< Mithali 15 >

1 Jawabu la upole huondoa ghadhabu, bali neno la ukatili huchochea hasira.
A gentle answer turns away wrath, but a harsh word stirs up anger.
2 Ulimi wa watu mwenye hekima husifu maarifa, bali kinywa cha wapumbavu humwaga upuuzi.
The tongue of the wise commends knowledge, but the mouths of fools gush out folly.
3 Macho ya Yehova yapo kila mahali, yakiwatazama juu ya waovu na wema.
The LORD’s eyes are everywhere, keeping watch on the evil and the good.
4 Ulimi unaoponya ni mti wa uzima, bali ulimi wa udanganyifu huvunja moyo.
A gentle tongue is a tree of life, but deceit in it crushes the spirit.
5 Mpumbavu hudharau marudi ya baba yake, bali yeye anayejifunza kutokana na masahihisho ni mwenye hekima.
A fool despises his father’s correction, but he who heeds reproof shows prudence.
6 Katika nyumba ya wale watendao haki kuna hazina kubwa, bali mapato ya watu waovu huwapa taabu.
In the house of the righteous is much treasure, but the income of the wicked brings trouble.
7 Midomo ya wenye hekima husambaza maarifa, bali mioyo ya wapumbavu haifanyi hivyo.
The lips of the wise spread knowledge; not so with the heart of fools.
8 Yehova anachukia sadaka za watu waovu, bali maombi ya watu waadilifu ndiyo furaha yake.
The sacrifice made by the wicked is an abomination to the LORD, but the prayer of the upright is his delight.
9 Yehova anachukia njia ya watu waovu, bali anampenda yule ambaye huandama haki.
The way of the wicked is an abomination to the LORD, but he loves him who follows after righteousness.
10 Marudi ya ukatili hungojea kwa yeyote ambaye huiacha njia na yule ambaye huchukia masahihisho atakufa.
There is stern discipline for one who forsakes the way. Whoever hates reproof shall die.
11 Kuzimu na uharibifu vipo wazi mbele za Yehova; je si zaidi sana mioyo ya wana wa wanadamu? (Sheol h7585)
Sheol and Abaddon are before the LORD— how much more then the hearts of the children of men! (Sheol h7585)
12 Mwenye mzaha huchukia masahihisho; hatakwenda kwa wenye hekima.
A scoffer doesn’t love to be reproved; he will not go to the wise.
13 Moyo wenye furaha husababisha uchangamfu wa uso, bali huzuni huvunja moyo.
A glad heart makes a cheerful face, but an aching heart breaks the spirit.
14 Moyo wa mwenye ufahamu hutafuta maarifa, bali kinywa cha wapumbavu hujilisha kwenye upuuzi.
The heart of one who has understanding seeks knowledge, but the mouths of fools feed on folly.
15 Siku zote za watu waliokandamizwa ni taabu, bali moyo wenye furaha unakaramu daima.
All the days of the afflicted are wretched, but one who has a cheerful heart enjoys a continual feast.
16 Bora kitu kidogo pamoja na kumcha Mungu kuliko hazina kubwa pamoja na ghasia.
Better is little, with the fear of the LORD, than great treasure with trouble.
17 Bora mlo wenye mboga kukiwa na upendo kuliko kuandaliwa ndama aliyenona kwa chuki.
Better is a dinner of herbs, where love is, than a fattened calf with hatred.
18 Mtu mwenye hasira huchochea mabishano, bali mtu ambaye hukawia kukasirika hutuliza ugomvi.
A wrathful man stirs up contention, but one who is slow to anger appeases strife.
19 Mapito ya mtu goigoi ni kama sehemu yenye uwa wa miiba, bali mapito ya mtu mwadilifu ni njia kuu iliyojengwa imara.
The way of the sluggard is like a thorn patch, but the path of the upright is a highway.
20 Mwana mwenye busara huleta furaha kwa baba yake, bali mtu mpumbavu humdharau mama yake.
A wise son makes a father glad, but a foolish man despises his mother.
21 Upuuzi humfurahia mtu ambaye amepungukiwa akili, bali mwenye ufahamu hutembea katika njia nyofu.
Folly is joy to one who is void of wisdom, but a man of understanding keeps his way straight.
22 Mipango huharibika ambapo hakuna ushauri, bali washauri wengi wanafanikiwa.
Where there is no counsel, plans fail; but in a multitude of counsellors they are established.
23 Mtu anapata furaha wakati anapotoa jibu la kufaa; je ni zuri kiasi gani neno kwa wakati muafaka!
Joy comes to a man with the reply of his mouth. How good is a word at the right time!
24 Njia ya uzima huwapeleka juu watu wenye hekima, ili waondoke kutoka chini kuzimu. (Sheol h7585)
The path of life leads upward for the wise, to keep him from going downward to Sheol. (Sheol h7585)
25 Yehova hurarua urithi wa mwenye kiburi, bali huzilinda mali za mjane.
The LORD will uproot the house of the proud, but he will keep the widow’s borders intact.
26 Yehova huyachukia mawazo ya watu waovu, bali maneno ya upole ni safi.
The LORD detests the thoughts of the wicked, but the thoughts of the pure are pleasing.
27 Mporaji huleta shida kwenye familia yake, bali yeye ambaye huchukia rushwa ataishi.
He who is greedy for gain troubles his own house, but he who hates bribes will live.
28 Moyo wa yule atendaye haki hutafakari kabla ya kujibu, bali kinywa cha watu waovu humwanga ubaya wake wote.
The heart of the righteous weighs answers, but the mouth of the wicked gushes out evil.
29 Yehova yupo mbali na watu waovu, bali husikia maombi ya wale watendao haki.
The LORD is far from the wicked, but he hears the prayer of the righteous.
30 Nuru ya macho huleta furaha moyoni na habari njema ni afya kwenye mwili.
The light of the eyes rejoices the heart. Good news gives health to the bones.
31 Kama utazingatia wakati mtu anapokurekebisha jinsi ya kuishi, utabaki miongoni mwa watu wenye busara.
The ear that listens to reproof lives, and will be at home amongst the wise.
32 Yeye anayekataa karipio hujidharau mwenyewe, bali yule asikilizaye masahihisho hujipatia ufahamu.
He who refuses correction despises his own soul, but he who listens to reproof gets understanding.
33 Kumcha Yehova hufundisha hekima na unyenyekevu huja kabla ya heshima.
The fear of the LORD teaches wisdom. Before honour is humility.

< Mithali 15 >