< Mithali 17 >

1 Ni bora kuwa na utulivu pamoja chembe za mkate kuliko nyumba yenye sherehe nyingi pamoja na ugomvi.
Betere is a drie mussel with ioye, than an hous ful of sacrifices with chidyng.
2 Mtumishi mwenye busara atatawala juu ya mwana atendaye kwa aibu na atashiriki urithi kama mmoja wa ndugu.
A wijs seruaunt schal be lord of fonned sones; and he schal departe eritage among britheren.
3 Kalibu ni kwa fedha na tanuu ni kwa dhahabu, bali Yehova huisafisha mioyo.
As siluer is preued bi fier, and gold is preued bi a chymnei, so the Lord preueth hertis.
4 Mtu atendaye mabaya huwasikiliza wale wanaosema maovu; muongo anausikivu kwa wale wanaosema mambo mabaya.
An yuel man obeieth to a wickid tunge; and a fals man obeieth to false lippis.
5 Mwenye kumdhihaki masikini humtukana Muumba wake na anayefurahia msiba hatakosa adhabu.
He that dispisith a pore man, repreueth his maker; and he that is glad in the fallyng of another man, schal not be vnpunyschid.
6 Wajukuu ni taji ya wazee na wazazi huleta heshima kwa watoto wao.
The coroun of elde men is the sones of sones; and the glorie of sones is the fadris of hem.
7 Hotuba ya ushawishi haifai kwa mpumbavu; kidogo zaidi midomo ya uongo inafaa kwa ufalme.
Wordis wel set togidere bisemen not a fool; and a liynge lippe bicometh not a prince.
8 Rushwa ni kama jiwe la kiini macho kwa yule ambaye atoaye; yeye anayeiacha, hufanikiwa.
A preciouse stoon moost acceptable is the abiding of hym that sekith; whidur euere he turneth hym silf, he vndurstondith prudentli.
9 Anayesamehe kosa hutafuta upendo, bali yeye anayerudia jambo huwatenganisha marafiki wa karibu.
He that helith trespas, sekith frenschipis; he that rehersith bi an hiy word, departith hem, that ben knyt togidere in pees.
10 Karipio hupenya ndani ya mtu mwenye ufahamu kuliko mapigo mamia kwenda kwa mpumbavu.
A blamyng profitith more at a prudent man, than an hundryd woundis at a fool.
11 Mtu mbaya hutafuta uasi tu, hivyo mjumbe katiri atatumwa dhidi yake.
Euere an yuel man sekith stryues; forsothe a cruel aungel schal be sent ayens hym.
12 Ni bora kukutana na dubu aliyeporwa watoto wake kuliko kukutana na mpumbavu katika upumbavu wake.
It spedith more to meete a femal bere, whanne the whelpis ben rauyschid, than a fool tristynge to hym silf in his foli.
13 Mtu anaporudisha mabaya badala ya mema, mabaya hayatatoka katika nyumba yake.
Yuel schal not go a wei fro the hous of hym, that yeldith yuels for goodis.
14 Mwanzo wa mafarakano ni kama mtu anayefungulia maji kila mahali, hivyo ondoka kwenye mabishano kabla ya kutokea.
He that leeueth watir, is heed of stryues; and bifor that he suffrith wrong, he forsakith dom.
15 Yeye ambaye huwaachilia watu waovu au kuwalaumu wale wanaotenda haki - watu hawa wote ni chukizo kwa Yehova.
Bothe he that iustifieth a wickid man, and he that condempneth a iust man, euer ethir is abhomynable at God.
16 Kwa nini mpumbavu alipe fedha kwa kujifunza hekima, wakati hana uwezo wa kujifunza?
What profitith it to a fool to haue richessis, sithen he mai not bie wisdom? He that makith his hous hiy, sekith falling; and he that eschewith to lerne, schal falle in to yuels.
17 Rafiki hupenda kwa nyakati zote na ndugu amezaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu.
He that is a frend, loueth in al tyme; and a brother is preuyd in angwischis.
18 Mtu asiyekuwa na akili hufanya ahadi zenye mashariti na kuanza kuwajibika kwa madeni ya jirani yake.
A fonned man schal make ioie with hondis, whanne he hath bihiyt for his frend.
19 Apendaye mafarakano anapenda dhambi; ambaye hutengeneza kizingiti kirefu sana kwenye mlango wake husababisha kuvunjia kwa mifupa.
He that bithenkith discordis, loueth chidingis; and he that enhaunsith his mouth, sekith fallyng.
20 Mtu mwenye moyo wa udanganyifu hapati chochote ambacho ni chema; na mwenye ulimi wa ukaidi huanguka kwenye janga.
He that is of weiward herte, schal not fynde good; and he that turneth the tunge, schal falle in to yuel.
21 Mzazi wa mpumbavu huleta majonzi kwake mwenyewe; baba wa mpumbavu hana furaha.
A fool is borun in his schenschipe; but nether the fadir schal be glad in a fool.
22 Moyo mchangamfu ni dawa njema, bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.
A ioiful soule makith likinge age; a sorewful spirit makith drie boonys.
23 Mtu mwovu hukubali rushwa ya siri ili kupotosha njia za haki.
A wickid man takith yiftis fro the bosum, to mys turne the pathis of doom.
24 Mwenye ufahamu huelekeza uso wake kwenye hekima, bali macho ya mpumbavu huelekea ncha za dunia.
Wisdom schyneth in the face of a prudent man; the iyen of foolis ben in the endis of erthe.
25 Mwana mpumbavu ni huzuni kwa baba yake na uchungu kwa mwanamke aliyemzaa.
A fonned sone is the ire of the fadir, and the sorewe of the modir that gendride hym.
26 Pia, si vizuri kumwadhibu mwenye kutenda haki; wala si vema kuwachapa mjeledi watu waadilifu wenye ukamilifu.
It is not good to brynge in harm to a iust man; nether to smyte the prince that demeth riytfuli.
27 Mwenye maarifa hutumia maneno machache na mwenye ufahamu ni mtulivu.
He that mesurith his wordis, is wijs and prudent; and a lerud man is of preciouse spirit.
28 Hata mpumbavu hudhaniwa kuwa na busara kama akikaa kimya; wakati anapokaa amefunga kinywa chake, anafikiriwa kuwa na akili.
Also a foole, if he is stille, schal be gessid a wijs man; and, if he pressith togidre hise lippis, he `schal be gessid an vndurstondynge man.

< Mithali 17 >