< Luka 22 >

1 Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu, iitwayo Pasaka, ilikuwa inakaribia.
Now the feast of unleavened bread, which is called the Passover, was approaching.
2 Makuhani wakuu na walimu wa Sheria wakawa wanatafuta njia ya kumwua Yesu, lakini waliwaogopa watu.
The chief priests and the scribes sought how they might put him to death, for they feared the people.
3 Basi, Shetani akamwingia Yuda aitwae Iskarioti, mmoja wa wale mitume kumi na wawili.
Satan entered into Judah, who was also called Iscariot, who was counted with the twelve.
4 Yuda akaenda akajadiliana na makuhani wakuu na walinzi wa Hekalu kuhusu atakavyomsaliti Yesu kwao.
He went away and talked with the chief priests and captains about how he might deliver him to them.
5 Nao wakafurahi na kupatana naye kumlipa fedha.
They were glad, and agreed to give him money.
6 Yuda akakubali, na akawa anatafuta nafasi nzuri ya kumkabidhi kwao bila umati wa watu kujua.
He consented and sought an opportunity to deliver him to them in the absence of the multitude.
7 Basi, siku ya Mikate Isiyotiwa chachu ikafika. Hiyo ndiyo siku ambayo mwana kondoo wa Pasaka huchinjwa.
The day of unleavened bread came, on which the Passover must be sacrificed.
8 Hivyo Yesu akawatuma Petro na Yohane, akawaambia, “Nendeni mkatuandalie karamu ili tupate kula Pasaka.”
Yeshua sent Peter and Yochanan, saying, “Go and prepare the Passover for us, that we may eat.”
9 Nao wakamwuliza, “Unataka tuiandae wapi?”
They said to him, “Where do you want us to prepare?”
10 Akawaambia, “Sikilizeni! Mtakapokuwa mnakwenda mjini, mtakutana na mwanamume anayebeba mtungi wa maji. Mfuateni mpaka ndani ya nyumba atakayoingia.
He said to them, “Behold, when you have entered into the city, a man carrying a pitcher of water will meet you. Follow him into the house which he enters.
11 Mwambieni mwenye nyumba: Mwalimu anakuuliza, kiko wapi kile chumba ambamo nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu?
Tell the master of the house, ‘The Rabbi says to you, “Where is the guest room, where I may eat the Passover with my disciples?”’
12 Naye atawaonyesheni chumba kikubwa ghorofani ambacho kimepambwa. Andalieni humo.”
He will show you a large, furnished upper room. Make preparations there.”
13 Basi, wakaenda, wakakuta kila kitu sawa kama Yesu alivyokuwa amewaambia; wakaandaa karamu ya Pasaka.
They went, found things as Yeshua had told them, and they prepared the Passover.
14 Saa ilipotimia, Yesu akakaa kula chakula pamoja na mitume wake.
When the hour had come, he sat down with the twelve emissaries.
15 Akawaambia, “Nimetamani sana kula Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu.
He said to them, “I have earnestly desired to eat this Passover with you before I suffer,
16 Maana nawaambieni, sitaila tena hadi hapo itakapokamilika katika Ufalme wa Mungu.”
for I tell you, I will no longer by any means eat of it until it is fulfilled in God’s Kingdom.”
17 Kisha akatwaa kikombe, akashukuru akasema, “Pokeeni, mgawanye ninyi kwa ninyi.
He received a cup, and when he had given thanks, he said, “Take this and share it amongst yourselves,
18 Kwa maana nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka Ufalme wa Mungu utakapokuja.”
for I tell you, I will not drink at all again from the fruit of the vine, until God’s Kingdom comes.”
19 Halafu akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa akisema, “Huu ni mwili wangu, unaotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa kunikumbuka.”
He took bread, and when he had given thanks, he broke and gave it to them, saying, “This is my body which is given for you. Do this in memory of me.”
20 Akafanya vivyo hivyo na kikombe, baada ya chakula, akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya linalothibitishwa kwa damu yangu inayomwagika kwa ajili yenu.
Likewise, he took the cup after supper, saying, “This cup is the new covenant in my blood, which is poured out for you.
21 “Lakini, tazameni! Yule atakayenisaliti yuko nami hapa mezani.
But behold, the hand of him who betrays me is with me on the table.
22 Kweli Mwana wa Mtu anakwenda kuuawa kama ilivyopangwa, lakini ole wake mtu anayemsaliti.”
The Son of Man indeed goes as it has been determined, but woe to that man through whom he is betrayed!”
23 Hapo wakaanza kuulizana wao kwa wao ni nani kati yao atakayefanya jambo hilo.
They began to question amongst themselves which of them it was who would do this thing.
24 Kulitokea ubishi kati ya hao mitume kuhusu nani miongoni mwao anayefikiriwa kuwa mkuu zaidi kuliko wengine.
A dispute also arose amongst them, which of them was considered to be greatest.
25 Yesu akawaambia, “Wafalme wa mataifa huwatawala watu wao kwa mabavu, nao huitwa wafadhili wa watu.
He said to them, “The kings of the nations lord it over them, and those who have authority over them are called ‘benefactors.’
26 Lakini isiwe hivyo kati yenu; bali, yule aliye mkuu kati yenu ni lazima awe mdogo wa wote, na aliye kiongozi lazima awe kama mtumishi.
But not so with you. Rather, the one who is greater amongst you, let him become as the younger, and one who is governing, as one who serves.
27 Kwa maana, ni nani aliye mkuu: yule anayeketi mezani kula chakula, ama yule anayetumikia? Bila shaka ni yule anayeketi mezani kula chakula! Hata hivyo, mimi niko hapa kati yenu kama mtumishi.
For who is greater, one who sits at the table, or one who serves? Isn’t it he who sits at the table? But I am amongst you as one who serves.
28 “Ninyi ndio mliobaki nami wakati wote wa majaribu yangu;
“But you are those who have continued with me in my trials.
29 na, kama vile Baba yangu alivyonikabidhi Ufalme, vivyo hivyo nami nitawakabidhi ninyi Ufalme.
I confer on you a kingdom, even as my Father conferred on me,
30 Mtakula na kunywa mezani pangu katika ufalme wangu, na mtaketi katika viti vya enzi kuyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
that you may eat and drink at my table in my Kingdom. You will sit on thrones, judging the twelve tribes of Israel.”
31 “Simoni, Simoni! Sikiliza! Shetani alitaka kuwapepeta ninyi kama mtu anavyopepeta ngano.
The Lord said, “Simon, Simon, behold, Satan asked to have all of you, that he might sift you as wheat,
32 Lakini mimi nimekuombea ili imani yako isipungue. Nawe utakaponirudia, watie moyo ndugu zako.”
but I prayed for you, that your faith wouldn’t fail. You, when once you have turned again, establish your brothers.”
33 Naye Petro akamjibu, “Bwana, mimi niko tayari kwenda pamoja nawe gerezani, na hata kufa.”
He said to him, “Lord, I am ready to go with you both to prison and to death!”
34 Yesu akamjibu, “Nakwambia wewe Petro, kabla jogoo hajawika leo utakuwa umenikana mara tatu.”
He said, “I tell you, Peter, the rooster will by no means crow today until you deny that you know me three times.”
35 Kisha, Yesu akawauliza wanafunzi wake, “Wakati nilipowatuma bila mfuko wa fedha wala mkoba wala viatu, mlitindikiwa chochote?” Wakajibu, “La.”
He said to them, “When I sent you out without purse, bag, and sandals, did you lack anything?” They said, “Nothing.”
36 Naye akawaambia, “Lakini sasa, yule aliye na mfuko wa fedha auchukue; na aliye na mkoba, hali kadhalika. Na yeyote asiye na upanga, auze koti lake anunue mmoja.
Then he said to them, “But now, whoever has a purse, let him take it, and likewise a bag. Whoever has none, let him sell his cloak, and buy a sword.
37 Maana nawaambieni, haya maneno ya Maandiko Matakatifu: Aliwekwa kundi moja na wahalifu, ni lazima yatimie. Naam, yale yanayonihusu yanafikia ukamilifu wake.”
For I tell you that this which is written must still be fulfilled in me: ‘He was counted with transgressors.’ For that which concerns me is being fulfilled.”
38 Nao wakasema, “Bwana, tazama; hapa kuna panga mbili.” Naye akasema, “Basi!”
They said, “Lord, behold, here are two swords.” He said to them, “That is enough.”
39 Yesu akatoka, na kama ilivyokuwa desturi yake, akaenda katika mlima wa Mizeituni; wanafunzi wake wakamfuata.
He came out and went, as his custom was, to the Mount of Olives. His disciples also followed him.
40 Alipofika huko akawaambia, “Salini, msije mkaingia katika kishawishi.”
When he was at the place, he said to them, “Pray that you don’t enter into temptation.”
41 Kisha akawaacha, akaenda umbali wa mtu kuweza kutupa jiwe, akapiga magoti, akasali:
He was withdrawn from them about a stone’s throw, and he knelt down and prayed,
42 “Baba, kama wapenda, ukiondoe kwangu kikombe hiki; hata hivyo, mapenzi yako yatimizwe, wala siyo yangu.”
saying, “Father, if you are willing, remove this cup from me. Nevertheless, not my will, but yours, be done.”
43 Hapo, malaika kutoka mbinguni, akamtokea ili kumtia moyo.
An angel from heaven appeared to him, strengthening him.
44 Akiwa katika uchungu mkubwa, alisali kwa bidii zaidi; na jasho likamtoka, kama matone ya damu, likatiririka mpaka chini.
Being in agony, he prayed more earnestly. His sweat became like great drops of blood falling down on the ground.
45 Baada ya kusali, aliwarudia wanafunzi wake, akawakuta wamelala, kwani walikuwa na huzuni.
When he rose up from his prayer, he came to the disciples and found them sleeping because of grief,
46 Akawaambia, “Mbona mnalala? Amkeni msali, msije mkaingia katika kishawishi.”
and said to them, “Why do you sleep? Rise and pray that you may not enter into temptation.”
47 Alipokuwa bado anaongea, kundi la watu likaja likiongozwa na yule aliyeitwa Yuda, mmoja wa wale mitume kumi na wawili. Yuda akaenda kumsalimu Yesu kwa kumbusu.
While he was still speaking, a crowd appeared. He who was called Judah, one of the twelve, was leading them. He came near to Yeshua to kiss him.
48 Lakini Yesu akamwambia, “Yuda! Je, unamsaliti Mwana wa Mtu kwa kumbusu?”
But Yeshua said to him, “Judah, do you betray the Son of Man with a kiss?”
49 Wale wanafunzi wake walipoona hayo wakasema, “Bwana, tutumie panga zetu?”
When those who were around him saw what was about to happen, they said to him, “Lord, shall we strike with the sword?”
50 Na mmoja wao akampiga upanga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio lake la kulia.
A certain one of them struck the servant of the high priest, and cut off his right ear.
51 Hapo, Yesu akasema, “Acha! Hii inatosha.” Akaligusa sikio la mtu huyo akaliponya.
But Yeshua answered, “Let me at least do this”—and he touched his ear and healed him.
52 Kisha Yesu akawaambia makuhani wakuu, wakubwa wa walinzi wa Hekalu na wazee waliokuja kumkamata: “Je, mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyang'anyi?
Yeshua said to the chief priests, captains of the temple, and elders, who had come against him, “Have you come out as against a robber, with swords and clubs?
53 Nilipokuwa pamoja nanyi kila siku Hekaluni hamkunitia nguvuni. Lakini, huu ndio wakati wenu hasa, ndio wakati wa utawala wa giza.”
When I was with you in the temple daily, you didn’t stretch out your hands against me. But this is your hour, and the power of darkness.”
54 Basi, wakamkamata, wakamchukua na kwenda naye nyumbani kwa Kuhani Mkuu. Petro akawa anamfuata nyuma kwa mbali.
They seized him and led him away, and brought him into the high priest’s house. But Peter followed from a distance.
55 Moto ulikuwa umewashwa katikati ya ua, nao wakawa wameketi pamoja Petro akiwa miongoni mwao.
When they had kindled a fire in the middle of the courtyard and had sat down together, Peter sat amongst them.
56 Mjakazi mmoja alipomwona Petro ameketi karibu na moto, akamkodolea macho, akasema, “Mtu huyu alikuwa pia pamoja na Yesu.”
A certain servant girl saw him as he sat in the light, and looking intently at him, said, “This man also was with him.”
57 Lakini Petro akakana akisema, “Wee! simjui mimi.”
He denied Yeshua, saying, “Woman, I don’t know him.”
58 Baadaye kidogo, mtu mwingine akamwona Petro, akasema, “Wewe ni mmoja wao.” Lakini Petro akajibu “Bwana we; si mimi!”
After a little while someone else saw him and said, “You also are one of them!” But Peter answered, “Man, I am not!”
59 Kama saa moja baadaye, mtu mwingine akasisitiza, “Hakika huyu alikuwa pamoja naye; ametoka Galilaya ati.”
After about one hour passed, another confidently affirmed, saying, “Truly this man also was with him, for he is a Galilean!”
60 Lakini Petro akasema, “Bwana wee; sijui hata unachosema!” Na papo hapo, akiwa bado anaongea, jogoo akawika.
But Peter said, “Man, I don’t know what you are talking about!” Immediately, while he was still speaking, a rooster crowed.
61 Bwana akageuka na kumtazama Petro, naye Petro akakumbuka yale aliyokuwa ameambiwa na Bwana: “Leo kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
The Lord turned and looked at Peter. Then Peter remembered the Lord’s word, how he said to him, “Before the rooster crows you will deny me three times.”
62 Hapo akatoka nje, akalia sana.
He went out, and wept bitterly.
63 Wale watu waliokuwa wanamchunga Yesu, walimpiga na kumdhihaki.
The men who held Yeshua mocked him and beat him.
64 Walimfunga kitambaa usoni, wakawa wanamwuliza, “Ni nani aliyekupiga? Hebu bashiri tuone!”
Having blindfolded him, they struck him on the face and asked him, “Prophesy! Who is the one who struck you?”
65 Wakamtolea maneno mengi ya matusi.
They spoke many other things against him, insulting him.
66 Kulipokucha, kikao cha wazee wa watu kilifanyika, ambacho kilihudhuriwa na makuhani wakuu na walimu wa Sheria. Yesu akaletwa mbele ya Baraza hilo.
As soon as it was day, the assembly of the elders of the people were gathered together, both chief priests and scribes, and they led him away into their council, saying,
67 Nao wakamwambia, “Twambie! Je, wewe ndiwe Kristo?” Lakini Yesu akawaambia, “Hata kama nikiwaambieni, hamtasadiki;
“If you are the Messiah, tell us.” But he said to them, “If I tell you, you won’t believe,
68 na hata kama nikiwaulizeni swali, hamtanijibu.
and if I ask, you will in no way answer me or let me go.
69 Lakini tangu sasa, Mwana wa Mtu atakuwa ameketi upande wa kulia wa Mungu Mwenyezi.”
From now on, the Son of Man will be seated at the right hand of the power of God.”
70 Hapo wote wakasema, “Ndiyo kusema wewe ni Mwana wa Mungu?” Naye akasema, “Ninyi mnasema kwamba mimi ndiye.”
They all said, “Are you then the Son of God?” He said to them, “You say it, because I am.”
71 Nao wakasema, “Je, tunahitaji ushahidi mwingine? Sisi wenyewe tumesikia akisema kwa mdomo wake mwenyewe.”
They said, “Why do we need any more witness? For we ourselves have heard from his own mouth!”

< Luka 22 >