< Zaburi 79 >

1 Zaburi ya Asafu. Mungu, Mataifa ya kigeni yameingia kwenye urithi wako; wamelinajisi hekalu lako takatifu; wameigeuza Yerusalemu kuwa chungu cha magofu.
A Psalm of Asaph. O God, nations have come into Thy inheritance, They have defiled Thy holy temple, They made Jerusalem become heaps,
2 Wamezitoa maiti za watumishi wako ziwe chakula cha ndege wa angani, miili ya watakatifu wako iwe chakula cha wanyama wa nchi.
They gave the dead bodies of Thy servants Food for the fowls of the heavens, The flesh of Thy saints For the wild beast of the earth.
3 Wamemwaga damu zao kama maji sehemu zote za Yesrusalemu, na hakuwepo wa kuwazika.
They have shed their blood As water round about Jerusalem, And there is none burying.
4 Sisi tumekuwa aibu kwa majirani zetu, tukidhihakiwa na kuzomewa na wale wanaotuzunguka.
We have been a reproach to our neighbours, A scorn and a derision to our surrounders.
5 Mpaka lini Yahwe? Utabaki kuwa na hasira milele? Ni kwa muda gani hasira yako ya wivu itawaka kama moto?
Till when, O Jehovah? art Thou angry for ever? Thy jealousy doth burn as fire.
6 Mwaga hasira yako juu ya mataifa ambayo hayakujui wewe na ufalme ambao hauliiti jina lako.
Pour Thy fury on the nations who have not known Thee, And on kingdoms that have not called in Thy name.
7 Kwa maana walimvamia Yakobo na waliharibu kijiji chake.
For [one] hath devoured Jacob, And his habitation they have made desolate.
8 Usiendelee kukumbuka dhambi za baba zetu dhidi yetu; matendo yako ya huruma yaje kwetu, maana tuko chini.
Remember not for us the iniquities of forefathers, Haste, let Thy mercies go before us, For we have been very weak.
9 Utusaidie, Mungu wa wokovu wetu, kwa ajili ya utukufu wa jina lako; utuokoe na usamehe dhambi zetu kwa ajili ya jina lako.
Help us, O God of our salvation, Because of the honour of Thy name, And deliver us, and cover over our sins, For Thy name's sake.
10 Kwa nini mataifa yalazimike kusema, “Mungu wao yuko wapi?” Damu ya watumishi wako ambayo ilimwagwa na ilipize kisasi juu ya mataifa mbele ya macho yako.
Why do the nations say, 'Where [is] their God?' Let be known among the nations before our eyes, The vengeance of the blood of Thy servants that is shed.
11 Kilio cha wafungwa na kije mbele zako; kwa uweza wa nguvu zako uwaweke ai wana wa mauti.
Let the groaning of the prisoner come in before Thee, According to the greatness of Thine arm, Leave Thou the sons of death.
12 Uwalipize majirani zetu vifuani mwao mara saba zaidi ya walivyo kutukana wewe, Bwana.
And turn Thou back to our neighbours, Sevenfold unto their bosom, their reproach, Wherewith they reproached Thee, O Lord.
13 Hivyo sisi watu wako na kondoo wa malisho yako tutakushukuru milele. Tutazisimulia sifa zako kwa vizazi vyote.
And we, Thy people, and the flock of Thy pasture, We give thanks to Thee to the age, To all generations we recount Thy praise!

< Zaburi 79 >