< Mithali 10 >

1 Mithali za Sulemani. Mwana mwenye hekima humfurahisha baba yake lakini mwana mpumbavu huleta majonzi kwa mama yake.
משלי שלמה בן חכם ישמח-אב ובן כסיל תוגת אמו
2 Hazina zilizolimbikizwa kwa uovu hakosa thamani, bali kwa kutenda haki hujilinda mbali na kifo.
לא-יועילו אוצרות רשע וצדקה תציל ממות
3 Yehova hawaachi wale watendao haki wapate njaa, bali hamu ya waovu huizuia.
לא-ירעיב יהוה נפש צדיק והות רשעים יהדף
4 Mkono mlegevu humfanya mtu awe masikini, bali mkono wa mtu mwenye bidii hupata utajiri.
ראש--עשה כף-רמיה ויד חרוצים תעשיר
5 Mwana mwenye busara hukusanya mazao wakati wa kiangazi, bali ni aibu kwake alalaye wakati wa mavuno.
אגר בקיץ בן משכיל נרדם בקציר בן מביש
6 Zawadi kutoka kwa Mungu zipo juu ya kichwa cha wale watendao haki; bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
ברכות לראש צדיק ופי רשעים יכסה חמס
7 Mtu atendaye haki anatufurahisha tunapomkumbuka, bali jina la mwovu litaoza.
זכר צדיק לברכה ושם רשעים ירקב
8 Wale wenye akili hukubali maagiza, bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataangamia.
חכם-לב יקח מצות ואויל שפתים ילבט
9 Yeye anayetembea katika uadilifu hutembea katika usalama, bali yule anayepotosha njia zake, ataonekana.
הולך בתם ילך בטח ומעקש דרכיו יודע
10 Yeye ambaye hukonyeza kwa jicho lake huleta majonzi, bali mpumbavu mwenye maneno mengi atatupwa chini.
קרץ עין יתן עצבת ואויל שפתים ילבט
11 Kinywa cha mwenye kutenda haki ni kama chemchemi ya maji ya uzima, bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
מקור חיים פי צדיק ופי רשעים יכסה חמס
12 Chuki huchochea mafarakano, bali upendo hufunika juu ya makwazo yote.
שנאה תערר מדנים ועל כל-פשעים תכסה אהבה
13 Hekima inapatikana kwenye kinywa cha mtu mwenye ufahamu, bali fimbo ni kwa ajili ya mgongo wa yule asiye na akili.
בשפתי נבון תמצא חכמה ושבט לגו חסר-לב
14 Watu wenye hekima hutunza maarifa, bali kinywa cha mpumbavu huleta uharibifu karibu.
חכמים יצפנו-דעת ופי-אויל מחתה קרבה
15 Mali ya mtu tajiri ni mji wake mwenye ngome; ufukara wa masikini ni uharibifu wao.
הון עשיר קרית עזו מחתת דלים רישם
16 Mshahara wa watenda haki huelekea kwenye uzima; manufaa ya waovu huelekea dhambini.
פעלת צדיק לחיים תבואת רשע לחטאת
17 Kuna njia kwenda kwenye uzima kwa yule anayefuata maongozo, bali anayekataa maonyo hupotea.
ארח לחיים שומר מוסר ועזב תוכחת מתעה
18 Yeye afichaye chuki anamidomo ya uongo, na yeye anayesambaza kashfa ni mpumbavu.
מכסה שנאה שפתי-שקר ומוצא דבה הוא כסיל
19 Katika maneno mengi, hapakosi uhalifu, bali aliyemwangalifu katika usemi wake ni mwenye busara.
ברב דברים לא יחדל-פשע וחושך שפתיו משכיל
20 Ulimi wa yule atendaye haki ni fedha safi; kuna thamani ndogo katika moyo wa mbaya.
כסף נבחר לשון צדיק לב רשעים כמעט
21 Midomo ya yule atendaye haki huwastawisha wengi, bali wapumbavu hufa kwa sababu ya kukosa akili.
שפתי צדיק ירעו רבים ואוילים בחסר-לב ימותו
22 Zawadi njema za Yehova huleta utajiri na haweki maumivu ndani yake.
ברכת יהוה היא תעשיר ולא-יוסף עצב עמה
23 Uovu ni mchezo achezao mpumbavu, bali hekima ni furaha kwa mtu mwenye ufahamu.
כשחוק לכסיל עשות זמה וחכמה לאיש תבונה
24 Hofu ya mwenye uovu humkumba ghafla, bali shauku ya mwenye haki itatimizwa.
מגורת רשע היא תבואנו ותאות צדיקים יתן
25 Waovu ni kama dhoruba inayopita, na hawapo tena, bali mwenye haki ni msingi unaodumu milele.
כעבור סופה ואין רשע וצדיק יסוד עולם
26 Kama siki kwenye meno na moshi kwenye macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
כחמץ לשנים--וכעשן לעינים כן העצל לשלחיו
27 Hofu ya Yehova huongeza maisha, bali miaka ya waovu itakuwa mifupi.
יראת יהוה תוסיף ימים ושנות רשעים תקצרנה
28 Matumaini ya wale watendao haki ndiyo furaha yao, bali miaka ya waovu itakuwa mifupi.
תוחלת צדיקים שמחה ותקות רשעים תאבד
29 Njia ya Yehova huwalinda wale wenye uadilifu, bali kwa waovu ni uhalibifu.
מעוז לתם דרך יהוה ומחתה לפעלי און
30 Wale watendao haki hawataondolewa, bali waovu hawatabaki katika nchi.
צדיק לעולם בל-ימוט ורשעים לא ישכנו-ארץ
31 Katika kinywa cha wale watendao haki hutoka tunda la hekima, bali ulimi wa kupotosha utakatwa.
פי-צדיק ינוב חכמה ולשון תהפכות תכרת
32 Midomo ya wale watendao mema huyajua yanayokubalika, bali kinywa cha waovu, huyajua yanayopotosha.
שפתי צדיק ידעון רצון ופי רשעים תהפכות

< Mithali 10 >