< Yohana 3 >

1 Kulikuwa na kiongozi mmoja Myahudi, wa kikundi cha Mafarisayo, jina lake Nikodemo.
And there was a man of the Pharisees, his name Nicodemus, a ruler of the Jews;
2 Siku moja alimwendea Yesu usiku, akamwambia, “Rabi, tunajua kwamba wewe ni mwalimu uliyetumwa na Mungu, maana hakuna mtu awezaye kufanya ishara unazozifanya Mungu asipokuwa pamoja naye.”
this one came to Him by night and said to Him, “Rabbi, we have known that You have come from God—a teacher, for no one is able to do these signs that You do, if God may not be with him.”
3 Yesu akamwambia, “Kweli nakwambia, mtu asipozaliwa upya hataweza kuuona ufalme wa Mungu.”
Jesus answered and said to him, “Truly, truly, I say to you, if anyone may not be born from above, he is not able to see the Kingdom of God”;
4 Nikodemo akamwuliza, “Mtu mzima awezaje kuzaliwa tena? Hawezi kuingia tumboni mwa mama yake na kuzaliwa mara ya pili!”
Nicodemus says to Him, “How is a man able to be born, being old? Is he able to enter into the womb of his mother a second time, and to be born?”
5 Yesu akamjibu, “Kweli nakwambia, mtu asipozaliwa kwa maji na Roho, hawezi kamwe kuingia katika ufalme wa Mungu.
Jesus answered, “Truly, truly, I say to you, if anyone may not be born of water and the Spirit, he is not able to enter into the Kingdom of God;
6 Mtu huzaliwa kimwili kwa baba na mama, lakini huzaliwa kiroho kwa Roho.
that which has been born of the flesh is flesh, and that which has been born of the Spirit is spirit.
7 Usistaajabu kwamba nimekwambia kuwa ni lazima kuzaliwa upya.
You may not wonder that I said to you, It is required for you to be born from above;
8 Upepo huvuma kuelekea upendako; waisikia sauti yake, lakini hujui unakotoka wala unakokwenda. Ndivyo ilivyo kwa mtu aliyezaliwa kwa Roho.”
the Spirit blows where [that] One wills, and you hear [that] One’s voice, but you have not known from where [that] One comes, and to where [that] One goes; thus is everyone who has been born of the Spirit.”
9 Nikodemo akamwuliza, “Mambo haya yanawezekanaje?”
Nicodemus answered and said to Him, “How are these things able to happen?”
10 Yesu akamjibu, “Je, wewe ni mwalimu katika Israel na huyajui mambo haya?
Jesus answered and said to him, “You are the teacher of Israel and you do not know these things?
11 Kweli nakwambia, sisi twasema tunayoyajua na kushuhudia tuliyoyaona, lakini ninyi hamkubali ujumbe wetu.
Truly, truly, I say to you, what We have known We speak, and what We have seen We testify, and you do not receive Our testimony;
12 Ikiwa nimewaambieni mambo ya kidunia nanyi hamniamini, mtawezaje kuamini nikiwaambieni mambo ya mbinguni?
if I spoke to you of the earthly things, and you do not believe, how, if I will speak to you of the heavenly things, will you believe?
13 Hakuna mtu aliyepata kwenda juu mbinguni isipokuwa Mwana wa Mtu ambaye ameshuka kutoka mbinguni.
And no one has gone up to Heaven, except He who came down out of Heaven—the Son of Man who is in Heaven.
14 “Kama vile Mose alivyomwinua juu nyoka wa shaba kule jangwani, naye Mwana wa Mtu atainuliwa juu vivyo hivyo,
And as Moses lifted up the serpent in the wilderness, so it is necessary for the Son of Man to be lifted up,
15 ili kila anayemwamini awe na uzima wa milele. (aiōnios g166)
that everyone who is believing in Him may not perish, but may have continuous life, (aiōnios g166)
16 Maana Mungu aliupenda ulimwengu hivi hata akamtoa Mwana wake wa pekee, ili kila amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. (aiōnios g166)
for God so loved the world that He gave the only begotten Son, that everyone who is believing in Him may not perish, but may have continuous life. (aiōnios g166)
17 Maana Mungu hakumtuma Mwanae ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali aukomboe ulimwengu.
For God did not send His Son into the world that He may judge the world, but that the world may be saved through Him;
18 “Anayemwamini Mwana hahukumiwi; asiyemwamini amekwisha hukumiwa kwa sababu hakumwamini Mwana wa pekee wa Mungu.
he who is believing in Him is not judged, but he who is not believing has been judged already, because he has not believed in the Name of the only begotten Son of God.
19 Na hukumu yenyewe ndiyo hii: Mwanga umekuja ulimwenguni lakini watu wakapenda giza kuliko mwanga, kwani matendo yao ni maovu.
And this is the judgment, that the light has come into the world, and men loved the darkness rather than the light, for their works were evil;
20 Kila mtu atendaye maovu anauchukia mwanga, wala haji kwenye mwanga, maana hapendi matendo yake maovu yamulikwe.
for everyone who is doing wicked things hates the light, and does not come into the light, that his works may not be detected;
21 Lakini mwenye kuuzingatia ukweli huja kwenye mwanga, ili matendo yake yaonekane yametendwa kwa kumtii Mungu.”
but he who is doing the truth comes into the light, that his works may be revealed, that in God they are having been worked.”
22 Baada ya hayo, Yesu alifika mkoani Yudea pamoja na wanafunzi wake. Alikaa huko pamoja nao kwa muda, akibatiza watu.
After these things Jesus and His disciples came into the land of Judea, and there He tarried with them, and was immersing;
23 Yohane pia alikuwa akibatiza watu huko Ainoni, karibu na Salemu, maana huko kulikuwa na maji mengi. Watu walimwendea, naye akawabatiza.
and John was also immersing in Aenon, near to Salem, because there were many waters there, and they were coming and were being immersed—
24 (Wakati huo Yohane alikuwa bado hajafungwa gerezani.)
for John was not yet cast into the prison—
25 Ubishi ulitokea kati ya baadhi ya wanafunzi wa Yohane na Myahudi mmoja kuhusu desturi za kutawadha.
there arose then a question from the disciples of John with [some] Jews about purifying,
26 Basi, wanafunzi hao wakamwendea Yohane na kumwambia, “Mwalimu, yule mtu aliyekuwa pamoja nawe ng'ambo ya Yordani na ambaye wewe ulimshuhudia, sasa naye anabatiza, na watu wote wanamwendea.”
and they came to John and said to him, “Rabbi, He who was with you beyond the Jordan, to whom you testified, behold, this One is immersing, and all are coming to Him.”
27 Yohane akawaambia, “Mtu hawezi kuwa na kitu asipopewa na Mungu.
John answered and said, “A man is not able to receive anything if it may not have been given him from Heaven;
28 Nanyi wenyewe mwaweza kushuhudia kuwa nilisema: Mimi siye Kristo, lakini nimetumwa ili nimtangulie!
you yourselves testify to me that I said, I am not the Christ, but that I am having been sent before Him;
29 Bibiarusi ni wake bwanaarusi, lakini rafiki yake bwana arusi, anayesimama na kusikiliza, hufurahi sana anapomsikia bwana arusi akisema. Ndivyo furaha yangu ilivyokamilishwa.
He who is having the bride is bridegroom, and the friend of the bridegroom, who is standing and hearing Him, rejoices with joy because of the voice of the bridegroom; this, then, my joy has been fulfilled.
30 Ni lazima yeye azidi kuwa maarufu, na mimi nipungue.
It is necessary [for] Him to increase, and me to become less;
31 “Anayekuja kutoka juu ni mkuu kuliko wote; atokaye duniani ni wa dunia, na huongea mambo ya kidunia. Lakini anayekuja kutoka mbinguni ni mkuu kuliko wote.
He who is coming from above is above all; he who is from the earth, from the earth he is, and from the earth he speaks; He who is coming from Heaven is above all.
32 Yeye husema yale aliyoyaona na kuyasikia, lakini hakuna mtu anayekubali ujumbe wake.
And what He has seen and heard—this He testifies, and none receives His testimony;
33 Lakini mtu yeyote anayekubali ujumbe wake anathibitisha kwamba Mungu ni kweli.
he who is receiving His testimony sealed that God is true;
34 Yule aliyetumwa na Mungu husema maneno ya Mungu, maana Mungu humjalia mtu huyo Roho wake bila kipimo.
for He whom God sent, He speaks the sayings of God; for God does not give the Spirit by measure;
35 Baba anampenda Mwana na amemkabidhi vitu vyote.
the Father loves the Son, and has given all things into His hand;
36 Anayemwamini Mwana anao uzima wa milele; asiyemtii Mwana hatakuwa na uzima wa milele, bali ghadhabu ya Mungu hubaki juu yake.” (aiōnios g166)
he who is believing in the Son has continuous life; and he who is not believing the Son will not see life, but the wrath of God remains on him.” (aiōnios g166)

< Yohana 3 >