< Zaburi 44 >

1 Mungu, tumesikia kwa masikio yetu, baba zetu wametuambia kazi uliyofanya katika siku zao, siku za kale.
למנצח לבני-קרח משכיל ב אלהים באזנינו שמענו-- אבותינו ספרו-לנו פעל פעלת בימיהם בימי קדם
2 Uliwafukuza mataifa kwa mkono wako, lakini ukawafanya watu wetu kuishi humo; wewe uliwataabisha mataifa, lakini ukawaeneza watu wetu katika nchi.
אתה ידך גוים הורשת-- ותטעם תרע לאמים ותשלחם
3 Kwa maana hawakupata umiliki wa nchi kwa upanga wao, wala mkono wao wenyewe haukuwaokoa; bali mkono wako wakuume, mkono wako, na nuru ya uso wako, na kwa sababu uliwaridhia.
כי לא בחרבם ירשו ארץ וזרועם לא-הושיעה-למו כי-ימינך וזרועך ואור פניך-- כי רציתם
4 Mungu, wewe ni Mfalme wangu, amuru ushindi kwa ajili ya Yakobo.
אתה-הוא מלכי אלהים צוה ישועות יעקב
5 Kwa uweza wako tutawaangusha chini maadui zetu; kwa jina lako tutatembea juu yao, wale wanao inuka dhidi yetu.
בך צרינו ננגח בשמך נבוס קמינו
6 Kwa maana sitauamini upinde wangu, wala upanga wangu hautaniokoa.
כי לא בקשתי אבטח וחרבי לא תושיעני
7 Bali wewe ndeye uliyetuokoa na adui zetu, na umewaaibisha wale watuchukiao.
כי הושעתנו מצרינו ומשנאינו הבישות
8 Katika Mungu tumefanywa kujivuna siku zote, nasi tutalishukuru jina lako milele. (Selah)
באלהים הללנו כל-היום ושמך לעולם נודה סלה
9 Lakini sasa umetutupa na kutufedhehesha, na hauendi na majeshi yetu.
אף-זנחת ותכלימנו ולא-תצא בצבאותינו
10 Umetufanya kuwakimbia maadui zetu; na wale watuchukiao huchukua vitu vyetu vya thamani kwa ajili yao wenyewe.
תשיבנו אחור מני-צר ומשנאינו שסו למו
11 Umetufanya kama kondoo aliyeandaliwa kwa ajili ya chakula na umetutawanya kati ya mataifa.
תתננו כצאן מאכל ובגוים זריתנו
12 Wewe unawauza watu wako bure; kwa kufanya hivyo haukupata faida.
תמכר-עמך בלא-הון ולא-רבית במחיריהם
13 Wewe umetufanya kukemewa na majirani zetu, kuchekwa, na kudhihakiwa na wale wanao tuzunguka.
תשימנו חרפה לשכנינו לעג וקלס לסביבותינו
14 Umetufaya kituko kati ya mataifa, .......................................................
תשימנו משל בגוים מנוד-ראש בלאמים
15 Siku zote fedheha yangu iko mbele yangu, na aibu ya uso wangu imenifunika
כל-היום כלמתי נגדי ובשת פני כסתני
16 kwa sababu ya sauti yake iliyo kemea na kutukana, kwa sababu ya adui na kisasi.
מקול מחרף ומגדף מפני אויב ומתנקם
17 Yote haya yametupata sisi; bado hatukukusahau wewe wala kulikosea agano lako.
כל-זאת באתנו ולא שכחנוך ולא-שקרנו בבריתך
18 Mioyo yetu haikukengeuka; hatua zetu hazikuiacha njia yako.
לא-נסוג אחור לבנו ותט אשרינו מני ארחך
19 Bali wewe umetuadhibu vikali katika mahali pa mbweha na kutufunika na uvuli wa mauti.
כי דכיתנו במקום תנים ותכס עלינו בצלמות
20 Ikiwa tumelisahau jina la Mungu wetu au kueneza mikono yetu kwa Mungu mgeni,
אם-שכחנו שם אלהינו ונפרש כפינו לאל זר
21 Mungu asingeligundua hili? Kwa maana yeye anazijua siri za moyo.
הלא אלהים יחקר-זאת כי-הוא ידע תעלמות לב
22 Hakika, kwa ajili ya jina lako tutauawa siku zote; tunahesabiwa kuwa kondoo kwa ajili ya kuchinjwa.
כי-עליך הרגנו כל-היום נחשבנו כצאן טבחה
23 Bwana, amka, kwa nini unalala? Inuka, usitutupe moja kwa moja.
עורה למה תישן אדני הקיצה אל-תזנח לנצח
24 Kwa nini unaficha uso wako na kusahau mateso yetu na kukandamizwa kwetu?
למה-פניך תסתיר תשכח ענינו ולחצנו
25 Kwa maana tumeyeyushwa kwenye mavumbi; miili yetu imeshikamana na ardhi.
כי שחה לעפר נפשנו דבקה לארץ בטננו
26 Inuka utusaidie na utuokoe kwa ajili ya uaminifu wa agano lako.
קומה עזרתה לנו ופדנו למען חסדך

< Zaburi 44 >