< Luka 1 >

1 Mheshimiwa Theofilo: Watu wengi wamejitahidi kuandika juu ya mambo yale yaliyotendeka kati yetu.
Since many have undertaken to set in order a narrative concerning those matters which have been fulfilled among us,
2 Waliandika kama tulivyoelezwa na wale walioyaona kwa macho yao tangu mwanzo, na waliotangaza ujumbe huo.
even as those who from the beginning were eyewitnesses and servants of the word delivered them to us,
3 Inafaa nami pia, Mheshimiwa, baada ya kuchunguza kwa makini mambo yote tangu mwanzo, nikuandikie kwa mpango,
it seemed good to me also, having traced the course of all things accurately from the first, to write to you in order, most excellent Theophilus;
4 ili nawe uweze kujionea mwenyewe ukweli wa mambo yale uliyofundishwa.
that you might know the certainty concerning the things in which you were instructed.
5 Wakati Herode alipokuwa mfalme wa Yudea, kulikuwa na kuhani mmoja jina lake Zakaria, wa kikundi cha Abia. Mke wake alikuwa anaitwa Elisabeti, naye alikuwa wa ukoo wa kuhani Aroni.
There was in the days of Herod, the king of Judea, a certain priest named Zechariah, of the division of Abijah. He had a wife of the daughters of Aaron, and her name was Elizabeth.
6 Wote wawili walikuwa wanyofu mbele ya Mungu, wakiishi kwa kufuata amri na maagizo yote ya Bwana bila lawama.
They were both righteous before God, walking blamelessly in all the commandments and ordinances of the Lord.
7 Lakini hawakuwa wamejaliwa watoto kwa vile Elisabeti alikuwa tasa, nao wote wawili walikuwa wazee sana.
But they had no child, because Elizabeth was barren, and they both were well advanced in years.
8 Siku moja, ilipokuwa zamu yake ya kutoa huduma ya ukuhani mbele ya Mungu,
Now it happened, while he was performing the priest's office before God in the order of his division,
9 Zakariya alichaguliwa kwa kura, kama ilivyokuwa desturi, kuingia hekaluni ili afukize ubani.
according to the custom of the priest's office, his lot was to enter into the temple of the Lord and burn incense.
10 Watu, umati mkubwa, walikuwa wamekusanyika nje wanasali wakati huo wa kufukiza ubani.
And the whole crowd of people were praying outside at the hour of incense.
11 Malaika wa Bwana akamtokea humo ndani, akasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia ubani.
An angel of the Lord appeared to him, standing on the right side of the altar of incense.
12 Zakariya alipomwona alifadhaika, hofu ikamwingia.
Zechariah was troubled when he saw him, and fear fell upon him.
13 Lakini malaika akamwambia, “Zakariya, usiogope, kwa maana sala yako imesikilizwa, na Elisabeti mkeo atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utampa jina Yohane.
But the angel said to him, "Do not be afraid, Zechariah, because your request has been heard, and your wife, Elizabeth, will bear you a son, and you are to name him John.
14 Utakuwa na furaha kubwa na watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
You will have joy and gladness; and many will rejoice at his birth.
15 Atakuwa mkuu mbele ya Bwana. Hatakunywa divai wala kileo, atajazwa Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.
For he will be great in the sight of the Lord, and he must never drink wine or strong drink, and he will be filled with the Holy Spirit, even from his mother's womb.
16 Atawaelekeza wengi wa watu wa Israeli kwa Bwana Mungu wao.
He will turn many of the children of Israel to the Lord, their God.
17 Atamtangulia Bwana akiongozwa na nguvu na roho kama Eliya. Atawapatanisha kina baba na watoto wao; atawafanya wasiotii wawe na fikira za uadilifu, na hivyo amtayarishie Bwana watu wake.”
He will go before him in the spirit and power of Elijah, 'to turn the hearts of the fathers to the children,' and the disobedient to the wisdom of the just; to make ready a people prepared for the Lord."
18 Zakariya akamwambia huyo malaika, “Ni kitu gani kitakachonihakikishia jambo hilo? Mimi ni mzee, hali kadhalika na mke wangu.”
Zechariah said to the angel, "How can I be sure of this? For I am an old man, and my wife is well advanced in years."
19 Malaika akamjibu, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele ya Mungu, na nimetumwa niseme nawe, nikuletee hii habari njema.
The angel answered him, "I am Gabriel, who stands in the presence of God. I was sent to speak to you, and to bring you this good news.
20 Sikiliza, utakuwa bubu kwa sababu huyasadiki haya maneno yatakayotimia kwa wakati wake. Hutaweza kusema mpaka hayo niliyokuambia yatakapotimia.”
And look, you will be silent and not able to speak, until the day that these things will happen, because you did not believe my words, which will be fulfilled in their proper time."
21 Wakati huo, wale watu walikuwa wanamngoja Zakariya huku wakishangaa juu ya kukawia kwake Hekaluni.
The people were waiting for Zechariah, and they were wondering why he was delayed in the temple.
22 Alipotoka nje, hakuweza kusema nao. Ikawa dhahiri kwao kwamba alikuwa ameona maono Hekaluni. Lakini akawa anawapa ishara kwa mikono, akabaki bubu.
When he came out, he could not speak to them, and they perceived that he had seen a vision in the temple. He continued making signs to them, and remained mute.
23 Zamu yake ya kuhudumu ilipokwisha, alirudi nyumbani.
It happened, when the days of his service were fulfilled, he departed to his house.
24 Baadaye Elisabeti mkewe akapata mimba. Akajificha nyumbani kwa muda wa miezi mitano, akisema:
After these days Elizabeth, his wife, conceived, and she hid herself five months, saying,
25 “Hivi ndivyo alivyonitendea Bwana; ameniangalia na kuniondolea aibu niliyokuwa nayo mbele ya watu.”
"Thus has the Lord done to me in the days in which he looked at me, to take away my disgrace among people."
26 Mnamo mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu aende kwenye mji uitwao Nazareti huko Galilaya,
Now in the sixth month, the angel Gabriel was sent from God to a city of Galilee, named Nazareth,
27 kwa msichana mmoja aitwaye Maria, mchumba wa mtu mmoja jina lake Yosefu, wa ukoo wa Daudi.
to a virgin pledged to be married to a man whose name was Joseph, of the house of David. The virgin's name was Mary.
28 Malaika akamwendea, akamwambia, “Salamu Maria! Umejaliwa neema nyingi! Bwana yu pamoja nawe.”
Having come in, the angel said to her, "Greetings, favored one. The Lord is with you."
29 Maria aliposikia maneno hayo alifadhaika sana, akawaza: maneno haya yanamaanisha nini?
But when she saw him, she was greatly troubled at the saying, and considered what kind of greeting this might be.
30 Malaika akamwambia, “Usiogope Maria, kwa maana Mungu amekujalia neema.
The angel said to her, "Do not be afraid, Mary, for you have found favor with God.
31 Utachukua mimba, utamzaa mtoto wa kiume na utampa jina Yesu.
And look, you will conceive in your womb, and bring forth a son, and will call his name 'Jesus.'
32 Yeye atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Mungu Mkuu. Bwana Mungu atampa kiti cha mfalme Daudi, babu yake.
He will be great, and will be called the Son of the Most High. The Lord God will give him the throne of his father, David,
33 Kwa hivyo atautawala ukoo wa Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (aiōn g165)
and he will reign over the house of Jacob forever. There will be no end to his Kingdom." (aiōn g165)
34 Maria akamjibu, “Yatawezekanaje hayo, hali mimi ni bikira?”
Mary said to the angel, "How can this be, seeing I am a virgin?"
35 Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakushukia, na uwezo wake Mungu Mkuu utakujia kama kivuli; kwa sababu hiyo, mtoto atakayezaliwa ataitwa Mtakatifu, Mwana wa Mungu.
The angel answered her, "The Holy Spirit will come on you, and the power of the Most High will overshadow you. Therefore also the holy one who is born will be called the Son of God.
36 Ujue pia kwamba hata Elisabeti, jamaa yako, naye amepata mimba ingawa ni mzee, na sasa ni mwezi wa sita kwake yeye ambaye watu walimfahamu kuwa tasa.
And look, Elizabeth, your relative, also has conceived a son in her old age; and this is the sixth month with her who was called barren.
37 Kwa maana hakuna jambo lisilowezekana kwa Mungu.”
For with God nothing will be impossible."
38 Maria akasema, “Mimi ni mtumishi wa Bwana, nitendewe kama ulivyosema.” Kisha yule malaika akaenda zake.
And Mary said, "See, the handmaid of the Lord; be it to me according to your word." The angel departed from her.
39 Siku kadhaa baadaye, Maria alifunga safari akaenda kwa haraka hadi mji mmoja ulioko katika milima ya Yuda.
Mary arose in those days and went into the hill country with haste, into a city of Judah,
40 Huko, aliingia katika nyumba ya Zakariya, akamsalimu Elisabeti.
and entered into the house of Zechariah and greeted Elizabeth.
41 Mara tu Elisabeti aliposikia sauti ya Maria, mtoto mchanga tumboni mwake Elisabeti akaruka. Naye Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifiu,
It happened, when Elizabeth heard Mary's greeting, that the baby leaped in her womb, and Elizabeth was filled with the Holy Spirit.
42 akasema kwa sauti kubwa, “Umebarikiwa kuliko wanawake wote, naye utakayemzaa amebarikiwa.
She called out with a loud voice, and said, "Blessed are you among women, and blessed is the fruit of your womb.
43 Mimi ni nani hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
Why am I so favored, that the mother of my Lord should come to me?
44 Nakwambia, mara tu niliposikia sauti yako, mtoto mchanga tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
For look, when the voice of your greeting came into my ears, the baby leaped in my womb for joy.
45 Heri yako wewe uliyesadiki kwamba yatatimia yale Bwana aliyokwambia.”
Blessed is she who believed, for there will be a fulfillment of the things which have been spoken to her from the Lord."
46 Naye Maria akasema,
Mary said, "My soul magnifies the Lord.
47 “Moyo wangu wamtukuza Bwana, roho yangu inafurahi kwa sababu ya Mungu Mwokozi wangu.
And my spirit rejoices in God my Savior,
48 Kwa kuwa amemwangalia kwa huruma mtumishi wake mnyenyekevu. Hivyo tangu sasa watu wote wataniita mwenye heri.
for he has looked at the humble state of his servant girl. For look, from now on all generations will call me blessed.
49 Kwa kuwa Mwenyezi Mungu amenitendea makuu, jina lake ni takatifu.
For he who is mighty has done great things for me, and holy is his name.
50 Huruma yake kwa watu wanaomcha hudumu kizazi hata kizazi.
His mercy is for generations of generations on those who fear him.
51 Amefanya mambo makuu kwa mkono wake: amewatawanya wenye kiburi katika mawazo ya mioyo yao;
He has shown strength with his arm. He has scattered the proud in the imagination of their hearts.
52 amewashusha wenye nguvu kutoka vitu vyao vya enzi, akawakweza wanyenyekevu.
He has put down princes from their thrones. And has exalted the lowly.
53 Wenye njaa amewashibisha mema, matajiri amewaacha waende mikono mitupu.
He has filled the hungry with good things. He has sent the rich away empty.
54 Amemsaidia Israeli mtumishi wake, akikumbuka huruma yake.
He has given help to Israel, his servant, that he might remember mercy,
55 Kama alivyowaahidia wazee wetu Abrahamu na wazawa wake hata milele.” (aiōn g165)
As he spoke to our fathers, to Abraham and his offspring forever." (aiōn g165)
56 Maria alikaa na Elisabeti kwa muda upatao miezi mitatu, halafu akarudi nyumbani kwake.
Mary stayed with her about three months, and then returned to her house.
57 Wakati wa kujifungua kwake Elisabeti ulifika, akajifungua mtoto wa kiume.
Now the time that Elizabeth should give birth was fulfilled, and she brought forth a son.
58 Jirani na watu wa jamaa yake walipopata habari kwamba Bwana amemwonea huruma kubwa, walifurahi pamoja naye.
Her neighbors and her relatives heard that the Lord had magnified his mercy towards her, and they rejoiced with her.
59 Halafu siku ya nane walifika kumtahiri mtoto, wakataka kumpa jina la baba yake, Zakariya.
It happened on the eighth day, that they came to circumcise the child; and they would have called him Zechariah, after the name of the father.
60 Lakini mama yake akasema, “La, sivyo, bali ataitwa Yohane.”
His mother answered, "Not so; but he will be called John."
61 Wakamwambia, “Mbona hakuna yeyote katika ukoo wake mwenye jina hilo?”
They said to her, "There is no one among your relatives who is called by this name."
62 Basi, wakamwashiria baba yake wapate kujua alitaka mtoto wake apewe jina gani.
They made signs to his father, what he would have him called.
63 Naye akaomba kibao cha kuandikia, akaandika hivi: “Yohane ndilo jina lake.” Wote wakastaajabu.
And he asked for a writing tablet, and wrote, "His name is John." And they were all amazed.
64 Papo hapo midomo na ulimi wake Zakariya vikafunguliwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
His mouth was opened immediately, and his tongue freed, and he spoke, blessing God.
65 Hofu ikawaingia jirani wote, na habari hizo zikaenea kila mahali katika milima ya Yudea.
Fear came on all who lived around them, and all these sayings were talked about throughout all the hill country of Judea.
66 Wote waliosikia mambo hayo waliyatafakari mioyoni mwao wakisema: “Mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana, hakika nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye.
All who heard them laid them up in their heart, saying, "What then will this child be?" The hand of the Lord was with him.
67 Zakariya, baba yake mtoto, akajazwa Roho Mtakatifu, akatamka ujumbe wa Mungu:
His father, Zechariah, was filled with the Holy Spirit, and prophesied, saying,
68 “Asifiwe Bwana Mungu wa Israeli, kwani amekuja kuwasaidia na kuwakomboa watu wake.
"Blessed be the Lord, the God of Israel, for he has visited and worked redemption for his people;
69 Ametupatia Mwokozi shujaa, mzawa wa Daudi mtumishi wake.
and has raised up a horn of salvation for us in the house of his servant David
70 Aliahidi hapo kale kwa njia ya manabii wake watakatifu, (aiōn g165)
(as he spoke by the mouth of his holy prophets who have been from of old), (aiōn g165)
71 kwamba atatuokoa mikononi mwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
salvation from our enemies, and from the hand of all who hate us;
72 Alisema atawahurumia wazee wetu, na kukumbuka agano lake takatifu.
to show mercy towards our fathers, to remember his holy covenant,
73 Kiapo alichomwapia Abrahamu baba yetu, ni kwamba atatujalia sisi
the oath which he spoke to Abraham, our father,
74 tukombolewe kutoka adui zetu, tupate kumtumikia bila hofu,
to grant to us that we, being delivered out of the hand of our enemies, should serve him without fear,
75 kwa unyofu na uadilifu mbele yake, siku zote za maisha yetu.
In holiness and righteousness before him all our days.
76 Nawe mwanangu, utaitwa, nabii wa Mungu Mkuu, utamtangulia Bwana kumtayarishia njia yake;
And you, child, will be called a prophet of the Most High, for you will go before the Lord to make ready his ways,
77 kuwatangazia watu kwamba wataokolewa kwa kuondolewa dhambi zao.
to give knowledge of salvation to his people by the forgiveness of their sins,
78 Mungu wetu ni mpole na mwenye huruma. Atasababisha pambazuko angavu la ukombozi litujie kutoka juu,
because of the tender mercy of our God, whereby the dawn from on high will visit us,
79 na kuwaangazia wote wanaokaa katika giza kuu la kifo, aongoze hatua zetu katika njia ya amani.”
to shine on those who sit in darkness and the shadow of death; to guide our feet into the way of peace."
80 Mtoto akakua, akapata nguvu rohoni. Alikaa jangwani mpaka alipojionyesha rasmi kwa watu wa Israeli.
The child was growing, and becoming strong in spirit, and was in the desert until the day of his public appearance to Israel.

< Luka 1 >