< Luka 4 >

1 Yesu alitoka katika mto Yordani akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akaongozwa na Roho mpaka jangwani.
And Jesus, being full of the Holy Spirit, returned from the Jordan. And the Spirit led him into the wilderness,
2 Huko alijaribiwa na Ibilisi kwa muda wa siku arubaini. Wakati huo wote hakula chochote, na baada ya siku hizo akasikia njaa.
forty days, to be tempted by the Calumniator. And during those days, he ate nothing; and when he had completed them, he was at last hungry.
3 Ndipo Ibilisi akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, amuru jiwe hili liwe mkate.”
And the Calumniator said to him: If thou art the Son of God, command this stone to become bread.
4 Yesu akamjibu, “Imeandikwa: Mtu haishi kwa mkate tu.”
Jesus replied, and said to him: It is written, Not by bread only, doth man live; but by every thing of God.
5 Kisha Ibilisi akamchukua hadi mahali pa juu, akamwonyesha kwa mara moja falme zote za ulimwengu. Huyo Shetani akamwambia,
And Satan conducted him to a high mountain and showed him all the kingdoms of the land, in a little time.
6 “Nitakupa uwezo juu ya falme zote hizi na fahari zake, kwa maana nimepewa hivi vyote; nikitaka kumpa mtu ninaweza.
And the Calumniator said to him: To thee will I give all this dominion, and the glory of it, which is committed to me, and to whom I please, I give it:
7 Hivi vyote vitakuwa mali yako wewe, kama ukiniabudu.”
if therefore thou wilt worship before me, the whole shall be thine.
8 Yesu akamjibu, “Imeandikwa: Utamwabudu Bwana Mungu wako, na utamtumikia yeye peke yake.”
But Jesus replied, and said to him: It is written Thou shalt worship the Lord thy God, and him only shalt thou serve.
9 Ibilisi akamchukua mpaka Yerusalemu, kwenye mnara wa Hekalu, akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu,
And he brought him to Jerusalem, and set him on a pinnacle of the temple, and said to him: If thou art the Son of God, cast thyself down hence:
10 kwa maana imeandikwa: Atawaamuru malaika wake wakulinde,
for it is written, He will give his angels charge over thee, to keep thee:
11 na tena, Watakuchukua mikononi mwao usije ukajikwaa mguu wako kwenye jiwe.”
and in their arms will they sustain thee, lest thou strike thy foot against a stone.
12 Lakini Yesu akamjibu, “Imeandikwa: Usimjaribu Bwana Mungu wako.”
And Jesus replied and said to him: It is said, Thou shalt not tempt the Lord thy God.
13 Ibilisi alipokwishamjaribu kwa kila njia, akamwacha kwa muda.
And when the Calumniator had finished all his temptations, he departed from him for a time.
14 Yesu alirudi Galilaya akiwa amejaa nguvu za Roho Mtakatifu, na habari zake zikaenea katika sehemu zote za jirani.
And Jesus returned, in the power of the Spirit, to Galilee; and fame concerning him spread in all the region around them.
15 Naye akawa anawafundisha watu katika masunagogi yao, akasifiwa na wote.
And he taught in their synagogues, and was lauded by every one.
16 Basi, Yesu alikwenda Nazareti, mahali alipolelewa, na siku ya Sabato, aliingia katika sunagogi, kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama ili asome Maandiko Matakatifu kwa sauti.
And he came to Nazareth, where he had been brought up: and he went, as he was accustomed, into the synagogue on the sabbath day, and rose up to read.
17 Akapokea kitabu cha nabii Isaya, akakifungua na akakuta mahali palipoandikwa:
And there was delivered to him the book of Isaiah the prophet. And Jesus opened the book, and found the place where it is written:
18 “Roho wa Bwana yu juu yangu, kwani amenipaka mafuta niwahubirie maskini Habari Njema. Amenituma niwatangazie mateka watapata uhuru, vipofu watapata kuona tena; amenituma niwakomboe wanaoonewa,
The Spirit of the Lord is upon me; and therefore he hath anointed me to proclaim tidings to the poor; and hath sent me to heal the contrite in heart, and to proclaim release to the captives, and sight to the blind; and to send away the contrite with forgiveness of their sins;
19 na kutangaza mwaka wa neema ya Bwana.”
and to proclaim the acceptable year of the Lord.
20 Baada ya kusoma, akafunga kile kitabu, akampa mtumishi, kisha akaketi; watu wote wakamkodolea macho.
And he rolled up the book, and gave it to the servitor, and went and sat down. And the eyes of all in the synagogue were gazing upon him.
21 Naye akaanza kuwaambia, “Andiko hili mlilosikia likisomwa, limetimia leo.”
And he began to say to them: This day, is this scripture which ye have heard, fulfilled.
22 Wote wakavutiwa sana naye, wakastaajabia maneno mazuri aliyosema. Wakanena, “Je, huyu si mwana wa Yosefu?”
And all bare him witness, and admired the gracious words which proceeded from his mouth; and they said: Is not this the son of Joseph?
23 Naye akawaambia, “Bila shaka mtaniambia msemo huu: Mganga jiponye mwenyewe, na pia mtasema: Yote tuliyosikia umeyafanya kule Kafarnaumu, yafanye hapa pia katika kijiji chako.”
Jesus said to them: Perhaps, ye will speak to me this proverb, Physician, heal thyself: and whatever we have heard of thy doing in Capernaum, do thou here also in thy city.
24 Akaendelea kusema, “Hakika nawaambieni, nabii hatambuliwi katika kijiji chake.
And he said to them: Verily I say to you, There is no prophet who is acceptable in his own city.
25 Lakini, sikilizeni! Kweli kulikuwa na wajane wengi katika nchi ya Israeli nyakati za Eliya. Wakati huo mvua iliacha kunyesha kwa muda wa miaka mitatu na nusu; kukawa na njaa kubwa katika nchi yote.
And I tell you the truth, that there were many widows in the house of Israel, in the days of Elijah the prophet, when the heavens were closed up three years and six months, and there was a great famine in all the land:
26 Hata hivyo, Eliya hakutumwa kwa mjane yeyote ila kwa mwanamke mjane wa Sarepta, Sidoni.
but to no one of them was Elijah sent, except to Sarepta of Sidon, unto a widow woman.
27 Tena, katika nchi ya Israeli nyakati za Elisha kulikuwa na wenye ukoma wengi. Hata hivyo, hakuna yeyote aliyetakaswa ila tu Naamani, mwenyeji wa Siria.”
And there were many leprous in the house of Israel, in the days of Elisha the prophet; but none of them was cleansed, except Naaman the Syrian.
28 Wote waliokuwa katika lile sunagogi waliposikia hayo walikasirika sana.
And when they heard these things, those in the synagogue were all filled with wrath.
29 Wakasimama, wakamtoa nje ya mji wao uliokuwa umejengwa juu ya kilima, wakampeleka mpaka kwenye ukingo wa kilima hicho ili wamtupe chini.
And they rose up, and thrust him out of the city, and brought him to the top of the hill on which the city was built, that they might cast him down from the rock.
30 Lakini Yesu akapita katikati yao, akaenda zake.
But he passed through the midst of them, and went away.
31 Kisha Yesu akashuka mpaka Kafarnaumu katika mkoa wa Galilaya, akawa anawafundisha watu siku ya Sabato.
And he went down to Capernaum, a city of Galilee; and taught them on sabbath days.
32 Wakastaajabia uwezo aliokuwa nao katika kufundisha.
And they were astonished at his teaching, for his word was authoritative.
33 Na katika lile sunagogi kulikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na roho ya pepo mchafu; akapiga ukelele wa kuziba masikio:
And there was in the synagogue a man, in whom was an unclean demon: and he cried out, with a loud voice,
34 “We! Yesu wa Nazareti! Kwa nini unatuingilia? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakufahamu wewe ni nani. Wewe ni mjumbe Mtakatifu wa Mungu!”
and said: Let me alone: What have I to do with thee, Jesus, thou Nazarean? Hast thou come to destroy us? I know thee, who thou art, the Holy One of God.
35 Lakini Yesu akamkemea huyo pepo akisema: “Nyamaza! Mtoke mtu huyu!” Basi, huyo pepo baada ya kumwangusha yule mtu chini, akamtoka bila kumdhuru hata kidogo.
And Jesus rebuked him, and said: Shut thy mouth; and come out of him. And the demon threw him down in the midst, and came out of him, having not harmed him at all.
36 Watu wote wakashangaa, wakawa wanaambiana, “Hili ni jambo la ajabu, maana kwa uwezo na nguvu anawaamuru pepo wachafu watoke, nao wanatoka!”
And wonder seized every one, and they talked together, and said: What a word is this! For, with authority and efficiency, he commandeth the unclean spirits, and they come out
37 Habari zake zikaenea mahali pote katika mkoa ule.
And his fame went out into all the surrounding region.
38 Yesu alitoka katika lile sunagogi, akaenda nyumbani kwa Simoni. Mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa na homa kali; wakamwomba amponye.
And when Jesus went out of the synagogue, he entered the house of Simon. And the mother-in-law of Simon was afflicted with a severe fever: and they besought him in her behalf.
39 Yesu akaenda akasimama karibu naye, akaikemea ile homa, nayo ikamwacha. Mara yule mama akainuka, akawatumikia.
And he stood over her, and rebuked the fever; and it left her. And immediately she arose and ministered to them.
40 Jua lilipokuwa linatua, wote waliokuwa na wagonjwa wao mbalimbali waliwaleta kwake; naye akaweka mikono yake juu ya kila mmoja wao, akawaponya wote.
And when the sun was set, all those that had sick persons, afflicted with divers diseases, brought them to him; and he laid his hand on every one of them, and healed them.
41 Pepo waliwatoka watu wengi, wakapiga kelele wakisema: “Wewe u Mwana wa Mungu!” Lakini Yesu akawakemea, wala hakuwaruhusu kusema, maana walimfahamu kwamba yeye ndiye Kristo.
And demons went out of many, crying out and saying: Thou art the Messiah, the Son of God. And he rebuked them, and suffered them not to say, that they knew him to be Messiah.
42 Kesho yake asubuhi Yesu aliondoka akaenda mahali pa faragha. Watu wakawa wanamtafuta, na walipofika mahali alipokuwa, wakajaribu kumzuia ili asiondoke kwao.
And at the dawn of day, he went out and retired to a desert place. And the multitudes sought him, and went out to him, and held him fast, that he might not retire from them.
43 Lakini yeye akawaambia, “Ninapaswa kuhubiri Habari Njema za Ufalme wa Mungu katika miji mingine pia, maana nilitumwa kwa ajili hiyo.”
And Jesus said to them: It behooveth me to announce the kingdom of God to other cities also; for therefore was I sent.
44 Akawa anahubiri katika masunagogi ya Yudea.
And he preached in the synagogues of Galilee.

< Luka 4 >