< Mithali 22 >

1 Jina jema huchaguliwa dhidi ya utajiri mwingi na fadhila ni bora kuliko fedha na dhahabu.
Une bonne renommée est préférable à de grandes richesses, et la bonne grâce à l’argent et à l’or.
2 Watu matajiri na masikini wanafanana katika hili - Yehova ni muumba wao wote.
Le riche et le pauvre se rencontrent: l’Éternel les a tous faits.
3 Mtu mwenye hekima huiona taabu na kujificha mwenyewe, bali mjinga huendelea mbele na huumia kwa ajili yake.
L’homme avisé voit le mal et se cache; mais les simples passent outre et en portent la peine.
4 Thawabu ya unyenyekevu na kumcha Yehova ni utajiri, heshima na uzima.
La fin de la débonnaireté, de la crainte de l’Éternel, c’est la richesse, et la gloire, et la vie.
5 Miiba na mitego hulala katika njia ya wakaidi; yeye anayelinda maisha yake atakuwa mbali navyo.
Il y a des épines, des pièges, sur la voie du pervers; celui qui garde son âme s’en éloigne.
6 Mfundishe mtoto njia inayompasa na wakati akiwa mzee hatayaacha mafundisho hayo.
Élève le jeune garçon selon la règle de sa voie; même lorsqu’il vieillira, il ne s’en détournera point.
7 Watu matajiri huwatawala watu masikini na mwenye kukopa ni mtumwa wa yule anayekopesha.
Le riche gouverne les pauvres, et celui qui emprunte est serviteur de l’homme qui prête.
8 Yule anayepanda udhalimu atavuna taabu na fimbo ya hasira yake itanyauka.
Qui sème l’injustice moissonnera le malheur, et la verge de son courroux prendra fin.
9 Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa, maana anashiriki mkate wake pamoja na masikini.
[Celui qui a] l’œil bienveillant sera béni, car il donne de son pain au pauvre.
10 Mfukuze mbali mwenye dhihaka, na ugomvi utaondoka, mashindano na matukano yatakoma.
Chasse le moqueur, et la querelle s’en ira, et les disputes et la honte cesseront.
11 Anayependa moyo safi na mwenye maneno ya neema, atakuwa rafiki yake mfalme.
Celui qui aime la pureté de cœur a la grâce sur les lèvres, [et] le roi est son ami.
12 Macho ya Yehova huyaangalia maarifa, bali huyapindua maneno ya wadanganyifu.
Les yeux de l’Éternel gardent la connaissance, mais il renverse les paroles du perfide.
13 Mtu mvivu husema, “Kuna simba mtaani! Nitauwawa sehemu za njia.”
Le paresseux dit: Il y a un lion là dehors, je serai tué au milieu des rues!
14 Kinywa cha malaya ni shimo lenye kina kirefu; hasira ya Yehova huchochewa dhidi ya yule anayetumbukia ndani yake.
La bouche des étrangères est une fosse profonde; celui contre qui l’Éternel est irrité y tombera.
15 Upumbavu umefungwa katika moyo wa mtoto, lakini marudi ya fimbo huutoa.
La folie est liée au cœur du jeune enfant; la verge de la correction l’éloignera de lui.
16 Anayewanyanyasa watu masikini ili kuongeza mali yake, au kuwapa matajiri, atakuwa masikini.
Celui qui opprime le pauvre, ce sera pour l’enrichir; celui qui donne au riche, ce sera pour le faire tomber dans l’indigence.
17 Tega sikio lako na usikilize maneno ya wenye busara na utumia moyo wako katika maarifa yangu,
Incline ton oreille et écoute les paroles des sages, et applique ton cœur à ma science;
18 maana itakuwa furaha kwako kama utayaweka ndani yako, kama yote yatakuwa katika midomo yako.
car c’est une chose agréable si tu les gardes au-dedans de toi: elles seront disposées ensemble sur tes lèvres.
19 Basi tumaini lako liwe kwa Yehova, ninayafundisha kwako leo- hata kwako.
Afin que ta confiance soit en l’Éternel, je te [les] ai fait connaître à toi, aujourd’hui.
20 Sijakuandikia wewe misemo thelathini ya mafundisho na maarifa,
Ne t’ai-je pas écrit des choses excellentes en conseils et en connaissance,
21 kwa kukufundisha kweli katika maneno haya yenye uaminifu, ili uwe na majibu yenye kutegemewa kwa waliokutuma?
pour te faire connaître la sûre norme des paroles de vérité, afin que tu répondes des paroles de vérité à ceux qui t’envoient?
22 Usimwibie masikini kwa sababu ni masikini, au kumponda kwenye lango,
Ne pille pas le pauvre, parce qu’il est pauvre, et ne foule pas l’affligé à la porte;
23 maana Yehova ataitetea kesi yao, na atawaibia uzima wale waliowaibia masikini.
car l’Éternel prendra en main leur cause, et dépouillera l’âme de ceux qui les dépouillent.
24 Usifanye urafiki na mtu mwenye kutawaliwa na hasira na wala usiambatane pamoja na mwenye hasira kali,
Ne sois pas l’ami de l’homme colère, et n’entre pas chez l’homme violent;
25 au utajifunza njia zake na utakuwa chambo kwa nafsi yako.
de peur que tu n’apprennes ses sentiers, et que tu n’emportes un piège dans ton âme.
26 Usiwe miongoni mwao wapigao mikono, mwenye kuahidi madeni.
Ne sois point parmi ceux qui frappent dans la main, parmi ceux qui se rendent caution pour des dettes:
27 Kama umekosa njia za kulipa, nini kitaweza kuzuia mtu kuchukua kitanda chako chini yako?
si tu n’avais pas de quoi payer, pourquoi voudrais-tu qu’on prenne ton lit de dessous toi?
28 Usiondoe jiwe la mpaka la wahenga ambalo baba zako wameweka.
Ne recule pas la borne ancienne que tes pères ont faite.
29 Je umemwona mtu aliyeuwawa kwenye kazi yake? Atasimama mbele ya wafalme; hatasimama mbele ya watu wa kawaida.
As-tu vu un homme diligent dans son travail? il se tiendra devant les rois, il ne se tiendra pas devant des gens obscurs.

< Mithali 22 >