< Yohana 13 >

1 Ilikuwa kabla ya sikukuu ya Pasaka. Yesu alijua kwamba saa yake ya kuondoka ulimwenguni na kwenda kwa Baba ilikuwa imefika. Alikuwa amewapenda daima watu wake walioko duniani; naam, aliwapenda mpaka mwisho!
Before the feast of ester whe Iesus knewe that his houre was come that he shuld departe out of this worlde vnto the father. When he loved his which were in the worlde vnto the ende he loved the.
2 Basi, Yesu na wanafunzi wake walikuwa mezani kwa chakula cha jioni. Ibilisi alikwisha mtia Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti, nia ya kumsaliti Yesu.
And when supper was ended after that the devyll had put in the hert of Iudas Iscariot Simos sonne to betraye him:
3 Yesu alijua kwamba Baba alikuwa amemkabidhi kila kitu, na kwamba alikuwa ametoka kwa Mungu na anarudi kwa Mungu.
Iesus knowinge that the father had geve all thinges into his hondes. And that he was come from God and went to God
4 Basi, Yesu aliondoka mezani, akaweka kando vazi lake, akachukua kitambaa na kujifunga kiunoni.
he rose from supper and layde a syde his vpper garmentes and toke a towell and gyrd him selfe.
5 Kisha akatia maji katika bakuli, akaanza kuwaosha wanafunzi wake miguu na kuipangusa kwa kile kitambaa alichojifungia.
After that poured he water into a basyn and beganne to wash his disciples fete and to wype them with the towell wherwith he was gyrde.
6 Basi, akamfikia Simoni Petro; naye Petro akasema, “Bwana, wewe utaniosha miguu mimi?”
Then came he to Simon Peter. And Peter sayde to him: Lorde shalt thou wesshe my fete?
7 Yesu akamjibu, “Huelewi sasa ninachofanya lakini utaelewa baadaye.”
Iesus answered and sayde vnto him: what I do thou wotest not now but thou shalt knowe herafter.
8 Petro akamwambia, “Wewe hutaniosha miguu kamwe!” Yesu akamjibu, “Nisipokuosha hutakuwa na uhusiano nami tena.” (aiōn g165)
Peter sayd vnto him: thou shalt not wesshe my fete whill ye worlde stondeth. Iesus answered him: yf I wasshe ye not thou shalt have no part with me. (aiōn g165)
9 Simoni Petro akamwambia, “Bwana, nioshe, si miguu tu, bali na mikono yangu na kichwa pia.”
Simon Peter sayde vnto him: Lorde not my fete only: but also my handes and my heed.
10 Yesu akamwambia, “Aliyekwisha oga hana lazima ya kunawa isipokuwa miguu, maana amekwisha takata mwili wote. Ninyi mmetakata, lakini si nyote.”
Iesus sayde to him: he that is wesshed nedeth not save to wesshe his fete and is clene every whit. And ye are clene: but not all.
11 (Yesu alimjua yule ambaye atamsaliti, ndiyo maana alisema: “Ninyi mmetakata, lakini si nyote.”)
For he knewe his betrayer. Therfore sayde he: ye are not all clene.
12 Alipokwisha waosha miguu na kuvaa tena vazi lake, aliketi mezani, akawaambia, “Je, mmeelewa hayo niliyowatendeeni?
After he had wesshed their fete and receaved his clothes and was set doune agayne he sayde vnto them? wot ye what I have done to you?
13 Ninyi mwaniita Mwalimu na Bwana, nanyi mwasema vyema, kwa kuwa ndimi.
Ye call me master and Lorde and ye saye well for so am I.
14 Basi, ikiwa mimi niliye Bwana na Mwalimu, nimewaosha ninyi miguu, nanyi pia mnapaswa kuoshana miguu.
If I then youre Lorde and master have wesshed youre fete ye also ought to wesshe one anothers fete.
15 Nimewapeni mfano, ili nanyi pia mfanye kama nilivyowafanyieni.
For I have geven you an ensample that ye shuld do as I have done to you.
16 Kweli nawaambieni, mtumishi si mkuu zaidi kuliko bwana wake, wala mtume si mkuu zaidi kuliko yule aliyemtuma.
Verely verely I saye vnto you the servaunt is not greater then his master nether the messenger greater then he that sent him.
17 Basi, ikiwa mwayajua hayo, mtakuwa na heri mkiyatekeleza.
If ye vnderstonde these thinges happy are ye yf ye do them.
18 “Haya nisemayo hayawahusu ninyi nyote. Mimi nawajua wale niliowachagua. Lakini lazima yatimie Maandiko Matakatifu yasemayo: Yule aliyeshiriki chakula changu amegeuka kunishambulia.
I speake not of you all I knowe whom I have chosen. But that ye scripture be fulfilled: he that eateth breed wt me hath lyfte vp his hele agaynste me.
19 Mimi nimewaambieni mambo haya sasa kabla hayajatokea, ili yatakapotokea mpate kuamini kuwa mimi ndimi.
Now tell I you before it come: that when it is come to passe ye might beleve that I am he.
20 Kweli nawaambieni anayempokea yule ninayemtuma anaponipokea mimi; na anayenipokea mimi, anampokea yule aliyenituma.”
Verely verely I saye vnto you. He that receaveth who soever I sende receaveth me. And he that receaveth me receaveth him that sent me.
21 Alipokwisha sema hayo, Yesu alifadhaika sana rohoni, akasema wazi, “Kweli nawaambieni, mmoja wenu atanisaliti!”
When Iesus had thus sayd he was troubled in the sprete and testified sayinge: verely verely I saye vnto you that one of you shall betraye me.
22 Wanafunzi wakatazama wasiweze kabisa kujua anasema nani.
And then the disciples loked one on another doutinge of who he spake.
23 Mmoja wa wanafunzi, ambaye Yesu alikuwa anampenda sana, alikuwa ameketi karibu na Yesu.
Ther was one of his disciples which leaned on Iesus bosome whom Iesus loved.
24 Basi, Simoni Petro akamwashiria na kusema: “Mwulize anasema juu ya nani.”
To him beckened Simo Peter that he shuld axe who it was of whom he spake.
25 Mwanafunzi huyo akasogea karibu zaidi na Yesu, akamwuliza, “Bwana, ni nani?”
He then as he leaned on Iesus brest sayde vnto him: Lorde who ys it?
26 Yesu akajibu, “Yule nitakayempa kipande cha mkate nilichochovya katika sahani, ndiye.” Basi, akatwaa kipande cha mkate, akakichovya katika sahani, akampa Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti.
Iesus answered he yt ys to whom I geve a soppe when I have dept it. And he wet a soppe and gave it to Iudas Iscarioth Simons sonne.
27 Yuda alipokwisha pokea kipande hicho, Shetani akamwingia. Basi Yesu akamwambia, “Unachotaka kufanya, kifanye haraka!”
And after the soppe Satan entred into him. Then sayd Iesus vnto him: that thou dost do quickly.
28 Lakini hakuna hata mmoja wa wale waliokaa pale mezani aliyefahamu kwa nini alikuwa amemwambia hivyo.
That wist no ma at the table for what intent he spake vnto him.
29 Kwa kuwa Yuda alikuwa na wajibu wa kuutunza mfuko wa fedha, baadhi yao walidhani kwamba Yesu alikuwa amemwambia anunue vilivyohitajiwa kwa sikukuu, au kwamba alikuwa amemwambia akatoe chochote kwa maskini.
Some of the thought because Iudas had the bagge that Iesus had sayd vnto him bye those thinges that we have nede af agaynst ye feast: or that he shulde geve some thinge to the poore.
30 Basi, Yuda alipokwisha twaa kile kipande cha mkate, akatoka nje mara. Na ilikuwa usiku.
Assone then as he had receaved the soppe he wet immediatly out. And it was night.
31 Baada ya Yuda kuondoka, Yesu akasema, “Sasa Mwana wa Mtu ametukuzwa, naye Mungu ametukuzwa ndani yake.
Whe he was gone out Iesus sayde: now is the sonne of man glorified. And God is glorified by him.
32 Na kama utukufu wa Mungu umefunuliwa ndani ya Mwana, basi, naye Mungu ataudhihirisha utukufu wa Mwana ndani yake mwenyewe, na atafanya hivyo mara.
Yf God be glorified by him God shall also glorify him in him selfe: and shall strayght waye glorify him.
33 “Watoto wangu, bado niko nanyi kwa muda mfupi tu. Mtanitafuta, lakini sasa nawaambieni yale niliyowaambia viongozi wa Wayahudi: Niendako ninyi hamwezi kwenda!
Deare chyldren yet a lytell whyle am I with you. Ye shall seke me and as I sayde vnto the Iewes whither I goo thither can ye not come. Also to you saye I nowe.
34 Nawapeni amri mpya: pendaneni; pendaneni kama nilivyowapenda ninyi.
A newe commaundment geve I vnto you that ye love to gedder as I have loved you that even so ye love one another
35 Mkipendana, watu wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu.”
By this shall all me knowe yt ye are my disciples yf ye shall have love one to another.
36 Simoni Petro akamwuliza, “Bwana, unakwenda wapi?” Yesu akajibu, “Niendako huwezi kunifuata sasa, lakini utanifuata baadaye.”
Simon Peter sayd vnto him: Lorde whither goest thou? Iesus answered him: whither I goo thou canst not folowe me now but thou shalt folowe me afterwardes.
37 Petro akamwambia “Bwana, kwa nini siwezi kukufuata sasa? Niko tayari kufa kwa ajili yako!”
Peter sayd vnto him: Lorde why canot I folowe the now? I will geve my lyfe for thy sake?
38 Yesu akajibu, “Je, uko tayari kweli kufa kwa ajili yangu? Kweli nakwambia, kabla jogoo hajawika utanikana mara tatu!”
Iesus answered him: wilt thou geve thy lyfe for my sake? Verely verely I saye vnto the the cocke shall not crowe tyll thou have denyed me thryse.

< Yohana 13 >