< Mithali 29 >

1 Mtu aliyepokea makaripio mengi lakini anashupaza shingo yake atavunjika ndani ya muda mfupi na hata pona.
A man that hardeneth his necke when he is rebuked, shall suddenly be destroyed and can not be cured.
2 Watenda mema wanapoongezeka, watu wanafurahi, bali wakati mtu mwovu anapotawala, watu huugua.
When the righteous are in authoritie, the people reioyce: but when the wicked beareth rule, the people sigh.
3 Mwenye kupenda hekima baba yake anafurahi, bali anayeshikamana na makahaba huuharibu utajiri wake.
A man that loueth wisdome, reioyceth his father: but he that feedeth harlots, wasteth his substance.
4 Mfalme huimarisha nchi kwa haki, bali mwenye kudai rushwa huirarua.
A King by iudgement mainteineth ye countrey: but a man receiuing giftes, destroyeth it.
5 Mtu anayejipendekeza kwa jirani yake anatandaza wavu kwenye miguu yake.
A man that flattereth his neighbour, spreadeth a net for his steps.
6 Mtu mbaya hunaswa kwenye mtego wa dhambi yake mwenyewe, bali yeye atendaye haki huimba na kufurahi.
In the transgression of an euill man is his snare: but the righteous doeth sing and reioyce.
7 Atendaye haki hutetea madai ya masikini; mtu mwovu hafahamu maarifa kama hayo.
The righteous knoweth the cause of the poore: but the wicked regardeth not knowledge.
8 Mwenye dhihaka huutia moto mji, bali wale wenye busara huigeuza ghadhabu.
Scornefull men bring a citie into a snare: but wise men turne away wrath.
9 Mtu mwenye busara anapojadiliana na mpumbavu, hughadhabika na kucheka, hakutakuwa na utulivu.
If a wise man contend with a foolish man, whether he be angry or laugh, there is no rest.
10 Mkatili humchukia mwenye ukamilifu na hutafuta maisha ya mwenye haki.
Bloodie men hate him that is vpright: but the iust haue care of his soule.
11 Mpumabavu huonyesha hasira yake, bali mtu mwenye busara huishikilia na kujituliza mwenyewe.
A foole powreth out all his minde: but a wise man keepeth it in till afterward.
12 Kama matawala atazinagatia uongo, maafisa wake wote watakuwa waovu.
Of a prince that hearkeneth to lyes, all his seruants are wicked.
13 Mtu masikini na mkandamizaji wanafanana, maana Yehova huyapa nuru macho yao wote.
The poore and the vsurer meete together, and the Lord lighteneth both their eyes.
14 Kama mfalme atamhukumu masikini kwa uaminifu, kiti chake cha enzi kitaimarishwa milele.
A King that iudgeth the poore in trueth, his throne shalbe established for euer.
15 Fimbo na maonyo huleta hekima, bali mtoto huru mbali na makaripio humwaibisha mama yake.
The rodde and correction giue wisdome: but a childe set a libertie, maketh his mother ashamed.
16 Watu waovu wanapotawala, uovu huongezeka, bali wenye kutenda haki wataona anguko la watu waovu.
When the wicked are increased, transgression increaseth: but ye righteous shall see their fall.
17 Mwadibishe mwanao naye atakupa pumziko; ataleta furaha katika maisha yako.
Correct thy sonne and he will giue thee rest, and will giue pleasures to thy soule.
18 Pasipo na maono ya kinabii watu huenda bila utaratibu, bali mwenye kuitunza sheria amebarikiwa.
Where there is no vision, the people decay: but he that keepeth the Lawe, is blessed.
19 Mtumwa hawezi kurekebishwa kwa maneno, maana ingawa anaelewa, hakuna mwitikio.
A seruant will not be chastised with words: though he vnderstand, yet he will not answere.
20 Je unamwona mtu mwenye haraka katika maneno yake? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
Seest thou a man hastie in his matters? there is more hope of a foole, then of him.
21 Mwenye kumdekeza mtumwa wake tangu ujana, mwisho wake itakuwa taabu.
He that delicately bringeth vp his seruant from youth, at length he will be euen as his sone.
22 Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi na bwana mwenye hasira sana hutenda dhambi nyingi.
An angrie man stirreth vp strife, and a furious man aboundeth in transgression.
23 Kiburi cha mtu humshusha chini, bali mwenye roho ya unyenyekevu atapewa heshima.
The pride of a man shall bring him lowe: but the humble in spirit shall enioy glory.
24 Anayeshirikiana na mwizi huyachukia maisha yake mwenyewe; husikia laana na wala hasemi chochote.
He that is partner with a thiefe, hateth his owne soule: he heareth cursing, and declareth it not.
25 Kumwogopa binadamu ni mtego, bali mwenye kumtumaini Yehova atalindwa.
The feare of man bringeth a snare: but he that trusteth in the Lord, shalbe exalted.
26 Wengi huutafuta uso wa mtawala, bali kutoka kwa Yehova huja haki kwa ajili yake.
Many doe seeke the face of the ruler: but euery mans iudgement commeth from the Lord.
27 Mtu dhalimu ni chukizo kwa wenye kutenda haki, bali mwenye njia ya haki ni chukizo kwa watu waovu.
A wicked man is abomination to the iust, and he that is vpright in his way, is abomination to the wicked.

< Mithali 29 >