< Zaburi 78 >

1 Watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
Intellectus Asaph. [Attendite, popule meus, legem meam; inclinate aurem vestram in verba oris mei.
2 Nitafungua kinywa changu katika mifano; nitaimba kuhusu mambo yaliyofichika yahusuyo yaliyopita.
Aperiam in parabolis os meum; loquar propositiones ab initio.
3 Haya ni mambo ambayo tumeyasikia na kujifunza mambo ambayo mababu zetu wametuambia sisi. Hatutawaficha uzao wao.
Quanta audivimus, et cognovimus ea, et patres nostri narraverunt nobis.
4 Tutawaambia kizazi kijacho kuhusu sifa anazostahili Yahwe kwa matendo yake, nguvu zake, na maajabu ambayo ameyafanya.
Non sunt occultata a filiis eorum in generatione altera, narrantes laudes Domini et virtutes ejus, et mirabilia ejus quæ fecit.
5 Kwa kuwa yeye alianzisha agano la amri katika Yakobo na sheria maalumu katika Israeli. Yeye aliamuru mababu zetu kuwa walipaswa kuzifundisha kwa watoto wao.
Et suscitavit testimonium in Jacob, et legem posuit in Israël, quanta mandavit patribus nostris nota facere ea filiis suis:
6 Aliamuru hivi ili kwamba kizazi kijacho kiweze kuzijua amri zake, ili wawafundishe wana ambao bado hawajazaliwa.
ut cognoscat generatio altera: filii qui nascentur et exsurgent, et narrabunt filiis suis,
7 Kisha wangeweka tumaini lao katika Mungu na kutokusahau matendo yake bali wazishike amri zake.
ut ponant in Deo spem suam, et non obliviscantur operum Dei, et mandata ejus exquirant:
8 Ndipo wasingekuwa kama mababu zao, ambao walikuwa wakaidi na wenye uasi, kizazi ambacho mioyo yao haikuwa kamilifu, na ambao roho zao hazikuwa na nia thabiti na aminifu kwa Mungu.
ne fiant, sicut patres eorum, generatio prava et exasperans; generatio quæ non direxit cor suum, et non est creditus cum Deo spiritus ejus.
9 Waefraimu walikuwa na silaha na upinde, lakini walikimbia siku ya vita.
Filii Ephrem, intendentes et mittentes arcum, conversi sunt in die belli.
10 Hawakutunza agano na Mungu, na walikataa kutii sheria yake.
Non custodierunt testamentum Dei, et in lege ejus noluerunt ambulare.
11 Walisahau matendo yake, mambo ya ajabu ambayo yeye amewaonesha wao.
Et obliti sunt benefactorum ejus, et mirabilium ejus quæ ostendit eis.
12 Walisahau mambo ya ajabu aliyofayafanya machoni pa mababu zao katika nchi ya Misri, katika ardhi ya Soani.
Coram patribus eorum fecit mirabilia in terra Ægypti, in campo Taneos.
13 Aliigawa bahari na akawaongoza katikati ya bahari; aliyafanya maji yasimame kama kuta.
Interrupit mare, et perduxit eos, et statuit aquas quasi in utre:
14 Wakati wa mchana aliwaongoza kwa wingu na usiku wote kwa nuru ya moto.
et deduxit eos in nube diei, et tota nocte in illuminatione ignis.
15 Alipasua miamba jangwani, na aliwapa maji mengi, ya kutosha kujaza vina virefu vya bahari.
Interrupit petram in eremo, et adaquavit eos velut in abysso multa.
16 Alifanya maporomoko ya maji kutiririka tokea mwambani na aliyafanya maji yatiririke kama mito.
Et eduxit aquam de petra, et deduxit tamquam flumina aquas.
17 Lakini bado waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi dhidi ya Aliye Juu katika jangwa.
Et apposuerunt adhuc peccare ei; in iram excitaverunt Excelsum in inaquoso.
18 Walimjaribu Mungu mioyoni mwao kwa kuomba chakula cha kuwatosheleza hamu zao.
Et tentaverunt Deum in cordibus suis, ut peterent escas animabus suis.
19 Waliongea dhidi ya Mungu; walisema, “Kweli Mungu anaweza kuweka meza ya chakula kwa ajili yetu jangwani?
Et male locuti sunt de Deo; dixerunt: Numquid poterit Deus parare mensam in deserto?
20 Tazama, wakati alipoupiga mwamba, maji yalibubujika, mito ikafurika. Lakini anaweza kutoa mkate tena? Ataweza kuleta nyama kwa watu wake?”
quoniam percussit petram, et fluxerunt aquæ, et torrentes inundaverunt. Numquid et panem poterit dare, aut parare mensam populo suo?
21 Yahwe aliposikia haya, alikasirika; moto wake uliwaka dhidi ya Yakobo, hasira yake ikamshambulia Israeli,
Ideo audivit Dominus et distulit; et ignis accensus est in Jacob, et ira ascendit in Israël:
22 kwa sababu hawakumwamini Mungu na hawakuamini katika wokovu wake.
quia non crediderunt in Deo, nec speraverunt in salutari ejus.
23 Lakini yeye bado aliziamuru mbingu juu na kufungua milango ya mbingu.
Et mandavit nubibus desuper, et januas cæli aperuit.
24 Aliwanyeshea mana ili wale, na aliwapa nafaka kutoka mbinguni.
Et pluit illis manna ad manducandum, et panem cæli dedit eis.
25 Watu walikula mikate ya malaika. Aliwatumia chakula kingi.
Panem angelorum manducavit homo; cibaria misit eis in abundantia.
26 Alisababisha upepo wa mashariki kupiga mawinguni, na kwa uweza wake aliuongoza upepo wa kusini.
Transtulit austrum de cælo, et induxit in virtute sua africum.
27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, na ndege kama wingi wa mchanga wa baharini.
Et pluit super eos sicut pulverem carnes, et sicut arenam maris volatilia pennata.
28 Walianguka katikati ya kambi yao, na maeneo yote karibu na hema zao.
Et ceciderunt in medio castrorum eorum, circa tabernacula eorum.
29 Hivyo walikula na walishiba. Maana aliwapa kile walichokitamani sana.
Et manducaverunt, et saturati sunt nimis, et desiderium eorum attulit eis:
30 Lakini walikuwa bado hawajatosheka; chakula chao kilikuwa bado kinywani mwao.
non sunt fraudati a desiderio suo. Adhuc escæ eorum erant in ore ipsorum,
31 Ndipo hasira ya Mungu iliwashambulia na kuwaua wenye nguvu kati yao. Aliwaangusha chini vijana wa Israeli.
et ira Dei ascendit super eos: et occidit pingues eorum, et electos Israël impedivit.
32 Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
In omnibus his peccaverunt adhuc, et non crediderunt in mirabilibus ejus.
33 Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
Et defecerunt in vanitate dies eorum, et anni eorum cum festinatione.
34 Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
Cum occideret eos, quærebant eum et revertebantur, et diluculo veniebant ad eum.
35 Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.
Et rememorati sunt quia Deus adjutor est eorum, et Deus excelsus redemptor eorum est.
36 Lakini walimsifia tu kwa vinywa vyao na kumdanganya kwa maneno yao.
Et dilexerunt eum in ore suo, et lingua sua mentiti sunt ei;
37 Maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, na hawakuwa waaminifu kwa agano lake.
cor autem eorum non erat rectum cum eo, nec fideles habiti sunt in testamento ejus.
38 Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.
Ipse autem est misericors, et propitius fiet peccatis eorum, et non disperdet eos. Et abundavit ut averteret iram suam, et non accendit omnem iram suam.
39 Alikumbuka kuwa waliumbwa kwa mwili, upepo ambao hupita nao haurudi.
Et recordatus est quia caro sunt, spiritus vadens et non rediens.
40 Mara ngapi wameasi dhidi yake jangwani na kumuhuzunisha nyikani!
Quoties exacerbaverunt eum in deserto; in iram concitaverunt eum in inaquoso?
41 Tena na tena walimjaribu Mungu na wakamtilia mashaka Mtakatifu wa Israeli.
Et conversi sunt, et tentaverunt Deum, et sanctum Israël exacerbaverunt.
42 Hawakufikiria kuhusu uweza wake, jinsi alivyo waokoa dhidi ya adui
Non sunt recordati manus ejus, die qua redemit eos de manu tribulantis:
43 alipofanya ishara za kutisha katika Misri na maajabu yake katika konde la Soani.
sicut posuit in Ægypto signa sua, et prodigia sua in campo Taneos;
44 Aligeuza mito ya Wamisri kuwa damu ili wasipate kunywa kutoka katika vijito vyao.
et convertit in sanguinem flumina eorum, et imbres eorum, ne biberent.
45 Alituma makundi ya inzi yaliyowavamia na vyura ambao walisambaa katika nchi yao.
Misit in eos cœnomyiam, et comedit eos, et ranam, et disperdidit eos;
46 Aliwapa mazao yao panzi na kazi yao nzige.
et dedit ærugini fructus eorum, et labores eorum locustæ;
47 Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na miti ya mikuyu kwa mvua ya mawe zaidi.
et occidit in grandine vineas eorum, et moros eorum in pruina;
48 Aliinyeshea mifugo yao mvua ya mawe na alirusha radi ya umeme ikapiga mifugo yao. Ukali wa hasira yake ulielekea dhidi yao.
et tradidit grandini jumenta eorum, et possessionem eorum igni;
49 Alituma gadhabu, uchungu na taabu kama wakala aletaye maafa.
misit in eos iram indignationis suæ, indignationem, et iram, et tribulationem, immissiones per angelos malos.
50 Aliifanyia njia hasira yake; hakuwakinga dhidi ya kifo bali aliwakabidhi kwa pigo.
Viam fecit semitæ iræ suæ: non pepercit a morte animabus eorum, et jumenta eorum in morte conclusit:
51 Aliwaua wazaliwa wote wa kwanza katika Misri, wazaliwa wa kwanza wa nguvu zao katika mahema ya Hamu.
et percussit omne primogenitum in terra Ægypti; primitias omnis laboris eorum in tabernaculis Cham:
52 Aliwaongoza nje watu wake mwenyewe kama kondoo na aliwaelekeza kupitia jangwani kama kundi.
et abstulit sicut oves populum suum, et perduxit eos tamquam gregem in deserto:
53 Aliwaongoza salama na pasipo na woga, lakini bahari iliwaelemea adui zao.
et deduxit eos in spe, et non timuerunt, et inimicos eorum operuit mare.
54 Kisha aliwaleta mpaka wa nchi yake takatifu, kwenye mlima huu ambao aliutwaa kwa mkono wake wa kuume.
Et induxit eos in montem sanctificationis suæ, montem quem acquisivit dextera ejus; et ejecit a facie eorum gentes, et sorte divisit eis terram in funiculo distributionis;
55 Aliwafukuza mataifa mbele yao na akawapa urithi wao. Aliwakalisha makabila ya Israeli katika mahema yao.
et habitare fecit in tabernaculis eorum tribus Israël.
56 Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
Et tentaverunt, et exacerbaverunt Deum excelsum, et testimonia ejus non custodierunt.
57 Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
Et averterunt se, et non servaverunt pactum: quemadmodum patres eorum, conversi sunt in arcum pravum.
58 Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
In iram concitaverunt eum in collibus suis, et in sculptilibus suis ad æmulationem eum provocaverunt.
59 Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
Audivit Deus, et sprevit, et ad nihilum redegit valde Israël.
60 Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
Et repulit tabernaculum Silo, tabernaculum suum, ubi habitavit in hominibus.
61 Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
Et tradidit in captivitatem virtutem eorum, et pulchritudinem eorum in manus inimici.
62 Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
Et conclusit in gladio populum suum, et hæreditatem suam sprevit.
63 Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
Juvenes eorum comedit ignis, et virgines eorum non sunt lamentatæ.
64 Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
Sacerdotes eorum in gladio ceciderunt, et viduæ eorum non plorabantur.
65 Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
Et excitatus est tamquam dormiens Dominus, tamquam potens crapulatus a vino.
66 Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
Et percussit inimicos suos in posteriora; opprobrium sempiternum dedit illis.
67 Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
Et repulit tabernaculum Joseph, et tribum Ephraim non elegit:
68 Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
sed elegit tribum Juda, montem Sion, quem dilexit.
69 Alipajenga patakatifu pake kama mbinguni, na kama nchi aliyoiimarisha milele.
Et ædificavit sicut unicornium sanctificium suum, in terra quam fundavit in sæcula.
70 Alimchagua Daudi, mtumishi wake, alimchukua kutoka zizi la kondoo.
Et elegit David, servum suum, et sustulit eum de gregibus ovium; de post fœtantes accepit eum:
71 Alimtoa kutoka katika kufuata kondoo pamoja na wana wao, na kumweka kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake.
pascere Jacob servum suum, et Israël hæreditatem suam.
72 Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo wake, naye aliwaongoza kwa ujuzi wa mikono yake.
Et pavit eos in innocentia cordis sui, et in intellectibus manuum suarum deduxit eos.]

< Zaburi 78 >