarovan do tretjega dne, da ne pridejo ponoči njegovi učenci ter ga skrivaj odnesejo in rečejo ljudem: ›Obujen je od mrtvih; ‹ tako bo zadnja prevara hujša kakor prva.«
65 Pilato akawaambia, “Haya, mnao walinzi; nendeni mkalinde kadiri mjuavyo.”
Pilat jim je rekel: »Imate stražo; pojdite svojo pot, naredite to tako varno kakor lahko.«
66 Basi, wakaenda, wakalilinda kaburi, wakatia mhuri juu ya lile jiwe na kuacha hapo askari walinzi.
Tako so šli in zapečatili kamen ter postavili stražo in mavzolej naredili varen.

< Mathayo 27 >