< Mithali 14 >

1 Mwanamke mwenye busara huijenga nyumba yake, bali mwanamke mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
La mujer sabia edifica su casa; mas la loca con sus manos la derriba.
2 Yeye aendaye kwa uaminifu humcha Yehova, bali mkaidi humdharau katika njia zake.
El que camina en su rectitud teme al SEÑOR; mas el pervertido en sus caminos lo menosprecia.
3 Katika kinywa cha mpumbavu hutoka chipukizi la kiburi chake, bali midomo ya wenye busara itawalinda.
En la boca del loco está la vara de la soberbia; mas los labios de los sabios los guardarán.
4 Pale pasipo na mifugo hori la kulishia ni safi, bali mazao mengi huweza kupatikana kwa nguvu za maksai.
Sin bueyes el alfolí está limpio; mas por la fuerza del buey hay abundancia de pan.
5 Shahidi mwaminifu hasemi uongo, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
El testigo verdadero no mentirá; mas el testigo falso hablará mentiras.
6 Mwenye dharau hutafuta hekima na hakuna hata, bali maarifa huja kwa urahisi kwa mwenye ufahamu.
El burlador buscó la sabiduría, y no la halló; mas la sabiduría al hombre entendido viene fácil.
7 Nenda mbali kutoka kwa mtu mpumbavu, maana hutapata maarifa kwenye midomo yake.
Vete de delante del hombre loco, pues no le conociste labios de ciencia.
8 Hekima ya mtu mwenye busara ni kuifahamu njia yake mwenyewe, bali upuuzi wa wapumbavu ni udanganyifu.
La sabiduría del cuerdo es entender su camino; mas la locura de los locos es engaño.
9 Wapumbavu hudharau wakati sadaka ya hatia inapotolewa, bali miongoni mwao waaminifu hushiriki fadhila.
Los locos se hablan pecado; mas entre los rectos hay amor.
10 Moyo unayajua machungu yake mwenyewe na hakuna mgeni anayeshiriki furaha yake.
El corazón conoce la amargura de su alma; y extraño no se entremeterá en su alegría.
11 Nyumba ya waovu itaangamizwa, bali hema ya watu waaminifu itasitawi.
La casa de los impíos será asolada; mas la tienda de los rectos florecerá.
12 Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, lakini mwisho wake huelekea mauti tu.
Hay camino que al hombre parece derecho; pero su fin son caminos de muerte.
13 Moyo unaweza kucheka lakini bado ukawa katika maumivu na furaha inaweza kukoma ikawa huzuni.
Aun en la risa el burlador tendrá dolor en el corazón; y el término de aquella alegría es congoja.
14 Yule asiyemwaminifu atapata anachostahili kwa njia zake, bali mtu mwema atapata kilicho chake.
De sus caminos será harto el desviado de corazón; y el hombre de bien será apartado de él.
15 Yeye ambaye hakufundishwa huamini kila kitu, bali mtu mwenye hekima huzifikiria hatua zake.
El simple cree a toda palabra; mas el entendido entiende sus pasos.
16 Mtu mwenye hekima huogopa na kutoka kwenye ubaya, bali mpumbavu huliacha onyo kwa ujasiri.
El sabio teme, y se aparta del mal; mas el loco se arrebata, y confía.
17 Yeye ambaye anakuwa na hasira kwa haraka hufanya mambo ya kipumbavu, na mtu anayefanya hila mbaya huchukiwa.
El que presto se enoja, hará locura; y el hombre malicioso será aborrecido.
18 Wajinga hurithi upumbavu, lakini watu wenye hekima wamezingirwa kwa maarifa.
Los simples heredarán la locura; mas los cuerdos se coronarán de sabiduría.
19 Hao ambao ni waovu watainama mbele yao walio wema na wale wenye uovu watasujudu kwenye malango ya wenye haki.
Los malos se inclinarán delante de los buenos, y los impíos a las puertas del justo.
20 Mtu masikini huchukiwa hata na marafiki zake, bali watu matajiri wanamarafiki wengi.
El pobre es odioso aun a su amigo; pero muchos son los que aman al rico.
21 Yeye ambaye huonyesha dharau kwa jirani yake anafanya dhambi, bali yule ambaye huonyesha fadhila kwa masikini anafuraha.
El pecador menosprecia a su prójimo; mas el que tiene misericordia de los pobres, es bienaventurado.
22 Je wale wanaofanya njama mbaya hawapotei? Bali wale wenye mpango wa kutenda mema watapokea agano la uaminifu na udhamini
¿No yerran los que piensan mal? Pero los que piensan bien alcanzarán misericordia y verdad.
23 Katika kazi zote ngumu huja faida, bali palipo na maongezi tu, huelekea kwenye umasikini.
En toda labor hay fruto; mas el hablar y no hacer, empobrece.
24 Taji ya watu wenye busara ni utajiri wao, bali upuuzi wa wapumbavu huwaletea upuu zaidi.
La corona de los sabios es su sabiduría; mas lo que distingue a los locos es su locura.
25 Shahidi mkweli huokoa maisha, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
El testigo verdadero libra las almas; mas el engañoso hablará mentiras.
26 Mtu anapokuwa na hofu ya Yehova, pia anakuwa na matumaini zaidi ndani yake; vitu hivi vitakuwa kama sehemu imara ya ulinzi kwa watoto wa mtu huyu.
En el temor del SEÑOR está la fuerte confianza; y allí sus hijos tendrán esperanza.
27 Kumcha Yehova ni chemchemi ya uzima, ili kwamba mtu aweze kujiepusha kutoka katika mitego ya mauti.
El temor del SEÑOR es manantial de vida, para ser apartado de los lazos de la muerte.
28 Utukufu wa mfalme upo katika idadi kubwa ya watu wake, bali pasipo watu mfalme huangamia.
En la multitud del pueblo está la gloria del rey; y en la falta del pueblo la flaqueza del príncipe.
29 Mtu mvumilivu anaufahamu mkubwa, bali mtu mwepesi wa kuhamaki hukuza upuuzi.
El que tarde se aíra, es grande de entendimiento; mas el corto de espíritu engrandece la locura.
30 Moyo wenye raha ni uzima wa mwili, bali husuda huozesha mifupa.
El corazón apacible es vida a la carne; mas la envidia, pudrimiento de huesos.
31 Anayemkandamiza masikini humlaani Muumba wake, bali anayeonyesha fadhila kwa wahitaji humtukuza yeye.
El que oprime al pobre, afrenta a su Hacedor; mas el que tiene misericordia del pobre, lo honra.
32 Mtu mwovu huangushwa chini kwa matendo yake mabaya, bali mtu mwenye haki anakimbilio hata katika kifo.
Por su maldad será lanzado el impío; mas el justo en su muerte tiene esperanza.
33 Hekima hukaa katika moyo wa ufahamu, bali hata miongoni mwa wapumbavu hujiachilia mwenyewe kwa kujulikana
En el corazón del cuerdo reposará la sabiduría; y es dado a conocer en medio de los locos.
34 Kutenda haki huliinua taifa, bali dhambi ni chukizo kwa watu wowote.
La justicia engrandece un pueblo; mas el pecado es afrenta de las naciones.
35 Fadhila ya mfalme ni kwa mtumishi mwenye kutenda kwa hekima, bali hasira yake ni kwa yule atendaye kwa kuaibisha.
La benevolencia del rey es para con el siervo entendido; mas su enojo contra el que lo avergüenza.

< Mithali 14 >