< Zaburi 59 >

1 Uniokoe dhidi ya adui zangu, Mungu wangu; uniweke mahali pa juu mbali na wale wanaoinuka dhidi yangu.
Au chef des chantres. “Ne détruis pas.” Hymne de David. Lorsque Saül envoya cerner la maison, pour le faire mourir. Mon Dieu! Délivre-moi de mes ennemis, Protège-moi contre mes adversaires!
2 Uniweke salama mbali na wafanyao kazi ya uovu, na uniokoe dhidi ya watu wenye kiu ya damu.
Délivre-moi des malfaiteurs, Et sauve-moi des hommes de sang!
3 Maana, tazama, wanasubiria uvamizini waniue. Wafanya maovu wenye nguvu hujikusanya wenyewe pamoja dhidi yangu, lakini sio kwa sababu ya makosa yangu au dhambi yangu, Yahwe.
Car voici, ils sont aux aguets pour m’ôter la vie; Des hommes violents complotent contre moi, Sans que je sois coupable, sans que j’aie péché, ô Éternel!
4 Wao wanajiandaa kunikimbiza ingawa sina kosa; amka unisaidie na unitazame.
Malgré mon innocence, ils courent, ils se préparent: Réveille-toi, viens à ma rencontre, et regarde!
5 Ewe, Yahwe Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, inika uwaadhibu mataifa yote; usiwe na huruma kwa mhalifu mwovu yeyote. (Selah)
Toi, Éternel, Dieu des armées, Dieu d’Israël, Lève-toi, pour châtier toutes les nations! N’aie pitié d’aucun de ces méchants infidèles! (Pause)
6 Wao wanarudi jioni, wanabweka kama mbwa na kuuzungukia mji.
Ils reviennent chaque soir, ils hurlent comme des chiens, Ils font le tour de la ville.
7 Tazama, wanapiga kelele mbaya kwa midomo yao; panga ziko kwenye midomo yao, maana wanasema, “Ni nani anaye tusikia?”
Voici, de leur bouche ils font jaillir le mal, Des glaives sont sur leurs lèvres; Car, qui est-ce qui entend?
8 Lakini wewe, Yahwe, utawacheka; wewe huwadhihaki mataifa yote.
Et toi, Éternel, tu te ris d’eux, Tu te moques de toutes les nations.
9 Mungu, nguvu yangu, nitakuwa msikivu kwako; wewe ni mnara wangu mrefu.
Quelle que soit leur force, c’est en toi que j’espère, Car Dieu est ma haute retraite.
10 Mungu atakutana nami akiwa na uaminifu wa agano lake; Mungu atanifanya nione shauku yangu juu ya adui zangu.
Mon Dieu vient au-devant de moi dans sa bonté, Dieu me fait contempler avec joie ceux qui me persécutent.
11 Usiwaue, hivyo watu watasahau. Uwatawanye kwa nguvu zako na uwaangushe, Bwana ngao yetu.
Ne les tue pas, de peur que mon peuple ne l’oublie; Fais-les errer par ta puissance, et précipite-les, Seigneur, notre bouclier!
12 Kwa ajili ya dhambi za midomo yao na maneno ya midomo yao, wakamatwe katika majivuno yao, na kwa laana na uongo ambao wao huelezea.
Leur bouche pèche à chaque parole de leurs lèvres: Qu’ils soient pris dans leur propre orgueil! Ils ne profèrent que malédictions et mensonges.
13 Uwamalize katika gadhabu yako, uwamalize ili kwamba wasiwepo tena; wajue kuwa Mungu anatawala katika Yakobo na mwisho wa nchi. (Selah)
Détruis-les, dans ta fureur, détruis-les, et qu’ils ne soient plus! Qu’ils sachent que Dieu règne sur Jacob, Jusqu’aux extrémités de la terre! (Pause)
14 Wakati wa jioni wao hurudi, wakibweka kama mbwa wakiuzungukia mji.
Ils reviennent chaque soir, ils hurlent comme des chiens, Ils font le tour de la ville.
15 Wanatangatanga wakitafuta chakula na wanabweka kama mbwa kama hawajatosheka.
Ils errent çà et là, cherchant leur nourriture, Et ils passent la nuit sans être rassasiés.
16 Lakini nitaimba kuhusu nguvu zako, na asubuhi nitaimba kuhusu upendo wako imara! maana umekuwa mnara wangu mrefu na kimbilio la usalama katika siku ya taabu.
Et moi, je chanterai ta force; Dès le matin, je célébrerai ta bonté. Car tu es pour moi une haute retraite, Un refuge au jour de ma détresse.
17 Kwako, nguvu yangu, nitaimba sifa; kwa kuwa Mungu ni mnara wangu mrefu, Mungu wa uaminifu wa agano.
O ma force! C’est toi que je célébrerai, Car Dieu, mon Dieu tout bon, est ma haute retraite.

< Zaburi 59 >