< Matendo 4 >

1 Petro na Yohane walipokuwa bado wanawahutubia watu, makuhani na mkuu wa walinzi wa Hekalu pamoja na Masadukayo walifika.
And while they were talking to the people, the priests and the captain of the Temple and the Sadducees came up to them,
2 Walikasirika sana, maana hao mitume walikuwa wanawahubiria watu kwamba Yesu alifufuka, jambo ambalo linaonyesha wazi kwamba wafu watafufuka.
Being greatly troubled because they were teaching the people and preaching Jesus as an example of the coming back from the dead.
3 Basi, waliwatia nguvuni na kwa kuwa usiku ulikuwa umekaribia, wakawaweka chini ya ulinzi mpaka kesho yake.
And they took them and put them in prison till the morning, for it was now evening.
4 Lakini wengi kati ya wale waliosikia ujumbe wao waliamini, na idadi ya waumini ikawa imefika karibu elfu tano.
But a number of those who gave hearing to the word had faith; and they were now about five thousand.
5 Kesho yake, viongozi wa Wayahudi, wazee na walimu wa Sheria, walikusanyika pamoja huko Yerusalemu.
And on the day after, the rulers and those in authority and the scribes came together in Jerusalem;
6 Walikutana pamoja na Anasi, Kayafa, Yohane, Aleksanda na wengine waliokuwa wa ukoo wa Kuhani Mkuu.
And Annas, the high priest, was there, and Caiaphas and John and Alexander, and all the relations of the high priest.
7 Waliwasimamisha mitume mbele yao, wakawauliza, “Ninyi mmefanya jambo hili kwa nguvu gani na kwa jina la nani?”
Then sending for Peter and John, they said, By what power and in whose name have you done this?
8 Hapo, Petro, akiwa amejawa na Roho Mtakatifu, akawaambia, “Viongozi na wazee wa watu!
Then Peter, being full of the Holy Spirit, said to them, O you rulers of the people and men of authority,
9 Ikiwa mnatuuliza leo juu ya kile kitendo chema alichofanyiwa yule mtu aliyekuwa kiwete na jinsi alivyopata kuwa mzima,
If we are questioned today about a good work done to a man who was ill, as to how he has been made well,
10 basi, ninyi na watu wote wa Israeli mnapaswa kujua kwamba mtu huyu anasimama mbele yenu leo, mzima kabisa, kwa nguvu ya jina lake Yesu wa Nazareti ambaye ninyi mlimsulubisha, lakini Mungu akamfufua kutoka wafu.
Take note, all of you, and all the people of Israel, that in the name of Jesus Christ of Nazareth, whom you put to death on the cross, whom God gave back from the dead, even through him is this man now before you completely well.
11 Huyu ndiye ambaye Maandiko Matakatifu yanasema: Jiwe mlilokataa ninyi waashi, sasa limekuwa jiwe kuu la msingi.
He is the stone which you builders had no use for, but which has been made the chief stone of the building.
12 Wokovu haupatikani kwa mtu mwingine yeyote, kwa maana duniani pote, binadamu hawakupewa jina la mtu mwingine ambaye sisi tunaweza kuokolewa naye.”
And in no other is there salvation: for there is no other name under heaven, given among men, through which we may have salvation.
13 Hao wazee wa baraza, wakiwa wanajua kwamba Petro na Yohane walikuwa watu wasio na kisomo wala elimu yoyote, walishangaa juu ya jinsi walivyosema kwa uhodari. Wakatambua kwamba walikuwa wamejiunga na Yesu.
Now when they saw that Peter and John were without fear, though they were men of no education or learning, they were greatly surprised; and they took note of them that they had been with Jesus.
14 Lakini walipomwona yule mtu aliyeponywa amesimama pamoja nao, hawakuweza kusema kitu.
And, seeing that the man who had been made well was there with them, they were not able to say anything against it.
15 Hivyo, waliwaamuru watoke nje ya baraza, nao wakabaki ndani wakizungumza kwa faragha.
But when they had given them orders to go out of the Sanhedrin, they had a discussion among themselves,
16 Wakaulizana, “Tufanye nini na watu hawa? Kila mtu anayeishi Yerusalemu anajua kwamba mwujiza huu wa ajabu umefanyika, nasi hatuwezi kukana jambo hilo.
Saying, What are we to do with these men? for certainly it is clear to all who are living in Jerusalem that a most important sign has been done by them, and it is not possible to say that it is not so.
17 Lakini ili tupate kuzuia jambo hili lisienee zaidi kati ya watu, tuwaonye wasiongee na mtu yeyote kwa jina la Yesu.”
But so that it may not go farther among the people, let us put them in fear of punishment if they say anything in future in this name.
18 Kwa hiyo wakawaita tena ndani, wakawaonya wasiongee tena hadharani, wala kufundisha kwa jina la Yesu.
And they sent for them, and gave them orders not to make statements or give teaching in the name of Jesus.
19 Lakini Petro na Yohane wakawajibu, “Amueni ninyi wenyewe kama ni haki mbele ya Mungu kuwatii ninyi kuliko kumtii yeye.
But Peter and John in answer said to them, It is for you to say if it is right in the eyes of God to give attention to you more than to God:
20 Kwa maana hatuwezi kuacha kusema juu ya mambo yale tuliyoyaona na kuyasikia.”
For it is not possible for us to keep from saying what we have seen and have knowledge of.
21 Basi, hao wazee wa Baraza wakawaonya kwa ukali zaidi, halafu wakawaacha huru. Hawakuweza kuwapa adhabu kwa sababu watu wote walikuwa wakimtukuza Mungu kwa sababu ya tukio hilo.
And when they had said more sharp words to them, they let them go, not seeing what punishment they might give them, because of the people; for all men were giving praise to God for what had taken place.
22 Huyo mtu aliyeponywa alikuwa na umri wa miaka zaidi ya arobaini.
For the man on whom this act of power was done was more than forty years old.
23 Mara tu walipoachwa huru, Petro na Yohane walirudi kwa wenzao, wakawaeleza yale waliyoambiwa na makuhani wakuu na wazee.
And when they had been made free, they came back to their friends, and gave an account of all the things which the chief priests and the authorities had said to them.
24 Waliposikia habari hiyo waliungana pamoja katika kumwomba Mungu wakisema, “Bwana, wewe ni Muumba wa mbingu na nchi, bahari na vyote vilivyomo!
And hearing it, they all, with one mind, made prayer to God and said, O Lord, maker of heaven and earth and the sea and all things in them:
25 Ndiwe uliyemfanya mtumishi wako, babu yetu Daudi, aseme kwa nguvu ya Roho Mtakatifu: Kwa nini mataifa yameghadhibika? Mbona watu wamefanya mipango ya bure?
Who has said, by the Holy Spirit, through the mouth of our father David your servant, Why are the nations so violently moved, and why are the thoughts of the people so foolish?
26 Wafalme wa dunia walijiweka tayari, na watawala walikutana pamoja, ili kumwasi Bwana na Kristo wake.
The kings of the earth were lifted up, the rulers came together, against the Lord, and against his Christ:
27 “Maana, kwa hakika, ndivyo Herode, Pontio Pilato, watu wa Israeli na watu wa mataifa walivyokutanika papa hapa mjini, kumpinga Yesu Mtumishi wako Mtakatifu ambaye umemtia mafuta.
For, truly, in this town, against your holy servant, Jesus, who was marked out by you as Christ, Herod, and Pontius Pilate, with the Gentiles and the people of Israel, came together,
28 Naam, walikutana ili wafanye yale ambayo ulikusudia na kupanga tangu mwanzo kwa uwezo wako na mapenzi yako.
To do that which had been fixed before by your hand and your purpose.
29 Lakini sasa, ee Bwana, angalia vitisho vyao. Utuwezeshe sisi watumishi wako kuhubiri neno lako kwa uhodari.
And now, Lord, take note of their cruel words, and give your servants power to be preachers of your word without fear,
30 Nyosha mkono wako uponye watu. Fanya ishara na maajabu kwa jina la Yesu Mtumishi wako Mtakatifu.”
While your hand is stretched out to do works of mercy; so that signs and wonders may be done through the name of your holy servant Jesus.
31 Walipomaliza kusali, pale mahali walipokuwa wamekutanika pakatikiswa, nao wote wakajazwa Roho Mtakatifu. Wote wakaanza kuhubiri neno la Mungu bila uoga.
And when their prayer was ended, the place where they were was violently moved, and they all became full of the Holy Spirit, preaching the word of God without fear.
32 Jumuiya yote ya waumini ilikuwa moyo mmoja na roho moja. Hakuna hata mmoja aliyekuwa na kitu chochote akakiweka kuwa mali yake binafsi, ila waligawana vyote walivyokuwa navyo.
And all those who were of the faith were one in heart and soul: and not one of them said that any of the things which he had was his property only; but they had all things in common.
33 Mitume walishuhudia kwa nguvu nyingi kufufuka kwa Bwana Yesu, naye Mungu akawapa baraka nyingi.
And with great power the Apostles gave witness of the coming back of the Lord Jesus from the dead; and grace was on them all.
34 Hakuna mtu yeyote aliyetindikiwa kitu, maana waliokuwa na mashamba au nyumba walikuwa wanaviuza
And no one among them was in need; for everyone who had land or houses, exchanging them for money, took the price of them,
35 na kuwakabidhi mitume fedha hizo, zikagawiwa kila mmoja kadiri ya mahitaji yake.
And put it at the feet of the Apostles for distribution to everyone as he had need.
36 Kulikuwa na Mlawi mmoja, mzaliwa wa Kupro, jina lake Yosefu, ambaye mitume walimwita jina Barnaba (maana yake, “Mtu mwenye kutia moyo”).
And Joseph, who was given by the Apostles the name of Barnabas (the sense of which is, Son of comfort), a Levite and a man of Cyprus by birth,
37 Yeye pia alikuwa na shamba lake, akaliuza; akazichukua zile fedha, akawakabidhi mitume.
Having a field, got money for it and put the money at the feet of the Apostles.

< Matendo 4 >