< Zaburi 76 >

1 Mungu amefanya mwenyewe kujulikana katika Yuda; jina lake ni kuu katika Israeli.
For the end, among the Hymns, a Psalm for Asaph; a Song for the Assyrian. God is known in Judea: his name is great in Israel.
2 Hema yake iko salemu; makao yake yako yako Sayuni.
And his place has been in peace, and his dwelling-place in Sion.
3 Huko ndiko alivunja mishale ya upinde, ngao, upanga, na silaha zingine za vita. (Selah)
There he broke the power of the bows, the shield, and the sword, and the battle. (Pause)
4 Wewe unang'aa sana na huufunua utukufu wako, ushukapo kutoka milimani, ambako uliwauwa mateka.
You do wonderfully shine forth from the everlasting mountains.
5 Wenye moyo shujaa walitekwa nyara; walilala mauti. Mashujaa wote walikuwa wanyonge.
All the simple ones in heart were troubled; all the men of wealth have slept their sleep, and have found nothing in their hands.
6 Kwa kukemea kwako, ewe Mungu wa Yakobo, wote gari na farasi walilala mauti.
At your rebuke, O God of Jacob, the riders on horses slumbered.
7 Wewe, ndiyo wewe, ni wa kuogopwa; ni nani awezaye kusimama mbele yako wakati ukiwa na hasira?
You are terrible; and who shall withstand you, because of your anger?
8 Kutoka mbinguni wewe uliifanya hukumu yako isikike; nchi iliogopa na ikaa kimya
You did cause judgment to be heard from heaven; the earth feared, and was still,
9 wakati wewe, Mungu, ulipoinuka kutekeleza hukumu na kuwaokoa wote wa nchi walio onewa. (Selah)
when God arose to judgment, to save all the meek in heart. (Pause)
10 Hakika hukumu ya hasira yako dhidi ya binadamu itakuletea wewe sifa; wewe hujifunga mwenyewe hasira yako iliyo baki.
For the inward thought of man shall give thanks to you: and the memorial of his inward thought shall keep a feast to you.
11 Wekeni nadhiri kwa Yahwe Mungu wenu na kuzihifadhi. Nao wote wamzungukao yeye mleteeni zawadi yeye ambaye ni wa kuogopwa.
Vow, and pay [your vows] to the Lord our God; all that are round about him shall bring gifts, [even] to him that is terrible,
12 Yeye huzikata roho za wakuu; huogopwa na wafalme wa nchi.
and that takes away the spirits of princes; to him that is terrible among the kings of the earth.

< Zaburi 76 >