< Zaburi 137 >

1 Kando ya mito ya Babeli tuliketi na tulilia tulipokumbuka kuhusu Sayuni.
Nad rzekami Babilonu, tam siedzieliśmy i płakaliśmy, wspominając Syjon.
2 Tulitundika vinubi vyetu kwenye miti ya Babylon.
Na wierzbach tamtej krainy zawiesiliśmy nasze harfy;
3 Huko watekaji wetu walitaka tuwaimbie, na wale walio tudhihaki walitutaka sisi tufurahi, wakisema, “Tuimbieni moja ya nyimbo za Sayuni.”
Bo tam ci, którzy nas wzięli w niewolę, żądali od nas pieśni, a nasi ciemięzcy – radości, [mówiąc]: Śpiewajcie nam [którąś] z pieśni Syjonu.
4 Tungewezaje kuimba wimbo unaomuhusu Yahwe katika nchi ya ugeni?
Jakże możemy śpiewać pieśń PANA na obcej ziemi?
5 Kama nikikusahau wewe, Yerusalemu, basi mkono wangu wa kuume na usahau ujuzi wake.
Jeśli zapomnę o tobie, Jeruzalem, niech sama o sobie zapomni moja prawica.
6 Ulimi wangu na ushikamane juu ya kinywa changu kama nisipokufikiria tena, na kama sipendelei zaidi Yerusalemu kuliko furaha yangu kuu.
Niech mi język przylgnie do podniebienia, jeśli nie będę pamiętał o tobie, jeśli nie postawię Jeruzalem ponad największą moją radość.
7 Kumbuka, Ee Yahwe, kile walichofanya Waedomu siku ya anguko la Yerusalemu. Walisema, “Ibomoeni, ibomoeni mpaka chini kwenye misingi yake.”
Pamiętaj, PANIE, synów Edomu [i] dzień Jeruzalem, gdy mówili: Zburzcie, zburzcie [je] aż do jego fundamentu.
8 Binti za Babeli, hivi karibuni wataharibiwa- mtu na abalikiwe, yeyote atakaye walipizia yale mliotufanyia sisi.
O córko Babilonu, i ty będziesz spustoszona. Błogosławiony, kto ci odpłaci [za] zło, jakie nam uczyniłaś.
9 Mtu na abarikiwe, yeyote achukuaye na kusambaratisha watoto wenu juu ya jiwe.
Błogosławiony, kto schwyci i roztrzaska twe dzieci o skałę.

< Zaburi 137 >