< Mithali 15 >

1 Jawabu la upole huondoa ghadhabu, bali neno la ukatili huchochea hasira.
LA blanda respuesta quita la ira: mas la palabra áspera hace subir el furor.
2 Ulimi wa watu mwenye hekima husifu maarifa, bali kinywa cha wapumbavu humwaga upuuzi.
La lengua de los sabios adornará la sabiduría: mas la boca de los necios hablará sandeces.
3 Macho ya Yehova yapo kila mahali, yakiwatazama juu ya waovu na wema.
Los ojos de Jehová están en todo lugar, mirando á los malos y á los buenos.
4 Ulimi unaoponya ni mti wa uzima, bali ulimi wa udanganyifu huvunja moyo.
La sana lengua es árbol de vida: mas la perversidad en ella es quebrantamiento de espíritu.
5 Mpumbavu hudharau marudi ya baba yake, bali yeye anayejifunza kutokana na masahihisho ni mwenye hekima.
El necio menosprecia el consejo de su padre: mas el que guarda la corrección, vendrá á ser cuerdo.
6 Katika nyumba ya wale watendao haki kuna hazina kubwa, bali mapato ya watu waovu huwapa taabu.
En la casa del justo hay gran provisión; empero turbación en las ganancias del impío.
7 Midomo ya wenye hekima husambaza maarifa, bali mioyo ya wapumbavu haifanyi hivyo.
Los labios de los sabios esparcen sabiduría: mas no así el corazón de los necios.
8 Yehova anachukia sadaka za watu waovu, bali maombi ya watu waadilifu ndiyo furaha yake.
El sacrificio de los impíos es abominación á Jehová: mas la oración de los rectos es su gozo.
9 Yehova anachukia njia ya watu waovu, bali anampenda yule ambaye huandama haki.
Abominación es á Jehová el camino del impío: mas él ama al que sigue justicia.
10 Marudi ya ukatili hungojea kwa yeyote ambaye huiacha njia na yule ambaye huchukia masahihisho atakufa.
La reconvención es molesta al que deja el camino: y el que aborreciere la corrección, morirá.
11 Kuzimu na uharibifu vipo wazi mbele za Yehova; je si zaidi sana mioyo ya wana wa wanadamu? (Sheol h7585)
El infierno y la perdición están delante de Jehová: ¡cuánto más los corazones de los hombres! (Sheol h7585)
12 Mwenye mzaha huchukia masahihisho; hatakwenda kwa wenye hekima.
El escarnecedor no ama al que le reprende; ni se allega á los sabios.
13 Moyo wenye furaha husababisha uchangamfu wa uso, bali huzuni huvunja moyo.
El corazón alegre hermosea el rostro: mas por el dolor de corazón el espíritu se abate.
14 Moyo wa mwenye ufahamu hutafuta maarifa, bali kinywa cha wapumbavu hujilisha kwenye upuuzi.
El corazón entendido busca la sabiduría: mas la boca de los necios pace necedad.
15 Siku zote za watu waliokandamizwa ni taabu, bali moyo wenye furaha unakaramu daima.
Todos los días del afligido son trabajosos: mas el de corazón contento [tiene] un convite continuo.
16 Bora kitu kidogo pamoja na kumcha Mungu kuliko hazina kubwa pamoja na ghasia.
Mejor es lo poco con el temor de Jehová, que el gran tesoro donde hay turbación.
17 Bora mlo wenye mboga kukiwa na upendo kuliko kuandaliwa ndama aliyenona kwa chuki.
Mejor es la comida de legumbres donde hay amor, que de buey engordado donde hay odio.
18 Mtu mwenye hasira huchochea mabishano, bali mtu ambaye hukawia kukasirika hutuliza ugomvi.
El hombre iracundo mueve contiendas: mas el que tarde se enoja, apaciguará la rencilla.
19 Mapito ya mtu goigoi ni kama sehemu yenye uwa wa miiba, bali mapito ya mtu mwadilifu ni njia kuu iliyojengwa imara.
El camino del perezoso es como seto de espinos: mas la vereda de los rectos [como] una calzada.
20 Mwana mwenye busara huleta furaha kwa baba yake, bali mtu mpumbavu humdharau mama yake.
El hijo sabio alegra al padre: mas el hombre necio menosprecia á su madre.
21 Upuuzi humfurahia mtu ambaye amepungukiwa akili, bali mwenye ufahamu hutembea katika njia nyofu.
La necedad es alegría al falto de entendimiento: mas el hombre entendido enderezará su proceder.
22 Mipango huharibika ambapo hakuna ushauri, bali washauri wengi wanafanikiwa.
Los pensamientos son frustrados donde no hay consejo; mas en la multitud de consejeros se afirman.
23 Mtu anapata furaha wakati anapotoa jibu la kufaa; je ni zuri kiasi gani neno kwa wakati muafaka!
Alégrase el hombre con la respuesta de su boca: y la palabra á su tiempo, ¡cuán buena es!
24 Njia ya uzima huwapeleka juu watu wenye hekima, ili waondoke kutoka chini kuzimu. (Sheol h7585)
El camino de la vida [es] hacia arriba al entendido, para apartarse del infierno abajo. (Sheol h7585)
25 Yehova hurarua urithi wa mwenye kiburi, bali huzilinda mali za mjane.
Jehová asolará la casa de los soberbios: mas él afirmará el término de la viuda.
26 Yehova huyachukia mawazo ya watu waovu, bali maneno ya upole ni safi.
Abominación son á Jehová los pensamientos del malo: mas las expresiones de los limpios [son] limpias.
27 Mporaji huleta shida kwenye familia yake, bali yeye ambaye huchukia rushwa ataishi.
Alborota su casa el codicioso: mas el que aborrece las dádivas vivirá.
28 Moyo wa yule atendaye haki hutafakari kabla ya kujibu, bali kinywa cha watu waovu humwanga ubaya wake wote.
El corazón del justo piensa para responder: mas la boca de los impíos derrama malas cosas.
29 Yehova yupo mbali na watu waovu, bali husikia maombi ya wale watendao haki.
Lejos está Jehová de los impíos: mas él oye la oración de los justos.
30 Nuru ya macho huleta furaha moyoni na habari njema ni afya kwenye mwili.
La luz de los ojos alegra el corazón; y la buena fama engorda los huesos.
31 Kama utazingatia wakati mtu anapokurekebisha jinsi ya kuishi, utabaki miongoni mwa watu wenye busara.
La oreja que escucha la corrección de vida, entre los sabios morará.
32 Yeye anayekataa karipio hujidharau mwenyewe, bali yule asikilizaye masahihisho hujipatia ufahamu.
El que tiene en poco la disciplina, menosprecia su alma: mas el que escucha la corrección, tiene entendimiento.
33 Kumcha Yehova hufundisha hekima na unyenyekevu huja kabla ya heshima.
El temor de Jehová es enseñanza de sabiduría: y delante de la honra [está] la humildad.

< Mithali 15 >