< Zaburi 71 >

1 Katika wewe, Yahwe, napatakimbilio salama; usiniache niaibishwe.
耶和華啊,我投靠你; 求你叫我永不羞愧!
2 Uniokoe na kunifanya salama katika haki yako; geuzia sikio lako kwangu.
求你憑你的公義搭救我,救拔我; 側耳聽我,拯救我!
3 Uwe kwagu mwamba kwa ajili ya kimbilio salama ambako naweza kwenda siku zote; wewe umeamuru kuniokoa, kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu.
求你作我常住的磐石; 你已經命定要救我, 因為你是我的巖石,我的山寨。
4 Uniokoe mimi, Mungu wangu, kutoka katika mkono wa asiye haki na katili.
我的上帝啊,求你救我脫離惡人的手, 脫離不義和殘暴之人的手。
5 Maana wewe ni tumaini langu, Bwana Yahwe. Nimekuamini wewe siku zote tangu nilipokuwa mtoto.
主-耶和華啊,你是我所盼望的; 從我年幼,你是我所倚靠的。
6 Nimekuwa nikisaidiwa na wewe tangu tumboni; wewe ndiye yule uliyenitoa tumboni mwa mama yangu; sifa zangu zitakuhusu wewe siku zote.
我從出母胎被你扶持; 使我出母腹的是你。 我必常常讚美你!
7 Mimi ni mfano bora kwa watu wangu; wewe ni kimbilio langu lenye nguvu.
許多人以我為怪, 但你是我堅固的避難所。
8 Mama yangu atajawa na sifa zako, siku zote akikuheshimu.
你的讚美,你的榮耀 終日必滿了我的口。
9 Usinitupe katika siku za miaka ya uzee wangu; usiniache wakati nguvu zangu zitakapoisha.
我年老的時候,求你不要丟棄我! 我力氣衰弱的時候,求你不要離棄我!
10 Maana adui zangu wanazungumza kuhusu mimi; wale wanao fatilia uhai wangu wanapanga njama pamoja.
我的仇敵議論我; 那些窺探要害我命的彼此商議,
11 Wao husema, “Mungu amemuacha; mfuateni na mumchukue, maana hakuna yeyote awezaye kumuokoa yeye.”
說:上帝已經離棄他; 我們追趕他,捉拿他吧! 因為沒有人搭救。
12 Mungu, usiwe mbali nami; Mungu wangu, harakisha kunisaidia mimi.
上帝啊,求你不要遠離我! 我的上帝啊,求你速速幫助我!
13 Waaibishwe na kuharibiwa, wale walio adui wa uhai wangu; wavishwe laumu na kudharauliwa, wale watafutao kuniumiza.
願那與我性命為敵的,羞愧被滅; 願那謀害我的,受辱蒙羞。
14 Lakini nitakutumainia wewe siku zote na nitakusifu wewe zaidi na zaidi.
我卻要常常盼望, 並要越發讚美你。
15 Kinywa changu kitaongea kuhusu haki yako na wokovu wako mchana kutwa, ingawa ziwezi kuzielewa maana ni nyingi mno.
我的口終日要述說你的公義和你的救恩, 因我不計其數。
16 Nitakuja na matendo yenye nguvu ya Bwana Yahwe; nitataja haki yako, yako pekee.
我要來說主-耶和華大能的事; 我單要提說你的公義。
17 Mungu, tangu ujana wangu wewe umenifundisha; hata sasa ninatangaza matendo yako ya ajabu.
上帝啊,自我年幼時,你就教訓我; 直到如今,我傳揚你奇妙的作為。
18 Hakika, hata niwapo mzee na mvi kichwani, Mungu, usiniache mimi, kama ambavyo nimekuwa nikitanga nguvu yako kwa vizazi vijavyo, na uweza wako kwa yeyote ajaye.
上帝啊,我到年老髮白的時候, 求你不要離棄我! 等我將你的能力指示下代, 將你的大能指示後世的人。
19 Pia haki yako, Mungu, iko juu sana; wewe ambaye umefanya mambo makuu, Mungu, ni nani aliye kama wewe?
上帝啊,你的公義甚高; 行過大事的上帝啊,誰能像你!
20 Wewe ambaye umetuonesha sisi mateso mengi utatuhuisha tena na utatupandisha tena juu kutoka kwenye kina cha nchi.
你是叫我們多經歷重大急難的, 必使我們復活, 從地的深處救上來。
21 Uiongeze heshima yangu; rudi tena na unifariji.
求你使我越發昌大, 又轉來安慰我。
22 Nami pia nitakushukuru kwa kinubi kwa ajili ya uaminifu wako, Mungu wangu; kwako nitaimba sifa kwa kinubi, Mtakatifu wa Israel.
我的上帝啊,我要鼓瑟稱讚你, 稱讚你的誠實! 以色列的聖者啊,我要彈琴歌頌你!
23 Midomo yangu itapiga kelele kwa sababu ya furaha wakati nikikuimbia sifa, hata kwa roho yangu, ambayo wewe umeikomboa.
我歌頌你的時候, 我的嘴唇和你所贖我的靈魂都必歡呼;
24 Ulimi wangu pia utaongea kuhusu haki yangu mchana kutwa; maana wameaibishwa na kuvurugwa, wale waliotafuta kuniumiza.
並且我的舌頭必終日講論你的公義, 因為那些謀害我的人已經蒙羞受辱了。

< Zaburi 71 >