< Zaburi 135 >

1 Msifuni Yahwe. Lisifuni jina la Yahwe. Msifuni yeye, enyi watumishi wa Yahwe,
Let the Lord be praised. O you servants of the Lord, give praise to the name of the Lord.
2 ninyi msimamao katika nyumba ya Yahwe, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
You who are in the house of the Lord, and in the open spaces of the house of our God,
3 Msifuni Yahwe, kwa kuwa ni mwema; liimbieni sifa jina lake, maana ni vizuri kufanya hivyo.
Give praise to Jah, for he is good: make melody to his name, for it is pleasing.
4 Kwa kuwa Yahwe amemchagua Yakobo kwa ajili yake mwenyewe, Israeli kama urithi wake.
For the Lord has taken Jacob for himself, and Israel for his property.
5 Najua ya kuwa Yahwe ni mkuu, na kwamba Bwana wetu yuko juu ya miungu yote.
I know that the Lord is great, and that our Lord is greater than all other gods.
6 Chochote Yahwe apendacho, hufanya mbinguni, duniani, katika bahari na katika vilindi vyote.
The Lord has done whatever was pleasing to him, in heaven, and on the earth, in the seas and in all the deep waters.
7 Hushusha mawingu kutoka mbali, akifanya mianga ya radi kuongozana na mvua na kuleta upepo toka katika ghala yake.
He makes the mists go up from the ends of the earth; he makes thunder-flames for the rain; he sends out the winds from his store-houses.
8 Aliua mzaliwa wa kwanza wa Misri, wote wanadamu na wanyama.
He put to death the first-fruits of Egypt, of man and of beast.
9 Alituma ishara na maajabu kati yako Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
He sent signs and wonders among you, O Egypt, on Pharaoh, and on all his servants.
10 Aliwashambulia mataifa mengi na aliua wafalme wenye nguvu,
He overcame great nations, and put strong kings to death;
11 Sihoni mfalme wa Waamori na Ogu mfalme wa Bashani na falme zote za Kanaani.
Sihon, king of the Amorites, and Og, king of Bashan, and all the kingdoms of Canaan;
12 Alitupatia sisi nchi yao kama urithi, urithi wa Israeli watu wake.
And gave their land for a heritage, even for a heritage to Israel his people.
13 Jina lako, Yahwe, inadumu milele; Yahwe, kumbukumbu lako vizazi hata vizazi.
O Lord, your name is eternal; and the memory of you will have no end.
14 Kwa kuwa Bwana huwatetea watu wake na anahuruma juu ya watumishi wake.
For the Lord will be judge of his people's cause; his feelings will be changed to his servants.
15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
The images of the nations are silver and gold, the work of men's hands.
16 Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
They have mouths, but no voice, they have eyes, but they do not see;
17 zina masikio, lakini hazisikii, wala vinywani mwao hamna pumzi.
They have ears, but no hearing; and there is no breath in their mouths.
18 Wale wazitengenezao wanafanana nazo, vilevile kila anaye zitumainia.
Those who make them are like them; and so is everyone who puts his hope in them.
19 Enyi kizazi cha Israeli, mtukuzeni Yahwe; kizazi cha Haruni, mtukuzeni Yahwe.
Give praise to the Lord, O children of Israel: give praise to the Lord, O sons of Aaron:
20 Kizazi cha Lawi, mtukuzeni Yahwe.
Give praise to the Lord, O sons of Levi: let all the worshippers of the Lord give him praise.
21 Atukuzwe Yahwe katika Sayuni, yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Yahwe.
Praise be to the Lord out of Zion, even to the Lord whose house is in Jerusalem, Let the Lord be praised.

< Zaburi 135 >