< Luka 23 >

1 Kisha, wote kwa jumla, wakasimama, wakampeleka Yesu mbele ya Pilato.
And the whole multitude of them arose and ledde him vnto Pylate.
2 Wakaanza kumshtaki wakisema: “Tulimkuta mtu huyu akiwapotosha watu wetu, akipinga kulipa kodi kwa Kaisari na kujiita ati yeye ni Kristo, Mfalme.”
And they beganne to accuse him sayinge: We have founde this felowe pervertynge the people and forbiddynge to paye tribute to Cesar: sayinge that he is Christ a kynge.
3 Pilato akamwuliza Yesu, “Wewe ni Mfalme wa Wayahudi?” Yesu akamjibu, “Wewe umesema.”
And Pylate apposed him sayinge: arte thou the kynge of the iewes? He answered him and sayde: thou sayest it.
4 Pilato akawaambia makuhani wakuu na umati wa watu, “Sioni kosa lolote katika mtu huyu.”
Then sayde Pylate to the hye prestes and to the people: I fynde noo faute in this man.
5 Lakini wao wakasisitiza wakisema: “Anawachochea watu kwa mafundisho yake katika nchi yote ya Yudea; alianza Galilaya, na sasa yuko hapa.”
And they were the moore fearce sayinge. He moveth the people teachynge thorowout all Iewry and beganne at Galile even to this place.
6 Pilato aliposikia hayo, akauliza, “Je, mtu huyu ni mwenyeji wa Galilaya?”
When Pilate hearde mencion of Galile he axed whether the ma were of Galile.
7 Alipojua kwamba Yesu alikuwa chini ya utawala wa Herode, akampeleka kwa Herode, ambaye wakati huo alikuwa Yerusalemu.
And assone as he knewe that he was of Herodes iurisdiccion he sent him to Herode which was also at Ierusalem in those dayes.
8 Herode alifurahi sana alipomwona Yesu. Alikuwa amekwisha sikia habari zake, na hivyo alikuwa anatazamia kwa muda mrefu kumwona kwa macho yake mwenyewe. Zaidi ya hayo, alikuwa anatumaini kumwona Yesu akitenda mwujiza.
And when Herode sawe Iesus he was excedinglie gladde. For he was desyrous to se him of a longe season because he had hearde many thinges of him and trusted to have sene some myracle done by him.
9 Basi, akamwuliza maswali mengi kwa muda mrefu, lakini Yesu hakumjibu neno.
Then questeoned he with him of many thinges. But he answered him not one worde.
10 Makuhani wakuu na walimu wa Sheria wakajitokeza mbele, wakatoa mashtaka yao kwa nguvu sana.
The hye prestes and scribes stode forthe and accused him straytly.
11 Basi, herode pamoja na maaskari wake, wakamwaibisha Yesu na kumfanyia mzaha; kisha wakamvika vazi la kifalme, wakamrudisha kwa Pilato.
And Herod wt his men of warre despysed him and mocked him and arayed him in whyte and sent him agayne to Pylate.
12 Herode na Pilato, ambao hapo awali walikuwa maadui, tangu siku hiyo wakawa marafiki.
And the same daye Pylate and Herod were made frendes togeder. For before they were at variaunce.
13 Basi, Pilato akaitisha mkutano wa makuhani wakuu, viongozi na watu,
And Pylate called to geder the hye prestes and the rulers and the people
14 akawaambia, “Mmemleta mtu huyu kwangu mkisema kwamba alikuwa anawapotosha watu. Sasa sikilizeni! Baada ya kuchunguza jambo hilo mbele yenu, sikumpata na kosa lolote kuhusu mashtaka yenu juu yake.
and sayde vnto them: Ye have brought this man vnto me as one that perverted the people. And beholde I have examined him before you and have founde no faute in this man of those thinges where of ye accuse him.
15 Wala si mimi tu, bali hata Herode hakuona kosa lolote, kwa maana amemrudisha kwangu. Ni dhahiri kwamba mtu huyu hakufanya chochote kinachostahili adhabu ya kifo.
No nor yet Herode. For I sent you to him: and lo no thinge worthy of deeth is done to him.
16 Hivyo, nitaamuru apigwe viboko, halafu nitamwachilia.”
I will therfore chasten him and let him lowsse.
17 Kila sikukuu ya Pasaka, ilimlazimu Pilato kuwafungulia mfungwa mmoja.
For of necessite he must have let one lowse vnto them at that feast.
18 Lakini wote wakapiga kelele pamoja: “Mwondoe huyo, utufungulie Baraba!”
And all the people cryed at once sayinge: awaye with him and delyvre to vs Barrabas:
19 (Baraba alikuwa ametiwa ndani kwa kusababisha uasi katika mji na pia kwa sababu ya kuua.)
which for insurrccion made in the cite and morther was cast into preson.
20 Pilato alitaka kumwachilia Yesu, hivyo akasema nao tena;
Pylate spake agayne to them willynge to let Iesus lowse.
21 lakini wao wakapiga kelele: “Msulubishe, msulubishe!”
And they cryed sayinge: Crucify him Crucify him
22 Pilato akawaambia mara ya tatu, “Amefanya kosa gani? Sioni kosa lolote kwake linalomstahili auawe; kwa hiyo nitampiga viboko, halafu nimwachilie.”
He sayde vnto them the thyrde tyme. What evyll hath he done? I fynde no cause of deeth in him. I will therfore chasten him and let him lowse.
23 Lakini wao wakazidi kupiga kelele kwa nguvu sana, kwamba Yesu ni lazima asulubiwe. Mwishowe, sauti zao zikashinda.
And they cryed with loude voyce and required that he myght be crucifyed. And the voyce of them and of the hye Prestes prevayled.
24 Basi, Pilato akaamua kwamba matakwa yao yatimizwe.
And Pylate gave sentence that it shuld be as they required
25 Akamfungua kutoka gerezani yule waliyemtaka, ambaye alikuwa ametiwa gerezani kwa sababu ya uasi na kuua; akamtoa Yesu kwao, wamfanyie walivyotaka.
and let lowse vnto them him that for insurreccion and morther was cast into preson whom they desyred: and delyvered Iesus to do with him what they wolde.
26 Walipokuwa wakimpeleka, walikutana na mtu mmoja, aitwaye Simoni wa Kurene, aliyekuwa anatoka shambani. Basi, walimkamata, wakamtwika ule msalaba auchukue nyuma ya Yesu.
And as they ledde him awaye they caught one Symon of Syrene commynge out of the felde: and on him layde they the crosse to beare it after Iesus.
27 Watu, umati kwa umati, walimfuata; miongoni mwao wakiwemo wanawake waliokuwa wanaomboleza na kumlilia.
And ther folowed him a greate company of people and of wemen which weme bewayled and lamented him.
28 Yesu akawageukia, akasema, “Enyi kina mama wa Yerusalemu! Msinililie mimi, ila lieni kwa ajili yenu wenyewe na kwa ajili ya watoto wenu.
But Iesus turned backe vnto them and sayde: Doughters of Ierusalem wepe not for me: but wepe for youre selves and for youre chyldren.
29 Maana, hakika siku zitakuja ambapo watasema: Heri yao wale walio tasa, ambao hawakupata kuzaa wala kunyonyesha watoto!
For beholde the dayes will come when men shall saye: happy are the baren and the wombes that never bare and the pappes which never gave sucke.
30 Wakati huo, ndipo watu wataanza kuiambia milima: Tuangukieni! na vilima, Tufunikeni!
Then shall they beginne to saye to the mountaynes fall on vs: and to the hilles cover vs.
31 Kwa maana, kama watu wanautendea mti mbichi namna hiyo, itakuwaje kwa mti mkavu?”
For yf they do this to a grene tree what shalbe done to the drye?
32 Waliwachukua pia watu wengine wawili, wahalifu, wauawe pamoja naye.
And ther were two evyll doers ledde with him to be slayne.
33 Walipofika mahali paitwapo, “Fuvu la Kichwa,” ndipo wakamsulubisha Yesu pamoja na wale wahalifu wawili, mmoja upande wake wa kulia na mwingine upande wake wa kushoto.
And when they were come to the place which is called Calvary there they crucified him and the evyll doers one on ryght honde and the other on the lefte.
34 Yesu akasema, “Baba, uwasamehe kwa maana hawajui wanalofanya.” Kisha wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura.
Then sayde Iesus: father forgeve them for they woot not what they do. And they parted his rayment and cast loottes.
35 Watu wakawa wamesimama pale wakitazama. Nao viongozi wakamdhihaki wakisema: “Amewaokoa wengine; sasa na ajiokoe mwenyewe, kama yeye ndiye Kristo, mteule wa Mungu!”
And the people stode and behelde. And the rulers mocked him with thee saying: he holpe other men let him helpe him selfe yf he be Christ the chosen of god.
36 Askari nao walimdhihaki pia; walimwendea wakampa siki
The soudiers also mocked him and came and gave him veneger
37 wakisema: “Kama kweli wewe ni Mfalme wa Wayahudi, jiokoe mwenyewe.”
and sayde: yf thou be that kynge of ye Iewes save thy silfe.
38 Vilevile maandishi haya yalikuwa yameandikwa na kuwekwa juu yake: “Huyu ndiye Mfalme wa Wayahudi.”
And his superscripcio was writte over him in greke in latine and Ebreu: This is the kynge of the Iewes.
39 Mmoja wa wale wahalifu waliotundikwa msalabani, alimtukana akisema: “Je, si kweli kwamba wewe ndiwe Kristo? Basi, jiokoe mwenyewe, utuokoe na sisi pia.”
And one of the evyll doers which hanged rayled on him sayinge: If thou be Christ save thy selfe and vs.
40 Lakini yule mhalifu mwingine akamkemea mwenzake akisema: “Wewe humwogopi Mungu hata kidogo? Wewe umepata adhabu hiyohiyo.
The other answered and rebuked him sayinge. Net herfearest thou god because thou arte in the same damnacion?
41 Wewe na mimi tunastahili, maana haya ni malipo ya yale tuliyotenda. Lakini mtu huyu hakufanya chochote kibaya.”
We are ryghteously punesshed for we receave accordynge to oure dedes: But this man hath done nothinge amysse.
42 Kisha akasema, “Ee Yesu! Unikumbuke wakati utakapoingia katika ufalme wako.”
And he sayde vnto Iesus: Lorde remember me when thou comest into thy kyngdome.
43 Yesu akamwambia, “Nakwambia kwa hakika, leo utakuwa pamoja nami peponi.”
And Iesus sayde vnto him: Verely I saye vnto the to daye shalt thou be with me in Paradyse.
44 Ilikuwa yapata saa sita mchana; jua likaacha kuangaza, giza likafunika nchi yote mpaka saa tisa,
And it was about the sixt houre. And ther came a darcknes over all the londe vntyll ye nynth houre
45 na pazia lililokuwa limetundikwa Hekaluni likapasuka vipande viwili.
and the sonne was darckened. And the vayle of the temple dyd rent even thorow the myddes.
46 Yesu akalia kwa sauti kubwa: “Baba, naiweka roho yangu mikononi mwako.” Alipokwisha sema hayo, akakata roho.
And Iesus cryed with a greate voyce and sayd: Father into thy hondes I comende my sprete. And when he thus had sayd he gave vp the goost.
47 Hapo, yule jemadari alipoona yaliyotukia akamsifu Mungu akisema: “Hakika huyu alikuwa mtu mwema.”
When ye Centurion sawe what had happened he glorified God sayinge: Of a surtie this man was perfecte.
48 Watu wale wote waliokuwa wamekusanyika hapo kwa ajili ya tukio hilo, walipoona hayo yaliyotukia, walirudi makwao wakijipiga vifua kwa huzuni.
And all the people that came to geder to that sight beholdynge the thinges which were done: smoote their bestes and returned home.
49 Marafiki zake wote pamoja na wale wanawake walioandamana naye kutoka Galilaya, walisimama kwa mbali kutazama tukio hilo.
And all his acquayntaunce and the wemen that folowed him from Galile stode a farre of beholdynge these thinges.
50 Kulikuwa na mtu mmoja jina lake Yosefu, mwenyeji wa kijiji kimoja cha Wayahudi kiitwacho Armathaya. Alikuwa mtu mwema anayeheshimika;
And beholde ther was a man named Ioseph a councelloure and was a good man and a iuste
51 Alikuwa akitazamia kuja kwa Ufalme wa Mungu. Ingawa alikuwa mmoja wa Baraza kuu la Wayahudi, hakuwa amekubaliana nao katika kitendo chao.
and dyd not consent to the counsell and dede of them which was of Aramathia a cite of the Iewes: which same also wayted for ye kyngdome of God:
52 Basi, yeye alikwenda kwa Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu.
he went vnto Pilate and begged the boddy of Iesus
53 Kisha, akaushusha mwili huo kutoka msalabani, akauzungushia sanda ya kitani, akauweka katika kaburi lililokuwa limechongwa kwenye mwamba, ambalo halikuwa limetumika.
and toke it doune and wrapped it in a lynnen clooth and layed it in an hewen toumbe wherin was never man before layed.
54 Siku hiyo ilikuwa Ijumaa, na maandalio ya siku ya Sabato yalikuwa yanaanza.
And that daye was ye Saboth even and the Saboth drue on.
55 Wale wanawake walioandamana na Yesu kutoka Galilaya walimfuata Yosefu, wakaliona lile kaburi na jinsi mwili wake Yesu ulivyowekwa
The wemen that folowed after which came with him from Galile behelde the sepulcre and how his body was layed.
56 Halafu, walirudi nyumbani, wakatayarisha manukato na marashi kuyapaka mwili wa Yesu. Siku ya Sabato walipumzika kama ilivyoamriwa na sheria.
And they returned and prepared odoures and oyntmetes: but rested the Saboth daye accordynge to the commaundement.

< Luka 23 >