< Warumi 10 >

1 Ndugu, nia ya moyo wangu na ombi langu kwa Mungu ni kwa ajili yao, kwa ajili ya wokovu wao.
Brethren, the delight of my own heart and my supplication which [I address] to God for them is for salvation.
2 Kwa kuwa nawashuhudia kwamba wanajuhudi kwa ajili ya Mungu, lakini si kwa ajili ya ufahamu.
For I bear them witness that they have zeal for God, but not according to knowledge.
3 Kwa kuwa hawajui haki ya Mungu, na wanatafuta kujenga haki yao wenyewe. Hawakuwa watiifu kwa haki ya Mungu.
For they, being ignorant of God's righteousness, and seeking to establish their own [righteousness], have not submitted to the righteousness of God.
4 Kwa kuwa Kristo ndiye utimilifu wa sheria kwa ajili ya haki ya kila mtu aaminiye.
For Christ is [the] end of law for righteousness to every one that believes.
5 Kwa kuwa Musa anaandika kuhusu haki ambayo huja kutokana na sheria: “Mtu ambaye hutenda haki ya sheria ataishi kwa haki hii.”
For Moses lays down in writing the righteousness which is of the law, The man who has practised those things shall live by them.
6 Lakini haki ambayo inatokana na imani husema hivi, “Usiseme moyoni mwako, 'Nani atapaa kwenda mbinguni?' (Hii ni kumleta Kristo chini).
But the righteousness of faith speaks thus: Do not say in thine heart, Who shall ascend to the heavens? that is, to bring Christ down;
7 Na usiseme, 'Nani atashuka katika shimo?”' (Hii ni, kumleta Kristo juu kutoka kwa wafu). (Abyssos g12)
or, Who shall descend into the abyss? that is, to bring up Christ from among [the] dead. (Abyssos g12)
8 Lakini inasema nini? “Neno liko karibu na wewe, katika kinywa chako na katika moyo wako.” Hilo ni neno la imani, ambalo tunatangaza.
But what says it? The word is near thee, in thy mouth and in thy heart: that is, the word of faith, which we preach:
9 Kwa kuwa kama kwa kinywa chako unamkiri Yesu ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako kwamba Mungu alimfufua kutoka kwa wafu, utaokoka.
that if thou shalt confess with thy mouth Jesus as Lord, and shalt believe in thine heart that God has raised him from among [the] dead, thou shalt be saved.
10 Kwa kuwa kwa moyo mtu huamini na kupata haki, na kwa kinywa hukiri na kupata wokovu.
For with [the] heart is believed to righteousness; and with [the] mouth confession made to salvation.
11 Kwa kuwa andiko lasema, “Kila amwaminiye hata aibika.”
For the scripture says, No one believing on him shall be ashamed.
12 kwa kuwa hakuna tofauti kati ya Myahudi na Myunani. Kwa kuwa Bwana yule yule ni Bwana wa wote, na ni tajiri kwa wote wamwitao.
For there is no difference of Jew and Greek; for the same Lord of all [is] rich towards all that call upon him.
13 Kwa kuwa kila mtu ambaye huliitia jina la Bwana ataokoka.
For every one whosoever, who shall call on the name of the Lord, shall be saved.
14 Kwa jinsi gani wanaweza kumwita yeye ambaye hawajamwamini? Na jinsi gani wanaweza kuamini katika yeye ambaye hawajamsikia? Na watasikiaje pasipo muhubiri?
How then shall they call upon him in whom they have not believed? and how shall they believe on him of whom they have not heard? and how shall they hear without one who preaches?
15 Na jinsi gani wanaweza kuhubiri, isipokuwa wametumwa? - Kama ilivyoandikwa, “Jinsi gani ni mizuri miguu ya wale ambao wanatangaza habari za furaha za mambo mema!”
and how shall they preach unless they have been sent? according as it is written, How beautiful the feet of them that announce glad tidings of peace, of them that announce glad tidings of good things!
16 Lakini wote hawakusikiliza injili. Kwa kuwa Isaya hunena, “Bwana, ni nani aliyesikia ujumbe wetu?”
But they have not all obeyed the glad tidings. For Esaias says, Lord, who has believed our report?
17 Hivyo imani huja kutokana na kusikia, na kusikia kwa neno la Kristo.
So faith then [is] by a report, but the report by God's word.
18 Lakini nasema, “Je hawakusikia?” Ndiyo, kwa hakika sana. “Sauti yao imekwisha toka nje katika nchi yote, na maneno yao kwenda miisho ya dunia.”
But I say, Have they not heard? Yea, surely, Their voice has gone out into all the earth, and their words to the extremities of the habitable world.
19 Zaidi ya yote, Ninasema, “Je Israel hakujua?” Kwanza Musa hunena, “Nitawachokoza kuwatia wivu kwa watu ambao si taifa. Kwa njia ya taifa lisilo na uelewa, nitawachochea hadi mkasirike.”
But I say, Has not Israel known? First, Moses says, I will provoke you to jealousy through [them that are] not a nation: through a nation without understanding I will anger you.
20 Na Isaya ni jasiri sana na husema, “Nilipatikana na wale ambao hawakunitafuta. Nilionekana kwa wale ambao hawakunihitaji.”
But Esaias is very bold, and says, I have been found by those not seeking me; I have become manifest to those not inquiring after me.
21 Lakini kwa Israel husema, “Siku zote nilinyoosha mikono yangu kwa wasiotii na kwa watu wagumu.”
But unto Israel he says, All the day long I have stretched out my hands unto a people disobeying and opposing.

< Warumi 10 >