< Yohana 17 >

1 Yesu alipokwisha sema hayo, alitazama juu mbinguni, akasema, “Baba, saa imefika! Mtukuze Mwanao ili naye Mwana apate kukutukuza.
耶稣说了这话,就举目望天,说:“父啊,时候到了,愿你荣耀你的儿子,使儿子也荣耀你;
2 Maana ulimpa Mwanao mamlaka juu ya watu wote ili awape uzima wa milele wote hao uliompa. (aiōnios g166)
正如你曾赐给他权柄管理凡有血气的,叫他将永生赐给你所赐给他的人。 (aiōnios g166)
3 Na uzima wa milele ndio huu: kukujua wewe uliye peke yako Mungu wa kweli, na kumjua Yesu Kristo uliyemtuma. (aiōnios g166)
认识你—独一的真神,并且认识你所差来的耶稣基督,这就是永生。 (aiōnios g166)
4 Mimi nimekutukuza hapa duniani; nimeikamilisha ile kazi uliyonipa nifanye.
我在地上已经荣耀你,你所托付我的事,我已成全了。
5 Sasa, Baba, nitukuze mbele yako kwa ule utukufu niliokuwa nao kabla ya kuumbwa ulimwengu.
父啊,现在求你使我同你享荣耀,就是未有世界以先,我同你所有的荣耀。
6 “Nimekufanya ujulikane kwa watu wale ulionipa kutoka duniani. Walikuwa watu wako, nawe ukanipa wawe wangu; nao wamelishika neno lako.
“你从世上赐给我的人,我已将你的名显明与他们。他们本是你的,你将他们赐给我,他们也遵守了你的道。
7 Sasa wanajua kwamba kila ulichonipa kimetoka kwako.
如今他们知道,凡你所赐给我的,都是从你那里来的;
8 Mimi nimewapa ule ujumbe ulionipa nao wameupokea; wanajua kwamba kweli nimetoka kwako, na wanaamini kwamba wewe ulinituma.
因为你所赐给我的道,我已经赐给他们,他们也领受了,又确实知道,我是从你出来的,并且信你差了我来。
9 “Nawaombea hao; siuombei ulimwengu, ila nawaombea hao ulionipa, maana ni wako.
我为他们祈求,不为世人祈求,却为你所赐给我的人祈求,因他们本是你的。
10 Yote niliyo nayo ni yako, na yako ni yangu; na utukufu wangu umeonekana ndani yao.
凡是我的,都是你的;你的也是我的,并且我因他们得了荣耀。
11 Na sasa naja kwako; simo tena ulimwenguni, lakini wao wamo ulimwenguni. Baba Mtakatifu! Kwa nguvu ya jina lako ulilonipa, tafadhali uwaweke salama ili wawe kitu kimoja kama sisi tulivyo mmoja.
从今以后,我不在世上,他们却在世上;我往你那里去。圣父啊,求你因你所赐给我的名保守他们,叫他们合而为一像我们一样。
12 Nilipokuwa nao, mimi niliwaweka salama kwa nguvu ya jina lako ulilonipa. Mimi nimewalinda, wala hakuna hata mmoja wao aliyepotea, isipokuwa yule aliyelazimika kupotea ili Maandiko Matakatifu yapate kutimia.
我与他们同在的时候,因你所赐给我的名保守了他们,我也护卫了他们;其中除了那灭亡之子,没有一个灭亡的,好叫经上的话得应验。
13 Basi, sasa naja kwako, na nimesema mambo haya ulimwenguni, ili waweze kushiriki kikamilifu furaha yangu.
现在我往你那里去,我还在世上说这话,是叫他们心里充满我的喜乐。
14 Mimi nimewapa neno lako, nao ulimwengu ukawachukia, kwa sababu wao si wa ulimwengu kama vile nami nisivyo wa ulimwengu.
我已将你的道赐给他们。世界又恨他们;因为他们不属世界,正如我不属世界一样。
15 Siombi uwatoe ulimwenguni, bali naomba uwakinge na yule Mwovu.
我不求你叫他们离开世界,只求你保守他们脱离那恶者。
16 Wao si wa ulimwengu, kama vile nami nisivyo wa ulimwengu.
他们不属世界,正如我不属世界一样。
17 Waweke wakfu kwa ukweli; neno lako ni ukweli.
求你用真理使他们成圣;你的道就是真理。
18 Kama vile ulivyonituma ulimwenguni, nami pia nimewatuma wao ulimwenguni;
你怎样差我到世上,我也照样差他们到世上。
19 na kwa ajili yao mimi mwenyewe najiweka wakfu ili nao pia wafanywe wakfu katika ukweli.
我为他们的缘故,自己分别为圣,叫他们也因真理成圣。
20 “Siwaombei hao tu, bali nawaombea pia wote watakaoamini kutokana na ujumbe wao.
“我不但为这些人祈求,也为那些因他们的话信我的人祈求,
21 Naomba ili wote wawe kitu kimoja. Baba! Naomba wawe ndani yetu kama vile wewe ulivyo ndani yangu nami ndani yako. Naomba wawe kitu kimoja kusudi ulimwengu upate kuamini kwamba wewe ulinituma.
使他们都合而为一。正如你父在我里面,我在你里面,使他们也在我们里面,叫世人可以信你差了我来。
22 Mimi nimewapa utukufu uleule ulionipa mimi, ili wawe kitu kimoja kama nasi tulivyo mmoja;
你所赐给我的荣耀,我已赐给他们,使他们合而为一,像我们合而为一。
23 mimi niwe ndani yao, nawe uwe ndani yangu; naomba wakamilishwe na kuwa kitu kimoja, ili ulimwengu upate kujua kwamba wewe ulinituma, na kwamba unawapenda wao kama unavyonipenda mimi.
我在他们里面,你在我里面,使他们完完全全地合而为一,叫世人知道你差了我来,也知道你爱他们如同爱我一样。
24 “Baba! Nataka wao ulionipa wawe pamoja nami pale nilipo, ili wauone utukufu wangu ulionipa; kwa kuwa ulinipenda kabla ya kuumbwa ulimwengu.
父啊,我在哪里,愿你所赐给我的人也同我在那里,叫他们看见你所赐给我的荣耀;因为创立世界以前,你已经爱我了。
25 Baba Mwema! Ulimwengu haukujui, lakini mimi nakujua. Hawa nao wanajua kwamba wewe ulinituma.
公义的父啊,世人未曾认识你,我却认识你;这些人也知道你差了我来。
26 Nimekufanya ujulikane kwao na nitaendelea kufanya hivyo, ili upendo ulio nao kwangu uwe ndani yao, nami niwe ndani yao.”
我已将你的名指示他们,还要指示他们,使你所爱我的爱在他们里面,我也在他们里面。”

< Yohana 17 >