< Hesabu 7 >

1 Siku ambayo Musa alikamilsha masikani, alitia mafuta na kuiweka wakfu kwa BWANA, pamoja na mapambo yake. Aliifanyia hivyo madhabahu na vyombo vyake. Aliitia mafuta na kuiweka wakfu kwa BWANA.
Le jour où Moïse acheva de dresser la Demeure, de l’oindre et de la sanctifier avec tous ses ustensiles, ainsi que l’autel avec tous ses ustensiles; lorsqu’il les eut oints et sanctifiés,
2 Siku hiyo, viongozi wa Israeli na wale vichwa vya familia za mababu walitoa sadaka. Hawa wanaume walikuwa viongozi wa makabila. Walisaidia kuhesabu watu kwenye ile sensa.
les princes d’Israël, chefs de leurs maisons patriarcales, présentèrent leurs offrandes: c’étaient les princes des tribus, ceux qui avaient présidé au dénombrement.
3 Walileta sadaka zao kwa BWANA. Walileta magari sita yaliyofunikwa na mafahari kumi na mbili. Walileta gari moja kwa kila viongozi wawili, kila kiongozi alileta fahari moja. Walileta vitu hivi mbele ya masikani.
Ils amenèrent leur offrande devant Yahweh: six chars couverts et douze bœufs, soit un char pour deux princes et un bœuf pour chaque prince, et ils les présentèrent devant la Demeure.
4 Kisha BWANA akanena na Musa, akamwambia,
Yahweh parla à Moïse, en disant:
5 “Uzipokee hizo sadaka kutoka kwao na uzitumie kwa matumizi ya kazi ya hema ya kukutania. Uwape hizo sadaka Walawi, kwa kila mmoja kadri ya uhitaji wa kazi yake.”
« Reçois d’eux ces choses, et qu’elles soient employées pour le service de la tente de réunion; tu les donneras aux Lévites, à chacun selon les besoins de son service. »
6 Musa akayatwaa yale magari na mafahari. na kuwapatia Walawi.
Moïse, ayant pris les chars et les bœufs, les remit aux Lévites.
7 Aliwapa magari mawili na mafahari wanne wale wa uzao wa Gerishoni, kwa sababu ndivyo kazi yao ilivyohitaji.
Il donna deux chars et quatre bœufs aux fils de Gerson, selon les besoins de leur service;
8 Aliwapatia uzao wa Merari magari manne na mafahari nane, chini ya uangalizi wa Ithamari mwana wa Haruni kuhani. Alifanya hivi kwa sababu ya uhitaji wa kazi yao.
il donna quatre chars et huit bœufs aux fils de Mérari, selon les besoins de leur service, sous la surveillance d’Ithamar, fils d’Aaron, le prêtre.
9 Lakini wale wa uzao wa Kohathi hakuwapa chochote kwa sababu wao waliangalia vitu vtakatifu amabvyo vilipaswa vibebwe mabagani mwao, siyo kwa magari.
Mais il n’en donna pas aux fils de Caath, parce que, ayant le service des objets sacrés, ils devaient les porter sur leurs épaules.
10 Viongozi walitoa bidhaa zo zingine kwa ajili ya kuwekwa wakfu kwa madhabahu katika siku ile ambayo Musa aliitia mafuta madhabahu. Viongozi walitoa sadaka zao mbele ya madhabahu hiyo.
Les princes présentèrent leur offrande pour la dédicace de l’autel, le jour où on l’oignit; les princes présentèrent leur offrande devant l’autel.
11 BWANA akasema na Musa, “kila kiongozi atatoa sadaka kwa siku yake kwa ajili ya kuiweka wakfu madhabahu.”
Et Yahweh dit à Moïse: « Que chaque jour un prince vienne présenter son offrande pour la dédicace de l’autel. »
12 Katika siku ya kwanza, Nashoni mwana wa Aminadabu, wa kabila ya Yuda, alitoa sadaka yake.
Celui qui présenta son offrande le premier jour fut Nahasson, fils d’Aminadab, de la tribu de Juda.
13 Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli 130 na bakuli moja ya fedha ambayo uzito wake ni shekeli sabini, kwa kipimo cha mahali patakatifu. Vyombo vyote hivi vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
Il offrit: un plat d’argent du poids de cent trente sicles, une coupe d’argent de soixante-dix sicles, selon le sicle du sanctuaire, l’un et l’autre pleins de fleur de farine pétrie à l’huile, pour l’oblation;
14 Pia alimpa unga wa dhahabu kiasi cha bakuli moja chenye uzani wa shekeli kumi kilichojaa ubani
un godet d’or de dix sicles, plein de parfum;
15 Alitoa sadaka ya kuteketezwa fahari mchanga, kondoo dume mmoja na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja.
un jeune taureau, un bélier et un agneau d’un an pour l’holocauste;
16 Alitoa beberu kama kama sadaka ya hatia.
un bouc pour le sacrifice pour le péché,
17 Alitoa makisai mbili, kondoo waume watano, beberu watano na wanakondoo dume watano wenye umri wa mwaka mmoja mmoja, kama sadaka ya amani. Hii ilikuwa sadaka ya Nashoni mwana wa Aminadabu.
et, pour le sacrifice pacifique, deux bœufs, cinq béliers, cinq boucs et cinq agneaux d’un an. Telle fut l’offrande de Nahasson, fils d’Aminadab.
18 Siku ya pili, Nethanel mwana wa Zuari, kiongozi wa Isakari, alitoa sadaka yake.
Le second jour, Nathanaël, fils de Suar, prince de la tribu d’Issachar, présenta son offrande.
19 Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha ya uzito wa shekeli130 na bakuli moja la fedha lenye uzani wa sheli sabini, kwa kipimo cha mahali patakatifu. Viyombo vyote hivi vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kwa sadaka ya unga.
Il offrit: un plat d’argent du poids de cent trente sicles, une coupe d’argent de soixante-dix sicles, selon le sicle du sanctuaire, l’un et l’autre pleins de fleur de farine pétrie à l’huile, pour l’oblation;
20 Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzito wa shekeli kumi, iliyojaa ubani.
un godet d’or de dix sicles, plein de parfum;
21 Alitoa sadaka ya kuteketezwa fahari mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo mmoja dume.
un jeune taureau, un bélier et un agneau d’un an pour l’holocauste;
22 Alitoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi.
un bouc pour le sacrifice pour le péché,
23 Alitoa makisai wawili, Kondoo dume watano, beberu watano, na wanakondoo dume watano wa mwaka mmoja mmoja kuwa sadaka ya amani. Hiii likuwa sadaka ya Nethaneli mwana wa Zuari.
et, pour le sacrifice pacifique, deux bœufs, cinq béliers, cinq boucs et cinq agneaux d’un an. Telle fut l’offrande de Nathanaël, fils de Suar.
24 Siku ya tatu, Eliabu mwana wa Heloni, kiongozi wa uzao wa Zabuloni alitoa sadaka yake.
Le troisième jour vint le prince des fils de Zabulon, Eliab, fils de Hélon;
25 Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha lenye uzito wa shekeli sabini kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. vyombo vyote hivi vilikuwa vimeja unga mwembemba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
il offrit: un plat d’argent du poids de cent trente sicles, et une coupe d’argent de soixante-dix sicles, selon le sicle du sanctuaire, l’un et l’autre pleins de fleur de farine pétrie à l’huile, pour l’oblation;
26 Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzani wa shekeli kumi, kilichojaa ubani.
un godet d’or de dix sicles, plein de parfum;
27 Alitoa sadaka ya fahari mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja.
un jeune taureau, un bélier et un agneau d’un an pour l’holocauste;
28 Alitoa beberu mmoja kama sadaka ya dhambi.
un bouc pour le sacrifice pour le péché,
29 Alitoa makisai wawili, kondoo dume watano, beberu watano, na wanakondoo dume watano wa mwaka mmoja mmoja. kuwa sadaka ya amani. Hii ilikuwa sadaka ya Eliabu mwana Heloni.
et, pour le sacrifice pacifique, deux bœufs, cinq béliers, cinq boucs et cinq agneaux d’un an. Telle fut l’offrande d’Eliab, fils de Hélon.
30 Siku ya nne, Elizuri mwana wa shedeuri, kiongozi wa uzao wa Reubeni, alitoa sadaka yake.
Le quatrième jour vint le prince des fils de Ruben, Elisur, fils de Sédéur;
31 Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzani wa shekeli sabini, kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. Vyombo hivi vyote vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
il offrit: un plat d’argent du poids de cent trente sicles, et une coupe d’argent de soixante-dix sicles, selon le sicle du sanctuaire, l’un et l’autre pleins de fleur de farine pétrie à l’huile, pour l’oblation;
32 Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzani wa shekeli kumi, kilichoo jaa ubani.
un godet d’or de dix sicles, plein de parfum;
33 Alitoa sadaka ya kuteketezwa fahari mmoja mchanga, mwanakondoo dume mmoja mchanga wa mwaka mmoja.
un jeune taureau, un bélier et un agneau d’un an pour l’holocauste;
34 Alitoa beberu moja kuwa sadaka ya dhambi.
un bouc pour le sacrifice pour le péché,
35 Alitoa maksai wawili, kondoo dume watano wa mwaka mmoja kuwa sadaka ya amani. Hii ilikuwa sadaka ya Elizuri mwana wa Shedeuri.
et, pour le sacrifice pacifique, deux bœufs, cinq béliers, cinq boucs et cinq agneaux d’un an. Telle fut l’offrande d’Elisur, fils de Sédéur.
36 Siku ya tano, Shelumieli mwana wa Zurishadai, kiongozi wa uzao wa Simeoni, alitoa sadaka yake.
Le cinquième jour vint le prince des fils de Siméon, Salamiel, fils de Surisaddaï;
37 Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shaekali 130 na bakuli mojala fedha lenye uzani wa shekeli sabini kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. Vyombo vyote hivi vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
il offrit: un plat d’argent du poids de cent trente sicles, et une coupe d’argent de soixante-dix sicles, selon le sicle du sanctuaire, l’un et l’autre pleins de fleur de farine pétrie à l’huile, pour l’oblation;
38 Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzani wa shekeli kumi, uliojaa ubani.
un godet d’or de dix sicles, plein de parfum;
39 Alitoa sadaka ya kuteketezwa fahari mchanga, dume la kondoo, na dume la mwanakondoo la mwaka mmoja.
un jeune taureau, un bélier et un agneau d’un an pour l’holocauste;
40 Alitoa beberu moja kuwa sadaka ya dhambi.
un bouc pour le sacrifice pour le péché,
41 Alitao maksai wawili, dume wawili wa kondoo, beberu watano, na dume watano wa wanakondoo wa mwaka mmoja mmoja kuwa sadaka y amani. Hiindiyo iliyokuwa sadka ya Shelumei mwana wa Zurishadai.
et, pour le sacrifice pacifique, deux bœufs, cinq béliers, cinq boucs et cinq agneaux d’un an. Telle fut l’offrande de Salamiel, fils de Surisaddaï.
42 Siku ya sita, Eliasafu mwana wa Deuli, kiongozi wa uzao wa Gadi, alitoa sadaka yake.
Le sixième jour vint le prince des fils de Gad, Eliasaph, fils de Duel;
43 Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli 130 na bakuli la shaba lenye uzani wa shekeli sabini, kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. Vyombo hivi vyote vilikuwa vimejaa unga mwembemba uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya sadaka ya unga.
il offrit: un plat d’argent du poids de cent trente sicles, et une coupe d’argent de soixante-dix sicles, selon le sicle du sanctuaire, l’un et l’autre pleins de fleur de farine pétrie à l’huile, pour l’oblation;
44 Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzani wa shekeli kumi, kilichojaa ubani.
un godet d’or de dix sicles, plein de parfum;
45 Alitoa sadaka ya kuteketezwa ya fahari changa, kondoo dume mmoja, na dume la mwanakondoo mmoja wa mwaka mmoja.
un jeune taureau, un bélier et un agneau d’un an pour l’holocauste;
46 Alitoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi.
un bouc pour le sacrifice pour le péché,
47 Alitoa maksai wawili, dume watano wa kondoo, beberu watano, na wanakondoo dume watano wa mwaka mmoja kuwa sadaka ya amani. Hii ndiyo iliyokuwa sadaka ya Eliasafu mwana wa Deuli.
et, pour le sacrifice pacifique, deux bœufs, cinq béliers, cinq boucs et cinq agneaux d’un an. Telle fut l’offrande d’Eliasaph, fils de Duel.
48 Siku ya saba, Elishama mwana wa Amihudi, kiongozi wa uzao wa Efraimu, alitoa sadaka yake.
Le septième jour vint le prince des fils d’Ephraïm, Elisama, fils d’Ammiud;
49 Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli 130 na bakuli la fedha lenye uzani wa shekeli sabini, kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. Vyombo hivi vyote ilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
il offrit: un plat d’argent du poids de cent trente sicles, et une coupe d’argent de soixante-dix sicles, selon le sicle du sanctuaire, l’un et l’autre pleins de fleur de farine pétrie à l’huile, pour l’oblation;
50 Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu, kilichojaa ubani
un godet d’or de dix sicles, plein de parfum;
51 Alitoa sadaka ya kuteketezwa, fahari mmoja, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja.
un jeune taureau, un bélier et un agneau d’un an pour l’holocauste;
52 Alitoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi.
un bouc pour le sacrifice pour le péché,
53 Alitoa maksai wawili, kondo dume watano, beberu watano, na na wanakondoo dume watano wa mwaka mmoja mmoja kuwa sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sdaka ya Elishama mwana wa Amidu.
et, pour le sacrifice pacifique, deux bœufs, cinq béliers, cinq boucs et cinq agneaux d’un an. Telle fut l’offrande d’Elisama, fils d’Ammiud.
54 Siku y a nane, Gamaliel mwana wa Pedazuri, kiongozi wa uzao wa Manase, alitoa sadaka yake.
Le huitième jour vint le prince des fils de Manassé, Gamaliel, fils de Phadassur;
55 Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli130 na bakuli moja la fedha lenye uzani wa shekeli sabini, kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. Vyombo vyote hivi vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
il offrit: un plat d’argent du poids de cent trente sicles, et une coupe d’argent de soixante-dix sicles, selon le sicle du sanctuaire, l’un et l’autre pleins de fleur de farine pétrie à l’huile, pour l’oblation;
56 Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzani wa shekeli kumi, kilichojaa ubani.
un godet d’or de dix sicles, plein de parfum;
57 Alitoa sadaka ya kuteketezwa ya fahari mmoja, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja.
un jeune taureau, un bélier et un agneau d’un an pour l’holocauste;
58 Alitoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi.
un bouc pour le sacrifice pour le péché,
59 Alitoa maksai wawili, kondoo dume watano, beberu watano, na wanakondoo dume watano wa mwaka mmoja mmoja kuwa sadaka ya amani. Hii ndiyo iliyokuwa sadaka ya Gamaliel mwana wa Pedazuri.
et, pour le sacrifice pacifique, deux bœufs, cinq béliers, cinq boucs et cinq agneaux d’un an. Telle fut l’offrande de Gamaliel, fils de Phadassur.
60 Siku ya tisa, Abidani mwana wa Gidioni, kiongozi wa uzao wa Benjamini, alitoa sadaka yake.
Le neuvième jour vint le prince des fils de Benjamin, Abidan, fils de Gédéon;
61 Sadaka yake ilikuwa sahani moja yafedha yenye uzani wa sheli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzito wa shekeli sabini, kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. Vyombo vyote hivi vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
il offrit: un plat d’argent du poids de cent trente sicles, et une coupe d’argent de soixante-dix sicles, selon le sicle du sanctuaire, l’un et l’autre pleins de fleur de farine pétrie à l’huile, pour l’oblation;
62 Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzani wa shekeli kumi, kilichojaa ubani.
un godet d’or de dix sicles, plein de parfum;
63 Alitoa sadaka ya kuteketezwa fahari mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja.
un jeune taureau, un bélier et un agneau d’un an pour l’holocauste;
64 Alitoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi.
un bouc pour le sacrifice pour le péché,
65 Alitoa makisai wawili, kondoo dume watano, beberu watano, na wanakondoo dume watano kuwa sadaka ya amani. Hii ndiyo iliyokuwa sadaka ya Abidani mwana wa Gidioni.
et, pour le sacrifice pacifique, deux bœufs, cinq béliers, cinq boucs et cinq agneaux d’un an. Telle fut l’offrande d’Abidan, fils de Gédéon.
66 Siku ya kumi, Ahizeri mwana wa Amishadai kiongozi wa Dani alitoa sadaka yake.
Le dixième jour vint le prince des fils de Dan, Ahiéser, fils d’Ammisaddaï;
67 Alitoa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shaekeli 130 na bakuli moja lenye uzani wa shekeli sabini, kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. Vyombo vyote hivi vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
il offrit: un plat d’argent du poids de cent trente sicles, et une coupe d’argent de soixante-dix sicles, selon le sicle du sanctuaire, l’un et l’autre pleins de fleur de farine pétrie à l’huile, pour l’oblation;
68 Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzito wa shekeli kumi, kilichojaa ubani.
un godet d’or de dix sicles, plein de parfum;
69 Alitoa sadaka ya kuteketezwa fahari mmoja mchanga, dume moja la kondoo, na dume moja la mwanakondoo wa mwaka mmoja.
un jeune taureau, un bélier et un agneau d’un an pour l’holocauste;
70 Alitoa beberu moja kuwa sadaka ya dhambi.
un bouc pour le sacrifice pour le péché,
71 Alitoa maksai wawili, kondoo dume watano, beberu watano, na wanakondoo dume watano wa mwaka mmoja mmoja, kuwa sadaka ya amani. Hii ndiyo iliyokuwa sadaka ya Ahizeri mwana wa Amishadai.
et, pour le sacrifice pacifique, deux bœufs, cinq béliers, cinq boucs et cinq agneaux d’un an. Telle fut l’offrande d’Ahiéser, fils d’Ammisaddaï.
72 Siku ya kumi na moja. Pagieli mwana wa Okrani kiongozi wa uzao wa Asheri alaitoa sadaka yake.
Le onzième jour vint le prince des fils d’Aser, Phégiel, fils d’Ochran;
73 Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzani wa shekeli sabani, kwa kipimo cha shekeli ya mahali patakatifu. Vyombo vyote hivi ilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
il offrit: un plat d’argent du poids de cent trente sicles, et une coupe d’argent de soixante-dix sicles, selon le sicle du sanctuaire, l’un et l’autre pleins de fleur de farine pétrie à l’huile, pour l’oblation;
74 Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzani wa shekeli kumi, kilichojaa ubani.
un godet d’or de dix sicles, plein de parfum;
75 Alitoa sadaka ya kuteketezwa fahari mmoja mchanga. dume la kondoo moja, dume moja la mwanakondoo wa mwaka mmoja.
un jeune taureau, un bélier et un agneau d’un an pour l’holocauste;
76 Alitoa beberu moja kuwa sadaka ya dhambi.
un bouc pour le sacrifice pour le péché,
77 Alitoa maksai wawili, dume watano wa kondoo, na wanakondoo dume watano kuwa sadaka ya amani. Hii ndiyo iliyokuwa sadaka ya Pagieli mwana wa Okrani.
et, pour le sacrifice pacifique, deux bœufs, cinq béliers, cinq boucs et cinq agneaux d’un an. Telle fut l’offrande de Phégiel, fils d’Ochran.
78 Siku ya kumi na mbili., Ahira mwana wa Enani, kiongozi wa uzao wa Naftali, alitoa sadaka yake.
Le douzième jour vint le prince des fils de Nephtali, Ahira, fils d’Enan;
79 Sadaka yake ailikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shaekeli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzani wa shekeli sabini, kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. Vyombo vyote hivi vilikuwa vimejaa unga mwembamba ulichanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
il offrit: un plat d’argent du poids de cent trente sicles, et une coupe d’argent de soixante-dix sicles, selon le sicle du sanctuaire, l’un et l’autre pleins de fleur de farine pétrie à l’huile, pour l’oblation;
80 Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzani wa shekeli kumi, kilichojaa ubani.
un godet d’or de dix sicles, plein de parfum;
81 Alitoa sadaka ya kuteketezwa fahari mmoja mchanga, dume moja la kondoo, na mwanakondoo dume moja wa mwaka mmoja.
un jeune taureau, un bélier et un agneau d’un an pour l’holocauste;
82 Alitoa beberu moja kuwa sadaka ya dhambi.
un bouc pour le sacrifice pour le péché,
83 Alitoa maksai wawili, kondoo dume watano, beberu watano, na wanakondoo dume watano wa mwaka mmoja mmoja kuwa sadaka ya amani. Hii ndiyo iliyokuwa sadaka ya Ahra mwana wa Enani.
et, pour le sacrifice pacifique, deux bœufs, cinq béliers, cinq boucs et cinq agneaux d’un an. Telle fut l’offrande d’Ahira, fils d’Enan.
84 Viongozi wa Israeli waliviweka wakfu hivi vitu vyote siku ambayo Musa alimimina mafuta kwenye madhabahu. Waliziweka wakfu zile sahani kumi na mbili za fedha, Bakuli kumi na mbili za fedha, na vijiko kumi na vili vya dhahabu.
Tels furent les dons des princes d’Israël pour la dédicace de l’autel, le jour où on l’oignit: douze plats d’argent, douze coupes d’argents et douze godets d’or;
85 Zile sahani za fedha kila moja ilikuwa na uzani wa shaekeli 130 na kila bakuli ye fedha ilikuwa na uzani wa shekeli sabini. Vyombo vyote vya fedh vilikuwa na ujumla ya uzani wa shekeli 2, 400, kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu.
chaque plat d’argent pesait cent trente sicles, et chaque coupe soixante-dix; total de l’argent de ces ustensiles: deux mille quatre cent sicles, selon le sicle du sanctuaire; —
86 Vile vijiko vya dhahabu vilivyokuwa vimejaa ubani, vilikuwa na uzani wa shekeli kumi kila kimoja. Vijiko vyote vya dhahabu vilikuwa na uzani wa shekeli 120.
les douze godets d’or pleins de parfum, chacun de dix sicles, selon le sicle du sanctuaire; total de l’or des godets: cent vingt sicles. —
87 Waliwatenga wanyama wote kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, fahari kumi na wawili, kondoo dume kumi na wawili, na wanakondoo dume kumi na wawili wa mwaka mmoja mmoja. Walitoa sadaka yao ya unga. Walitoa beberu kumi na wawili kuwa sadaka ya dhambi.
Total des animaux pour l’holocauste: douze jeunes taureaux, douze béliers et douze agneaux d’un an, avec leurs oblations. Douze boucs pour le sacrifice pour le péché. —
88 Kutokana na ng'ombe zao, walitoa fahari ishirini na nne, kondoo dume sitini beberu sitini, na wanakondoo dume sitini wa mwaka mmoja mmoja kuwa sadaka ya amani. Hii ilikuwa kwa ajiliya kuiweka wafu ile madhabahu baada ya kumiminiwa mafuta.
Total des animaux pour le sacrifice pacifique: vingt-quatre bœufs, soixante béliers, soixante boucs et soixante agneaux d’un an. Tels furent les dons offerts pour la dédicace de l’autel, après qu’on l’eut oint.
89 Musa alipoingia kwenye hema ya kukutania kusema na BWANA, ndipo alipoisikia sauti yake ikisema naye. BWANA alinena naye kutoka juu ya kiti cha rehema kilichokuwa juu ya sanduku la ushahidi, kutoka katikati ya makerubi. Alinena naye.
Lorsque Moïse entrait dans la tente de réunion pour parler avec Yahweh, il entendait la voix qui lui parlait de dessus le propitiatoire placé sur l’arche du témoignage, entre les deux chérubins. Et il lui parlait.

< Hesabu 7 >