< Zaburi 135 >

1 Msifuni Yahwe. Lisifuni jina la Yahwe. Msifuni yeye, enyi watumishi wa Yahwe,
Praise Yahweh. Praise the name of Yahweh. Praise him, you servants of Yahweh,
2 ninyi msimamao katika nyumba ya Yahwe, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
you who stand in Yahweh's house, in the courtyards of the house of our God.
3 Msifuni Yahwe, kwa kuwa ni mwema; liimbieni sifa jina lake, maana ni vizuri kufanya hivyo.
Praise Yahweh, for he is good; sing praises to his name, for it is pleasant to do so.
4 Kwa kuwa Yahwe amemchagua Yakobo kwa ajili yake mwenyewe, Israeli kama urithi wake.
For Yahweh has chosen Jacob for himself, Israel as his possession.
5 Najua ya kuwa Yahwe ni mkuu, na kwamba Bwana wetu yuko juu ya miungu yote.
I know that Yahweh is great, that our Lord is above all gods.
6 Chochote Yahwe apendacho, hufanya mbinguni, duniani, katika bahari na katika vilindi vyote.
Whatever Yahweh desires, he does in heaven, on earth, in the seas and all the ocean depths.
7 Hushusha mawingu kutoka mbali, akifanya mianga ya radi kuongozana na mvua na kuleta upepo toka katika ghala yake.
He brings the clouds from far away, making lightning bolts accompany the rain and bringing the wind out of his storehouse.
8 Aliua mzaliwa wa kwanza wa Misri, wote wanadamu na wanyama.
He killed the firstborn of Egypt, both of man and animals.
9 Alituma ishara na maajabu kati yako Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
He sent signs and wonders into your midst, Egypt, against Pharaoh and all his servants.
10 Aliwashambulia mataifa mengi na aliua wafalme wenye nguvu,
He attacked many nations and killed mighty kings,
11 Sihoni mfalme wa Waamori na Ogu mfalme wa Bashani na falme zote za Kanaani.
Sihon king of the Amorites and Og king of Bashan and all the kingdoms of Canaan.
12 Alitupatia sisi nchi yao kama urithi, urithi wa Israeli watu wake.
He gave us their land as an inheritance, an inheritance to Israel his people.
13 Jina lako, Yahwe, inadumu milele; Yahwe, kumbukumbu lako vizazi hata vizazi.
Your name, Yahweh, endures forever; your renown, Yahweh, endures throughout all generations.
14 Kwa kuwa Bwana huwatetea watu wake na anahuruma juu ya watumishi wake.
For Yahweh defends his people and has compassion on his servants.
15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
The nations' idols are silver and gold, the work of men's hands.
16 Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
Those idols have mouths, but they do not speak; they have eyes, but they do not see;
17 zina masikio, lakini hazisikii, wala vinywani mwao hamna pumzi.
they have ears, but they do not hear, nor is there breath in their mouths.
18 Wale wazitengenezao wanafanana nazo, vilevile kila anaye zitumainia.
Those who make them are like them, as is everyone who trusts in them.
19 Enyi kizazi cha Israeli, mtukuzeni Yahwe; kizazi cha Haruni, mtukuzeni Yahwe.
Descendants of Israel, bless Yahweh; descendants of Aaron, bless Yahweh.
20 Kizazi cha Lawi, mtukuzeni Yahwe.
Descendants of Levi, bless Yahweh; you who honor Yahweh, bless Yahweh.
21 Atukuzwe Yahwe katika Sayuni, yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Yahwe.
Blessed be Yahweh in Zion, he who lives in Jerusalem. Praise Yahweh.

< Zaburi 135 >