< Zaburi 81 >

1 Mwimbieni Mungu aliye nguvu yetu kwa sauti; pigeni kelele za furaha kwa Mungu wa Yakobo.
Dem Musikmeister, nach der gattitischen. Von Asaph. Jauchzet Gott, der unsere Stärke ist, jubelt dem Gotte Jakobs zu!
2 Imbeni wimbo na pigeni matari, kinubi chenye sauti nzuri pamoja na kinanda.
Stimmt Gesang an und laßt die Handpauke ertönen, die liebliche Zither samt der Harfe.
3 Pigeni panda mwandamo wa mwezi, katika siku ya mbalamwezi, mwanzoni mwa sikukuu.
Stoßt am Neumond in die Posaune, am Vollmond auf den Tag unseres Festes.
4 Kwa kuwa ni agizo kwa Israeli, amri iliyotolewa na Mungu wa Yakobo.
Denn das ist eine Satzung für Israel, ein Recht des Gottes Jakobs.
5 Aliitoa kama maelekezo kwa Yusufu alipoenda katika nchi ya Misri, ambako nilisikia sauti ambayo sikuweza kuitambua:
Er hat es als ein Zeugnis in Joseph festgesetzt, als er gegen Ägypten auszog; eine Sprache, die ich zuvor nicht kannte, vernehme ich:
6 “Niliutua mzigo kutoka mabegani mwake; mikono yake ilipumzishwa kubeba kikapu.
“Ich habe seinen Nacken von der Last befreit, seine Hände sind des Lastkorbes ledig.
7 Katika dhiki yako uliniita, nami nikakusaidia; nilikujibu kutoka katika wingu jeusi la radi. Nilikujaribu kwenye maji ya Meriba. (Selah)
“In der Not riefst du mich an und ich rettete dich; ich erhörte dich im Donnergewölk, prüfte dich am Haderwasser. (Sela)
8 Sikilizeni, watu wangu, nami nitawaonya, Israeli, kama tu ugalinisikiliza!
“Höre, mein Volk, damit ich dich vermahne, Israel, möchtest du auf mich hören!
9 Lazima kati yenu kusiwepo na mungu wa kigeni; haupaswi kumwabudu mungu wa kigeni.
“Es soll unter dir kein anderer Gott sein, einen fremden Gott darfst du nicht anbeten.
10 Mimi ni Yahwe niliyekutoa katika nchi ya Misri, fungua sana kinywa chako, nami nitakijaza.
“Ich, Jahwe, bin dein Gott, der dich aus Ägypten hergeführt hat: thue deinen Mund weit auf, damit ich ihn fülle!
11 Lakini watu wangu hawakusikiliza maneno yangu; Israeli hawakunitii.
“Aber mein Volk hörte nicht auf meine Stimme, und Israel hat mir nicht willfahrt.
12 Nikawaacha waende katika katika njia yao wenyewe ya ukaidi ili kwamba waweze kufanya kinachoonekana sahihi kwao.
“Da überließ ich sie der Verstocktheit ihres Herzens; sie wandelten nach ihren eigenen Anschlägen.
13 Oh, laiti watu wangu wangenisikiliza mimi; oh, watu wangu wangelitembea katika njia yangu.
“O daß doch mein Volk auf mich hören, Israel auf meinen Wegen wandeln wollte!
14 Kisha ningewatiisha adui zao haraka na kugeuzia mkono wangu dhidi ya watesi wao.
“Wie leicht wollte ich ihre Feinde demütigen und meine Hand gegen ihre Dränger wenden.
15 Wale wanaomchukia Yahwe katika hofu na waanguke chini mbele zake! Wawe wanyonge milele.
“Die Jahwe hassen, müßten ihm schmeicheln, und ihre Zeit sollte ewig währen.
16 Ningewalisha Israeli kwa ngano bora; Ningewatosheleza kwa asali itokayo mwambani.”
“Mit dem besten Weizen wollte ich ihn speisen und dich mit Honig aus dem Felsen sättigen.”

< Zaburi 81 >