< Matendo 18 >

1 Baada ya hayo, Paulo aliondoka Athene, akaenda Korintho.
After that Paul departed from Attens and came to Corinthu
2 Huko Korintho, alimkuta Myahudi mmoja aitwaye Akula, mzaliwa wa Ponto. Akula pamoja na mkewe aitwaye Priskila, walikuwa wamerudi kutoka Italia siku hizohizo kwa sababu Kaisari Klaudio alikuwa ameamuru Wayahudi wote waondoke Roma. Paulo alikwenda kuwaona,
and founde a certayne Iewe named Aquila borne in Ponthus latly come from Italie wt his wyfe Priscilla (because that the Emperour Claudius had comaunded all Iewes to departe fro Rome) and he drewe vnto them.
3 na kwa vile wao walikuwa mafundi wa kushona mahema kama alivyokuwa yeye, Paulo alikaa nao akafanya kazi.
And because he was of the same crafte he abode with them and wrought: their crafte was to make tentes.
4 Kila Sabato alifanya majadiliano katika sunagogi akijaribu kuwavuta Wayahudi na Wagiriki.
And he preached in ye synagoge every saboth daye and exhorted the Iewes and the gentyls.
5 Baada ya Sila na Timotheo kuwasili kutoka Makedonia, Paulo alianza kutumia wakati wake wote kwa ajili ya kuhubiri, akawathibitishia Wayahudi kwamba Yesu ndiye Kristo.
When Sylas and Timotheus were come from Macedonia Paul was constrayned by the sprete to testifie to the Iewes that Iesus was very Christ.
6 Walipompinga na kuanza kumtukana, aliyakung'uta mavazi yake mbele yao akisema, “Mkipotea ni shauri lenu wenyewe; mimi sina lawama yoyote juu ya jambo hilo. Na tangu sasa nitawaendea watu na mataifa mengine.”
And whe they sayde cotrary and blasphemed he shoke his rayment and sayde vnto the: youre bloud apon youre awne heeddes and fro hence forth I goo blamelesse vnto ye gentyls.
7 Basi, akatoka hapo akaenda kukaa nyumbani kwa mtu mmoja mcha Mungu aitwaye Tito Yusto. Nyumba yake Tito ilikuwa karibu na lile sunagogi.
And he departed thence and entred into a certayne manes housse named Iustus a worshiper of god whose housse ioyned harde to ye synagoge.
8 Lakini Krispo, mkuu wa sunagogi, alimwamini Bwana yeye pamoja na jamaa yake yote. Wakorintho wengi waliusikiliza ujumbe huo, wakaamini na kubatizwa.
How be it one Crispus ye chefe rular of the synagoge beleved on ye lorde with all his housholde and many of the Corinthias gave audience and beleved and were baptised.
9 Siku moja usiku, Bwana alimwambia Paulo katika maono: “Usiogope, endelea kuhubiri tu bila kufa moyo,
Then spake the lorde to Paul in the nyght by a vision: be not afrayde but speake and holde not thy peace:
10 maana mimi niko pamoja nawe. Hakuna mtu atakayejaribu kukudhuru maana hapa mjini pana watu wengi walio upande wangu.”
for I am with the and no man shall invade the that shall hurte the. For I have moche people in this cite.
11 Basi, Paulo alikaa huko akifundisha neno la Mungu kati yao kwa muda wa mwaka mmoja na nusu.
And he continued there a yeare and sixe monethes and taught them the worde of God.
12 Lakini wakati Galio alipokuwa mkuu wa mkoa wa Akaya, Wayahudi walimvamia Paulo kwa pamoja na kumpeleka mahakamani.
When Gallio was rular of the countre of Acaia the Iewes made insurreccion with one accorde agaynst Paul and brought him to the iudgement seate
13 Wakasema, “Tunamshtaki mtu huyu kwa sababu ya kuwashawishi watu wamwabudu Mungu kwa namna inayopingana na Sheria.”
saying: this felow counceleth men to worship God contrary to ye lawe.
14 Kabla tu Paulo hajaanza kusema, Galio aliwaambia Wayahudi, “Sikilizeni enyi Wayahudi! Kama kweli jambo hili lingekuwa juu ya uhalifu au uovu ningekuwa tayari kuwasikilizeni.
And as Paul was about to open his mouth Gallio sayde vnto ye Iewes: yf it were a matter of wronge or an evyll dede (o ye Iewes) reason wolde that I shuld heare you:
15 Lakini kama ni shauri la ubishi kuhusu maneno na majina ya Sheria yenu, amueni ninyi wenyewe. Mimi sitaki kuwa hakimu wa mambo haya!”
but yf it be a question of wordes or of names or of youre lawe loke ye to it youre selves. For I wilbe no iudge in soche maters
16 Basi, akawafukuza kutoka mahakamani.
and he drave them from the seate.
17 Nao wote wakamkamata Sosthene ambaye alikuwa kiongozi wa sunagogi, wakampiga palepale mbele ya mahakama. Lakini Galio hakujali kitendo hicho hata kidogo.
Then toke all the Grekes Sostenes the chefe rular of the synagoge and smote him before the iudges seate. And Gallio cared for none of tho thinges.
18 Paulo alikaa bado na wale ndugu huko Korintho kwa siku nyingi. Kisha aliwaaga, akapanda meli kwenda Siria pamoja na Priskila na Akula. Huko Kenkrea, alinyoa nywele zake kwa sababu ya nadhiri aliyokuwa ameweka.
Paul after this taryed there yet a good whyle and then toke his leave of the brethren and sayled thence into Ciria Priscilla and Aquila accompanyinge him. And he shore his heed in Cenchrea for he had a vowe.
19 Walifika Efeso na hapo Paulo aliwaacha Priskila na Akula, akaenda katika sunagogi, akajadiliana na Wayahudi.
And he came to Ephesus and lefte them there: but he him selfe entred into the synagoge and reasoned with the Iewes.
20 Walimwomba akae nao muda mrefu zaidi, lakini hakupenda.
When they desyred him to tary longer tyme with the he consented not
21 Bali alipokuwa anaondoka, alisema, “Mungu akipenda nitakuja kwenu tena.” Akaondoka Efeso kwa meli.
but bad the fare well sayinge. I must nedes at this feast that cometh be in Ierusalem: but I will returne agayne vnto you yf God will. And he departed from Ephesus
22 Meli ilitia nanga Kaisarea, naye Paulo akaenda Yerusalemu kulisalimia lile kanisa, kisha akaenda Antiokia.
and came vnto Cesarea: and ascended and saluted the congregacion and departed vnto Antioche
23 Alikaa huko muda mfupi, halafu akaendelea na safari kwa kupitia sehemu za Galatia na Frugia akiwatia moyo wafuasi wote.
and when he had taryed there a whyle he departed. And went over all the countre of Galacia and Phrigia by order strengthynge all the disciples.
24 Myahudi mmoja aitwaye Apolo, mzaliwa wa Aleksandria, alifika Efeso. Alikuwa mtu mwenye ufasaha wa kuongea na mwenye ujuzi mkubwa wa Maandiko Matakatifu.
And a certayne Iewe named Apollos borne at Alexandria came to Ephesus an eloquent man and myghty in the scriptures.
25 Alikuwa amefundishwa juu ya hiyo njia ya Bwana, na akiwa motomoto, aliongea juu ya habari za Yesu. Akafundisha kwa usahihi ingawa alikuwa amepata ubatizo wa Yohane tu.
The same was informed in the waye of the Lorde and he spake fervently in the sprete and taught diligently the thinges of the Lorde and knewe but the baptim of Iohn only.
26 Priskila na Akula walipomsikia akiongea kwa uhodari ndani ya sunagogi, walimchukua kwao wakamfundisha hiyo Njia ya Mungu kwa usahihi zaidi.
And the same began to speake boldely in the synagoge. And when Aquila and Priscilla had hearde him: they toke him vnto them and expounded vnto him the waye of God more perfectly.
27 Apolo alipoamua kwenda Akaya, wale ndugu walimtia moyo kwa kuwaandikia wafuasi kule Akaya wampokee. Alipofika huko, aliweza kwa msaada wa neema ya Mungu, kuwasaidia sana wale ndugu waliopata kuwa waumini;
And when he was disposed to goo into Acaia the brethren wrote exhortynge the disciples to receave him. After he was come thyther he holpe them moche which had beleved thorowe grace.
28 kwa maana aliendelea kwa uhodari kuwashinda Wayahudi hadharani akithibitisha kwa Maandiko Matakatifu kuwa Yesu ni Kristo.
And myghtely he overcame the Iewes and that openly shewynge by the scriptures that Iesus was Christ.

< Matendo 18 >