< Zaburi 106 >

1 Msifuni Yahwe. Mshukuruni Yahwe, kwa kuwa ni mwema, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
Alelu-JAH. Alabad al SEÑOR, porque es bueno; porque para siempre es su misericordia.
2 Ni nani awezaye kuyahesabu mataendo makuu ya yahwe au kutangaza katika ukamilifu sifa zote za matendo yake ya kuaminika.
¿Quién expresará las valentías del SEÑOR? ¿Quién contará sus alabanzas?
3 Wamebarikiwa wale watendao yaliyo mema na matendo yao yaliyo haki siku zote.
Dichosos los que guardan juicio, los que hacen justicia en todo tiempo.
4 Ukumbuke, Ee Yahwe, unapowaonesha watu wako neema; unisaidie unapowaokoa.
Acuérdate de mí, oh SEÑOR, en la buena voluntad para con tu pueblo; visítame con tu salud;
5 Ndipo nitaona mafanikio ya wateule wako, wakifurahia katika furaha ya taifa lako, na utukufu pamoja na urithi wako.
para que yo vea el bien de tus escogidos, para que me goce en la alegría de tu nación, y me gloríe con tu heredad.
6 Tumefanya dhambi kama babu zetu, tumekosea, na kufanya uovu.
Pecamos con nuestros padres, pervertimos, hicimos impiedad.
7 Baba zetu hawakuyatambua matendo yako ya ajabu katika Misri; walipuuzia matendo yako mengi ya uaminifu wa agano; waliasi penye bahari, bahari ya Shamu.
Nuestros padres en Egipto no entendieron tus maravillas; no se acordaron de la muchedumbre de tus misericordias; sino que se rebelaron junto al mar, en el mar Bermejo.
8 Hata hivyo, yeye aliwaokoa kwa ajili ya jina lake ili kwamba aweze kuzifunua nguvu zake.
Los salvó por su Nombre, para hacer notoria su fortaleza.
9 Aliikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka. Kisha akawaongoza vilindini, kana kwamba ni jangwani.
Y reprendió al mar Bermejo, y lo secó; y les hizo ir por el abismo, como por un desierto.
10 Aliwaokoa kutoka mkononi mwa wale waliowachukia, na aliwaokoa kutoka mkononi mwa adui.
Y los salvó de mano del enemigo, y los rescató de mano del adversario.
11 Lakini maji yaliwafunika washindani wao; hakuna hata mmoja aliye okolewa.
Y cubrieron las aguas a sus enemigos; no quedó uno de ellos.
12 Ndipo waliyaamini maneno yake, nao waliimba sifa zake.
Entonces creyeron a sus palabras, y cantaron su alabanza.
13 Lakini walisahau haraka kile alichofanya; hawakuyasubiri maelekezo yake.
Se apresuraron, se olvidaron de sus obras; no esperaron en su consejo.
14 Walikuwa na tamaa isiyotoshelezwa jangwani, wakamjaribu Mungu nyikani.
Se entregaron a un deseo desordenado en el desierto; y tentaron a Dios en la soledad.
15 Aliwapa ombi lao, lakini alituma gonjwa ambalo lilishambulia miili yao.
Y él les dio lo que pidieron; mas envió flaqueza en sus almas.
16 Katika kambi wakawa na wivu juu Musa na Haruni, kuhani mtakatifu wa Yahwe.
Tomaron después celo contra Moisés en el campamento, y contra Aarón el santo del SEÑOR.
17 Nchi ilifunguka na ilimmeza Dathani na iliwafunika wafuasi wa Abiramu.
Se abrió la tierra, y tragó a Datán, y cubrió la compañía de Abiram.
18 Moto uliwaka kati yao; moto uliwaangamiza waovu.
Y se encendió el fuego en su compañía; la llama quemó los impíos.
19 Walitengeneza ndama huko Horebu na kuabudu sanamu ya kuyeyuka.
Hicieron el becerro en Horeb, y adoraron a un vaciadizo.
20 Wakaubadili utukufu wa Mungu kuwa mfano wa ng'ombe alaye majani.
Así trocaron su gloria por la imagen de un buey que come hierba.
21 Walimsahau Mungu wokozi wao, aliyefanya mambo makuu katika Misri.
Olvidaron al Dios de su salud, que había hecho grandezas en Egipto;
22 Alifanya matendo ya ajabu katika nchi ya Hamu na matendo makuu penye Bahari ya Shamu.
maravillas en la tierra de Cam, temerosas cosas sobre el mar Bermejo.
23 Mungu angetangaza uharibifu wao, kama sio Musa, mteule wake, aliingilia kati kugeuza hasira yake dhidi ya kuwaangamiza.
Y trató de destruirlos, a no haberse puesto Moisés su escogido al portillo delante de él, a fin de apartar su ira, para que no los destruyese.
24 Kisha waliidharau nchi yenye matunda; hawakuiamini ahadi yake,
Y aborrecieron la tierra deseable; no creyeron a su palabra;
25 bali walilalamiaka katika mahema yao, na hawakumtii Yahwe.
antes murmuraron en sus tiendas, y no oyeron la voz del SEÑOR.
26 Kwa hiyo aliinua mkono wake na kuapa kwao kuwa atawaacha wafe jangwani,
Por lo que alzó su mano a ellos, para postrarlos en el desierto,
27 akitawanya uzao wao kati ya mataifa, na kuwatawanya katika nchi za kigeni.
y humillar su simiente entre los gentiles, y esparcirlos por las tierras.
28 Waliabudu Baal ya Poeri na walizila dhabihu zilizotolewa kwa wafu.
Se allegaron asimismo a Baal-peor, y comieron los sacrificios por los muertos.
29 Walimkasirisha kwa matendo yao, na pigo la gonjwa baya liliwashambulia kati yao.
Y ensañaron a Dios con sus obras, y aumentó la mortandad en ellos.
30 Ndipo Finehasi aliinuka kuingilia kati, na pigo likakoma.
Entonces se puso Finees, y juzgó; y se detuvo la mortandad.
31 Ilihesabika kwake kama tendo la haki kwa vizazi vyote hata milele.
Y le fue contado a justicia de generación en generación para siempre.
32 Pia walimkasirisha Yahwe penye maji ya Meriba, na Musa aliteseka kwa ajili yao.
También le irritaron en las aguas de Meriba; e hizo mal a Moisés por causa de ellos;
33 Walimghadhabisha Musa naye akaongea haraka.
porque hicieron rebelar a su espíritu, como lo expresó con sus labios.
34 Hawakuyaharibu mataifa kama Yahwe alivyowaamuru,
No destruyeron los pueblos que el SEÑOR les dijo;
35 bali walichangamana na mataifa na walijifunza njia zao
antes se mezclaron con los gentiles, y aprendieron sus obras.
36 nao waliabudu sanamu, nazo zikawa mtego kwao.
Y sirvieron a sus ídolos; los cuales les fueron por ruina.
37 Waliwatoa wana wao na binti zao kwa mapepo.
Y sacrificaron sus hijos y sus hijas a los demonios;
38 Walimwaga damu isiyo na hatia, damu ya wana na binti zao, ambao waliwatoa kama dhabihu kwa sanamu za Kanaani, waliinajisi nchi kwa damu.
y derramaron la sangre inocente, la sangre de sus hijos y de sus hijas, que sacrificaron a los ídolos de Canaán; y la tierra fue contaminada con sangre.
39 Walinajisiwa kwa matendo yao; katika matendo yao walikuwa kama malaya.
Se contaminaron así con sus propias obras, y fornicaron con sus hechos.
40 Hivyo Yahwe aliwakasilikia watu wake, akawadharau watu wake mwenyewe.
Se encendió por tanto el furor del SEÑOR sobre su pueblo, y abominó su heredad:
41 Akawaruhusu mataifa, na wale walio wachukia wakawatawala.
Y los entregó en poder de los gentiles, y se enseñorearon de ellos los que los aborrecían.
42 Maadui zao wakawaonea, wakatiishwa chini ya mamlaka yao.
Y sus enemigos los oprimieron, y fueron quebrantados debajo de su mano.
43 Mara nyingi alienda kuwasaidia, lakini waliendelea kuasi nao walishushwa chini kwa dhambi zao wenyewe.
Muchas veces los libró; mas ellos se rebelaron a su consejo, y fueron humillados por su maldad.
44 Hata hivyo, aliiangalia dhiki yao aliposikia kilio chao kwa ajili ya msaada.
El con todo, miraba cuando estaban en angustia, y oía su clamor;
45 Alikumbuka agano lake pamoja nao na alijirudi kwa sababu ya upendo wake thabiti.
y se acordaba de su pacto con ellos, y se arrepentía conforme a la muchedumbre de sus misericordias.
46 Aliwafanya wote waliowateka wawahurumie.
Hizo asimismo que tuviesen de ellos misericordia todos los que los tenían cautivos.
47 Utuokoe, Ee Yahwe, Mungu wetu. Utukusanye kutoka kati ya mataifa ili kwamba tuweze kulishukuru jina lako takatifu na utukufu katika sifa zako. Yahwe,
Sálvanos, SEÑOR Dios nuestro, y júntanos de entre los gentiles, para que loemos tu santo Nombre, para que nos gloriemos de tus alabanzas.
48 Mungu wa Israeli, na asifiwe toka milele na milele. watu wote walisema, “Amen.” Msifuni Yahwe. Kitabu cha tano.
Bendito el SEÑOR Dios de Israel, desde el siglo y hasta el siglo; y diga todo el pueblo, Amén. Alelu-JAH.

< Zaburi 106 >