< Luka 23 >

1 Kisha, wote kwa jumla, wakasimama, wakampeleka Yesu mbele ya Pilato.
Then they all rose in a body and led Jesus before Pilate.
2 Wakaanza kumshtaki wakisema: “Tulimkuta mtu huyu akiwapotosha watu wetu, akipinga kulipa kodi kwa Kaisari na kujiita ati yeye ni Kristo, Mfalme.”
And they began to accuse him, ‘This is a man whom we found misleading our people, preventing them from paying taxes to the Emperor, and giving out that he himself is “Christ, a king.”’
3 Pilato akamwuliza Yesu, “Wewe ni Mfalme wa Wayahudi?” Yesu akamjibu, “Wewe umesema.”
‘Are you the king of the Jews?’ Pilate asked him. ‘It is true,’ replied Jesus.
4 Pilato akawaambia makuhani wakuu na umati wa watu, “Sioni kosa lolote katika mtu huyu.”
But Pilate, turning to the chief priests and the people, said, ‘I do not see anything to find fault with in this man.’
5 Lakini wao wakasisitiza wakisema: “Anawachochea watu kwa mafundisho yake katika nchi yote ya Yudea; alianza Galilaya, na sasa yuko hapa.”
But they insisted, ‘He is stirring up the people by his teaching all through Judea; he began with Galilee and has now come here.’
6 Pilato aliposikia hayo, akauliza, “Je, mtu huyu ni mwenyeji wa Galilaya?”
Hearing this, Pilate asked if the man was a Galilean;
7 Alipojua kwamba Yesu alikuwa chini ya utawala wa Herode, akampeleka kwa Herode, ambaye wakati huo alikuwa Yerusalemu.
and, having satisfied himself that Jesus came under Herod’s jurisdiction, he sent him to Herod, who also was at Jerusalem at the time.
8 Herode alifurahi sana alipomwona Yesu. Alikuwa amekwisha sikia habari zake, na hivyo alikuwa anatazamia kwa muda mrefu kumwona kwa macho yake mwenyewe. Zaidi ya hayo, alikuwa anatumaini kumwona Yesu akitenda mwujiza.
When Herod saw Jesus, he was exceedingly pleased, for he had been wanting to see him for a long time, having heard a great deal about him; and he was hoping to see some sign given by him.
9 Basi, akamwuliza maswali mengi kwa muda mrefu, lakini Yesu hakumjibu neno.
So he questioned him at some length, but Jesus made no reply.
10 Makuhani wakuu na walimu wa Sheria wakajitokeza mbele, wakatoa mashtaka yao kwa nguvu sana.
Meanwhile the chief priests and the teachers of the Law stood by and vehemently accused him.
11 Basi, herode pamoja na maaskari wake, wakamwaibisha Yesu na kumfanyia mzaha; kisha wakamvika vazi la kifalme, wakamrudisha kwa Pilato.
And Herod, with his soldiers, treated Jesus with scorn; he mocked him by throwing a gorgeous robe round him, and then sent him back to Pilate.
12 Herode na Pilato, ambao hapo awali walikuwa maadui, tangu siku hiyo wakawa marafiki.
And Herod and Pilate became friends that very day, for before that there had been ill-will between them.
13 Basi, Pilato akaitisha mkutano wa makuhani wakuu, viongozi na watu,
So Pilate summoned the chief priests, and the leading men, and the people,
14 akawaambia, “Mmemleta mtu huyu kwangu mkisema kwamba alikuwa anawapotosha watu. Sasa sikilizeni! Baada ya kuchunguza jambo hilo mbele yenu, sikumpata na kosa lolote kuhusu mashtaka yenu juu yake.
and said to them, ‘You brought this man before me charged with misleading the people; and yet, for my part, though I examined him before you, I did not find this man to blame for any of the things of which you accuse him;
15 Wala si mimi tu, bali hata Herode hakuona kosa lolote, kwa maana amemrudisha kwangu. Ni dhahiri kwamba mtu huyu hakufanya chochote kinachostahili adhabu ya kifo.
nor did Herod either; for he has sent him back to us. And, as a fact, he has not done anything deserving death;
16 Hivyo, nitaamuru apigwe viboko, halafu nitamwachilia.”
so I will have him scourged, and then release him.’
17 Kila sikukuu ya Pasaka, ilimlazimu Pilato kuwafungulia mfungwa mmoja.
18 Lakini wote wakapiga kelele pamoja: “Mwondoe huyo, utufungulie Baraba!”
But they began to shout as one man, ‘Kill this fellow, but release Barabbas for us.’
19 (Baraba alikuwa ametiwa ndani kwa kusababisha uasi katika mji na pia kwa sababu ya kuua.)
(Barabbas was a man who had been put in prison for a riot that had broken out in the city and for murder.)
20 Pilato alitaka kumwachilia Yesu, hivyo akasema nao tena;
Pilate, however, wanting to release Jesus, called to them again;
21 lakini wao wakapiga kelele: “Msulubishe, msulubishe!”
but they kept calling out, ‘Crucify, crucify him!’
22 Pilato akawaambia mara ya tatu, “Amefanya kosa gani? Sioni kosa lolote kwake linalomstahili auawe; kwa hiyo nitampiga viboko, halafu nimwachilie.”
‘Why, what harm has this man done?’ Pilate said to them for the third time. ‘I have found nothing in him for which he could be condemned to death. So I will have him scourged, and then release him.’
23 Lakini wao wakazidi kupiga kelele kwa nguvu sana, kwamba Yesu ni lazima asulubiwe. Mwishowe, sauti zao zikashinda.
But they persisted in loudly demanding his crucifixion; and their clamour gained the day.
24 Basi, Pilato akaamua kwamba matakwa yao yatimizwe.
Pilate decided that their demand should be granted.
25 Akamfungua kutoka gerezani yule waliyemtaka, ambaye alikuwa ametiwa gerezani kwa sababu ya uasi na kuua; akamtoa Yesu kwao, wamfanyie walivyotaka.
He released the man who had been put in prison for riot and murder, as they demanded, and gave Jesus up to be dealt with as they pleased.
26 Walipokuwa wakimpeleka, walikutana na mtu mmoja, aitwaye Simoni wa Kurene, aliyekuwa anatoka shambani. Basi, walimkamata, wakamtwika ule msalaba auchukue nyuma ya Yesu.
And, as they were leading Jesus away, they laid hold of Simon from Cyrene, who was on his way in from the country, and they put the cross on his shoulders, for him to carry it behind Jesus.
27 Watu, umati kwa umati, walimfuata; miongoni mwao wakiwemo wanawake waliokuwa wanaomboleza na kumlilia.
There was a great crowd of people following him, many being women who were beating their breasts and wailing for him.
28 Yesu akawageukia, akasema, “Enyi kina mama wa Yerusalemu! Msinililie mimi, ila lieni kwa ajili yenu wenyewe na kwa ajili ya watoto wenu.
So Jesus turned and said to them, ‘Women of Jerusalem, do not weep for me, but weep for yourselves and for your children.
29 Maana, hakika siku zitakuja ambapo watasema: Heri yao wale walio tasa, ambao hawakupata kuzaa wala kunyonyesha watoto!
A time, I tell you, is coming, when it will be said – “Happy are the women who are barren, and those who have never borne children or nursed them!”
30 Wakati huo, ndipo watu wataanza kuiambia milima: Tuangukieni! na vilima, Tufunikeni!
At that time people will begin to say to the mountains “Fall on us,” and to the hills “Cover us.”
31 Kwa maana, kama watu wanautendea mti mbichi namna hiyo, itakuwaje kwa mti mkavu?”
If what you see is done while the tree is green, what will happen when it is dry?’
32 Waliwachukua pia watu wengine wawili, wahalifu, wauawe pamoja naye.
There were two others also, criminals, led out to be executed with Jesus.
33 Walipofika mahali paitwapo, “Fuvu la Kichwa,” ndipo wakamsulubisha Yesu pamoja na wale wahalifu wawili, mmoja upande wake wa kulia na mwingine upande wake wa kushoto.
When they had reached the place called “The Skull,” there they crucified Jesus and the criminals, one on the right, and one on the left.
34 Yesu akasema, “Baba, uwasamehe kwa maana hawajui wanalofanya.” Kisha wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura.
Then Jesus said, ‘Father, forgive them; they do not know what they are doing.’ His clothes they divided among them by casting lots.
35 Watu wakawa wamesimama pale wakitazama. Nao viongozi wakamdhihaki wakisema: “Amewaokoa wengine; sasa na ajiokoe mwenyewe, kama yeye ndiye Kristo, mteule wa Mungu!”
Meanwhile the people stood looking on. Even the leading men said with a sneer, ‘He saved others, let him save himself, if he is God’s Christ, his chosen one.’
36 Askari nao walimdhihaki pia; walimwendea wakampa siki
The soldiers, too, came up in mockery, bringing him common wine,
37 wakisema: “Kama kweli wewe ni Mfalme wa Wayahudi, jiokoe mwenyewe.”
and saying as they did so, ‘If you are the king of the Jews, save yourself.’
38 Vilevile maandishi haya yalikuwa yameandikwa na kuwekwa juu yake: “Huyu ndiye Mfalme wa Wayahudi.”
Above him were the words – “THIS IS THE KING OF THE JEWS.”
39 Mmoja wa wale wahalifu waliotundikwa msalabani, alimtukana akisema: “Je, si kweli kwamba wewe ndiwe Kristo? Basi, jiokoe mwenyewe, utuokoe na sisi pia.”
One of the criminals who were hanging beside Jesus railed at him. ‘Aren’t you the Christ? Save yourself and us,’ he said.
40 Lakini yule mhalifu mwingine akamkemea mwenzake akisema: “Wewe humwogopi Mungu hata kidogo? Wewe umepata adhabu hiyohiyo.
But the other rebuked him. ‘Haven’t you,’ he said, ‘any fear of God, now that you are under the same sentence?
41 Wewe na mimi tunastahili, maana haya ni malipo ya yale tuliyotenda. Lakini mtu huyu hakufanya chochote kibaya.”
And we justly so, for we are only reaping our deserts, but this man has not done anything wrong.
42 Kisha akasema, “Ee Yesu! Unikumbuke wakati utakapoingia katika ufalme wako.”
Jesus,’ he went on, ‘do not forget me when you have come to your kingdom.’
43 Yesu akamwambia, “Nakwambia kwa hakika, leo utakuwa pamoja nami peponi.”
And Jesus answered, ‘I tell you, this very day you will be with me in Paradise.’
44 Ilikuwa yapata saa sita mchana; jua likaacha kuangaza, giza likafunika nchi yote mpaka saa tisa,
It was nearly midday, when a darkness came over the whole country, lasting until three in the afternoon,
45 na pazia lililokuwa limetundikwa Hekaluni likapasuka vipande viwili.
the sun being eclipsed; and the Temple curtain was torn down the middle.
46 Yesu akalia kwa sauti kubwa: “Baba, naiweka roho yangu mikononi mwako.” Alipokwisha sema hayo, akakata roho.
Then Jesus, with a loud cry, said, ‘Father, into your hands I commit my spirit.’ And with these words he expired.
47 Hapo, yule jemadari alipoona yaliyotukia akamsifu Mungu akisema: “Hakika huyu alikuwa mtu mwema.”
The Roman centurion, on seeing what had happened, praised God, exclaiming, ‘This must have been a good man!’
48 Watu wale wote waliokuwa wamekusanyika hapo kwa ajili ya tukio hilo, walipoona hayo yaliyotukia, walirudi makwao wakijipiga vifua kwa huzuni.
All the people who had collected to see the sight watched what occurred, and then went home beating their breasts.
49 Marafiki zake wote pamoja na wale wanawake walioandamana naye kutoka Galilaya, walisimama kwa mbali kutazama tukio hilo.
All the friends of Jesus had been standing at a distance, with the women who accompanied him from Galilee, watching all this.
50 Kulikuwa na mtu mmoja jina lake Yosefu, mwenyeji wa kijiji kimoja cha Wayahudi kiitwacho Armathaya. Alikuwa mtu mwema anayeheshimika;
Now there was a man of the name of Joseph, who was a member of the Council, and who bore a good and upright character.
51 Alikuwa akitazamia kuja kwa Ufalme wa Mungu. Ingawa alikuwa mmoja wa Baraza kuu la Wayahudi, hakuwa amekubaliana nao katika kitendo chao.
(This man had not assented to the decision and action of the Council.) He belonged to Arimathea, a town in Judea, and lived in expectation of the kingdom of God.
52 Basi, yeye alikwenda kwa Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu.
He now went to see Pilate, and asked for the body of Jesus;
53 Kisha, akaushusha mwili huo kutoka msalabani, akauzungushia sanda ya kitani, akauweka katika kaburi lililokuwa limechongwa kwenye mwamba, ambalo halikuwa limetumika.
and, when he had taken it down, he wrapped it in a linen sheet, and laid him in a tomb cut out of stone, in which no one had yet been buried.
54 Siku hiyo ilikuwa Ijumaa, na maandalio ya siku ya Sabato yalikuwa yanaanza.
It was the Preparation day, and just before the Sabbath began.
55 Wale wanawake walioandamana na Yesu kutoka Galilaya walimfuata Yosefu, wakaliona lile kaburi na jinsi mwili wake Yesu ulivyowekwa
The women who had accompanied Jesus from Galilee followed, and saw the tomb and how the body of Jesus was laid,
56 Halafu, walirudi nyumbani, wakatayarisha manukato na marashi kuyapaka mwili wa Yesu. Siku ya Sabato walipumzika kama ilivyoamriwa na sheria.
and then went home, and prepared spices and perfumes. During the Sabbath they rested, as directed by the commandment.

< Luka 23 >