< Luka 1 >

1 Mheshimiwa Theofilo: Watu wengi wamejitahidi kuandika juu ya mambo yale yaliyotendeka kati yetu.
Forasmuch as many haue taken in hand to set foorth the storie of those things, whereof we are fully persuaded,
2 Waliandika kama tulivyoelezwa na wale walioyaona kwa macho yao tangu mwanzo, na waliotangaza ujumbe huo.
As they haue deliuered them vnto vs, which from the beginning saw them their selues, and were ministers of ye word,
3 Inafaa nami pia, Mheshimiwa, baada ya kuchunguza kwa makini mambo yote tangu mwanzo, nikuandikie kwa mpango,
It seemed good also to me (most noble Theophilus) assoone as I had searched out perfectly all things from the beginning, to write vnto thee thereof from point to point,
4 ili nawe uweze kujionea mwenyewe ukweli wa mambo yale uliyofundishwa.
That thou mightest acknowledge the certaintie of those things, whereof thou hast bene instructed.
5 Wakati Herode alipokuwa mfalme wa Yudea, kulikuwa na kuhani mmoja jina lake Zakaria, wa kikundi cha Abia. Mke wake alikuwa anaitwa Elisabeti, naye alikuwa wa ukoo wa kuhani Aroni.
In the time of Herod King of Iudea, there was a certaine Priest named Zacharias, of the course of Abia: and his wife was of the daughters of Aaron, and her name was Elisabet.
6 Wote wawili walikuwa wanyofu mbele ya Mungu, wakiishi kwa kufuata amri na maagizo yote ya Bwana bila lawama.
Both were iust before God, and walked in all the commandements and ordinances of the Lord, without reproofe.
7 Lakini hawakuwa wamejaliwa watoto kwa vile Elisabeti alikuwa tasa, nao wote wawili walikuwa wazee sana.
And they had no childe, because that Elisabet was barren: and both were well stricken in age.
8 Siku moja, ilipokuwa zamu yake ya kutoa huduma ya ukuhani mbele ya Mungu,
And it came to passe, as he executed the Priestes office before God, as his course came in order,
9 Zakariya alichaguliwa kwa kura, kama ilivyokuwa desturi, kuingia hekaluni ili afukize ubani.
According to the custome of the Priests office, his lot was to burne incense, when he went into the Temple of the Lord.
10 Watu, umati mkubwa, walikuwa wamekusanyika nje wanasali wakati huo wa kufukiza ubani.
And the whole multitude of the people were without in prayer, while the incense was burning.
11 Malaika wa Bwana akamtokea humo ndani, akasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia ubani.
Then appeared vnto him an Angel of the Lord standing at the right side of the altar of incense.
12 Zakariya alipomwona alifadhaika, hofu ikamwingia.
And when Zacharias sawe him, he was troubled, and feare fell vpon him.
13 Lakini malaika akamwambia, “Zakariya, usiogope, kwa maana sala yako imesikilizwa, na Elisabeti mkeo atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utampa jina Yohane.
But the Angel saide vnto him, Feare not, Zacharias: for thy prayer is heard, and thy wise Elisabet shall beare thee a sonne, and thou shalt call his name Iohn.
14 Utakuwa na furaha kubwa na watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
And thou shalt haue ioy and gladnes, and many shall reioyce at his birth.
15 Atakuwa mkuu mbele ya Bwana. Hatakunywa divai wala kileo, atajazwa Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.
For he shalbe great in the sight of the Lord, and shall neither drinke wine, nor strong drinke: and he shalbe filled with the holy Ghost, euen from his mothers wombe.
16 Atawaelekeza wengi wa watu wa Israeli kwa Bwana Mungu wao.
And many of the children of Israel shall he turne to their Lord God.
17 Atamtangulia Bwana akiongozwa na nguvu na roho kama Eliya. Atawapatanisha kina baba na watoto wao; atawafanya wasiotii wawe na fikira za uadilifu, na hivyo amtayarishie Bwana watu wake.”
For he shall goe before him in the spirite and power of Elias, to turne the hearts of the fathers to the children, and the disobedient to the wisedome of the iust men, to make ready a people prepared for the Lord.
18 Zakariya akamwambia huyo malaika, “Ni kitu gani kitakachonihakikishia jambo hilo? Mimi ni mzee, hali kadhalika na mke wangu.”
Then Zacharias said vnto ye Angel, Whereby shall I knowe this? for I am an olde man, and my wife is of a great age.
19 Malaika akamjibu, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele ya Mungu, na nimetumwa niseme nawe, nikuletee hii habari njema.
And the Angell answered, and sayde vnto him, I am Gabriel that stand in the presence of God, and am sent to speake vnto thee, and to shew thee these good tidings.
20 Sikiliza, utakuwa bubu kwa sababu huyasadiki haya maneno yatakayotimia kwa wakati wake. Hutaweza kusema mpaka hayo niliyokuambia yatakapotimia.”
And beholde, thou shalt be domme, and not be able to speake, vntill the day that these things be done, because thou beleeuedst not my words, which shalbe fulfilled in their season.
21 Wakati huo, wale watu walikuwa wanamngoja Zakariya huku wakishangaa juu ya kukawia kwake Hekaluni.
Now the people waited for Zacharias, and marueiled that he taried so long in the Temple.
22 Alipotoka nje, hakuweza kusema nao. Ikawa dhahiri kwao kwamba alikuwa ameona maono Hekaluni. Lakini akawa anawapa ishara kwa mikono, akabaki bubu.
And when hee came out, hee coulde not speake vnto them: then they perceiued that hee had seene a vision in the Temple: For he made signes vnto them, and remained domme.
23 Zamu yake ya kuhudumu ilipokwisha, alirudi nyumbani.
And it came to passe, when the daies of his office were fulfilled, that he departed to his owne house.
24 Baadaye Elisabeti mkewe akapata mimba. Akajificha nyumbani kwa muda wa miezi mitano, akisema:
And after those daies, his wife Elisabet conceiued, and hid her selfe fiue moneths, saying,
25 “Hivi ndivyo alivyonitendea Bwana; ameniangalia na kuniondolea aibu niliyokuwa nayo mbele ya watu.”
Thus hath the Lord dealt with me, in the daies wherein he looked on me, to take from me my rebuke among men.
26 Mnamo mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu aende kwenye mji uitwao Nazareti huko Galilaya,
And in the sixth moneth, the Angell Gabriel was sent from God vnto a citie of Galile, named Nazareth,
27 kwa msichana mmoja aitwaye Maria, mchumba wa mtu mmoja jina lake Yosefu, wa ukoo wa Daudi.
To a virgin affianced to a man whose name was Ioseph, of the house of Dauid, and the virgins name was Marie.
28 Malaika akamwendea, akamwambia, “Salamu Maria! Umejaliwa neema nyingi! Bwana yu pamoja nawe.”
And the Angel went in vnto her, and said, Haile thou that art freely beloued: the Lord is with thee: blessed art thou among women.
29 Maria aliposikia maneno hayo alifadhaika sana, akawaza: maneno haya yanamaanisha nini?
And when she saw him, she was troubled at his saying, and thought what maner of salutation that should be.
30 Malaika akamwambia, “Usiogope Maria, kwa maana Mungu amekujalia neema.
Then the Angel saide vnto her, Feare not, Marie: for thou hast found fauour with God.
31 Utachukua mimba, utamzaa mtoto wa kiume na utampa jina Yesu.
For loe, thou shalt conceiue in thy wobe, and beare a sonne, and shalt call his name Iesus.
32 Yeye atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Mungu Mkuu. Bwana Mungu atampa kiti cha mfalme Daudi, babu yake.
He shall be great, and shall be called the Sonne of the most High, and the Lord God shall giue vnto him the throne of his father Dauid.
33 Kwa hivyo atautawala ukoo wa Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (aiōn g165)
And hee shall reigne ouer the house of Iacob for euer, and of his kingdome shall bee none ende. (aiōn g165)
34 Maria akamjibu, “Yatawezekanaje hayo, hali mimi ni bikira?”
Then sayde Marie vnto the Angel, How shall this be, seeing I knowe not man?
35 Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakushukia, na uwezo wake Mungu Mkuu utakujia kama kivuli; kwa sababu hiyo, mtoto atakayezaliwa ataitwa Mtakatifu, Mwana wa Mungu.
And the Angel answered, and said vnto her, The holy Ghost shall come vpon thee, and the power of the most High shall ouershadowe thee: therefore also that holy thing which shall bee borne of thee, shall be called the Sonne of God.
36 Ujue pia kwamba hata Elisabeti, jamaa yako, naye amepata mimba ingawa ni mzee, na sasa ni mwezi wa sita kwake yeye ambaye watu walimfahamu kuwa tasa.
And behold, thy cousin Elisabet, she hath also conceiued a sonne in her olde age: and this is her sixt moneth, which was called barren.
37 Kwa maana hakuna jambo lisilowezekana kwa Mungu.”
For with God shall nothing be vnpossible.
38 Maria akasema, “Mimi ni mtumishi wa Bwana, nitendewe kama ulivyosema.” Kisha yule malaika akaenda zake.
Then Marie said, Behold the seruant of the Lord: be it vnto me according to thy woorde. So the Angel departed from her.
39 Siku kadhaa baadaye, Maria alifunga safari akaenda kwa haraka hadi mji mmoja ulioko katika milima ya Yuda.
And Marie arose in those daies, and went into ye hil countrey with hast to a citie of Iuda,
40 Huko, aliingia katika nyumba ya Zakariya, akamsalimu Elisabeti.
And entred into the house of Zacharias, and saluted Elisabet.
41 Mara tu Elisabeti aliposikia sauti ya Maria, mtoto mchanga tumboni mwake Elisabeti akaruka. Naye Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifiu,
And it came to passe, as Elisabet heard the salutation of Marie, the babe sprang in her bellie, and Elisabet was filled with the holy Ghost.
42 akasema kwa sauti kubwa, “Umebarikiwa kuliko wanawake wote, naye utakayemzaa amebarikiwa.
And she cried with a loud voice, and saide, Blessed art thou among women, because the fruit of thy wombe is blessed.
43 Mimi ni nani hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
And whence commeth this to mee, that the mother of my Lord should come to me?
44 Nakwambia, mara tu niliposikia sauti yako, mtoto mchanga tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
For loe, assoone as the voice of thy salutation sounded in mine eares, the babe sprang in my bellie for ioye,
45 Heri yako wewe uliyesadiki kwamba yatatimia yale Bwana aliyokwambia.”
And blessed is shee that beleeued: for those things shall be perfourmed, which were tolde her from the Lord.
46 Naye Maria akasema,
Then Marie sayde, My soule magnifieth the Lord,
47 “Moyo wangu wamtukuza Bwana, roho yangu inafurahi kwa sababu ya Mungu Mwokozi wangu.
And my spirite reioyceth in God my Sauiour.
48 Kwa kuwa amemwangalia kwa huruma mtumishi wake mnyenyekevu. Hivyo tangu sasa watu wote wataniita mwenye heri.
For hee hath looked on the poore degree of his seruaunt: for beholde, from henceforth shall all ages call me blessed,
49 Kwa kuwa Mwenyezi Mungu amenitendea makuu, jina lake ni takatifu.
Because hee that is mightie, hath done for me great things, and holy is his Name.
50 Huruma yake kwa watu wanaomcha hudumu kizazi hata kizazi.
And his mercie is from generation to generation on them that feare him.
51 Amefanya mambo makuu kwa mkono wake: amewatawanya wenye kiburi katika mawazo ya mioyo yao;
Hee hath shewed strength with his arme: hee hath scattered the proude in the imagination of their hearts.
52 amewashusha wenye nguvu kutoka vitu vyao vya enzi, akawakweza wanyenyekevu.
Hee hath put downe the mighty from their seates, and exalted them of lowe degree.
53 Wenye njaa amewashibisha mema, matajiri amewaacha waende mikono mitupu.
Hee hath filled the hungrie with good things, and sent away the rich emptie.
54 Amemsaidia Israeli mtumishi wake, akikumbuka huruma yake.
Hee hath vpholden Israel his seruaunt to be mindefull of his mercie
55 Kama alivyowaahidia wazee wetu Abrahamu na wazawa wake hata milele.” (aiōn g165)
(As hee hath spoken to our fathers, to wit, to Abraham, and his seede) for euer. (aiōn g165)
56 Maria alikaa na Elisabeti kwa muda upatao miezi mitatu, halafu akarudi nyumbani kwake.
And Marie abode with her about three moneths: after, shee returned to her owne house.
57 Wakati wa kujifungua kwake Elisabeti ulifika, akajifungua mtoto wa kiume.
Nowe Elisabets time was fulfilled, that shee should be deliuered, and shee brought foorth a sonne.
58 Jirani na watu wa jamaa yake walipopata habari kwamba Bwana amemwonea huruma kubwa, walifurahi pamoja naye.
And her neighbours, and cousins heard tell howe the Lord had shewed his great mercie vpon her, and they reioyced with her.
59 Halafu siku ya nane walifika kumtahiri mtoto, wakataka kumpa jina la baba yake, Zakariya.
And it was so that on the eight day they came to circumcise the babe, and called him Zacharias after the name of his father.
60 Lakini mama yake akasema, “La, sivyo, bali ataitwa Yohane.”
But his mother answered, and saide, Not so, but he shalbe called Iohn.
61 Wakamwambia, “Mbona hakuna yeyote katika ukoo wake mwenye jina hilo?”
And they saide vnto her, There is none of thy kindred, that is named with this name.
62 Basi, wakamwashiria baba yake wapate kujua alitaka mtoto wake apewe jina gani.
Then they made signes to his father, howe he would haue him called.
63 Naye akaomba kibao cha kuandikia, akaandika hivi: “Yohane ndilo jina lake.” Wote wakastaajabu.
So hee asked for writing tables, and wrote, saying, His name is Iohn, and they marueiled all.
64 Papo hapo midomo na ulimi wake Zakariya vikafunguliwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
And his mouth was opened immediately, and his tongue, and he spake and praised God.
65 Hofu ikawaingia jirani wote, na habari hizo zikaenea kila mahali katika milima ya Yudea.
Then feare came on all them that dwelt neere vnto them, and all these woordes were noised abroade throughout all the hill countrey of Iudea.
66 Wote waliosikia mambo hayo waliyatafakari mioyoni mwao wakisema: “Mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana, hakika nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye.
And al they that heard them, laid them vp in their hearts, saying, What maner childe shall this be! and the hand of the Lord was with him.
67 Zakariya, baba yake mtoto, akajazwa Roho Mtakatifu, akatamka ujumbe wa Mungu:
Then his father Zacharias was filled with the holy Ghost, and prophesied, saying,
68 “Asifiwe Bwana Mungu wa Israeli, kwani amekuja kuwasaidia na kuwakomboa watu wake.
Blessed be the Lord God of Israel, because he hath visited and redeemed his people,
69 Ametupatia Mwokozi shujaa, mzawa wa Daudi mtumishi wake.
And hath raised vp the horne of saluation vnto vs, in the house of his seruant Dauid,
70 Aliahidi hapo kale kwa njia ya manabii wake watakatifu, (aiōn g165)
As he spake by ye mouth of his holy Prophets, which were since the world began, saying, (aiōn g165)
71 kwamba atatuokoa mikononi mwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
That he would sende vs deliuerance from our enemies, and from the hands of all that hate vs,
72 Alisema atawahurumia wazee wetu, na kukumbuka agano lake takatifu.
That he might shewe mercie towards our fathers, and remember his holy couenant,
73 Kiapo alichomwapia Abrahamu baba yetu, ni kwamba atatujalia sisi
And the othe which he sware to our father Abraham.
74 tukombolewe kutoka adui zetu, tupate kumtumikia bila hofu,
Which was, that he would graunt vnto vs, that we being deliuered out of the handes of our enemies, should serue him without feare,
75 kwa unyofu na uadilifu mbele yake, siku zote za maisha yetu.
All the daies of our life, in holinesse and righteousnesse before him.
76 Nawe mwanangu, utaitwa, nabii wa Mungu Mkuu, utamtangulia Bwana kumtayarishia njia yake;
And thou, babe, shalt be called the Prophet of the most High: for thou shalt goe before the face of the Lord, to prepare his waies,
77 kuwatangazia watu kwamba wataokolewa kwa kuondolewa dhambi zao.
And to giue knowledge of saluation vnto his people, by the remission of their sinnes,
78 Mungu wetu ni mpole na mwenye huruma. Atasababisha pambazuko angavu la ukombozi litujie kutoka juu,
Through ye tender mercy of our God, wherby the day spring from an hie hath visited vs,
79 na kuwaangazia wote wanaokaa katika giza kuu la kifo, aongoze hatua zetu katika njia ya amani.”
To giue light to them that sit in darknes, and in the shadow of death, and to guide our feete into the way of peace.
80 Mtoto akakua, akapata nguvu rohoni. Alikaa jangwani mpaka alipojionyesha rasmi kwa watu wa Israeli.
And the childe grewe, and waxed strong in spirit, and was in the wildernesse, til the day came that he should shewe him selfe vnto Israel.

< Luka 1 >