< Mithali 25 >

1 Hizi tena ni mithali za Sulemani, zilinakiliwa na watu wa Hezekia, mfalme wa Yuda.
И ово су приче Соломунове које сабраше људи Језекије цара Јудиног.
2 Ni utukufu wa Mungu kuficha jambo, bali utukufu wa wafalme kutafiti juu ya jambo.
Слава је Божија скривати ствар, а слава је царска истраживати ствар.
3 Kama mbingu ni kwa kimo na dunia ni kwa kina, ndivyo hivyo moyo wa wafalme hauchunguziki.
Висина небу и дубина земљи и срце царевима не може се досегнути.
4 Ondoa takataka kutoka kwenye fedha na mfua vyuma anaweza kutumia fedha katika ufundi wake.
Узми од сребра троску, и изаћи ће ливцу заклад.
5 Pamoja na hayo, waondoe watu waovu mbele ya mfalme na kiti chake cha enzi kitaimarishwa kwa kutenda haki.
Узми безбожника испред цара, и утврдиће се правдом престо његов.
6 Usijitukuze mwenyewe mbele ya mfalme na usisimame katika sehemu iliyoteuliwa kwa watu wakuu.
Не величај се пред царем и не стај на место где стоје властељи.
7 Ni bora yeye akuambie, “Njoo hapa” kuliko wewe kujiaibisha mbele ya mkuu.
Јер је боље да ти се каже: Ходи горе, него да те понизе пред кнезом да видиш својим очима.
8 Usiharakishe kufanya kuhukumu, kwa kile ulichokishuhudia. Maana utafanya nini mwishoni, wakati jirani yako atakapokuaibisha?
Не иди одмах да се преш, гледај шта би чинио напослетку ако би те осрамотио ближњи твој.
9 Jitetee kesi yako kati ya jirani yako na wewe na usifunue siri ya mtu mwingine,
Расправи ствар своју с ближњим својим, али туђе тајне не откривај,
10 au vinginevyo anayekusikia ataleta aibu juu yako na taarifa mbaya juu yako haiwezi kunyamazishwa.
Да те не би псовао ко чује, и срамота твоја да не би остала на теби.
11 Kunena maneno yenye kuchaguliwa vizuri, ni kama nakshi za dhahabu iliyoungwa kwenye fedha.
Златне јабуке у сребрним судима јесу згодне речи.
12 Kama pete ya dhahabu au kito kilichotengenezwa kwa dhahabu safi ndivyo lilivyo karipio la busara kwenye sikio linalosikia.
Златна је гривна и накит од најбољег злата мудри карач ономе који слуша.
13 Kama baridi ya theluji wakati wa mavuno ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wenye kumtuma; huyahifadhi maisha ya mabwana wake.
Веран је посланик као студен снежна о жетви онима који га пошаљу, и расхлађује душу својим господарима.
14 Kama mawingu na upepo bila mvua ndivyo alivyo mwenye kujisifu kuhusu zawadi asiyoitoa.
Ко се хвали даром лажним, он је као облаци и ветар без дажда.
15 Kwa uvumilivu mtawala anaweza kushawishiwa na ulimi raini unaweza kuvunja mfupa.
Стрпљењем се ублажава кнез, и мек језик ломи кости.
16 Kama utapata asali, kula ya kutosha- vingenevyo, ukila nyingi sana, utaitapika.
Кад нађеш мед, једи колико ти је доста, да не би наједавши га се избљувао га.
17 Usiweke mguu wako kwenye nyumba ya jirani yako mara nyingi, anaweza kuchoshwa nawe na kukuchukia.
Ретко нека ти нога ступа у кућу ближњег твог, да не би наситивши се тебе омрзао на те.
18 Mtu anayetoa ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yake ni kama rungu lililotumiwa katika vita, au upanga, au mshale mkali.
Ко год говори лажно сведочанство на ближњег свог, он је као маљ и мач и оштра стрела.
19 Kumtumaini mtu asiye mwaminifu wakati wa taabu ni kama jino bovu au mguu unaoteleza.
Уздање је у неверника у невољи зуб сломљен и нога уганута.
20 Kama mtu anayevua nguo katika hali ya baridi, au kama siki iliyotiwa kwenye magadi, ndivyo alivyo anayeimba wimbo kwa mwenye moyo mzito.
Ко пева песме жалосном срцу, он је као онај који свлачи хаљину на зими, и као оцат на салитру.
21 Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale na kama ana kiu, mpe maji ya kunywa,
Ако је гладан ненавидник твој, нахрани га хлеба, и ако је жедан напој га воде.
22 maana utamwekea mkaa juu ya kichwa chake na Yehova atakupa thawabu.
Јер ћеш живо угљевље згрнути на главу његову, и Господ ће ти платити.
23 Ni hakika upepo wa kaskazini huleta mvua, ndivyo mtu anayesema siri hufanya sura zikasirike.
Северни ветар носи дажд, а потајни језик лице срдито.
24 Ni bora kuishi kwenye pembe ya darini kuliko kuchangia nyumba pamoja na mwanamke mgomvi.
Боље је седети у углу од крова него са женом свадљивом у кући заједничкој.
25 Kama maji ya baridi kwa mwenye kiu, ndivyo ilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.
Добар је глас из далеке земље као студена вода жедној души.
26 Kama chemchemi iliyochafuliwa au kisima kilichoharibiwa ndivyo alivyo mtu mwema ambaye huyumbayumba mbele ya watu waovu.
Праведник који пада пред безбожником јесте као извор ногама замућен и као студенац покварен.
27 Si vema kula asali nyingi mno; hivyo ni kama kutafuta heshima baada heshima.
Јести много меда није добро, и истраживати славу није славно.
28 Mtu bila kujitawala ni kama mji ulibomolewa na usiokuwa na kuta.
Ко нема власти над духом својим, он је град разваљен без зидова.

< Mithali 25 >