< Zaburi 27 >

1 Yahwe ni nuru yangu na wokovu wangu; nimuogope nani? Yahwe ni salama ya maisha yangu; ni mhofu nani?
[A Psalm] of David. The LORD is my light and my salvation; whom shall I fear? the LORD is the strength of my life; of whom shall I be afraid?
2 Wakati waovu waliponijia kunila mwili wangu, wapinzani wangu na adui zangu walijikwaa na wakaanguka.
When evil-doers came upon me to eat up my flesh, [even] mine adversaries and my foes, they stumbled and fell.
3 Ingawa jeshi hujipanga kupigana na mimi, moyo wangu hautaogopa; japo vita vijapo inuka kupigana nami hata hapo nitabaki kuwa jasiri.
Though an host should encamp against me, my heart shall not fear: though war should rise against me, even then will I be confident.
4 Kitu kimoja nimekiomba kwa Yahwe, nami nitakitafuta hicho: kwamba niweze kukaa katika nyumba ya Yahwe siku zote za maisha yangu, kuutazama uzuri wa Yahwe na kutafakari hekaruni mwake.
One thing have I asked of the LORD, that will I seek after; that I may dwell in the house of the LORD all the days of my life, to behold the beauty of the LORD, and to inquire in his temple.
5 Kwa kuwa katika siku ya shida atanificha nyumbani mwake; atanificha katika mfuniko wa hema lake. Yeye ataniinua juu ya mwamba!
For in the day of trouble he shall keep me secretly in his pavilion: in the covert of his tabernacle shall he hide me; he shall lift me up upon a rock.
6 Kisha kichwa changu kitainuliwa juu ya maadui wote wanizungukao, nami nitatoa sadaka ya furaha hemani mwake! Nitaimba na kutunga nyimbo kwa Yahwe!
And now shall mine head be lifted up above mine enemies round about me; and I will offer in his tabernacle sacrifices of joy; I will sing, yea, I will sing praises unto the LORD.
7 Sikia, sauti yangu nikuitapo, Yahwe! Unihurumie, na unijibu!
Hear, O LORD, when I cry with my voice: have mercy also upon me, and answer me.
8 Moyo wangu huongea kuhusu wewe, “Utafute uso wake!” Nami nautafuta uso wako, Yahwe!
[When thou saidst], Seek ye my face; my heart said unto thee, Thy face, LORD, will I seek.
9 Usiufiche uso wako mbali na mimi; usinikasirikie mimi mtumishi wako! Wewe umekuwa msaada wangu; usiniache wala kunitelekeza, Mungu wa wokovu wangu!
Hide not thy face from me; put not thy servant away in anger: thou hast been my help; cast me not off, neither forsake me, O God of my salvation.
10 Hata kama baba yangu na mama yangu wakiniacha, Yahwe utanitunza kwako.
For my father and my mother have forsaken me, but the LORD will take me up.
11 Unifundishe njia yako, Yahwe! Kwa sababu ya adui zangu uniongoze katika njia salama.
Teach me thy way, O LORD; and lead me in a plain path, because of mine enemies.
12 Usiwaache adui zangu wanifanyie watamanivyo, kwa sababu mashahidi wa uongo wameinuka kinyume namimi, nao wanapumua vurugu!
Deliver me not over unto the will of mine adversaries: for false witnesses are risen up against me, and such as breathe out cruelty.
13 Kitu gani kingeweza kunitokea kama nisingeamini kuwa nitauona uzuri wa Yahwe katika nchi ya walio hai?
[I had fainted], unless I had believed to see the goodness of the LORD in the land of the living.
14 Umngoje Yahwe; uwe imara, na moyo wako uwe jasiri! Umngoje Yahwe!
Wait on the LORD: be strong, and let thine heart take courage; yea, wait thou on the LORD.

< Zaburi 27 >