< Mithali 25 >

1 Hizi tena ni mithali za Sulemani, zilinakiliwa na watu wa Hezekia, mfalme wa Yuda.
Voici maintenant les sentences du roi Salomon qui n'ont point été classées et qu'ont transcrites les amis d'Ézéchias, roi de la Judée.
2 Ni utukufu wa Mungu kuficha jambo, bali utukufu wa wafalme kutafiti juu ya jambo.
La gloire de Dieu cèle sa parole; la gloire d'un roi apprécie toute chose.
3 Kama mbingu ni kwa kimo na dunia ni kwa kina, ndivyo hivyo moyo wa wafalme hauchunguziki.
Le ciel est haut, la mer est profonde; mais le cœur d'un roi ne peut être sondé.
4 Ondoa takataka kutoka kwenye fedha na mfua vyuma anaweza kutumia fedha katika ufundi wake.
Bats de l'argent rouillé, et il sera tout à fait purifié.
5 Pamoja na hayo, waondoe watu waovu mbele ya mfalme na kiti chake cha enzi kitaimarishwa kwa kutenda haki.
Extermine les impies devant le roi, et son trône se maintiendra dans la justice.
6 Usijitukuze mwenyewe mbele ya mfalme na usisimame katika sehemu iliyoteuliwa kwa watu wakuu.
Ne te vante pas en présence du roi; ne promets rien dans les demeures des princes.
7 Ni bora yeye akuambie, “Njoo hapa” kuliko wewe kujiaibisha mbele ya mkuu.
Car il vaut mieux que l'on te dise: Viens auprès de moi, que de t'humilier en présence d'un prince. Ne dis rien que tes yeux ne l'aient vu.
8 Usiharakishe kufanya kuhukumu, kwa kile ulichokishuhudia. Maana utafanya nini mwishoni, wakati jirani yako atakapokuaibisha?
Ne t'engage pas inopinément dans une querelle, de peur que tu ne t'en repentes à la fin. Si ton ami vient à te réprimander,
9 Jitetee kesi yako kati ya jirani yako na wewe na usifunue siri ya mtu mwingine,
retire-toi dans le secret avec lui, et ne le méprise pas,
10 au vinginevyo anayekusikia ataleta aibu juu yako na taarifa mbaya juu yako haiwezi kunyamazishwa.
de peur que ton ami n'en vienne aux reproches; car alors ce seraient des querelles et des haines sans fin, et qui seraient pour toi comme la mort. La grâce et l'amitié nous délivrent de tout mal; conserve-les en toi, pour ne point devenir un sujet d'outrages, et garde tes voies dans la paix.
11 Kunena maneno yenye kuchaguliwa vizuri, ni kama nakshi za dhahabu iliyoungwa kwenye fedha.
Parler raison vaut un collier de cornaline mêlé de grains d'or.
12 Kama pete ya dhahabu au kito kilichotengenezwa kwa dhahabu safi ndivyo lilivyo karipio la busara kwenye sikio linalosikia.
Une sage parole, dans une oreille docile, vaut un pendant d'oreille où l'or est entrelacé de cornalines de grand prix.
13 Kama baridi ya theluji wakati wa mavuno ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wenye kumtuma; huyahifadhi maisha ya mabwana wake.
Le messager fidèle est, pour ceux qui l'envoient, aussi agréable que le serait la neige au temps de la moisson; il réjouit le cœur de ceux qui l'ont envoyé.
14 Kama mawingu na upepo bila mvua ndivyo alivyo mwenye kujisifu kuhusu zawadi asiyoitoa.
L'homme qui se glorifie d'un présent trompeur ne vaut pas mieux que des fléaux éclatants, tels que la tempête, les sombres nuées ou les torrents de pluie.
15 Kwa uvumilivu mtawala anaweza kushawishiwa na ulimi raini unaweza kuvunja mfupa.
La patience fait la prospérité des rois, et une langue douce amollit jusqu'aux os.
16 Kama utapata asali, kula ya kutosha- vingenevyo, ukila nyingi sana, utaitapika.
Si tu trouves du miel, n'en mange que ce qui te suffit, de peur que tu ne vomisses, si tu t'en es gorgé.
17 Usiweke mguu wako kwenye nyumba ya jirani yako mara nyingi, anaweza kuchoshwa nawe na kukuchukia.
Entre rarement chez ton ami, de peur que, rassasié de toi, il ne te prenne en haine.
18 Mtu anayetoa ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yake ni kama rungu lililotumiwa katika vita, au upanga, au mshale mkali.
L'homme qui porte contre son ami un faux témoignage ressemble à une massue, à un glaive, à une flèche acérée.
19 Kumtumaini mtu asiye mwaminifu wakati wa taabu ni kama jino bovu au mguu unaoteleza.
La dent du méchant et le pied du pervers seront détruits au jour de l'adversité.
20 Kama mtu anayevua nguo katika hali ya baridi, au kama siki iliyotiwa kwenye magadi, ndivyo alivyo anayeimba wimbo kwa mwenye moyo mzito.
Comme le vinaigre ne vaut rien à un ulcère, ainsi la douleur du corps attriste le cœur; et comme le bois est rongé par la pourriture, et les vêtements par un ver, ainsi le cœur de l'homme est rongé par la tristesse.
21 Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale na kama ana kiu, mpe maji ya kunywa,
Si ton ennemi a faim, nourris-le; s'il a soif, donne-lui à boire.
22 maana utamwekea mkaa juu ya kichwa chake na Yehova atakupa thawabu.
En agissant ainsi, tu amasseras sur sa tête des charbons ardents, et le Seigneur te comblera de biens.
23 Ni hakika upepo wa kaskazini huleta mvua, ndivyo mtu anayesema siri hufanya sura zikasirike.
L'aquilon, excite les nuées; un front sans pudeur irrite la langue.
24 Ni bora kuishi kwenye pembe ya darini kuliko kuchangia nyumba pamoja na mwanamke mgomvi.
Mieux vaut demeurer dans un coin de la terrasse qu'avec une femme querelleuse, en une maison commune.
25 Kama maji ya baridi kwa mwenye kiu, ndivyo ilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.
Comme l'eau fraîche est douce à une âme altérée, ainsi est bonne la nouvelle arrivant d'une terre lointaine.
26 Kama chemchemi iliyochafuliwa au kisima kilichoharibiwa ndivyo alivyo mtu mwema ambaye huyumbayumba mbele ya watu waovu.
Si quelqu'un ferme un puits ou corrompt une source d'eau, c'est une chose funeste comme un juste tombant en présence de l'impie.
27 Si vema kula asali nyingi mno; hivyo ni kama kutafuta heshima baada heshima.
Il n'est pas bon de manger beaucoup de miel; mais il est juste d'honorer les sages discours.
28 Mtu bila kujitawala ni kama mji ulibomolewa na usiokuwa na kuta.
Comme une ville dont les remparts sont renversés, et qui n'est plus fortifiée, ainsi est un homme qui agit sans conseil.

< Mithali 25 >