< Mithali 28 >

1 Waovu hukimbia wakati hakuna mtu anayewafukuza, bali wale watendao haki ni thabiti kama simba kijana.
Fugit impius, nemine persequente: iustus autem quasi leo confidens, absque terrore erit.
2 Kwa sababu ya uhalifu wa nchi, kuna wakuu wengi, bali kwa mtu mwenye ufahamu na maarifa, itadumu kwa muda mrefu.
Propter peccata terræ multi principes eius: et propter hominis sapientiam, et horum scientiam quæ dicuntur, vita ducis longior erit.
3 Mtu masikini mwenye kukandamiza watu wengine masikini ni kama mvua inayopiga ambayo haisazi chakula.
Vir pauper calumnians pauperes, similis est imbri vehementi, in quo paratur fames.
4 Wale wanaokataa sheria huwatukuza watu waovu, bali wale wenye kuitunza sheria hupigana dhidi yao.
Qui derelinquunt legem, laudant impium: qui custodiunt, succenduntur contra eum.
5 Watu wabaya hawafahamu haki, bali wale wanaomtafuta Yehova wanafahamu kila kitu.
Viri mali non cogitant iudicium: qui autem inquirunt Dominum, animadvertunt omnia.
6 Ni bora mtu masikini ambaye anatembea katika uadilifu, kuliko mtu tajiri ambaye ni mdanganyifu katika njia zake.
Melior est pauper ambulans in simplicitate sua, quam dives in pravis itineribus.
7 Yeye anayetunza sheria ni mwana mwenye ufahamu, bali mwenye ushirika na walafi humwaibisha baba yake.
Qui custodit legem, filius sapiens est: qui autem comessatores pascit, confundit patrem suum.
8 Anayepata mafanikio kwa kutoza riba kubwa anakusanya utajiri wake kwa ajili ya mwingine ambaye atakuwa na huruma kwa watu masikini.
Qui coacervat divitias usuris et fœnore, liberali in pauperes congregat eas.
9 Kama mtu atageuzia mbali sikio lake kusikia sheria, hata maombi yake ni chukizo.
Qui declinat aures suas ne audiat legem, oratio eius erit execrabilis.
10 Yeye anayempotosha mwenye uadilifu katika njia ya uovu ataangukia kwenye shimo lake mwenyewe, bali wakamilifu watapata urithi mwema.
Qui decipit iustos in via mala, in interitu suo corruet: et simplices possidebunt bona eius.
11 Mtu tajiri anaweza kuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe, bali mtu masikini mwenye ufahamu atamtafuta.
Sapiens sibi videtur vir dives: pauper autem prudens scrutabitur eum.
12 Kunapokuwa na ushindi kwa wenye kutenda haki, kunafuraha kuu, bali wanapoinuka waovu, watu hujificha wenyewe.
In exultatione iustorum multa gloria est: regnantibus impiis ruinæ hominum.
13 Yeye afichaye dhambi zake hatafanikiwa, bali mwenye kutubu na kuziacha ataonyeshwa rehema.
Qui abscondit scelera sua, non dirigetur: qui autem confessus fuerit, et reliquerit ea, misericordiam consequetur.
14 Anafuraha ambaye huishi kwa unyenyekevu, bali anayeufanya moyo wake ataanguka katika taabu.
Beatus homo, qui semper est pavidus: qui vero mentis est duræ, corruet in malum.
15 Kama simba anayeunguruma au dubu anayeshabulia ni kama mtawala mwovu juu ya watu masikini.
Leo rugiens, et ursus esuriens, princeps impius super populum pauperem.
16 Mtawala anayekosa ufahamu ni mkandamizaji katili, bali mwenye kuchukia aibu atadumu katika siku zake.
Dux indigens prudentia, multos opprimet per calumniam: qui autem odit avaritiam, longi fient dies eius.
17 Kama mtu anahatia kwa sababu amemwaga damu ya mtu, atakuwa mkimbizi hadi kifo na hakuna atakayemsaidia.
Hominem, qui calumniatur animæ sanguinem, si usque ad lacum fugerit, nemo sustinet.
18 Mwenye kuenenda kwa ukaminifu atakuwa salama, bali mwenye njia ya udanganyifu ataanguka ghafla.
Qui ambulat simpliciter, salvus erit: qui perversis graditur viis, concidet semel.
19 Anayefanya kazi kwenye shamba lake atapata chakula kingi, bali afuataye shughuli za upuuzi atapata umasikini mkubwa.
Qui operatur terram suam, satiabitur panibus: qui autem sectatur otium, replebitur egestate.
20 Mtu mwaminifu atapata baraka nyingi bali apataye utajiri wa haraka hawezi kukosa adhabu.
Vir fidelis multum laudabitur: qui autem festinat ditari, non erit innocens.
21 Siyo vema kuonyesha upendeleo, lakini kwa kipande cha mkate mtu atafanya ubaya.
Qui cognoscit in iudicio faciem, non benefacit: iste et pro buccella panis deserit veritatem.
22 Mtu mchoyo huharakisha kwenye utajiri, lakini hajui ni umasikini gani utakuja juu yake.
Vir, qui festinat ditari, et aliis invidet, ignorat quod egestas superveniet ei.
23 Anayemkaripia mtu baadaye atapata fadhila zaidi kutoka kwake kuliko mwenye kumsifia sana kwa ulimi wake.
Qui corripit hominem, gratiam postea inveniet apud eum magis quam ille, qui per linguæ blandimenta decipit.
24 Yule anayemwibia baba yake na mama yake na kusema, “Hiyo siyo dhambi,” ni mshirika wa mwenye kuharibu.
Qui subtrahit aliquid a patre suo, et a matre: et dicit hoc non esse peccatum, particeps homicidæ est.
25 Mtu mwenye tamaa huchochea mafarakano, bali anayemtumaini Yehova atafanikiwa.
Qui se iactat, et dilatat, iurgia concitat: qui vero sperat in Domino, sanabitur.
26 Yule anayeutumaini moyo wake mwenyewe ni mpumbavu, bali anayekwenda kwa hekima atajilinda mbali na hatari.
Qui confidit in corde suo, stultus est: qui autem graditur sapienter, ipse salvabitur.
27 Mwenye kuwapa masikini hatapungukiwa kitu, bali anayewafumbia macho atapokea laana nyingi.
Qui dat pauperi, non indigebit: qui despicit deprecantem, sustinebit penuriam.
28 Watu waovu wanapoinuka, watu hujificha wenyewe, lakini watu waovu wataangamia, wale watendao haki wataongezeka.
Cum surrexerint impii, abscondentur homines: cum illi perierint, multiplicabuntur iusti.

< Mithali 28 >