< Zaburi 72 >

1 Mpe mfalme amri ya haki yako, Mungu, haki yako kwa wana wa mfalme.
[By Solomon.] God, give the king your justice; your righteousness to the royal son.
2 Naye awaamue watu wako kwa haki na maskini wako kwa haki sawa.
He will judge your people with righteousness, and your poor with justice.
3 Milima iwazalie watu amani; vilima navyo vizae haki.
The mountains shall bring prosperity to the people. The hills bring the fruit of righteousness.
4 Naye awahukumu watu maskini; awaokoe watoto wa wahitaji na kuwavunja vipande vipande wenye kuwatesa.
He will judge the poor of the people. He will save the children of the needy, and will break the oppressor in pieces.
5 Na wakuheshimu wewe wakati wa jua, na kwa kipindi cha kudumu kwa mwezi katika vizazi vyote.
They shall fear you while the sun endures; and as long as the moon, throughout all generations.
6 Naye apate kuja kama mvua juu ya nyasi zilizokatwa, kama manyuyu yanyunyizayo nchi.
He will come down like rain on the mown grass, as showers that water the earth.
7 Mwenye haki na astawi kwa wakati wake, na amani iwepo kwa wingi mpaka mwezi utakapotoweka.
In his days, the righteous shall flourish, and abundance of peace, until the moon is no more.
8 Na awe na mamlaka toka bahari na bahari, na kutoka Mto hadi miisho ya dunia.
He shall have dominion also from sea to sea, from the River to the farthest parts of the earth.
9 Na wote waishio jangwani wainame mbele zake; adui zake na walambe mavumbi.
Those who dwell in the wilderness shall bow before him. His enemies shall lick the dust.
10 Wafalme wa Tashishi na visiwa walete kodi; wafalme wa Sheba na Seba watoe zawadi.
The kings of Tarshish and of the islands will bring tribute. The kings of Sheba and Seba shall offer gifts.
11 Hakika wafalme wote wamwinamie yeye; mataifa yote yamtumikie yeye.
Yes, all kings shall fall down before him. All nations shall serve him.
12 Kwa kuwa yeye humsaidia mhitaji na maskini asiye na msaidizi.
For he will deliver the needy when he cries; the poor, who has no helper.
13 Yeye huwahurumia maskini na wahitaji, na huokoa maisha ya wahitaji.
He will have pity on the poor and needy. He will save the souls of the needy.
14 Huyaokoa maisha yao dhidi ya mateso na vurugu, na damu yao ni ya thamani machoni pake.
He will redeem their soul from oppression and violence. Their blood will be precious in his sight.
15 Naye apate kuishi! Na dhahabu za Sheba apewe yeye. Watu wamuombee yeye siku zote; Mungu ambariki daima.
And he shall live, and the gold of Sheba shall be given to him. Men shall pray for him continually. He shall bless him all day long.
16 Kuwepo na nafaka nyingi katika ardhi; juu ya milima kuwe na mawimbi ya mimea. Matunda yake yawe kama Lebanoni; watu wasitawi katika miji kama nyansi za kondeni.
There shall be abundance of grain throughout the land. Its fruit sways like Lebanon. Let it flourish, thriving like the grass of the field.
17 Jina lake lidumu milele; jina lake ilindelee kama vile jua ling'aavyo; watu wabarikiwe katika yeye; mataifa yote wamwite mbarikiwa.
His name endures forever. His name continues as long as the sun. Men shall be blessed by him. All nations will call him blessed.
18 Yahwe Mungu, Mungu wa Israel, atukuzwe, ambaye pekee hufanya mambo ya ajabu.
Praise be to YHWH, the God of Israel, who alone does marvelous deeds.
19 Jina lake tukufu litukuzawe milele, nayo nchi yote ijazwe na utukufu wake. Amina, Amina.
Blessed be his glorious name forever. Let the whole earth be filled with his glory. Amen and amen.
20 Maombi ya Daudi mwana wa Yese yamemalizika. Kutatu cha tatu
This ends the prayers by David, the son of Jesse.

< Zaburi 72 >