< Mithali 26 >

1 Kama theluji wakati wa joto au mvua kwenye mavuno, ndivyo mpumbavu asivyostahili heshima.
Come la neve non conviene all’estate, né la pioggia al tempo della mèsse, così non conviene la gloria allo stolto.
2 Kama shorowanda hurukaruka na kumeza wadudu wakati wa kuruka, ndivyo ilivyo laana isiyostahili haishuki.
Come il passero vaga qua e là e la rondine vola, così la maledizione senza motivo, non raggiunge l’effetto.
3 Mjeledi ni kwa ajili ya farasi, hatamu kwa ajili ya punda na fimbo ni kwa ajili mgongo wa wapumbavu.
La frusta per il cavallo, la briglia per l’asino, e il bastone per il dosso degli stolti.
4 Usimjibu mpumbavu na kujiunga katika upumbavu wake, au utakuwa kama yeye.
Non rispondere allo stolto secondo la sua follia, che tu non gli abbia a somigliare.
5 Mjibu mpumbavu na jiunge katika upumbavu wake, ili asiweze kuwa na busara katika macho yake mwenyewe.
Rispondi allo stolto secondo la sua follia, perché non abbia a credersi savio.
6 Anayetuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu huikata miguu yake mwenyewe na kunywa vurugu.
Chi affida messaggi a uno stolto si taglia i piedi e s’abbevera di pene.
7 Miguu ya kiwete inayoning'ia chini ni kama mithali kwenye kinywa cha wapumbavu.
Come le gambe dello zoppo son senza forza, così è una massima in bocca degli stolti.
8 Kujaribisha jiwe kwenye kombeo ni sawa na kumpa heshima mpumbavu.
Chi onora uno stolto fa come chi getta una gemma in un mucchio di sassi.
9 Mwiba unaochoma kwenye mkono wa mlevi ni kama mithali kwenye kinywa cha wapumbavu.
Una massima in bocca agli stolti è come un ramo spinoso in mano a un ubriaco.
10 Mpiga mishale anayejeruhi kila mtu ni kama mtu anayemwajiri mpumbavu au kila mtu anayepita karibu yake.
Chi impiega lo stolto e il primo che capita, è come un arciere che ferisce tutti.
11 Kama mbwa anavyorudia matapishi yake, ndivyo alivyo mpumbavu anayerudia upuuzi wake.
Lo stolto che ricade nella sua follia, è come il cane che torna al suo vomito.
12 Je unamwona mtu mwenye busara katika macho yake mwenyewe? Mpumbavu anamatumaini zaidi kuliko yeye.
Hai tu visto un uomo che si crede savio? C’è più da sperare da uno stolto che da lui.
13 Mtu mvivu husema “Kuna simba kwenye barabara! Kuna simba katikati ya njia kuu!”
Il pigro dice: “C’è un leone nella strada, c’è un leone per le vie!”
14 Kama mlango unavyogeuka kwenye bawaba zake, ndivyo alivyo mtu mvivu kwenye kitanda chake.
Come la porta si volge sui cardini così il pigro sul suo letto.
15 Mtu mvivu hutia mkono wake kwenye sufuria na bado hana nguvu kuunyanyua kwenda kwenye kinywa chake.
Il pigro tuffa la mano nel piatto; gli par fatica riportarla alla bocca.
16 Mtu mvivu ni mwenye hekima kwenye macho yake mwenyewe kuliko watu saba wenye ufahamu.
Il pigro si crede più savio di sette uomini che dànno risposte sensate.
17 Kama mtu anayeshikilia masikio ya mbwa, ndivyo alivyo mpitajia anayepata hasira kwenye ugomvi ambao si wake.
Il passante che si riscalda per una contesa che non lo concerne, è come chi afferra un cane per le orecchie.
18 Kama mtu mwendawazimu anayetupa mishale,
Come un pazzo che avventa tizzoni, frecce e morte,
19 ndivyo alivyo ambaye humdanganya jirani yake na kusema, “Je sikuwa naongea utani?”
così è colui che inganna il prossimo, e dice: “Ho fatto per ridere!”
20 Kwa kukosa kuni, moto huzimika; na pale pasipo na mmbea ugomvi hukoma.
Quando mancan le legna, il fuoco si spegne; e quando non c’è maldicente, cessan le contese.
21 Mkaa ni kwa kuwasha makaa na kuni kwa ajili ya moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuwasha ugomvi.
Come il carbone da la brace, e le legna dànno la fiamma, così l’uomo rissoso accende le liti.
22 Maneno ya mmbea ni kama chembe tamu; nazo zinashuka chini kwenye sehemu za ndani ya mwili.
Le parole del maldicente son come ghiottonerie, e penetrano fino nell’intimo delle viscere.
23 Kioo kinachofunika chombo cha udongo ni kama midomo inayoungua na moyo mbaya.
Labbra ardenti e un cuor malvagio son come schiuma d’argento spalmata sopra un vaso di terra.
24 Yule ambaye huwachukia wengine huficha hisia zake kwa midomo na hufunika uongo ndani yake mwenyewe.
Chi odia, parla con dissimulazione; ma, dentro, cova la frode.
25 Ataongea kwa huruma, lakini usimwamini, maana kuna machukizo saba kwenye moyo wake.
Quando parla con voce graziosa, non te ne fidare, perché ha sette abominazioni in cuore.
26 Ingawa chuki zake zimefunikwa kwa udanganyifu, uovu wake utakuwa wazi katika kusanyiko.
L’odio suo si nasconde sotto la finzione, ma la sua malvagità si rivelerà nell’assemblea.
27 Anayechimba shimo atatumbukia ndani yake na jiwe litamsaga yule anayelisukuma.
Chi scava una fossa vi cadrà, e la pietra torna addosso a chi la rotola.
28 Ulimi wa uongo huchukia watu unaowajeruhi na kinywa cha uongo husogeza karibu uharibifu.
La lingua bugiarda odia quelli che ha ferito, e la bocca lusinghiera produce rovina.

< Mithali 26 >