< Zaburi 137 >

1 Kando ya mito ya Babeli tuliketi na tulilia tulipokumbuka kuhusu Sayuni.
By the waters of Babylon there we sat, and we wept at the thought of Zion.
2 Tulitundika vinubi vyetu kwenye miti ya Babylon.
There on the poplars we hung our harps.
3 Huko watekaji wetu walitaka tuwaimbie, na wale walio tudhihaki walitutaka sisi tufurahi, wakisema, “Tuimbieni moja ya nyimbo za Sayuni.”
For there our captors called for a song: our tormentors, rejoicing, saying: ‘Sing us one of the songs of Zion.’
4 Tungewezaje kuimba wimbo unaomuhusu Yahwe katika nchi ya ugeni?
How can we sing the Lord’s song in the foreigner’s land?
5 Kama nikikusahau wewe, Yerusalemu, basi mkono wangu wa kuume na usahau ujuzi wake.
If I forget you, Jerusalem, may my right hand wither.
6 Ulimi wangu na ushikamane juu ya kinywa changu kama nisipokufikiria tena, na kama sipendelei zaidi Yerusalemu kuliko furaha yangu kuu.
May my tongue stick to the roof of my mouth, if I am unmindful of you, or don’t set Jerusalem above my chief joy.
7 Kumbuka, Ee Yahwe, kile walichofanya Waedomu siku ya anguko la Yerusalemu. Walisema, “Ibomoeni, ibomoeni mpaka chini kwenye misingi yake.”
Remember the Edomites, Lord, the day of Jerusalem’s fall, when they said, ‘Lay her bare, lay her bare, right down to her very foundation.’
8 Binti za Babeli, hivi karibuni wataharibiwa- mtu na abalikiwe, yeyote atakaye walipizia yale mliotufanyia sisi.
Babylon, despoiler, happy are those who pay you back for all you have done to us.
9 Mtu na abarikiwe, yeyote achukuaye na kusambaratisha watoto wenu juu ya jiwe.
Happy are they who seize and dash your children against the rocks.

< Zaburi 137 >