< Hesabu 7 >

1 Siku ambayo Musa alikamilsha masikani, alitia mafuta na kuiweka wakfu kwa BWANA, pamoja na mapambo yake. Aliifanyia hivyo madhabahu na vyombo vyake. Aliitia mafuta na kuiweka wakfu kwa BWANA.
And it came to pass in the day in which Moses finished the setting-up of the tabernacle, that he anointed it, and consecrated it, and all its furniture, and the altar and all its furniture, he even anointed them, and consecrated them.
2 Siku hiyo, viongozi wa Israeli na wale vichwa vya familia za mababu walitoa sadaka. Hawa wanaume walikuwa viongozi wa makabila. Walisaidia kuhesabu watu kwenye ile sensa.
And the princes of Israel brought [gifts], twelve princes of their fathers' houses: these were the heads of tribes, these are they that presided over the numbering.
3 Walileta sadaka zao kwa BWANA. Walileta magari sita yaliyofunikwa na mafahari kumi na mbili. Walileta gari moja kwa kila viongozi wawili, kila kiongozi alileta fahari moja. Walileta vitu hivi mbele ya masikani.
And they brought their gift before the Lord, six covered waggons, and twelve oxen; a waggon from two princes, and a calf from each: and they brought them before the tabernacle.
4 Kisha BWANA akanena na Musa, akamwambia,
And the Lord spoke to Moses, saying,
5 “Uzipokee hizo sadaka kutoka kwao na uzitumie kwa matumizi ya kazi ya hema ya kukutania. Uwape hizo sadaka Walawi, kwa kila mmoja kadri ya uhitaji wa kazi yake.”
Take of them, and they shall be for the works of the services of the tabernacle of witness: and you shall give them to the Levites, to each one according to his ministration.
6 Musa akayatwaa yale magari na mafahari. na kuwapatia Walawi.
And Moses took the waggons and the oxen, and gave them to the Levites.
7 Aliwapa magari mawili na mafahari wanne wale wa uzao wa Gerishoni, kwa sababu ndivyo kazi yao ilivyohitaji.
And he gave two waggons and four oxen to the sons of Gedson, according to their ministrations.
8 Aliwapatia uzao wa Merari magari manne na mafahari nane, chini ya uangalizi wa Ithamari mwana wa Haruni kuhani. Alifanya hivi kwa sababu ya uhitaji wa kazi yao.
And four waggons and eight oxen he gave to the sons of Merari according to their ministrations, by Ithamar the son of Aaron the priest.
9 Lakini wale wa uzao wa Kohathi hakuwapa chochote kwa sababu wao waliangalia vitu vtakatifu amabvyo vilipaswa vibebwe mabagani mwao, siyo kwa magari.
But to the sons of Caath he gave them not, because they have the ministrations of the sacred things: they shall bear them on their shoulders.
10 Viongozi walitoa bidhaa zo zingine kwa ajili ya kuwekwa wakfu kwa madhabahu katika siku ile ambayo Musa aliitia mafuta madhabahu. Viongozi walitoa sadaka zao mbele ya madhabahu hiyo.
And the rulers brought [gifts] for the dedication of the altar, in the day in which he anointed it, and the rulers brought their gifts before the altar.
11 BWANA akasema na Musa, “kila kiongozi atatoa sadaka kwa siku yake kwa ajili ya kuiweka wakfu madhabahu.”
And the Lord said to Moses, One chief each day, they shall offer their gifts a chief each day for the dedication of the altar.
12 Katika siku ya kwanza, Nashoni mwana wa Aminadabu, wa kabila ya Yuda, alitoa sadaka yake.
And he that offered his gift on the first day, was Naasson the son of Aminadab, prince of the tribe of Juda.
13 Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli 130 na bakuli moja ya fedha ambayo uzito wake ni shekeli sabini, kwa kipimo cha mahali patakatifu. Vyombo vyote hivi vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
And he brought his gift, one silver charger of a hundred and thirty shekels was its weight, one silver bowl, of seventy shekels according to the holy shekel; both full of fine flour kneaded with oil for a meat-offering.
14 Pia alimpa unga wa dhahabu kiasi cha bakuli moja chenye uzani wa shekeli kumi kilichojaa ubani
One golden censer of ten shekels full of incense.
15 Alitoa sadaka ya kuteketezwa fahari mchanga, kondoo dume mmoja na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja.
One calf of the herd, one ram, one he-lamb of a year old for a whole burnt offering;
16 Alitoa beberu kama kama sadaka ya hatia.
and one kid of the goats for a sin-offering.
17 Alitoa makisai mbili, kondoo waume watano, beberu watano na wanakondoo dume watano wenye umri wa mwaka mmoja mmoja, kama sadaka ya amani. Hii ilikuwa sadaka ya Nashoni mwana wa Aminadabu.
And for a sacrifice of peace-offering, two heifers, five rams, five he goats, five ewe-lambs of a year old: this [was] the gift of Naasson the son of Aminadab.
18 Siku ya pili, Nethanel mwana wa Zuari, kiongozi wa Isakari, alitoa sadaka yake.
On the second day Nathanael son of Sogar, the prince of the tribe of Issachar, brought [his offering].
19 Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha ya uzito wa shekeli130 na bakuli moja la fedha lenye uzani wa sheli sabini, kwa kipimo cha mahali patakatifu. Viyombo vyote hivi vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kwa sadaka ya unga.
And he brought his gift, one silver charger, its weight a hundred and thirty shekels, one silver bowl of seventy shekels according to the holy shekel; both full of fine flour kneaded with oil for a meat-offering.
20 Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzito wa shekeli kumi, iliyojaa ubani.
One censer of ten golden shekels, full of incense.
21 Alitoa sadaka ya kuteketezwa fahari mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo mmoja dume.
One calf of the herd, one ram, one he-lamb of a year old for a whole burnt offering,
22 Alitoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi.
and one kid of the goats for a sin-offering.
23 Alitoa makisai wawili, Kondoo dume watano, beberu watano, na wanakondoo dume watano wa mwaka mmoja mmoja kuwa sadaka ya amani. Hiii likuwa sadaka ya Nethaneli mwana wa Zuari.
And for a sacrifice, a peace-offering, two heifers, five rams, five he-goats, five ewe-lambs of a year old: this [was] the gift of Nathanael the son of Sogar.
24 Siku ya tatu, Eliabu mwana wa Heloni, kiongozi wa uzao wa Zabuloni alitoa sadaka yake.
On the third day the prince of the sons of Zabulon, Eliab the son of Chaelon.
25 Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha lenye uzito wa shekeli sabini kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. vyombo vyote hivi vilikuwa vimeja unga mwembemba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
[He brought] his gift, one silver charger, its weight a hundred and thirty shekels, one silver bowl of seventy shekels according to the holy shekel; both full of fine flour kneaded with oil for a meat-offering.
26 Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzani wa shekeli kumi, kilichojaa ubani.
One golden censer of ten shekels, full of incense.
27 Alitoa sadaka ya fahari mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja.
One calf of the herd, one ram, one he-lamb of a year old for a whole burnt offering,
28 Alitoa beberu mmoja kama sadaka ya dhambi.
and one kid of the goats for a sin-offering.
29 Alitoa makisai wawili, kondoo dume watano, beberu watano, na wanakondoo dume watano wa mwaka mmoja mmoja. kuwa sadaka ya amani. Hii ilikuwa sadaka ya Eliabu mwana Heloni.
And for a sacrifice of peace-offering, two heifers, five rams, five he-goats, five ewe-lambs of a year old: this [was] the gift of Eliab the son of Chaelon.
30 Siku ya nne, Elizuri mwana wa shedeuri, kiongozi wa uzao wa Reubeni, alitoa sadaka yake.
On the fourth day Elisur the son of Sediur, the prince of the children of Ruben.
31 Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzani wa shekeli sabini, kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. Vyombo hivi vyote vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
[He brought] his gift, one silver charger, its weight a hundred and thirty shekels, one silver bowl of seventy shekels according to the holy shekel; both full of fine flour kneaded with oil for a meat-offering.
32 Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzani wa shekeli kumi, kilichoo jaa ubani.
One golden censer of ten shekels full of incense.
33 Alitoa sadaka ya kuteketezwa fahari mmoja mchanga, mwanakondoo dume mmoja mchanga wa mwaka mmoja.
One calf of the herd, one ram, one he-lamb of a year old for a whole burnt offering,
34 Alitoa beberu moja kuwa sadaka ya dhambi.
and one kid of the goats for a sin-offering.
35 Alitoa maksai wawili, kondoo dume watano wa mwaka mmoja kuwa sadaka ya amani. Hii ilikuwa sadaka ya Elizuri mwana wa Shedeuri.
And for a sacrifice of peace-offering, two heifers, five rams, five he-goats, five ewe-lambs of a year old: this [was] the gift of Elisur the son of Sediur.
36 Siku ya tano, Shelumieli mwana wa Zurishadai, kiongozi wa uzao wa Simeoni, alitoa sadaka yake.
On the fifth day the prince of the children of Symeon, Salamiel the son of Surisadai.
37 Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shaekali 130 na bakuli mojala fedha lenye uzani wa shekeli sabini kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. Vyombo vyote hivi vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
[He brought] his gift, one silver charger, its weight one hundred and thirty shekels, one silver bowl of seventy shekels according to the holy shekel; both full of fine flour kneaded with oil for a meat-offering.
38 Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzani wa shekeli kumi, uliojaa ubani.
One golden censer of ten shekels, full of incense.
39 Alitoa sadaka ya kuteketezwa fahari mchanga, dume la kondoo, na dume la mwanakondoo la mwaka mmoja.
One calf of the herd, one ram, one he-lamb of a year old for a whole burnt offering,
40 Alitoa beberu moja kuwa sadaka ya dhambi.
and one kid of the goats for a sin-offering.
41 Alitao maksai wawili, dume wawili wa kondoo, beberu watano, na dume watano wa wanakondoo wa mwaka mmoja mmoja kuwa sadaka y amani. Hiindiyo iliyokuwa sadka ya Shelumei mwana wa Zurishadai.
And for a sacrifice of peace-offering, two heifers, five rams, five he-goats, five ewe-lambs of a year old: this [was] the gift of Salamiel the son of Surisadai.
42 Siku ya sita, Eliasafu mwana wa Deuli, kiongozi wa uzao wa Gadi, alitoa sadaka yake.
On the sixth day the prince of the sons of Gad, Elisaph the son of Raguel.
43 Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli 130 na bakuli la shaba lenye uzani wa shekeli sabini, kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. Vyombo hivi vyote vilikuwa vimejaa unga mwembemba uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya sadaka ya unga.
[He brought] his gift, one silver charger, its weight a hundred and thirty shekels, one silver bowl of seventy shekels according to the holy shekel; both full of fine flour kneaded with oil for a meat offering.
44 Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzani wa shekeli kumi, kilichojaa ubani.
One golden censer of ten shekels, full of incense.
45 Alitoa sadaka ya kuteketezwa ya fahari changa, kondoo dume mmoja, na dume la mwanakondoo mmoja wa mwaka mmoja.
One calf of the herd, one ram, one he-lamb of a year old for a whole burnt offering,
46 Alitoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi.
and one kid of the goats for a sin-offering.
47 Alitoa maksai wawili, dume watano wa kondoo, beberu watano, na wanakondoo dume watano wa mwaka mmoja kuwa sadaka ya amani. Hii ndiyo iliyokuwa sadaka ya Eliasafu mwana wa Deuli.
And for a sacrifice of peace-offering, two heifers, five rams, five he-goats, five ewe-lambs of a year old: this [was] the gift of Elisaph the son of Raguel.
48 Siku ya saba, Elishama mwana wa Amihudi, kiongozi wa uzao wa Efraimu, alitoa sadaka yake.
On the seventh day the prince of the sons of Ephraim, Elisama the son of Emiud.
49 Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli 130 na bakuli la fedha lenye uzani wa shekeli sabini, kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. Vyombo hivi vyote ilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
[He brought] his gift, one silver charger, its weight was a hundred and thirty shekels, one silver bowl of seventy shekels according to the holy shekel; both full of fine flour kneaded with oil for a meat-offering.
50 Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu, kilichojaa ubani
One golden censer of ten shekels, full of incense.
51 Alitoa sadaka ya kuteketezwa, fahari mmoja, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja.
One calf of the herd, one ram, one he-lamb of a year old for a whole burnt offering,
52 Alitoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi.
and one kid of the goats for a sin-offering.
53 Alitoa maksai wawili, kondo dume watano, beberu watano, na na wanakondoo dume watano wa mwaka mmoja mmoja kuwa sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sdaka ya Elishama mwana wa Amidu.
And for a sacrifice of peace-offering, two heifers, five rams, five he-goats, five ewe-lambs of a year old: this [was] the gift of Elisama the son of Emiud.
54 Siku y a nane, Gamaliel mwana wa Pedazuri, kiongozi wa uzao wa Manase, alitoa sadaka yake.
On the eighth day the prince of the sons of Manasse, Gamaliel the son of Phadassur.
55 Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli130 na bakuli moja la fedha lenye uzani wa shekeli sabini, kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. Vyombo vyote hivi vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
[He brought] his gift, one silver charger, its weight one hundred and thirty shekels, one silver bowl of seventy shekels according to the holy shekel; both full of fine flour mingled with oil for a meat-offering.
56 Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzani wa shekeli kumi, kilichojaa ubani.
One golden censer of ten shekels, full of incense.
57 Alitoa sadaka ya kuteketezwa ya fahari mmoja, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja.
One calf of the herd, one ram, one he-lamb of a year old for a whole burnt offering,
58 Alitoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi.
and one kid of the goats for a sin-offering.
59 Alitoa maksai wawili, kondoo dume watano, beberu watano, na wanakondoo dume watano wa mwaka mmoja mmoja kuwa sadaka ya amani. Hii ndiyo iliyokuwa sadaka ya Gamaliel mwana wa Pedazuri.
And for a sacrifice of peace-offering two heifers, five rams, five he-goats, five ewe-lambs of a year old: this [was] the gift of Gamaliel the son of Phadassur.
60 Siku ya tisa, Abidani mwana wa Gidioni, kiongozi wa uzao wa Benjamini, alitoa sadaka yake.
On the ninth day the prince of the sons of Benjamin, Abidan the son of Gadeoni.
61 Sadaka yake ilikuwa sahani moja yafedha yenye uzani wa sheli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzito wa shekeli sabini, kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. Vyombo vyote hivi vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
[He brought] his gift, one silver charger, its weight a hundred and thirty [shekels], one silver bowl of seventy shekels according to the holy shekel; both full of fine flour mingled with oil for a meat-offering.
62 Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzani wa shekeli kumi, kilichojaa ubani.
One golden censer of ten shekels, full of incense.
63 Alitoa sadaka ya kuteketezwa fahari mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja.
One calf of the herd, one ram, one he-lamb of a year old for a whole burnt offering,
64 Alitoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi.
and one kid of the goats for a sin-offering.
65 Alitoa makisai wawili, kondoo dume watano, beberu watano, na wanakondoo dume watano kuwa sadaka ya amani. Hii ndiyo iliyokuwa sadaka ya Abidani mwana wa Gidioni.
And for a sacrifice of peace-offering, two heifers, five rams, five he-goats, five ewe-lambs of a year old: this [was] the gift of Abidan the son of Gadeoni.
66 Siku ya kumi, Ahizeri mwana wa Amishadai kiongozi wa Dani alitoa sadaka yake.
On the tenth day the prince of the sons of Dan, Achiezer the son of Amisadai.
67 Alitoa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shaekeli 130 na bakuli moja lenye uzani wa shekeli sabini, kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. Vyombo vyote hivi vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
[He brought] his gift, one silver charger, its weight a hundred and thirty [shekels], one silver bowl of seventy shekels according to the holy shekel; both full of fine flour kneaded with oil for a meat-offering.
68 Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzito wa shekeli kumi, kilichojaa ubani.
One golden censer of ten shekels, full of incense.
69 Alitoa sadaka ya kuteketezwa fahari mmoja mchanga, dume moja la kondoo, na dume moja la mwanakondoo wa mwaka mmoja.
One calf of the herd, one ram, one he-lamb of a year old for a whole burnt offering,
70 Alitoa beberu moja kuwa sadaka ya dhambi.
and one kid of the goats for a sin-offering.
71 Alitoa maksai wawili, kondoo dume watano, beberu watano, na wanakondoo dume watano wa mwaka mmoja mmoja, kuwa sadaka ya amani. Hii ndiyo iliyokuwa sadaka ya Ahizeri mwana wa Amishadai.
And for a sacrifice of peace-offering, two heifers, five rams, five he-goats, five ewe-lambs of a year old. This [was] the gift of Achiezer the son of Amisadai.
72 Siku ya kumi na moja. Pagieli mwana wa Okrani kiongozi wa uzao wa Asheri alaitoa sadaka yake.
On the eleventh day the prince of the sons of Aser, Phageel the son of Echran.
73 Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzani wa shekeli sabani, kwa kipimo cha shekeli ya mahali patakatifu. Vyombo vyote hivi ilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
[He brought] his gift, one silver charger, its weight a hundred and thirty [shekels], one silver bowl of seventy shekels according to the holy shekel; both full of fine flour mingled with oil for a meat-offering.
74 Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzani wa shekeli kumi, kilichojaa ubani.
One golden censer of ten shekels, full of incense.
75 Alitoa sadaka ya kuteketezwa fahari mmoja mchanga. dume la kondoo moja, dume moja la mwanakondoo wa mwaka mmoja.
One calf of the herd, one ram, one he-lamb of a year old for a whole burnt offering,
76 Alitoa beberu moja kuwa sadaka ya dhambi.
and one kid of the goats for a sin-offering.
77 Alitoa maksai wawili, dume watano wa kondoo, na wanakondoo dume watano kuwa sadaka ya amani. Hii ndiyo iliyokuwa sadaka ya Pagieli mwana wa Okrani.
And for a sacrifice of peace-offering, two heifers, five rams, five he-goats, five ewe-lambs of a year old: this [was] the gift of Phageel the son of Echran.
78 Siku ya kumi na mbili., Ahira mwana wa Enani, kiongozi wa uzao wa Naftali, alitoa sadaka yake.
On the twelfth day the prince of the sons of Nephthali, Achire the son of Aenan.
79 Sadaka yake ailikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shaekeli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzani wa shekeli sabini, kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. Vyombo vyote hivi vilikuwa vimejaa unga mwembamba ulichanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
[He brought] his gift, one silver charger, its weight a hundred and thirty shekels; one silver bowl of seventy shekels according to the holy shekel; both full of fine flour mingled with oil for a meat offering.
80 Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzani wa shekeli kumi, kilichojaa ubani.
One golden censer of ten shekels, full of incense.
81 Alitoa sadaka ya kuteketezwa fahari mmoja mchanga, dume moja la kondoo, na mwanakondoo dume moja wa mwaka mmoja.
One calf of the herd, one ram, one he-lamb of a year old for a whole burnt offering,
82 Alitoa beberu moja kuwa sadaka ya dhambi.
and one kid of the goats for a sin-offering.
83 Alitoa maksai wawili, kondoo dume watano, beberu watano, na wanakondoo dume watano wa mwaka mmoja mmoja kuwa sadaka ya amani. Hii ndiyo iliyokuwa sadaka ya Ahra mwana wa Enani.
And for a sacrifice of peace-offering, two heifers, five rams, five he-goats, five ewe-lambs of a year old: this [was] the gift of Achire the son of Aenan.
84 Viongozi wa Israeli waliviweka wakfu hivi vitu vyote siku ambayo Musa alimimina mafuta kwenye madhabahu. Waliziweka wakfu zile sahani kumi na mbili za fedha, Bakuli kumi na mbili za fedha, na vijiko kumi na vili vya dhahabu.
This was the dedication of the altar in the day in which [Moses] anointed it, by the princes of the sons of Israel; twelve silver chargers, twelve silver bowls, twelve golden censers:
85 Zile sahani za fedha kila moja ilikuwa na uzani wa shaekeli 130 na kila bakuli ye fedha ilikuwa na uzani wa shekeli sabini. Vyombo vyote vya fedh vilikuwa na ujumla ya uzani wa shekeli 2, 400, kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu.
each charger of a hundred and thirty shekels, and each bowl of seventy shekels: all the silver of the vessels [was] two thousand four hundred shekels, the shekels according to the holy shekel.
86 Vile vijiko vya dhahabu vilivyokuwa vimejaa ubani, vilikuwa na uzani wa shekeli kumi kila kimoja. Vijiko vyote vya dhahabu vilikuwa na uzani wa shekeli 120.
Twelve golden censers full of incense: all the gold of the shekels, a hundred and twenty shekels.
87 Waliwatenga wanyama wote kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, fahari kumi na wawili, kondoo dume kumi na wawili, na wanakondoo dume kumi na wawili wa mwaka mmoja mmoja. Walitoa sadaka yao ya unga. Walitoa beberu kumi na wawili kuwa sadaka ya dhambi.
All the cattle for whole burnt offerings, twelve calves, twelve rams, twelve he-lambs of a year old, and their meat-offerings, and their drink-offerings: and twelve kids of the goats for sin-offering.
88 Kutokana na ng'ombe zao, walitoa fahari ishirini na nne, kondoo dume sitini beberu sitini, na wanakondoo dume sitini wa mwaka mmoja mmoja kuwa sadaka ya amani. Hii ilikuwa kwa ajiliya kuiweka wafu ile madhabahu baada ya kumiminiwa mafuta.
All the cattle for a sacrifice of peace-offering, twenty-four heifers, sixty rams, sixty he-goats of a year old, sixty ewe-lambs of a year old without blemish: this is the dedication of the altar, after that [Moses] consecrated [Aaron], and after he anointed him.
89 Musa alipoingia kwenye hema ya kukutania kusema na BWANA, ndipo alipoisikia sauti yake ikisema naye. BWANA alinena naye kutoka juu ya kiti cha rehema kilichokuwa juu ya sanduku la ushahidi, kutoka katikati ya makerubi. Alinena naye.
When Moses went into the tabernacle of witness to speak to God, then he heard the voice of the Lord speaking to him from off the mercy-seat, which is upon the ark of the testimony, between the two cherubs; and he spoke to him.

< Hesabu 7 >