< Wahebrania 10 >

1 Sheria ya Wayahudi si picha kamili ya mambo yale halisi: ni kivuli tu cha mema yanayokuja. Dhabihu zilezile hutolewa daima, mwaka baada ya mwaka. Sheria yawezaje, basi, kwa njia ya dhabihu hizo, kuwafanya wale wanaoabudu wawe wakamilifu?
For the lawe which hath but the shadowe of good thynges to come and not the thynges in their awne fassion can never with ye sacryfises which they offer yere by yere continually make the comers thervnto parfayte.
2 Kama hao watu wanaomwabudu Mungu wangekuwa wametakaswa dhambi zao kweli, hawangejisikia tena kuwa na dhambi, na dhabihu hizo zote zingekoma.
For wolde not then those sacrifises have ceased to have bene offered because that the offerers once pourged shuld have had no moare conscieces of sinnes.
3 Lakini dhabihu hizo hufanyika kila mwaka kuwakumbusha watu dhambi zao.
Neverthelesse in those sacrifises is ther mencion made of synnes every yeare.
4 Maana damu ya fahali na mbuzi haiwezi kamwe kuondoa dhambi.
For it is vnpossible that the bloud of oxen and of gotes shuld take awaye synnes.
5 Ndiyo maana Kristo alipokuwa anakuja ulimwenguni, alimwambia Mungu: “Hukutaka dhabihu wala sadaka, lakini umenitayarishia mwili.
Wherfore when he commeth into the worlde he sayth: Sacrifice and offeringe thou woldest not have: but a bodie hast thou ordeyned me.
6 Sadaka za kuteketezwa au za kuondoa dhambi hazikupendezi.
In sacrifices and synne offerynges thou hast no lust.
7 Hapo nikasema: Niko hapa ee Mungu, tayari kufanya mapenzi yako kama ilivyoandikwa juu yangu katika kitabu cha Sheria.”
Then I sayde: Lo I come in the chefest of the boke it is written of me that I shuld doo thy will o god.
8 Kwanza alisema: “Hutaki, wala hupendezwi na dhabihu na sadaka, sadaka za kuteketezwa na za kuondoa dhambi.” Alisema hivyo ingawa sadaka hizi zote hutolewa kufuatana na Sheria.
Above when he had sayed sacrifice and offerynge and burnt sacrifices and synne offerynges thou woldest not have nether hast alowed (which yet are offered by the lawe)
9 Kisha akasema: “Niko hapa, ee Mungu, tayari kufanya mapenzi yako.” Hivyo Mungu alibatilisha dhabihu za zamani na mahali pake akaweka dhabihu nyingine moja.
and then sayde: Lo I come to do thy will o god: he taketh awaye the fyrst to stablisshe the latter.
10 Kwa kuwa Yesu Kristo alitimiza mapenzi ya Mungu, sisi tunatakaswa dhambi zetu kwa ile dhabihu ya mwili wake aliyotoa mara moja tu, ikatosha.
By the which will we are sanctified by the offeringe of the body of Iesu Christe once for all.
11 Kila kuhani Myahudi humhudumia Mungu kila siku, akitoa dhabibu zilezile mara nyingi, dhabibu ambazo haziwezi kuondoa dhambi.
And every prest is redy dayly ministrynge and ofte tymes offereth one maner of offerynge which can never take awaye synnes.
12 Lakini Kristo alitoa dhabihu moja tu kwa ajili ya dhambi, dhabihu ifaayo milele, kisha akaketi upande wa kulia wa Mungu.
But this man after he had offered one sacrifyce for synnes sat him doune for ever on the right honde of god
13 Huko anangoja mpaka adui zake watakapowekwa kama kibao chini ya miguu yake.
and from hence forth tarieth till his foes be made his fotestole.
14 Basi, kwa dhabihu yake moja tu, amewafanya kuwa wakamilifu milele wale wanaotakaswa dhambi zao.
For with one offerynge hath he made parfecte for ever them yt are sanctified.
15 Naye Roho Mtakatifu anatupa ushahidi wake. Kwanza anasema:
And ye holy goost also beareth vs recorde of this even when he tolde before:
16 “Hili ndilo agano nitakalofanya nao, katika siku zijazo, asema Bwana: Nitaweka sheria zangu mioyoni mwao, na kuziandika akilini mwao.”
This is the testament that I will make vnto them after those dayes sayth the lorde. I will put my lawes in their hertes and in their mynde I will write them
17 Kisha akaongeza kusema: “Sitakumbuka tena dhambi zao, wala vitendo vyao vya uhalifu.”
and their synnes and iniquyties will I remember no moare.
18 Basi, dhambi zikisha ondolewa, hakutakuwa na haja tena ya kutoa dhabihu za kuondoa dhambi.
And where remission of these thinges is there is no moare offerynge for synne.
19 Basi, ndugu, kwa damu ya Yesu tunapewa moyo thabiti wa kuingia Mahali Patakatifu.
Seynge brethren that by the meanes of the bloud of Iesu we maye be bolde to enter into that holy place
20 Yeye ametufungulia njia mpya na yenye uzima kupitia lile pazia, yaani kwa njia ya mwili wake mwenyewe.
by the newe and livynge waye which he hath prepared for vs through the vayle that is to saye by his flesshe.
21 Basi, tunaye kuhani maarufu aliye na mamlaka juu ya nyumba ya Mungu.
And seynge also that we have an hye prest which is ruler over ye housse of god
22 Kwa hiyo tumkaribie Mungu kwa moyo mnyofu na imani timilifu, kwa mioyo iliyotakaswa dhamiri mbaya, na kwa miili iliyosafishwa kwa maji safi.
let vs drawe nye with a true herte in a full fayth sprynckeled in oure hertes from an evyll conscience and wesshed in oure bodies with pure water
23 Tushikilie imara tumaini lile tunalokiri, maana Mungu aliyefanya ahadi zake ni mwaminifu.
and let vs kepe the profession of oure hope with oute waveringe (for he is faythfull that promysed)
24 Tujitahidi kushughulikiana kwa ajili ya kuongezeana bidii ya kupendana na kutenda mema.
and let vs consyder one another to provoke vnto love and to good workes:
25 Tusiache ile desturi ya kukutana pamoja, kama vile wengine wanavyofanya. Bali tunapaswa kusaidiana kwani, kama mwonavyo, Siku ile ya Bwana inakaribia.
and let vs not forsake the felishippe that we have amoge oure selves as the maner of some is: but let vs exhorte one another and that so moche the more because ye se that the daye draweth nye.
26 Maana, tukiendelea kutenda dhambi makusudi baada ya kufahamu ukweli, hakuna dhabihu iwezayo kutolewa tena kwa ajili ya kuondoa dhambi.
For yf we synne willyngly after that we have receaved the knowledge of the trueth there remayneth no more sacrifice for synnes
27 Linalobaki ni kungojea tu kwa hofu hukumu ya Mungu na moto mkali utakaowaangamiza wote wanaompinga.
but a fearfull lokynge for iudgement and violent fyre which shall devoure the adversaries
28 Mtu yeyote asiyeitii Sheria ya Mose, huuawa bila ya huruma kukiwa na ushahidi wa watu wawili au watatu.
He that despiseth Moses lawe dyeth with out mercy vnder two or thre witnesses.
29 Je, mtu yule anayempuuza Mwana wa Mungu na kuidharau damu ya agano la Mungu iliyomtakasa, mtu anayemtukana Roho wa Mungu, anastahili kupata adhabu kali ya namna gani?
Of how moche sorer punyshment suppose ye shall he be counted worthy which treadeth vnderfote the sonne of god: and counteth the bloude of the testament as an vnholy thynge wherwith he was sanctified and doth dishonoure to the sprete of grace.
30 Maana tunamfahamu yule aliyesema, “Mimi nitalipiza kisasi, mimi nitalipiza,” na ambaye alisema pia, “Bwana atawahukumu watu wake.”
For we knowe him that hath sayde vengeaunce belongeth vnto me I will recompence sayth the lorde. And agayne: the lorde shall iudge his people.
31 Kuanguka mikononi mwa Mungu aliye hai ni jambo la kutisha mno!
It is a fearfull thynge to faule into the hondes of the livynge God.
32 Kumbukeni yaliyotokea siku zile za kwanza mlipoangaziwa mwanga wa Mungu. Ingawa siku zile mlipatwa na mateso mengi, ninyi mlistahimili.
Call to remebraunce the dayes that are passed in the which after ye had receaved light ye endured a greate fyght in adversities
33 Mara nyingine mlitukanwa na kufedheheshwa hadharani; mara nyingine mlikuwa radhi kuungana na wale walioteswa namna hiyohiyo.
partly whill all men wondred and gased at you for the shame and trioulacion that was done vnto you and partly whill ye became companyons of the which so passed their tyme.
34 Mlishiriki mateso ya wafungwa, na mliponyang'anywa mali yenu mlistahimili kwa furaha, maana mlijua kwamba mnayo mali bora zaidi na ya kudumu milele.
For ye suffered also with my bondes and toke a worth the spoylynge of youre goodes and that with gladnes knowynge in youre selves how that ye had in heven a better and an endurynge substaunce
35 Basi, msipoteze uhodari wenu, maana utawapatieni tuzo kubwa.
Cast not awaye therfore youre confidence which hath great rewarde to recopence.
36 Mnahitaji kuwa na uvumilivu, ili mweze kufanya anayotaka Mungu na kupokea kile alichoahidi.
For ye have nede of paciece that after ye have done ye will of god ye myght receave the promes.
37 Maana kama yasemavyo Maandiko: “Bado kidogo tu, na yule anayekuja, atakuja, wala hatakawia.
For yet a very lytell whyle and he that shall come will come and will not tary.
38 Lakini mtu wangu aliye mwadilifu ataamini na kuishi; walakini akirudi nyuma, mimi sitapendezwa naye.”
But the iust shall live by faith. And yf he withdrawe him silfe my soule shall have no pleasure in him.
39 Basi, sisi hatumo miongoni mwa wale wanaorudi nyuma na kupotea, ila sisi tunaamini na tunaokolewa.
We are not whiche withdrawe oure selves vnto dampnacio but partayne to fayth to the wynnynge of the soule.

< Wahebrania 10 >