< Yohana 12 >

1 Siku sita kabla ya sikukuu ya Pasaka, Yesu alifika Bethania alikoishi Lazaro ambaye Yesu alikuwa amemfufua kutoka wafu.
Potem je Jezus, šest dni pred pasho, prišel v Betanijo, kjer je bil Lazar, ki je bil mrtev, ki ga je obudil od mrtvih.
2 Huko walimwandalia chakula cha jioni, naye Martha akawa anawatumikia. Lazaro alikuwa mmoja wa wale waliokuwa mezani pamoja na Yesu.
Tam so mu pripravili večerjo in Marta je stregla, toda Lazar je bil eden izmed teh, ki je z njim sedel za mizo.
3 Basi, Maria alichukua chupa ya marashi ya nardo safi ya thamani kubwa, akampaka Yesu miguu na kuipangusa kwa nywele zake. Nyumba yote ikajaa harufu ya marashi.
Tedaj je Marija vzela funt zelo dragocenega mazila iz narde in mazilila Jezusova stopala in s svojimi lasmi obrisala njegova stopala, in hiša je bila napolnjena z vonjem mazila.
4 Basi, Yuda Iskarioti, mmoja wa wale kumi na wawili ambaye ndiye atakayemsaliti Yesu, akasema,
Potem reče eden izmed njegovih učencev, Juda Iškarijot, Simonov sin, ki naj bi ga izdal:
5 “Kwa nini marashi hayo hayakuuzwa kwa fedha dinari mia tatu, wakapewa maskini?”
»Zakaj ni bilo to mazilo prodano za tristo denarjev in dano revnim?«
6 Alisema hivyo, si kwa kuwa alijali chochote juu ya maskini, bali kwa sababu alikuwa mweka hazina, na kwa kuwa alikuwa mwizi, mara kwa mara aliiba kutoka katika hiyo hazina.
To je rekel, ne, ker bi skrbel za revne, temveč zato, ker je bil tat in je imel mošnjo ter nosil, kar je bilo dano vanjo.
7 Lakini Yesu akasema, “Msimsumbue huyu mama! Mwacheni ayaweke kwa ajili ya siku ya mazishi yangu.
Potem je Jezus rekel: »Pusti jo pri miru. To je zadržala za dan mojega pokopa.
8 Maskini mtakuwa nao siku zote, lakini hamtakuwa nami siku zote.”
Kajti revne imate vedno s seboj, mene pa nimate vedno.«
9 Wayahudi wengi walisikia kwamba Yesu alikuwa Bethania. Basi, wakafika huko si tu kwa ajili ya kumwona Yesu, ila pia wapate kumwona Lazaro ambaye Yesu alimfufua kutoka wafu.
Veliko ljudi izmed Judov je torej vedelo, da je bil tam. Niso pa prišli samo zaradi Jezusa, temveč, da bi lahko videli tudi Lazarja, ki ga je obudil od mrtvih.
10 Makuhani wakuu waliamua pia kumwua Lazaro,
Toda visoki duhovniki so se posvetovali, da bi mogli usmrtiti tudi Lazarja,
11 Maana kwa sababu ya Lazaro Wayahudi wengi waliwaasi viongozi wao, wakamwamini Yesu.
zato ker je zaradi tega razloga mnogo izmed Judov odšlo proč in verovalo v Jezusa.
12 Kesho yake, kundi kubwa la watu waliokuja kwenye sikukuu walisikia kuwa Yesu alikuwa njiani kuja Yerusalemu.
Naslednji dan je mnogo ljudi, ki so prišli na praznik, ko so slišali, da je v Jeruzalem prihajal Jezus,
13 Basi, wakachukua matawi ya mitende, wakatoka kwenda kumlaki; wakapaaza sauti wakisema: “Hosana! Abarikiwe huyo ajaye kwa jina la Bwana. Abarikiwe mfalme wa Israeli.”
vzelo mladike palmovih dreves in mu odšlo naproti, da ga srečajo ter klicali: »Hozana: ›Blagoslovljen je Izraelov Kralj, ki prihaja v Gospodovem imenu.‹«
14 Yesu akampata mwana punda mmoja akapanda juu yake kama yasemavyo Maandiko:
In Jezus, ko je našel mladega osla, je sédel nanj, kakor je pisano:
15 “Usiogope mji wa Sioni! Tazama, Mfalme wako anakuja, Amepanda mwana punda.”
»Ne boj se, hči sionska, glej, tvoj Kralj prihaja, sedeč na osličjem žrebetu.«
16 Wakati huo wanafunzi wake hawakuelewa mambo hayo, lakini Yesu alipokwisha tukuzwa, ndipo walipokumbuka kwamba hayo yalikuwa yameandikwa juu yake, na kwamba watu walikuwa wamemtendea hivyo.
Teh stvari njegovi učenci sprva niso razumeli, toda ko je bil Jezus poveličan, potem so se spomnili, da so bile te stvari pisane o njem in da so mu te stvari storili.
17 Kundi la watu wale waliokuwa pamoja naye wakati alipomwita Lazaro kutoka kaburini, akamfufua kutoka wafu, walisema yaliyotukia.
Množica torej, ki je bila z njim, ko je Lazarja poklical iz njegovega groba in ga obudil od mrtvih, je pričevala.
18 Kwa hiyo umati huo wa watu ulimlaki, maana wote walisikia kwamba Yesu alikuwa amefanya ishara hiyo.
Zaradi tega razloga ga je množica tudi srečala, ker so slišali, da je storil ta čudež.
19 Basi, Mafarisayo wakaambiana, “Mnaona? Hatuwezi kufanya chochote! Tazameni, ulimwengu wote unamfuata.”
Farizeji so torej med seboj govorili: » [Ali] ne zaznate, kako ničesar ne prevladate? Glejte, svet je odšel za njim.«
20 Kulikuwa na Wagiriki kadhaa miongoni mwa watu waliokuwa wamefika Yerusalemu kuabudu wakati wa sikukuu hiyo.
In med njimi so bili neki Grki, ki so ob prazniku prišli gor oboževat.
21 Hao walimwendea Filipo, mwenyeji wa Bethsaida katika Galilaya, wakasema, “Mheshimiwa, tunataka kumwona Yesu.”
Isti so torej prišli k Filipu, ki je bil iz Betsajde v Galileji in ga prosili, rekoč: »Gospod, mi bi videli Jezusa.«
22 Filipo akaenda akamwambia Andrea, nao wawili wakaenda kumwambia Yesu.
Filip prihaja ter pove Andreju in prav tako Andrej ter Filip povesta Jezusu.
23 Yesu akawaambia, “Saa ya kutukuzwa kwa Mwana wa Mtu imefika!
In Jezus jima je odgovoril, rekoč: »Ura je prišla, da naj bi bil Sin človekov poveličan.
24 Kweli nawaambieni, punje ya ngano hubaki punje tu isipokuwa ikianguka katika udongo na kufa. Kama ikifa, basi huzaa matunda mengi.
Resnično, resnično, povem vam: ›Razen če pšenično zrno ne pade na tla in ne umre, ostaja sámo; toda če umre, obrodi mnogo sadu.‹
25 Anayependa maisha yake, atayapoteza; anayeyachukia maisha yake katika ulimwengu huu, atayaweka kwa ajili ya uzima wa milele. (aiōnios g166)
Kdor ima rad svoje življenje, ga bo izgubil; kdor pa svoje življenje na tem svetu sovraži, ga bo ohranil za večno življenje. (aiōnios g166)
26 Anayetaka kunitumikia ni lazima anifuate, hivyo kwamba popote pale nilipo mimi ndipo na mtumishi wangu atakapokuwa. Mtu yeyote anayenitumikia Baba yangu atampa heshima.
Če katerikoli človek služi meni, naj mi sledi; in kjer sem jaz, tam bo tudi moj služabnik. Če katerikoli človek služi meni, ga bo moj Oče počastil.
27 “Sasa roho yangu imefadhaika, na niseme nini? Je, niseme: Baba, usiruhusu saa hii inifikie? Lakini ndiyo maana nimekuja—ili nipite katika saa hii.
Sedaj je moja duša vznemirjena in kaj naj rečem? ›Oče, reši me pred to uro.‹ Toda zaradi tega razloga sem prišel v to uro.
28 Baba, ulitukuze jina lako.” Hapo sauti ikasema kutoka mbinguni, “Nimelitukuza, na nitalitukuza tena.”
›Oče, proslavi svoje ime.‹« Tedaj je tja prišel glas iz nebes, rekoč: »Proslavil sem ga in ponovno ga bom proslavil.«
29 Umati wa watu waliokuwa wamesimama hapo walisikia sauti hiyo, na baadhi yao walisema, “Malaika ameongea naye!”
Množica torej, ki je stala poleg in to slišala, je rekla, da je zagrmelo; drugi so rekli: »Angel mu je govoril.«
30 Lakini Yesu akawaambia, “Sauti hiyo haikutokea kwa ajili yangu mimi, ila kwa ajili yenu.
Jezus je odgovoril in rekel: »Ta glas ni prišel zaradi mene, temveč zaradi vas.
31 Sasa ndio wakati wa ulimwengu huu kuhukumiwa; sasa mtawala wa ulimwengu huu atapinduliwa.
Sedaj je sodba tega sveta. Sedaj bo princ tega sveta izgnan ven.
32 Nami nitakapoinuliwa juu ya nchi nitamvuta kila mmoja kwangu.”
In jaz, če bom povzdignjen z zemlje, bom k sebi pritegnil vse ljudi.«
33 (Kwa kusema hivyo alionyesha atakufa kifo gani).
To je rekel, ker je naznanil, kakšne smrti naj bi umrl.
34 Basi, umati huo ukamjibu, “Sisi tunaambiwa na Sheria yetu kwamba Kristo atadumu milele. Wawezaje basi, kusema ati Mwana wa Mtu anapaswa kuinuliwa? Huyo Mwana wa Mtu ni nani?” (aiōn g165)
Množica mu je odgovorila: »Iz postave smo slišali, da Kristus ostaja večno; in kako praviš ti: ›Sin človekov mora biti dvignjen?‹ Kdo je ta Sin človekov?« (aiōn g165)
35 Yesu akawaambia, “Mwanga bado uko nanyi kwa muda mfupi. Tembeeni mngali mnao huo mwanga ili giza lisiwapate; maana atembeaye gizani hajui aendako.
Potem jim je Jezus rekel: »Še malo časa je z vami svetloba. Hodíte, dokler imate svetlobo, da ne bi nad vas prišla tema, kajti kdor hodi v temi, ne ve, kam gre.
36 Basi, wakati mnao huo mwanga uaminini ili mpate kuwa watu wa mwanga.” Baada ya kusema maneno hayo, Yesu alikwenda zake na kujificha mbali nao.
Dokler imate svetlobo, verujte v svetlobo, da boste lahko otroci svetlobe.« Te besede je govoril Jezus in odšel ter se skril pred njimi.
37 Ingawa Yesu alifanya miujiza hii yote mbele yao, wao hawakumwamini.
Toda čeprav je pred njimi storil toliko čudežev, kljub temu niso verovali vanj,
38 Hivyo maneno aliyosema nabii Isaya yakatimia: “Bwana, nani aliyeuamini ujumbe wetu? Na uwezo wa Bwana umedhihirishwa kwa nani?”
da se je lahko izpolnila beseda preroka Izaija, ki je govoril: ›Gospod, kdo je veroval našemu poročilu in komu se je razodel Gospodov laket?‹
39 Hivyo hawakuweza kuamini, kwani Isaya tena alisema:
Torej niso mogli verovati, zato ker je ta Izaija ponovno rekel:
40 “Mungu ameyapofusha macho yao, amezipumbaza akili zao; wasione kwa macho yao, wasielewe kwa akili zao; wala wasinigeukie, asema Bwana, ili nipate kuwaponya.”
›Oslepel je njihove oči in zakrknil njihovo srce, da ne bi mogli videti s svojimi očmi niti razumeti s svojim srcem in ne bi bili spreobrnjeni in bi jih jaz ne ozdravil.‹
41 Isaya alisema maneno haya kwa sababu aliuona utukufu wa Yesu, akasema habari zake.
Te besede je izrekel Izaija, ko je videl njegovo slavo in govoril o njem.
42 Hata hivyo, wengi wa viongozi wa Wayahudi walimwamini Yesu. Lakini kwa sababu ya Mafarisayo, hawakumkiri hadharani kwa kuogopa kwamba watatengwa na sunagogi.
Vendar so tudi med visokimi vladarji mnogi verovali vanj, toda zaradi farizejev ga niso priznali, da ne bi bili izločeni iz sinagoge,
43 Walipendelea kusifiwa na watu kuliko kusifiwa na Mungu
kajti bolj so ljubili hvalo ljudi kakor Božjo hvalo.
44 Kisha Yesu akasema kwa sauti kubwa, “Mtu aliyeniamini, haniamini mimi tu, ila anamwamini pia yule aliyenituma.
Jezus je zaklical in rekel: »Kdor veruje vame, ne veruje vame, temveč v tistega, ki me je poslal.
45 Anayeniona mimi anamwona pia yule aliyenituma.
In kdor vidi mene, vidi tistega, ki me je poslal.
46 Mimi ni mwanga, nami nimekuja ulimwenguni ili wote wanaoniamini wasibaki gizani.
Prišel sem, svetloba na svet, da kdorkoli veruje vame, ne bi ostal v temi.
47 Anayeyasikia maneno yangu lakini hayashiki mimi sitamhukumu; maana sikuja kuhukumu ulimwengu bali kuuokoa.
In če katerikoli človek sliši moje besede in ne veruje, ga ne sodim jaz, kajti nisem prišel, da svet sodim, temveč da svet rešim.
48 Asiyeyashika maneno yangu anaye wa kumhukumu: neno lile nililosema ni hakimu wake siku ya mwisho.
Kdor zavrača mene in ne sprejema mojih besed, ima nekoga, ki ga sodi. Beseda, ki sem jo govoril, ta ista ga bo sodila na poslednji dan.
49 Mimi sikunena kwa mamlaka yangu mwenyewe, ila Baba aliyenituma ndiye aliyeniamuru niseme nini na niongee nini.
Kajti nisem govoril sam od sebe, temveč Oče, ki me je poslal, mi je dal zapoved, kaj naj rečem in kaj naj govorim.
50 Nami najua kuwa amri yake huleta uzima wa milele. Basi, mimi nasema tu yale Baba aliyoniagiza niyaseme.” (aiōnios g166)
In jaz vem, da je njegova zapoved večno življenje. Karkoli torej govorim, govorim tako, celó kakor mi je rekel Oče.« (aiōnios g166)

< Yohana 12 >